Asali ya limao
Member
- Dec 27, 2018
- 57
- 104
SURA YA KWANZA
ASUBUHI YA HEKA HEKA
Utangulizi.
Richard Dawson, mrakibu mwandamizi wa jeshi la polisikanda maalum ya Dar es salaam, miaka mitano tu tangu ajiungena jeshi hilo, lenye jukumu la kulinda raia na mali zao lakiniilitosha jina lake kusemwa katika korido za makao makuu yajeshi hilo na hata ripoti za majaladya kesi mbali mali alizopewakuzisimamia hazikuacha maswali pale ziliposomwa na wakubwa zake kicheo waliomtuma kuyafanyia kazi. naam unaweza kumuita majina kama mfanyakazi mwenye weledi wa hali ya juu katika kazi yake hiyo ya kipolisi.
Kwa kufanikisha kufichua uhalifu pamoja na kuwakamata wahalifu wakubwa na wadogo kitu kilichofanya sifa zake kuenea kote ndani ya jeshi hilo pamoja na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ndani ya Tanzania.
vaa viatu, fuatana nami.
kama ilivyo kawaida kwa wakazi wengi wa mji huo wa raha na karaha yaani Dar es salaam, asubuhi ya kila siku huanza kwapilika na heka heka nyingi sana ili mradi familia na waowenyewe wawez kupata chochote kitu.
grrrrhh grrrrhh……mlio wamtetemo wa simu juu ya meza unamstua bwana Richard aliekuwa ametopea katika usingizi mzito sana alioupata mara baada ya kumaliza heka heka na kuanza likizo
yake.”msyuuuu”nisauti ya kusonya na kuonekana msonyaji alikereka na huenda hakutarajia kupata bugudha akiwa kati raha yausingizi ule uliokuwa umemlevya kiasi cha kutosha, akaurefusha mkono wake kuichukua simu yake kwnye kimeza kidogo kilicho karibu na kitanda na hapo akapigwa na butwaa baada ya kuitazamanamba ile namba ya simu iliyokuwa imekatisha usingizi wake haikuwa nyingine bali ilikuwa ya kamishina msaidiziwa jeshi la polisi SACP Joseph cherehani ambae pia ni kamandawa polisi wa mkoa huo
ASP Richard: “jambo afande, niko timamu tayari kwamaelekezo.” aliongea kikakamavu afisa huyo wa jeshi la polisiakisubiri sauti ya bosi wake ipate kuunguruma lakini badalayake,upande wa pili ulipopiga simu ulikuwa kimya kupimautulivu kikafatia mkoromo wa kitu kama kikohozi cha kulainisha koo na ndipo kisha likasika neno kwa sauti tulivu ilailiyojaa mamlaka na amri.
"NAKUHITAJI OFISINI KWANGU NDANI YA MASAA MAWILI TOKA SASA" nakilichofatia ni mlio wa Tiitiiih tiiitiiih kumaanisha mpigajiamekwisha kubonyeza kitufe chekundu yaani ameshaikata simuhiyo.
"Kumetokea kitu gani mpaka nihitajike kwa haraka kiasi hikikatika ofisi ya kamanda ndiyo kwanza nina siku ya kwanza tangu nimepewa barua ya likizo " alijiwazia ASP Richard alijiwazia mwisho aliingia katika chumba anachofanyiamazoezi, akatumia dakika thelathini katika kupasha viungo vyamwili joto, akaingia bafuni kwake na kuosha mwili wake kishaakajiandaa na kutoka katika nyumba anayokaa ambayo nimiongoni mwa nyumba alizozinunua kutoka shirika la nyumbala taifa (NHC).
Akawasha gari lake na kutokomea katika ofisi yakamanda.Wakati h , ayo yakiendelea kwa upande wa ASP Richard, upande mwingine asubuhi hii iliingia shubiri na vitiwalivyovikalia vilikuwa vya moto hapo katika chumba hikokulikuwa na kiyoyozi Ila wajumbe katika kikao hichowalionekana kufuta jasho jembamba kila dakika mbele Yao alikaa mwanamke wa makamo, naam hakuna mwingine Bali Mheshimiwa raisi Gloria Steven, mwanamke mwenye msimamomkali na aside na mzaha kwenye mambo ya msingiyanayolihusu taifa, leo hii aliitisha kikao cha dharula kilichowahusu wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, mbele take kulikuwa na mkuu wa jeshi la wananchi, inspekta jenerali wa polisi, Kamishnaa wa idara ya uhamiaji, kamishna wa magerezana mkurugenzi wa idara ya ujasusi, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa na jibu la kueleweka katika ripoti zao, wote ni kama walikuwa wamekalia kuti kavu Ambalo muda wowote lingekatika na kuwadondosha kwa uzito na ugumu wa mambo yanayoendelea kila Jua linapochomoza.
"Nina Imani kwamba mnafahamu na mmeweza kusikia mambo yanayotokea kila siku kwenye taifa hili, wananchi wangu wanaishi kwa hofu hawana uhakika wa usalama wao pamoja namali zao, uhalifu umekithiri kundi Fulani limeshajitangaziajamhuri na nyie wenye dhamana ya kuilinda Amani hiyommekaa tu ofisini mnazunguka tu na Ma V8 huku wanaofanyamuishi Maisha mazuri ninyi na Familia zenu kupitia kodi zaowanaishi kwa hofu huko mitaani"
"hakuna hata mmoja went hapa mwenye ripoti inayochimbakiini cha mambo haya, mmesahau majukumu yenu ya msingi, naKuna engine niliwapamba kwa speech nzuri wakati nawaapishakiasi Sasa najuta ni here ngeweka maneno Yale kama akiba, mzee wangu IGP unaweza kunambia ni kwanini mpaka leobiashara ya dawa za kulevya inazidi kushamiri, hakuna vitendeakazi?
Idadi ya watendaji wako ni pungufu kuliko ugumu wakazi? umebakiwa na muda wa mwaka mmoja na nusu iliutundike hizo buti ni chaguo lako kumaliza utumishi wako kwafuraha na bashasha au kumaliza kwa aibu na fedheha."
kiti alichokalia IGP kilikuwa ni kama kinawaka moto kwakufokewa kule na bosi wake na kuna muda alijilaumu kufanyakazi ya upolisi huenda sasa hivi angekuwa nyumbani kwake au mashambani kwake alipojiwazia kwamba sio ishu ya madawa yakulevya pekeake bali kuna mauaji ya mawaziri watatu ndani yausiku mmoja alijikuta akivuta punzi nyingi kwa ndanina kuzitoataratibu, alizama katika tafakari zito mpaka aliposhtushwa nasauti ya mheshimiwa raisi.
"mzee wangu wa magereza, unaweza kuwa na lolote kuhusu kutoroka kwa yule mshtakiwa wa kesi ya ugaidi tena katika gereza mnalojinasibu nyie watu wa magereza kuwa ulinzi wake ni kama ikulu hii, aliwezaje lutoroka gerezani ukonga kama hakuna watendaji unaowaongoza kushirikiana nae, hiii haikuoneshi picha ya wasi kwa namna yoyote vijana wako wasivyo na weledi na hatujuikwa muda huu gaidi huyo atakuwa bado nchini au kashaondokandiyo maana nimewaita wote hapa ili mjue madudu yenu"
"nahitaji mkurugenzi wa idara ya ujasusi uniletee ripoti yaupotevu wa fedha zilizokuwa zinapelekwa katika benki kuu tawila mwanza, mwalimu wangu katika medani hizi za usalamaaliwahi kusema kuwa usalama wa taifa ni akili sio ukali, kaziyake ni kukusanya, kuchanganua, kudurusu na kuunganishakwa makini, taarifa nyeti za ndani nje ya nchi kulilinda taifa nawatu wake, lakini mzee wangu hujafanya lolote kati ya hayomajukumu, unanishawishi kwa kipi nkuache ukitafuna kodi zao.Mzee wangu sihitaji kukukumbusha majukumu natambua uzoefu ulionao idarani na oparesheni ulizosimamia ndizozilizonifanya kukuweka hapo nakuomba tafadhari Sana usinitukanishe huko duniani.
"nawapa siku 14 muarobaini wa hili jambo uwe umepatikana naatakayeona ugumu wa jambo hili niko tayari kupokea barua yakujiuzuru kwa mikono miwili." akasimama na kuondoka hukuwalinzi na mpambe wake wakimsindikiza tayari kwa kwendakwenye kikao kingine na baraza la mawaziri.
viongozi wale wa ulinzi na usalama wakaamua na kukubalianakwa pamoja kuwa kiundwe kikosi maalum kitakachohusishawatu wa kazi kwa kila vyombo hvyo vya ulinzi na usalamawatakaoenda na kasi ya siku walizopewa kupata ripoti nan matokeo chanya yatakayo nusuru vibarua vyao kwani walijuajinsi mheshimiwa raisi alivyo na maamuzi magumu na hapepesimacho pale kunapotokea madudu, waliagana wakipeana mudawa saa moja kwa ajili ya kupendekeza jina kwa kila idara yaulinzi na usalamaa
Saa 10:05 asubuhi
ndiyo muda uliomkuta ASP Richard akiwanyuma ya mlango wa kamanda wa jeshi hilo kanda malum ya Dar es salaam baada ya kuwa amepewa maelekezo ya kutoshana katibu muhtasi wa kamanda huyo kwamba akifika apitilizemoja kwa moja ofisini kwake. akakinyonga kitasa cha mlangoule na sekunde iliyofatia alijikuta kwenye ofisi panailiyopangwa kwa ustadi wa hali ya juu huku ikinakishiwa nahewa safi inayopatikana katikana katika kiyoyozi kilekalichotengenezwa na kampuni ya LG (life is good) ubaridiwake kiasi usioumiza mfumo wa upumuaji wa mtu au watu, kwa aliebahatika kuivuta hewa katika ofisi ake hakustaajabu hilomaana ni kawaida kwa ofisi kama ile kuwa na mpangilio sahihiwa vitu na mazingira yanayoizunguka.
Alishtushwa na sura alizozikuta ndani ya ofisi ile, Naam kulikuwa na wanaume watatu na wanawake wawili waliokuwakatika mavazi ya suti zao nadhifu, pamoja na hurufu nzuri yamanukato ambayo iliwatambulisha kwamba watu hawa niwazito kinyadhifa na pia kiuchumi, ukiondoa wnaume hao nawanawake wanaofunga idadi ya kuwa watano mbele yao alikaamwanaume mmoja alionekana tu kuwa ni mkakamavu naasubuhi hiyo uso wake haukupambwa na tashititi yoyote yatabasamu. kwa ukakamavu wa hali ya juu alitoa heshima kwakupiga saluti mbele ya wakuu hao.
Hakuna hata mmoja alieshughulika nae badala vichwa vyao namawazo yao yalikuwa juu ya majalada matano ya kesi mbalimbali zilizotikisa vituo vikubwa vya polisi katika jiji hilo, kamanda wa polisi aliamua ukimya uliokuwa ndani mle uendelikizo kwa kumuomba kijana yule aketi na kisha akafunguamazungumzo yale kwa sauti ya utulivu.
SACP Cherehani:" ASP Richard nimekuita hapa nkiwa naimani kabisa ulikula kiapo cha kulitumikia taifa katikamazingira yote ya utumishi wako, nayasema haya kwasababunatambua umeanza likizo yako, lakini kikubwa tu nimepigiwasimu na afande IGP, akinitaka nkupe ujumbe kwambaunahitajika kufika makao makuu haraka iwezekanavyo, nkutakieutekelezaji mwema wa maagizo utakayopewa, mimi sina lolotela kukujibu kwa maana sijui utakachoelezwa huko ila wasiwasiwangu huenda ni haya matukio yanayoendelea kutupasuakichwa na kutunyima usingizi kila jua linapoamka na kuzama." ASP Richard akapiga salute na kuondoka kuwahi hukoanapohitajika.
*******************************
MAKAO MAKUU YA JESHI LA POLISI
Saa 11:35 asubuhi, huu ndiyo muda ambao mrakibu msaidizi wapolisi bwana Richard alikuwa mbele ya mapokezi na kuambiwaapite moja kwa moja hadi ofisini kwa IGP, akatoa heshima kwamkubwa wake huyo wa kazi na kukaribishwa tayari kwa ajili yamaagizo
"ASP Richard nimelipitia jalada lenye taarifa zako na taarifa yamwisho inaonesha uko likizo, asubuhi ya leo kulikua na kikaonyeti ili kujadiliana kuhusu hali ya ulinzi na usalama nchinikiukweli hali ni mbaya na kichwa changu kinapata moto, simuza viongozi wengi zinaita huku nyingi zikiwa ni za maswaliambayo hata mimi sina majibu nayasema haya kwa msisitizo iliupate kutambua uzito wa mambo haya, bila hivo taifa litakuwagizani katika sintofahamu hizi pia wengine kama sisi nafasi zetuziko rehani, mbali na uzalendo na mapenzi katika kazi hii lakinisitakuwa tayari kuwaona wahalifu wakijitangazia jamhuri yaona mimi nikirudishwa makao makuu nkasome magazeti nakurudi nyumbani nkacheze na wajukuu. nnakupa muda wamwezi mmoja nipate ripoti kamili pamoja na washalifuwaliohusika na matukio haya kama yalivyoainishwa kwenyemajalada haya kufikishwa mahakamani, utapewa ushirikiano wakutosha na wenzako hapa lakini ripoti ya mwisho utanileteamimi ili niifikishe kwa mheshimiwa raisi ,yangu ni hayo labdakama una swali ila jua swali lako litajibiwa hukoutakapoenda. napewa ujumbe kwamba usafiri wakukupeleka huko unakusubiri kwenye maegesho ya magarihapo chini, nkutakie majukumu mema na ukatuwakilishevyema.
akapiga saluti na kutoka ofisini kwa kigogo yule wa jeshi zimala polisi, akashuka kutoka ghorofa ya tano iliyopo ofisi ile nakutumia ngazi huku akitumia dakika 5 kuyafikia maegesho namara aliona gari imewesha taa na kuizima, akajongea mpakakwenye gari lile dereva akamfungulia mlango siti ya pembenikwa dereva nae bila ajizi alikaa huku akiwaza ni wapianapopelekwa
"tutatumia muda gani kufika huko" alimuuliza dereva huyoambaye hakufumbua kinywa kusema kitu chochote zaidi yakuwa bize na usukani, kuona hivyo alijiongeza kuwa derevahuyo hakutaka maongezi, alizama kwenye fikra kali na ndipokumbukumbu zikaja kichwani kwake kuwa kesho yake ni siku ya kuzaliwa kwa mtoto wake kelvin, mtoto aliyezaa namwanamke kisha kutengana kwa sababu ambazo zilikuwa nje yauwezo wake, kazi zilimfanya awe bize kiasi cha kupata mudakidogo sana wakukaa nayo, na hiyo ndiyo sababu iliyofanyaatengane na mwanamke baada ya kukosa huduma za kimwilikutoka kwa mwanaume huyo kiasi cha kujutia kwanini aliwahikumpenda mwanaume huyo, mbnli na kuwa bize sana katikakupambana na wahalifu lakini hakuwahi kuacha kuikumbuka nakuijali familia yake, hata baada ya kutengana na mke wake aliendelea kuwajali huku akijua ipo siku watarudi mikononimwake kama zamani
"tumeshafika shuka na utasubiri hapa kwa taratibu zingine, mimikazi yangu imeishia hapa" akafanya na muda sio mrefu akatokeajamaa mmoja mwenye upara na mkakamavu akiwa kwenye sutiyake nadhifu ya rangi nyeusi, "tuongozane chief anakusubiriASP Richard" hakutaka kujiuliza jamaa huyo kalijuaje jina lake ila aligundua huyo mtu aliekuja kumpokea atakuwa na taarifazake"
wakaingia katika jengo la nyumba hiyo ya gorofa moja iliyokaakama makazi ya mtu,lakini kiukweli ni miongoni mwa nyumbasalama(safe house) za idara ya usalama wa taifa,na ilizungukwana ulinzi mkali wa watu ambao hakusumbua akili yake kujiulizaikiwa anatambua haiba ya watu wale kama makomandoo wajeshi la wananchi na idara ya usalama wa taifa, akajua kuletwakwake hapo ni kwa ajili ya kukabidhiwa kazi nyeti sana au kuoneshwa kitu nyeti sana, mlangoo uligongwa mara mbili nakisha wa ukafunguliwa na kuingia.
"karibu sana ASP richard ni sauti iliyotoka kutoka kwa mtualiyekuwa amempa mgongo hakuwa mwingine bali mkurugenziwa idara ya ujasusi ya taifa, chifu Desmondi mkosamali, mtu wamiraba minne na mwenye macho makali wakati huo tabasamulake lilikuwa likizo kufutia kikao kilichofanyika asubuhi hiyokatika ikulu ya Tanzania.
kuweka umakini kwa mtu yule kulimsahaulisha kwamba mlendani kulikuwa na sura zingine sita, chifu aligeuka na hapo ASP Richard alitoa heshima kwa kumpigia salute mtu yule, "karibuuketi, hawa unaowaona ni watu ambao utashirikiana naokwenye hili ambalo muda si mrefu ntawenda kuwaeleza, akameza mate kisha akasema huyo bidada mrembo unaemuonahapo mwanzoni kwako kulia anaitwa luteni sabina chacha, komandoo wa jeshi la wananchi na mdunguaji, akasimama nakupiga saluti kikakamavu kabisa, huyo anaemfatia ni sajentimayunga samson kutoka kikosi cha kuzuia na kupambana nakulevya, nae akasima na kupiga saluti, huyo dogo hapo anaitwajames shayo kutoka idara ya ujasusi ni mtaalamu wa mitambo nateknolojia,kushoto kwako uliekaribu nae ni meja sadiki tumbaku, komandoo wa jeshi la wananchi, anaemfatia ni dianachiwawa kutoka idara ya ujasusi na huyo wa mwisho ni inspektajafari malingumu kutoka jeshi la polisi makao makuu na wewehapo ASP Richard Dawson kutoka jeshi la polisi, timu ya watusaba inayohitajika lufanya kazi kama mchwa wajengapokichuguu." hawakuelewa maana ya mstari wa mwisho wamaneno aliyosema chifu, wakastaajabu ndani ya nyumbakulikuwa kuna eneoambalo lipo chini ya ardhi baada ya chifukugusa ukuta kisha ukafunguka kisha akawasha taa na eneozima huko chini likawa na mwanga wa kutosha watu wotewalistaajabu walichokiona kompyuta za kisasa, silaha na dhanambali mbali ziliwafanya kupigia mstari na kengele ya taadhariikalia vichwani kwao kwamba' TAYARI KUMESHAKUCHA'
" tusikilizane wote mliopo hapa mpo kwa sababu ya kutafutauvumbuzi wa haya yanayoendelea nchini, kwa kifupi kunamatukio yametokea na ripoti za awali zinaonesha kunamuunganiko kati ya tukio moja na jingine na hili kufanya hatawakuu wenzangu kuhisi mhusika au wahusika kuwa ni hao haowanaotukosesha usingizi, tukianza na tukio la tarehe 20 mweziwa saba mwaka huu wiki tatu nyuma la kutekwa na kuuwawakwa mawaziri wawili wa wizara nyeti za serikali na gavana wabenki kuu linatajwa kuwa na ushabihiano wa tukio la kuvamiwamsafara uliokuwa ukisafirisha pesa kuzipeleka tawi la benki kuumwanza katikati ya mapori nje kidogo ya mji wa manyoni nakisha mauaji ya walinzi waliokuwawnazisafirisha haitofautianisana na wizi uliofanyika katika ghala la silaha katika kambi yajeshi huko mafinga masaa manne baadae ishara tosha kwambawatu hawa walijipanga"
mbali na hayo tukio jingine linalotuumiza kichwa ni hili la kutoroka kwa MUSTAPHA ABDI NUR AHMED gaidi sugualietafutwa kwa takribani miaka kumi na mashirika mbali mbaliya kijasusi duniani, mwaka jana tulimkamata na kumfungiakatika gereza la ukonga huku akisubiri hukumu yake ndipoalipotoroka wiki iliyoisha na kisha majuzi tulishuhudiakulipuliwa kwa bomu kiwanda cha sukari huko morogoro najana taarifa zimetufikia kuwa kiwanda ki nguine cha maziwahuko Tanga kimelipuliwa usiku wa jana, matukio yote hayayanatisha na kuwatia watu hofu"
"mna siku kumi na mbili za kunifikishia ripoti ya mambo hayayote mezani kwangu, na wahusika wa haya matukio nahitajikuwaona kwa sura zao, oparesheni hii ni ya kukamatainapoonekana kuna ugumu wa kufanya hvo muwafute katika usowa dunia hii, mna baraka zangu na vitambulisho vyenumtavipata mara baada ya kutoka humu kama kuna chochotemtanitaarifu ili nirahisishe kazi yenu, ripoti yote itanifikia mimiili niiwasilishe kwa mheshimiwa raisi, mwisho napendakuwataarifu kwamba meja Sadiki tumbaku ndiyo atakayekuwakiongozi wenu, niwatakie utendaji mwema na wenye weledi ilimtuletee matokeo chanya"
wakashusha pumzi huku wakikuna kichwa kwa majukumu hayowaliyopewa waliona kazi iliyopo ilivyo ngumu na uchache wa muda ili kuwapata wahusika vile vile. ********* itaendelea………….:unataka kujua kilichoendelea vuta kiti kaa tayari kwa kuona giza lenye kivuli. Tchao
NB: Simulizi hii iko katika mfumo wa PDF kwa mwenye uhitaji wa kuisoma yote ikiwa ni kuburudika na kuelemika sogelea kwenye PM yangu ukiwa na Tshs 5000/= nkuoe njia ya malipo ukaburudike nwapenda sana!!!
ASUBUHI YA HEKA HEKA
Utangulizi.
Richard Dawson, mrakibu mwandamizi wa jeshi la polisikanda maalum ya Dar es salaam, miaka mitano tu tangu ajiungena jeshi hilo, lenye jukumu la kulinda raia na mali zao lakiniilitosha jina lake kusemwa katika korido za makao makuu yajeshi hilo na hata ripoti za majaladya kesi mbali mali alizopewakuzisimamia hazikuacha maswali pale ziliposomwa na wakubwa zake kicheo waliomtuma kuyafanyia kazi. naam unaweza kumuita majina kama mfanyakazi mwenye weledi wa hali ya juu katika kazi yake hiyo ya kipolisi.
Kwa kufanikisha kufichua uhalifu pamoja na kuwakamata wahalifu wakubwa na wadogo kitu kilichofanya sifa zake kuenea kote ndani ya jeshi hilo pamoja na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ndani ya Tanzania.
vaa viatu, fuatana nami.
kama ilivyo kawaida kwa wakazi wengi wa mji huo wa raha na karaha yaani Dar es salaam, asubuhi ya kila siku huanza kwapilika na heka heka nyingi sana ili mradi familia na waowenyewe wawez kupata chochote kitu.
grrrrhh grrrrhh……mlio wamtetemo wa simu juu ya meza unamstua bwana Richard aliekuwa ametopea katika usingizi mzito sana alioupata mara baada ya kumaliza heka heka na kuanza likizo
yake.”msyuuuu”nisauti ya kusonya na kuonekana msonyaji alikereka na huenda hakutarajia kupata bugudha akiwa kati raha yausingizi ule uliokuwa umemlevya kiasi cha kutosha, akaurefusha mkono wake kuichukua simu yake kwnye kimeza kidogo kilicho karibu na kitanda na hapo akapigwa na butwaa baada ya kuitazamanamba ile namba ya simu iliyokuwa imekatisha usingizi wake haikuwa nyingine bali ilikuwa ya kamishina msaidiziwa jeshi la polisi SACP Joseph cherehani ambae pia ni kamandawa polisi wa mkoa huo
ASP Richard: “jambo afande, niko timamu tayari kwamaelekezo.” aliongea kikakamavu afisa huyo wa jeshi la polisiakisubiri sauti ya bosi wake ipate kuunguruma lakini badalayake,upande wa pili ulipopiga simu ulikuwa kimya kupimautulivu kikafatia mkoromo wa kitu kama kikohozi cha kulainisha koo na ndipo kisha likasika neno kwa sauti tulivu ilailiyojaa mamlaka na amri.
"NAKUHITAJI OFISINI KWANGU NDANI YA MASAA MAWILI TOKA SASA" nakilichofatia ni mlio wa Tiitiiih tiiitiiih kumaanisha mpigajiamekwisha kubonyeza kitufe chekundu yaani ameshaikata simuhiyo.
"Kumetokea kitu gani mpaka nihitajike kwa haraka kiasi hikikatika ofisi ya kamanda ndiyo kwanza nina siku ya kwanza tangu nimepewa barua ya likizo " alijiwazia ASP Richard alijiwazia mwisho aliingia katika chumba anachofanyiamazoezi, akatumia dakika thelathini katika kupasha viungo vyamwili joto, akaingia bafuni kwake na kuosha mwili wake kishaakajiandaa na kutoka katika nyumba anayokaa ambayo nimiongoni mwa nyumba alizozinunua kutoka shirika la nyumbala taifa (NHC).
Akawasha gari lake na kutokomea katika ofisi yakamanda.Wakati h , ayo yakiendelea kwa upande wa ASP Richard, upande mwingine asubuhi hii iliingia shubiri na vitiwalivyovikalia vilikuwa vya moto hapo katika chumba hikokulikuwa na kiyoyozi Ila wajumbe katika kikao hichowalionekana kufuta jasho jembamba kila dakika mbele Yao alikaa mwanamke wa makamo, naam hakuna mwingine Bali Mheshimiwa raisi Gloria Steven, mwanamke mwenye msimamomkali na aside na mzaha kwenye mambo ya msingiyanayolihusu taifa, leo hii aliitisha kikao cha dharula kilichowahusu wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, mbele take kulikuwa na mkuu wa jeshi la wananchi, inspekta jenerali wa polisi, Kamishnaa wa idara ya uhamiaji, kamishna wa magerezana mkurugenzi wa idara ya ujasusi, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa na jibu la kueleweka katika ripoti zao, wote ni kama walikuwa wamekalia kuti kavu Ambalo muda wowote lingekatika na kuwadondosha kwa uzito na ugumu wa mambo yanayoendelea kila Jua linapochomoza.
"Nina Imani kwamba mnafahamu na mmeweza kusikia mambo yanayotokea kila siku kwenye taifa hili, wananchi wangu wanaishi kwa hofu hawana uhakika wa usalama wao pamoja namali zao, uhalifu umekithiri kundi Fulani limeshajitangaziajamhuri na nyie wenye dhamana ya kuilinda Amani hiyommekaa tu ofisini mnazunguka tu na Ma V8 huku wanaofanyamuishi Maisha mazuri ninyi na Familia zenu kupitia kodi zaowanaishi kwa hofu huko mitaani"
"hakuna hata mmoja went hapa mwenye ripoti inayochimbakiini cha mambo haya, mmesahau majukumu yenu ya msingi, naKuna engine niliwapamba kwa speech nzuri wakati nawaapishakiasi Sasa najuta ni here ngeweka maneno Yale kama akiba, mzee wangu IGP unaweza kunambia ni kwanini mpaka leobiashara ya dawa za kulevya inazidi kushamiri, hakuna vitendeakazi?
Idadi ya watendaji wako ni pungufu kuliko ugumu wakazi? umebakiwa na muda wa mwaka mmoja na nusu iliutundike hizo buti ni chaguo lako kumaliza utumishi wako kwafuraha na bashasha au kumaliza kwa aibu na fedheha."
kiti alichokalia IGP kilikuwa ni kama kinawaka moto kwakufokewa kule na bosi wake na kuna muda alijilaumu kufanyakazi ya upolisi huenda sasa hivi angekuwa nyumbani kwake au mashambani kwake alipojiwazia kwamba sio ishu ya madawa yakulevya pekeake bali kuna mauaji ya mawaziri watatu ndani yausiku mmoja alijikuta akivuta punzi nyingi kwa ndanina kuzitoataratibu, alizama katika tafakari zito mpaka aliposhtushwa nasauti ya mheshimiwa raisi.
"mzee wangu wa magereza, unaweza kuwa na lolote kuhusu kutoroka kwa yule mshtakiwa wa kesi ya ugaidi tena katika gereza mnalojinasibu nyie watu wa magereza kuwa ulinzi wake ni kama ikulu hii, aliwezaje lutoroka gerezani ukonga kama hakuna watendaji unaowaongoza kushirikiana nae, hiii haikuoneshi picha ya wasi kwa namna yoyote vijana wako wasivyo na weledi na hatujuikwa muda huu gaidi huyo atakuwa bado nchini au kashaondokandiyo maana nimewaita wote hapa ili mjue madudu yenu"
"nahitaji mkurugenzi wa idara ya ujasusi uniletee ripoti yaupotevu wa fedha zilizokuwa zinapelekwa katika benki kuu tawila mwanza, mwalimu wangu katika medani hizi za usalamaaliwahi kusema kuwa usalama wa taifa ni akili sio ukali, kaziyake ni kukusanya, kuchanganua, kudurusu na kuunganishakwa makini, taarifa nyeti za ndani nje ya nchi kulilinda taifa nawatu wake, lakini mzee wangu hujafanya lolote kati ya hayomajukumu, unanishawishi kwa kipi nkuache ukitafuna kodi zao.Mzee wangu sihitaji kukukumbusha majukumu natambua uzoefu ulionao idarani na oparesheni ulizosimamia ndizozilizonifanya kukuweka hapo nakuomba tafadhari Sana usinitukanishe huko duniani.
"nawapa siku 14 muarobaini wa hili jambo uwe umepatikana naatakayeona ugumu wa jambo hili niko tayari kupokea barua yakujiuzuru kwa mikono miwili." akasimama na kuondoka hukuwalinzi na mpambe wake wakimsindikiza tayari kwa kwendakwenye kikao kingine na baraza la mawaziri.
viongozi wale wa ulinzi na usalama wakaamua na kukubalianakwa pamoja kuwa kiundwe kikosi maalum kitakachohusishawatu wa kazi kwa kila vyombo hvyo vya ulinzi na usalamawatakaoenda na kasi ya siku walizopewa kupata ripoti nan matokeo chanya yatakayo nusuru vibarua vyao kwani walijuajinsi mheshimiwa raisi alivyo na maamuzi magumu na hapepesimacho pale kunapotokea madudu, waliagana wakipeana mudawa saa moja kwa ajili ya kupendekeza jina kwa kila idara yaulinzi na usalamaa
Saa 10:05 asubuhi
ndiyo muda uliomkuta ASP Richard akiwanyuma ya mlango wa kamanda wa jeshi hilo kanda malum ya Dar es salaam baada ya kuwa amepewa maelekezo ya kutoshana katibu muhtasi wa kamanda huyo kwamba akifika apitilizemoja kwa moja ofisini kwake. akakinyonga kitasa cha mlangoule na sekunde iliyofatia alijikuta kwenye ofisi panailiyopangwa kwa ustadi wa hali ya juu huku ikinakishiwa nahewa safi inayopatikana katikana katika kiyoyozi kilekalichotengenezwa na kampuni ya LG (life is good) ubaridiwake kiasi usioumiza mfumo wa upumuaji wa mtu au watu, kwa aliebahatika kuivuta hewa katika ofisi ake hakustaajabu hilomaana ni kawaida kwa ofisi kama ile kuwa na mpangilio sahihiwa vitu na mazingira yanayoizunguka.
Alishtushwa na sura alizozikuta ndani ya ofisi ile, Naam kulikuwa na wanaume watatu na wanawake wawili waliokuwakatika mavazi ya suti zao nadhifu, pamoja na hurufu nzuri yamanukato ambayo iliwatambulisha kwamba watu hawa niwazito kinyadhifa na pia kiuchumi, ukiondoa wnaume hao nawanawake wanaofunga idadi ya kuwa watano mbele yao alikaamwanaume mmoja alionekana tu kuwa ni mkakamavu naasubuhi hiyo uso wake haukupambwa na tashititi yoyote yatabasamu. kwa ukakamavu wa hali ya juu alitoa heshima kwakupiga saluti mbele ya wakuu hao.
Hakuna hata mmoja alieshughulika nae badala vichwa vyao namawazo yao yalikuwa juu ya majalada matano ya kesi mbalimbali zilizotikisa vituo vikubwa vya polisi katika jiji hilo, kamanda wa polisi aliamua ukimya uliokuwa ndani mle uendelikizo kwa kumuomba kijana yule aketi na kisha akafunguamazungumzo yale kwa sauti ya utulivu.
SACP Cherehani:" ASP Richard nimekuita hapa nkiwa naimani kabisa ulikula kiapo cha kulitumikia taifa katikamazingira yote ya utumishi wako, nayasema haya kwasababunatambua umeanza likizo yako, lakini kikubwa tu nimepigiwasimu na afande IGP, akinitaka nkupe ujumbe kwambaunahitajika kufika makao makuu haraka iwezekanavyo, nkutakieutekelezaji mwema wa maagizo utakayopewa, mimi sina lolotela kukujibu kwa maana sijui utakachoelezwa huko ila wasiwasiwangu huenda ni haya matukio yanayoendelea kutupasuakichwa na kutunyima usingizi kila jua linapoamka na kuzama." ASP Richard akapiga salute na kuondoka kuwahi hukoanapohitajika.
*******************************
MAKAO MAKUU YA JESHI LA POLISI
Saa 11:35 asubuhi, huu ndiyo muda ambao mrakibu msaidizi wapolisi bwana Richard alikuwa mbele ya mapokezi na kuambiwaapite moja kwa moja hadi ofisini kwa IGP, akatoa heshima kwamkubwa wake huyo wa kazi na kukaribishwa tayari kwa ajili yamaagizo
"ASP Richard nimelipitia jalada lenye taarifa zako na taarifa yamwisho inaonesha uko likizo, asubuhi ya leo kulikua na kikaonyeti ili kujadiliana kuhusu hali ya ulinzi na usalama nchinikiukweli hali ni mbaya na kichwa changu kinapata moto, simuza viongozi wengi zinaita huku nyingi zikiwa ni za maswaliambayo hata mimi sina majibu nayasema haya kwa msisitizo iliupate kutambua uzito wa mambo haya, bila hivo taifa litakuwagizani katika sintofahamu hizi pia wengine kama sisi nafasi zetuziko rehani, mbali na uzalendo na mapenzi katika kazi hii lakinisitakuwa tayari kuwaona wahalifu wakijitangazia jamhuri yaona mimi nikirudishwa makao makuu nkasome magazeti nakurudi nyumbani nkacheze na wajukuu. nnakupa muda wamwezi mmoja nipate ripoti kamili pamoja na washalifuwaliohusika na matukio haya kama yalivyoainishwa kwenyemajalada haya kufikishwa mahakamani, utapewa ushirikiano wakutosha na wenzako hapa lakini ripoti ya mwisho utanileteamimi ili niifikishe kwa mheshimiwa raisi ,yangu ni hayo labdakama una swali ila jua swali lako litajibiwa hukoutakapoenda. napewa ujumbe kwamba usafiri wakukupeleka huko unakusubiri kwenye maegesho ya magarihapo chini, nkutakie majukumu mema na ukatuwakilishevyema.
akapiga saluti na kutoka ofisini kwa kigogo yule wa jeshi zimala polisi, akashuka kutoka ghorofa ya tano iliyopo ofisi ile nakutumia ngazi huku akitumia dakika 5 kuyafikia maegesho namara aliona gari imewesha taa na kuizima, akajongea mpakakwenye gari lile dereva akamfungulia mlango siti ya pembenikwa dereva nae bila ajizi alikaa huku akiwaza ni wapianapopelekwa
"tutatumia muda gani kufika huko" alimuuliza dereva huyoambaye hakufumbua kinywa kusema kitu chochote zaidi yakuwa bize na usukani, kuona hivyo alijiongeza kuwa derevahuyo hakutaka maongezi, alizama kwenye fikra kali na ndipokumbukumbu zikaja kichwani kwake kuwa kesho yake ni siku ya kuzaliwa kwa mtoto wake kelvin, mtoto aliyezaa namwanamke kisha kutengana kwa sababu ambazo zilikuwa nje yauwezo wake, kazi zilimfanya awe bize kiasi cha kupata mudakidogo sana wakukaa nayo, na hiyo ndiyo sababu iliyofanyaatengane na mwanamke baada ya kukosa huduma za kimwilikutoka kwa mwanaume huyo kiasi cha kujutia kwanini aliwahikumpenda mwanaume huyo, mbnli na kuwa bize sana katikakupambana na wahalifu lakini hakuwahi kuacha kuikumbuka nakuijali familia yake, hata baada ya kutengana na mke wake aliendelea kuwajali huku akijua ipo siku watarudi mikononimwake kama zamani
"tumeshafika shuka na utasubiri hapa kwa taratibu zingine, mimikazi yangu imeishia hapa" akafanya na muda sio mrefu akatokeajamaa mmoja mwenye upara na mkakamavu akiwa kwenye sutiyake nadhifu ya rangi nyeusi, "tuongozane chief anakusubiriASP Richard" hakutaka kujiuliza jamaa huyo kalijuaje jina lake ila aligundua huyo mtu aliekuja kumpokea atakuwa na taarifazake"
wakaingia katika jengo la nyumba hiyo ya gorofa moja iliyokaakama makazi ya mtu,lakini kiukweli ni miongoni mwa nyumbasalama(safe house) za idara ya usalama wa taifa,na ilizungukwana ulinzi mkali wa watu ambao hakusumbua akili yake kujiulizaikiwa anatambua haiba ya watu wale kama makomandoo wajeshi la wananchi na idara ya usalama wa taifa, akajua kuletwakwake hapo ni kwa ajili ya kukabidhiwa kazi nyeti sana au kuoneshwa kitu nyeti sana, mlangoo uligongwa mara mbili nakisha wa ukafunguliwa na kuingia.
"karibu sana ASP richard ni sauti iliyotoka kutoka kwa mtualiyekuwa amempa mgongo hakuwa mwingine bali mkurugenziwa idara ya ujasusi ya taifa, chifu Desmondi mkosamali, mtu wamiraba minne na mwenye macho makali wakati huo tabasamulake lilikuwa likizo kufutia kikao kilichofanyika asubuhi hiyokatika ikulu ya Tanzania.
kuweka umakini kwa mtu yule kulimsahaulisha kwamba mlendani kulikuwa na sura zingine sita, chifu aligeuka na hapo ASP Richard alitoa heshima kwa kumpigia salute mtu yule, "karibuuketi, hawa unaowaona ni watu ambao utashirikiana naokwenye hili ambalo muda si mrefu ntawenda kuwaeleza, akameza mate kisha akasema huyo bidada mrembo unaemuonahapo mwanzoni kwako kulia anaitwa luteni sabina chacha, komandoo wa jeshi la wananchi na mdunguaji, akasimama nakupiga saluti kikakamavu kabisa, huyo anaemfatia ni sajentimayunga samson kutoka kikosi cha kuzuia na kupambana nakulevya, nae akasima na kupiga saluti, huyo dogo hapo anaitwajames shayo kutoka idara ya ujasusi ni mtaalamu wa mitambo nateknolojia,kushoto kwako uliekaribu nae ni meja sadiki tumbaku, komandoo wa jeshi la wananchi, anaemfatia ni dianachiwawa kutoka idara ya ujasusi na huyo wa mwisho ni inspektajafari malingumu kutoka jeshi la polisi makao makuu na wewehapo ASP Richard Dawson kutoka jeshi la polisi, timu ya watusaba inayohitajika lufanya kazi kama mchwa wajengapokichuguu." hawakuelewa maana ya mstari wa mwisho wamaneno aliyosema chifu, wakastaajabu ndani ya nyumbakulikuwa kuna eneoambalo lipo chini ya ardhi baada ya chifukugusa ukuta kisha ukafunguka kisha akawasha taa na eneozima huko chini likawa na mwanga wa kutosha watu wotewalistaajabu walichokiona kompyuta za kisasa, silaha na dhanambali mbali ziliwafanya kupigia mstari na kengele ya taadhariikalia vichwani kwao kwamba' TAYARI KUMESHAKUCHA'
" tusikilizane wote mliopo hapa mpo kwa sababu ya kutafutauvumbuzi wa haya yanayoendelea nchini, kwa kifupi kunamatukio yametokea na ripoti za awali zinaonesha kunamuunganiko kati ya tukio moja na jingine na hili kufanya hatawakuu wenzangu kuhisi mhusika au wahusika kuwa ni hao haowanaotukosesha usingizi, tukianza na tukio la tarehe 20 mweziwa saba mwaka huu wiki tatu nyuma la kutekwa na kuuwawakwa mawaziri wawili wa wizara nyeti za serikali na gavana wabenki kuu linatajwa kuwa na ushabihiano wa tukio la kuvamiwamsafara uliokuwa ukisafirisha pesa kuzipeleka tawi la benki kuumwanza katikati ya mapori nje kidogo ya mji wa manyoni nakisha mauaji ya walinzi waliokuwawnazisafirisha haitofautianisana na wizi uliofanyika katika ghala la silaha katika kambi yajeshi huko mafinga masaa manne baadae ishara tosha kwambawatu hawa walijipanga"
mbali na hayo tukio jingine linalotuumiza kichwa ni hili la kutoroka kwa MUSTAPHA ABDI NUR AHMED gaidi sugualietafutwa kwa takribani miaka kumi na mashirika mbali mbaliya kijasusi duniani, mwaka jana tulimkamata na kumfungiakatika gereza la ukonga huku akisubiri hukumu yake ndipoalipotoroka wiki iliyoisha na kisha majuzi tulishuhudiakulipuliwa kwa bomu kiwanda cha sukari huko morogoro najana taarifa zimetufikia kuwa kiwanda ki nguine cha maziwahuko Tanga kimelipuliwa usiku wa jana, matukio yote hayayanatisha na kuwatia watu hofu"
"mna siku kumi na mbili za kunifikishia ripoti ya mambo hayayote mezani kwangu, na wahusika wa haya matukio nahitajikuwaona kwa sura zao, oparesheni hii ni ya kukamatainapoonekana kuna ugumu wa kufanya hvo muwafute katika usowa dunia hii, mna baraka zangu na vitambulisho vyenumtavipata mara baada ya kutoka humu kama kuna chochotemtanitaarifu ili nirahisishe kazi yenu, ripoti yote itanifikia mimiili niiwasilishe kwa mheshimiwa raisi, mwisho napendakuwataarifu kwamba meja Sadiki tumbaku ndiyo atakayekuwakiongozi wenu, niwatakie utendaji mwema na wenye weledi ilimtuletee matokeo chanya"
wakashusha pumzi huku wakikuna kichwa kwa majukumu hayowaliyopewa waliona kazi iliyopo ilivyo ngumu na uchache wa muda ili kuwapata wahusika vile vile. ********* itaendelea………….:unataka kujua kilichoendelea vuta kiti kaa tayari kwa kuona giza lenye kivuli. Tchao
NB: Simulizi hii iko katika mfumo wa PDF kwa mwenye uhitaji wa kuisoma yote ikiwa ni kuburudika na kuelemika sogelea kwenye PM yangu ukiwa na Tshs 5000/= nkuoe njia ya malipo ukaburudike nwapenda sana!!!