Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Sidhani wakati wote unahitaji local professionals kufanya kazi.Kuna suala la security na ufichaji teknolojia watu wasiibe wakaanza kuvitengeneza ovyo.

Swali ni je Mpiga chapa wa serikali anayo credibility ya kuficha siri ya tecknolojia yake ya kuchapisha document za siri? Wafayakazi wake waweza aminika na wana historia ya uaminifu wa kuficha siri na kutochapisha vya ziada na kuwapa wageni mamluki?

Documents nyingi zenye features za siri zikiwemo passport,fedha,cheki na kadhalika za nchi nyingi tu duniani huchapishwa na nchi nyingine si kuwa wataalamu wanakuwa hawapo katika nchi hizo nadhani hata marekani hawachapi passport na pesa zao huchapishwa kwingine pamoja na uwezo mkubwa wa teknolojia walionao.India pekee ndio nasikia wanachapa pesa zao wenyewe nchini mwao.Nadhani inawezekana kwao sababu culture ya wahindi ni wasiri mno wao labda wwanaweza mambo haya.Ila kwa watanzania sijui.Mtu akipewa hiyo kazi kusema akilewa hataropoka kwenye baa sijui.

Labda kama mpiganaji nitoe siri ndogo ya kivita kwa wanaojenga nyumba.Unapojenga nyumba unapoweka dari usimchukue fundi wa kupiga dari wa karibu na eneo unaloishi.Mtafute fundi toka mbali hata kama wapo mafundi wengi tu kwenye eneo unaloishi.Sababu ni kuwa kwenye dari kuna lile tundu unalomalizia kufunga dari ambalo mtu aweza kupanda akitaka kuingia darini.Lile tundu unalomalizia kufunika dari ni eneo la vita hatakiwi mtu ajue liko wapi asijue liko sebureni,chumbani,jikoni,au wapi.Wakija majambazi waweza panda kwa spidi ya mwewe darini ukawasubiria kwenye eneo la tundu ya dari na bastola au bunduki yako au jiwe lako la fatuma.Sasa majambazi yakikaribia hilo eneo unalifungua kwa spidi ya mwewe na kuwamiminia risasi na kurukia mbali eneo lingine ambako hata warushe risasi hawakupati au ukishawamiminia risasi kwa spidi unafumua bati au kigae na kuruka nje na kukimbia kwa spidi ya kenge aliyejeruhiwa kusalimisha maisha yako au kuitia msaada au kuhamishia vita nje kweupe kwenye uwanja mnapoweza kuonana vizuri.

Sasa kama kazi ya kumalizia dari ukimpa fundi wa maeneo jirani aweza mwaga siri kwa majambazi wakajua eneo lako la kujidai kivita liko wapi.Ina maana unampa fundi wa mbali si kwa sababu mafundi hawapo bali una vitu hutaki vijulikane hovyo kwa usalama wako.

Sipingi wazawa kuchapisha lakini kuna vitu vingine kinachoangaliwa si uwezo tu wa kufanya kazi lakini pia usiri,usalama n.k Kama waweza na wana historia ya usiri na usalama wapewe si kuchapa vitambulisho tu bali hata pasipoti na kazi za kuchapa pesa wawape tu.
Hivi kwa nini TUTUMIE cards zenye microchip? Mimi nafikiri kwa nchi masikini kama Tanzania laminate cards inatosha. Bei yake ni karibu na bure. Ila tu ni kukomputerise huo utambulisho wa wahusika NA HAPO ITACHUKUA BILLION KIDOGO SANA.
Vituo vya Police pamoja na uongozi wa kata/tarafa/WILAYA wangehusika kuhakikisha uraia wa mtu.
Kama lazima kutumia makampuni, basi ya nje yasihusishwe. Anyway ni sisi nchi wachovu tunaopenda kuchapisha pesa, passports, etc, nchi zingine. Nchi imara km China, Korea, US, Japan, etc, hawafanyi hivyo
 
Nyani Ngabu,
Mkuu unajua hakuna kitu kigumu duniani kama utatumia elimu yako ya darasa kwa wale ambao hawana elimu..Na ukijaribu kuwa kama wao ndipo unapozidi kuharibu...
Acha elimu tu exposure pia unaweza kuchekesha vilevile, nakumbuka mwaka 1995 nilitaka kupeleka nyumbani matairi ya gari tubeless jamaa wakanambia hayawezi kuuzika Tanzania..Nikajaribu kuwaelekeza hawakunielewa zaidi ya kuona kuwa Mkandara kachanganyikiwa! Ikabidi nianze kutafuta matairi ya tube... mkuu kila mtu niliyemuuliza huku aliniona hamnazo na dunia gani naishi..

Wanabodi,
Tatizo la Masha naweza kuliweka sehemu mbili, kwanza aidha yupo ktk Mtandao na alikuwa anafanya deal Ama alikuwa akijaribu kubadilisha mentality ya watu ktk udanganyifu na ma deal ambayo hayana maslahi ya Taifa. Kwa kufanya hivyo amejikuta akifanya makosa ambayo sii makosa ila kwa yule mwenye kukisia kuna mchezo!
Nina hakika hata mimi katika position yake ningejaribu kuhakikisha nakwenda sambamba na taasisi ya tender kwa sababu record ya taasisi hii ni mbaya sana na ndiyo iliyotuingiza ktk hasara nyingi kubwa za kitaifa hasa nikipata malalamiko ya shirika hata moja tu..Hivyo Masha kachemsha kweli lakini hadi leo nashindwa kuelewa kama alichemsha kwa nia nzuri au mbaya!
Ajabu basi pamoja na makosa yote ya Masha, sisi wananchi na hasa hapa JF tumemkalia Masha kooni tumesahahu kabisa kwamba Taasisi hii ya tender ndiye yenye scandals kubwa sana na ulaji wote huanzia pale..
Ni rahisi sana kumkamata Masha au kiongozi yeyote nje ya board ya tender kuliko kufahamu kinachoendelea humo na hakika kama mnakumbuka tuliwahi kusema kama kweli viongozi wetu wanataka UWAZI basi tender yoyote ya kitaifa ni lazima ipitishwe na Bunge... Hili limeshindikana na limepigwa vita sana na viongozi tena wamelijengea hema kuwa ni siri ya serikali.. WHY?..

Mkandara, wasalaam,

Naomba nikukumbushe kwamba samaki uanza kuoza kutoka kichwani na si tumboni au mkiani. Kama ujatibu huko kichwani utakuwa ni sawa na kubeba maji kwa kutumia tenga.

Hiyo suggestion yako ni nzuri lakini it sound like we want to create a storm in the cup of tea.

wasalaam, shadow.
 
Mpigachapa Mkuu aachiwe zabuni ya vitambulisho

TAHARIRI
Tanzania Daima~Sauti ya Watu​

JANA serikali, kupitia Bodi ya Zabuni ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, imeteua kampuni sita zitakazoingia katika mchakato wa kupata kampuni moja itakayopewa kazi ya kuandaa mfumo wa vitambulisho vya taifa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na msemaji wa wizara hiyo, Isaac Nantanga, kampuni zilizoteuliwa na nchi zinakotoka kwenye mabano ni Unisys (Afrika Kusini), Giesecke & Devrient Fze (India), Iris Corporation Berhad (Malaysia) na Madras Security Printers (India), Marubeni Corporation ikishirikiana na Zetes pamoja na Nec (Japan) na Tata Consultancy Services inayoshirikiana na Ontrack Innovations Ltd (India).

Kampuni hizo zitakazoendelea kuchujwa ili kupata kampuni moja itakayopewa kazi ya kuandaa vitambulisho hivyo, zimepatikana baada ya mchujo wa kwanza ulioshirikisha kampuni 54 zilizotuma maombi ya zabuni hiyo.

Mchakato wa kupata kampuni hizo umefanyika wakati Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha, akiwa na kashfa ya kuingilia mchakato wa zabuni hiyo kwa lengo la kuipendelea kampuni ya Sagem Securite kinyume cha Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2004.

Hii ilimfanya Mbunge wa Karatu, Dk.Wilbrod Slaa (CHADEMA), kutaka kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhoji sababu za waziri huyo kuingilia mchakato huo na kuweka shinikizo.

Hata hivyo, hoja hiyo ilishindwa kujadiliwa bungeni baada ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kuzuia kwa maelezo kwamba Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ya Bunge ilikuwa ikiendelea kumhoji Masha na kuitaka bodi inayochambua zabuni hiyo kuendelea na mchakato wake, na kama bado kuna kasoro, hoja hiyo ya Dk. Slaa inaweza kuletwa bungeni tena.

Wakati matokeo ya kampuni hizo sita yakitangazwa, Mpigachapa Mkuu wa Serikali amebainisha kuwa anaweza kuendesha mradi huo kwa sh. bilioni 95 badala ya sh.bilioni 222.

Kwetu sisi kutangazwa kwa kampuni hizo ni jambo jema, kwani ni moja ya hatua zinazoweza kuharakisha mchakato uliochelewa wa kupata vitambulisho vya kitaifa. Kwa muda mrefu sasa vitambulisho hivyo imekuwa vikisubiriwa kwa hamu. Umuhimu na haja ya kuwa na vitambulisho hivyo umekuwa ukiongezeka.

Hatua ya kutangazwa kwa kampuni hizo sita, huku kampuni ya Sagem Securite iliyopigiwa chapuo na Masha ikiwa haipo, ni jambo linalotia faraja kuwa kilio cha wananchi na wabunge waliolalamika waziri huyo kutaka kampuni hiyo ipewe nafasi hiyo (kwa sababu zisizojulikana), kimesikika.

Hata hivyo, baada ya taarifa ya Mpigachapa Mkuu wa Serikali tunalazimika kujiuliza, ni kwa nini kazi hiyo isifanywe na mpigachapa huyo kwa sh bilioni 95 badala ya sh bilioni 222? Kampuni hizo zina uwezo gani kuzidi ule wa mpigachapa wa serikali?

Kitendo cha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuacha kumtumia mpigachapa wa serikali na wakati huo huo mchakato huo wa zabuni kuwa umeingiliwa na Masha, kinafanya suala la gharama ya utayarishaji wa vitambulisho (sh bilioni 222) kuwa ni jambo linalotia shaka zaidi.

Tunaona kuwa ni vema kazi hiyo angepewa mpigachapa wa serikali ili kuokoa kiasi kikubwa cha fedha, ambacho kingeweza kutumika kwa shughuli nyingine za kumkomboa Mtanzania maskini. Kiasi cha sh bilioni 127 zingeweza kuokolewa iwapo kazi hiyo angepewa mpigachapa wa serikali.

Ikiwa mpigachapa wa serikali hana uwezo wa kuandaa mfumo wa kutayarishwa kwa vitambulisho hivyo, basi ushauri wetu kwa serikali ni kuijengea uwezo idara ya Mpigachapa Mkuu wa Serikali, ikiwa ni pamoja na uwezo wa vifaa na watendaji wanaoweza kufanya kazi katika teknolojia za kisasa mathalan teknolojia ya smart card, ili taifa lisiendelee kuingia gharama ya kutumia kampuni za nje.
 
tk,
Ripoti gani hiyo ya madini? Siye huyu huyu Masha aliyekuwa wakili wa kampuni ambazo hivi sasa zinapora madini ya Watz?

Ni katika ripoti ya tume aliyoiongoza kuchunguza uendeshaji wa shughuli za madini nchini. Ripoti yake ndiyo ilikuwa kati ya ripoti za mwamzo kuonyesha jinsi nchi hii inavyoliwa kwa kupitia mikataba mibovu ya madini. Toeni hoja based on facts na bila kupendelea. Myonge mnyogeni lakini haki yake mpeni. Mpaka sasa sijaona hoja inayoeleza wapi waziri Masha alipokosea katika points zilizotolewa. For your information mimi huyo Masha wala sijamtia machoni licha ya kumuona kwenye magazeti na TV. Please tulifanye JF kuwa jukwaa la kielimu na sio la kuangamizana. pale penye ukweli tuuseme na pale penye udhaifu tuukemee.. Lakini kwa hoja.
 
Hongera tk. Wewe ni mfano wa mawakili bora, wenye uwezo na upeo mkubwa na unaitumia vema elimu yako kumtetea Waziri Masha kwani hii si mara yake ya kwanza kupindua jahazi ukianzia ripoti ya kuvinjari Keko usiku.[/QUOTE/)

Mimi si wakili wa Masha bali mtu anayepima mambo kutokana na facts. Katika Points 5 nilizozitoa utausaidia umma zaidi kama utonyesha wapi huyu waziri alipokosea kipengele kwa kipengele. Tuachane na Majungu ya mambo binafsi hapa tunazungumzia masuala mazito ya kitaifa sio mambo ya keko usiku...what the hell is that!!!. I though JF was the home of great thinkers!!
 
Hongera tk. Wewe ni mfano wa mawakili bora, wenye uwezo na upeo mkubwa na unaitumia vema elimu yako kumtetea Waziri Masha kwani hii si mara yake ya kwanza kupindua jahazi ukianzia ripoti ya kuvinjari Keko usiku.

See my comments above..
 
Haya mkuu, tunazisubiri hizo habari,
asiishie kukanusha bila uthibitisho. Nakumbuka nipashe walitaja hoteli na chumba alichokutana nao, sasa atueleze kinagaubaga ukweli wa mambo maana isije ikawa ile bifu ya waziri kijana ndo inamtafuna!!!!Na kama ikithibitika kwamba hakukutana na SAGEM na kama hana mawasiliano yoyote ya siri ili kuunufaisha upande mmoja basi achukue tahadhari siku nyingine asijaribu kumtunishia misuli mfanyabiashara mwanasiasa!!!

Lakini tusisubiri sana. Nipashe na Sema Usikike kwa kuwa waliandika habari hizo, basi ushahidi wanao tayari. Kwa hiyo tunategemea kesho watautoa katika magazeti yao. Kinyume cha hapo Masha azidishe kutunisha misuli kwa kuwaburuza mahakamani.
 
Old wine in a new bottle...Masha kisha pre-empt
 
Hongera tk. Wewe ni mfano wa mawakili bora, wenye uwezo na upeo mkubwa na unaitumia vema elimu yako kumtetea Waziri Masha kwani hii si mara yake ya kwanza kupindua jahazi ukianzia ripoti ya kuvinjari Keko usiku.[/QUOTE/)

Mimi si wakili wa Masha bali mtu anayepima mambo kutokana na facts. Katika Points 5 nilizozitoa utausaidia umma zaidi kama utonyesha wapi huyu waziri alipokosea kipengele kwa kipengele. Tuachane na Majungu ya mambo binafsi hapa tunazungumzia masuala mazito ya kitaifa sio mambo ya keko usiku...what the hell is that!!!. I though JF was the home of great thinkers!!

TK with due respect, mbona umerukia bunduki mwenyewe na kuanza kuhukumu? you sound to be prejudice too. Slow down, utajibiwa hizo 'hoja zako 5' na wadau.
 
Unapokuwa Waziri wewe ni "Public Property" kwa maana kila unachofanya au kusema kinatazamwa na wengi. Hata hivyo bado kuna maswali yanayotakiwa kujibiwa na Masha
1. Kwenye barua yake kwa Waziri mkuu hakuambatanisha barua ya malalamiko toka SAGEM, sasa walimlalamikia WAPI, LINI na KWA LIPI???????????????

2. Kwenye " Expression of Interest" documents, ILIAGIZWA kuwa MAELEKEZO NA MALALAMIKO YOTE yapelekwe kwa TENDER BOARD - Addressed KATIBU MKUU, yeye alipewa na nani hayo malalamiko????????? Ifahamike kuwa kisheria Nyaraka zote kwa wizara hutumwa kwa KATIBU MKUU!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

3. MASHA aliingiaje Katika mtiririko wa MANUNUZI YA WIZARA, Waziri ana nafasi gani?????? KWA KIFUPI HANA NAFASI, KWANI HII NI YA WATENDAJI WA TENDER BOARD na hufuata sheria za PUBLIC PROCUREMENT toka PPRA.

MAsha kama mwanasheria aliyebobea alitakiwa ayajue yote hayo, ili asiwape nafasi wanaotaka kumzonga, SASA KAMA ALIFANYA NI KWA NINI?????????? Watu wanahaki ya kujua si swala la kumchukia au la, si swala la kukutana na SAGEM au la, si swala la kuwatetea au la,
SWALA LA MSINGI ni kwa nini MLINZI wa AMANI na MTETEZI wa SHERIA ndie anazivunja, je zilindwe na NANI????????????????

Ningependa kupewa ufunuo kwa hayo bila mimi kuamua nani mkosaji kwani si kazi yangu??!!
 
Hyperthetically speaking!..maswali tunayojiuliza leo kuhusiana na Masha yanatokana na wasiwasi yetu kwake kutokana na barua ile? au ni huu mradi mzima!
Je, iweje hatukuweza kujiuliza maswali kama hayo wakati Dr. Slaa alipowasilisha EPA au Zitto na Buzwagi!..still nadhani tungeweza kujenga maswali kama haya..

Wakuu, naomba kufahamishwa zaidi maanake sipendi kumhukumu mtu wakati hatuna ushahidi wa kutosha hata kwa kuunganisha unganisha mbali na kwamba kachemsha!..
Nitarudia swali langu..
Kama wewe upo ktk nafasi yake kama waziri wa mambo ya ndani na umenusa harufu ya Rushwa toka taasisi ambayo imewahi kufanya mabaya kama haya utachukua hatua gani?..
 
Hyperthetically speaking!..maswali tunayojiuliza leo kuhusiana na Masha yanatokana na wasiwasi yetu kwake kutokana na barua ile? au ni huu mradi mzima!
Je, iweje hatukuweza kujiuliza maswali kama hayo wakati Dr. Slaa alipowasilisha EPA au Zitto na Buzwagi!..still nadhani tungeweza kujenga maswali kama haya..

Wakuu, naomba kufahamishwa zaidi maanake sipendi kumhukumu mtu wakati hatuna ushahidi wa kutosha hata kwa kuunganisha unganisha mbali na kwamba kachemsha!..
Nitarudia swali langu..
Kama wewe upo ktk nafasi yake kama waziri wa mambo ya ndani na umenusa harufu ya Rushwa toka taasisi ambayo imewahi kufanya mabaya kama haya utachukua hatua gani?..[/QUOTE]

Nita-REPORT taasisi ya kupambana na rushwa... (Si tunahimizwa hivyo na hao kina Masha??? au?
 
Tungejikita tangu zamani katika KUZUIA/KUKINGA ufisadi kama ilivyotokea kwenye hili sakata la vitambulisho vya taifa, madudu kama IPTL, TICTS, RICHMOND, BUZWAGI, RADA, KIWIRA, EPA, MINARA PACHA ya BOT, MIKATABA FEKI kama ile ya NETGROUP, VITALU VYA UWINDAJI yasingetokea, na watoto wetu wesingekuwa wanakalia mawe madarasani!
 
Last edited:
Hyperthetically speaking!..maswali tunayojiuliza leo kuhusiana na Masha yanatokana na wasiwasi yetu kwake kutokana na barua ile? au ni huu mradi mzima!
Je, iweje hatukuweza kujiuliza maswali kama hayo wakati Dr. Slaa alipowasilisha EPA au Zitto na Buzwagi!..still nadhani tungeweza kujenga maswali kama haya..

Wakuu, naomba kufahamishwa zaidi maanake sipendi kumhukumu mtu wakati hatuna ushahidi wa kutosha hata kwa kuunganisha unganisha mbali na kwamba kachemsha!..
Nitarudia swali langu..
Kama wewe upo ktk nafasi yake kama waziri wa mambo ya ndani na umenusa harufu ya Rushwa toka taasisi ambayo imewahi kufanya mabaya kama haya utachukua hatua gani?..

Mkandara

Mbona maswali kuhusu Chenge hayaulizwi jamani? Huyu jamaa amefanya uzembe ulioliingiza taifa kwenye hasara ya mabillioni ya shilingi, na bado taifa litaendelea kupata hasara ya mabillioni ya shilingi.

Hali ya ATCL na TRL yote haya ni matunda ya Chenge mzee wa vijisenti...je tumeshasahau? Au ndio kusema tumeridhika na kiongozi kuachia ngazi au kuachishwa?
 
Hyperthetically speaking!..maswali tunayojiuliza leo kuhusiana na Masha yanatokana na wasiwasi yetu kwake kutokana na barua ile? au ni huu mradi mzima!
Je, iweje hatukuweza kujiuliza maswali kama hayo wakati Dr. Slaa alipowasilisha EPA au Zitto na Buzwagi!..still nadhani tungeweza kujenga maswali kama haya..

Wakuu, naomba kufahamishwa zaidi maanake sipendi kumhukumu mtu wakati hatuna ushahidi wa kutosha hata kwa kuunganisha unganisha mbali na kwamba kachemsha!..
Nitarudia swali langu..
Kama wewe upo ktk nafasi yake kama waziri wa mambo ya ndani na umenusa harufu ya Rushwa toka taasisi ambayo imewahi kufanya mabaya kama haya utachukua hatua gani?..

Mifano uliyotoa si sahihi. Anacholalamikiwa Masha ni kuingilia tenda wakati mchakato unaendelea. Wakina Dr. Slaa , Zitto na wengine walitoa taarifa za tenda zilizoishakamilika na mikataba kuingiwa. Mimi nisingemlaumu waziri kama angelalamika baada ya mchakato kukamilika. Na ningemsifia zaidi kama angezuia mkataba kusainiwa kutokana na mashaka yake.

Kama waziri na umenusa na una ushahidi wa vitendo vya rushwa ungemfahamisha Katibu Mkuu wako na Taasisi nyingine husika na mara BAADA ya mchakato kuisha ungekataa ripoti na kutangaza zoezi zima kuwa batili. Baada ya kutangaza hivyo ungewachukulia hatua wahusika wote ambao ulikuwa na ushahidi kuwa walijihusisha na vitendo vya rushwa. Kuingilia kwa kusema tu ulinusa hakutoshelezi. Tuhuma ya rushwa ni kitu kizito na si cha kufanyia mzaha.

Tuhuma za rushwa zinafanya zoezi zima kuwa batili na si kurudisha tu wale ambao tunadhani walionewa. Kama walionewa kwa sababu ya rushwa kuna uhakika gani watatendewa haki wakirudishwa? Au wahusika hawatawapendelea kwa kuogopa kuwa wasipofanya hivyo watathibitisha kuwa walipokea rushwa? Baada ya zoezi kufutwa, bodi mpya iundwe ili kuweza kurudia zoezi zima kama itaonekana kuna haja.

Amandla.............
 
Hyperthetically speaking!..maswali tunayojiuliza leo kuhusiana na Masha yanatokana na wasiwasi yetu kwake kutokana na barua ile? au ni huu mradi mzima!
Je, iweje hatukuweza kujiuliza maswali kama hayo wakati Dr. Slaa alipowasilisha EPA au Zitto na Buzwagi!..still nadhani tungeweza kujenga maswali kama haya..

Wakuu, naomba kufahamishwa zaidi maanake sipendi kumhukumu mtu wakati hatuna ushahidi wa kutosha hata kwa kuunganisha unganisha mbali na kwamba kachemsha!..
Nitarudia swali langu..
Kama wewe upo ktk nafasi yake kama waziri wa mambo ya ndani na umenusa harufu ya Rushwa toka taasisi ambayo imewahi kufanya mabaya kama haya utachukua hatua gani?..[/QUOTE]

Nita-REPORT taasisi ya kupambana na rushwa... (Si tunahimizwa hivyo na hao kina Masha??? au?

Wakuu Mkandara na Macho_Mdiliko, heshima kwenu. Mimi naamini kuwa Masha ameingia kwenye matatizo baada ya ku-challenge ulaji wa watu. Nasema hivyo kwasababu tender hiyo inaelekea kuwa ina interest za watu wengi sana na wenye uwezo na ushawishi mkubwa. Ni kweli kuwa Masha kuamua kuandika barua kwa PM na kumuelezea hofu yake kuhusiana na jinsi mambo yanavyokwenda, alikuwa akidhani kuwa alikuwa anafanya jambo jema kwa Taifa. Nadhani kama Waziri, alihisi pia kuwa kuandika kwake barua ile kusingeweza kumsababishia matatizo makubwa ya kimtazamo. Hayo yote ni mawazo yangu na yanatokana zaidi na kumsikia kwangu akielezea suala zima. Japokuwa maelezo yake hayakuwa straight na yenye kujitosheleza sana.

Mkandara umeuliza swali la maana sana. Swali la "Kama wewe upo ktk nafasi yake kama waziri wa mambo ya ndani na umenusa harufu ya Rushwa toka taasisi ambayo imewahi kufanya mabaya kama haya utachukua hatua gani?".

Jibu rahisi na lenye maana ni kuandika barua kuelezea hisia zangu za rushwa na jinsi inayoonekana kutokea katika utekelezaji mzima (kama alivyofanya, ila kwa maelezo zaidi). Hasa nikiamini kuwa serikali yangu inafanya kazi kwa kumbukumbu na taratibu kama hizo. Na pia kwa kuamini kuwa siri za serikali hutunzwa vizuri na sio rahisi maandishi hayo kuchukuliwa kinyume na makusudio yake.

Mkuu kujibu swali lako kwa namna tofauti ni kufuatilia bila kuacha traces. Yaani kuongea na PM bila kuandika ama kupigia kelele matatizo yanayojitokeza bila kuacha kumbukumbu za kimaandishi. Hii ingeweza kueleweka vizuri zaidi kwa maana labda angeweza kueleza kwa undani zaidi kuliko ilivyo kwenye barua yake.

Ila kwa upande mwingine, ni vyema angefahamu nafasi yake kama Waziri katika mchakato wa siri kama huo na kuepuka kulalamikia/kuzungumzia ama kutolea kauli mchakato kwa utetezi wa bidder mmoja tu (nadhani hapo ndipo kosa lake lilipo). Angelalamika bila kutaja bidder yeyote, angeweza kuwa na hoja. Ila kwa kulalamika kuwa bidder fulani anaonewa peke yake, wakati kuna wengine ambao pia walienguliwa, inazua maneno mengi na kumsababishia kashfa kama hizo zilizojitokeza.
 
Halafu cha kuchekesha eti tunaambiwa huyu Masha ni msomi....

Kama Masha kabobea sijui Johnnie Cochran alikuwaje....

Ni kweli Masha ni Msomi aliyebobea kwenye taaluma ya Sheria. Ameingia darasani shule ya kiukweli akasoma sheria.
Kubobea ni kile kitendo cha kusoma degree zote mbili za fani moja yaani 1st Degree na Advanced Degree (Masters).
Na sasa anajiandaa kufanya Ph.D ya sheria.

Kubobea kwenye sheria ni jambo moja na kuwa mahiri ni jambo jingine. Pia sheria nayo ina fani mbalimbali na wanasheria mbali mbali wana uwezo tofauti. Masha ni wakili lakini sio mahiri kiasi cha kumlinganisha na kina
Cochram. Hata hiyo IMMA ni ma Corporate Lawyers hawadeal na criminal cases hivyo no matter how Masha atapractice miaka mingapi, hawezi kuwa Cochram kwa vile its a different line. Hata hivyo, tunao akina Cochram wetu, akina Murtaza Lakha, Majura Magafu, Prof. Mgongo Fimbo, Prof. Issa Shivji.

Kuwa na heavy CV ni one thing na uwezo wa kujieleza is another and the ability to make sound decisions is yet something else. Mh. Masha anachemsha 'The American Style ya ki 'Watergate Watergate'.
 
kama masha , mh WAZIRI, amekashifiwa siaende mahakamani sasa vitisho vya nini? mara tunawasiliana na wanasheria, kumbuka hata baada ya orodha ya mafisadi 11 kutajwa pale Mwembe yanga, kila alietajwa kuanzia mgonja, na wengine wote walitishia kwenda mahakamani mara baada ya wanasheria wao kuandaa mashitaka, kinyume chake walipoenda mahakamani hawakurudi , Masha asitumie vitisho atanngulie tu mahakamani tutakuna huko tukifuatilia utetezi wake.
ni mawazo yangu.
 
=Recta;377208]
Mkandara umeuliza swali la maana sana. Swali la "Kama wewe upo ktk nafasi yake kama waziri wa mambo ya ndani na umenusa harufu ya Rushwa toka taasisi ambayo imewahi kufanya mabaya kama haya utachukua hatua gani?".

Jibu rahisi na lenye maana ni kuandika barua kuelezea hisia zangu za rushwa na jinsi inayoonekana kutokea katika utekelezaji mzima (kama alivyofanya, ila kwa maelezo zaidi). Hasa nikiamini kuwa serikali yangu inafanya kazi kwa kumbukumbu na taratibu kama hizo. Na pia kwa kuamini kuwa siri za serikali hutunzwa vizuri na sio rahisi maandishi hayo kuchukuliwa kinyume na makusudio yake.
Hapo mkuu sikubaliani na wewe au labda sikuelewi. Hivi Waziri ambaye kweli anajua kazi yake vizuri anaweza kuanza kulalamika kwa barua kwa jambo ambalo ana hakika nalo?? Kama huo ndo mwendo wa mawaziri wa JK kumwandikia PM au Rais barua za malalamiko tena ndefu namna hiyo basi au wakubwa watakuwa wanafanya kazi moja tu ya kusoma barua!!

Ila kwa upande mwingine, ni vyema angefahamu nafasi yake kama Waziri katika mchakato wa siri kama huo na kuepuka kulalamikia/kuzungumzia ama kutolea kauli mchakato kwa utetezi wa bidder mmoja tu (nadhani hapo ndipo kosa lake lilipo). Angelalamika bila kutaja bidder yeyote, angeweza kuwa na hoja. Ila kwa kulalamika kuwa bidder fulani anaonewa peke yake, wakati kuna wengine ambao pia walienguliwa, inazua maneno mengi na kumsababishia kashfa kama hizo zilizojitokeza.

Hapo uko sahihi.Hilo suala la kula sahani moja na Tender Board kwa ajili ya kampuni moja tu kati ya 54 lazima limpe mashaka kila mtu atakayesikia habari hizo. Kwamba LM ana undugu gani na Segem hadi awaonee huruma sana kwa kuenguliwa?? Hilo swali naona hakuna hata aliyediriki kumuuliza. Labda angetueleza kuwa hiyo kampuni sasa ina ubia na IMMA???🙄

Hata hivyo sina imani na viongozi wengi wa Tz na kwa hiyo hata hiyo orodha iliyotolewa inawezekana kila kampuni ilibebwa kwa mbeleko yake. Labda tunachoona ni kuwa mbeleko ya Masha ilizidiwa uzito na kuchanika. Hii ni Bongo na kila kitu si kama kinavyoonekana, USANII UNATISHA!!😕
 
Back
Top Bottom