Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Nilisema kuwa kelele za Slaa si bure lazima itakuwa amepokonywa tonge tu na kuzidiwa kete ?
 
Sober
Am sure we need National IDs. but when we will start using our proffesionals in our country? Wanatakiwa wafanye kazi ya ku-prove we always judge them wrong! Hatutaendelea kuabudu na kuamini kuwa vyote vilivyobora ni lazima vitoke ama vitengenezwe na watu wa nje.
Mfano
Wakati wa mkutano wa Sullivan pale arusha, tulikuwa na wataalamu wetu pale na walitengeneza Ids za chap chap na ni bora tu.

Sidhani wakati wote unahitaji local professionals kufanya kazi.Kuna suala la security na ufichaji teknolojia watu wasiibe wakaanza kuvitengeneza ovyo.

Swali ni je Mpiga chapa wa serikali anayo credibility ya kuficha siri ya tecknolojia yake ya kuchapisha document za siri? Wafayakazi wake waweza aminika na wana historia ya uaminifu wa kuficha siri na kutochapisha vya ziada na kuwapa wageni mamluki?

Documents nyingi zenye features za siri zikiwemo passport,fedha,cheki na kadhalika za nchi nyingi tu duniani huchapishwa na nchi nyingine si kuwa wataalamu wanakuwa hawapo katika nchi hizo nadhani hata marekani hawachapi passport na pesa zao huchapishwa kwingine pamoja na uwezo mkubwa wa teknolojia walionao.India pekee ndio nasikia wanachapa pesa zao wenyewe nchini mwao.Nadhani inawezekana kwao sababu culture ya wahindi ni wasiri mno wao labda wwanaweza mambo haya.Ila kwa watanzania sijui.Mtu akipewa hiyo kazi kusema akilewa hataropoka kwenye baa sijui.

Labda kama mpiganaji nitoe siri ndogo ya kivita kwa wanaojenga nyumba.Unapojenga nyumba unapoweka dari usimchukue fundi wa kupiga dari wa karibu na eneo unaloishi.Mtafute fundi toka mbali hata kama wapo mafundi wengi tu kwenye eneo unaloishi.Sababu ni kuwa kwenye dari kuna lile tundu unalomalizia kufunga dari ambalo mtu aweza kupanda akitaka kuingia darini.Lile tundu unalomalizia kufunika dari ni eneo la vita hatakiwi mtu ajue liko wapi asijue liko sebureni,chumbani,jikoni,au wapi.Wakija majambazi waweza panda kwa spidi ya mwewe darini ukawasubiria kwenye eneo la tundu ya dari na bastola au bunduki yako au jiwe lako la fatuma.Sasa majambazi yakikaribia hilo eneo unalifungua kwa spidi ya mwewe na kuwamiminia risasi na kurukia mbali eneo lingine ambako hata warushe risasi hawakupati au ukishawamiminia risasi kwa spidi unafumua bati au kigae na kuruka nje na kukimbia kwa spidi ya kenge aliyejeruhiwa kusalimisha maisha yako au kuitia msaada au kuhamishia vita nje kweupe kwenye uwanja mnapoweza kuonana vizuri.

Sasa kama kazi ya kumalizia dari ukimpa fundi wa maeneo jirani aweza mwaga siri kwa majambazi wakajua eneo lako la kujidai kivita liko wapi.Ina maana unampa fundi wa mbali si kwa sababu mafundi hawapo bali una vitu hutaki vijulikane hovyo kwa usalama wako.

Sipingi wazawa kuchapisha lakini kuna vitu vingine kinachoangaliwa si uwezo tu wa kufanya kazi lakini pia usiri,usalama n.k Kama waweza na wana historia ya usiri na usalama wapewe si kuchapa vitambulisho tu bali hata pasipoti na kazi za kuchapa pesa wawape tu.
 
Mkuu BUBU katika hoja za leo niligusia kuwa imefika mahali pa Watanzania kuonekana WAJINGA na WAJINGA NDIO WALIWAO. hebu mtu alete JUSTIFICATION kutoka bilioni 95 mpaka bilioni 222. Kuna WIZI wa mchana hapa nadhani ni bora tudai hili ZOEZI ZIMA LA VITAMBULISHO lismamishwe mara moja. nina hakika mahali fulani BLA BLAA ya faida ya hivyo vitambulisho itakuwa imezungumzwa au kuelezewa nafikiri kuna haja ya kusita na kufikiria tena.




Ni kweli unayosema lakini Je tenda hiyo akipewa mpigachapa wa serikali kazi itakuwa na ubora? ikiwa vitabu vya sheria tu ( Law reports za kuanzia 1983 kama sikosei) zilichapwa south na matokeo yake vinauzwa kwa dola,ndio iwe vitambulisho? Lakini jambo kubwa hapa ni ufisadi,kila kazi inajengewa asilimia kumi,ndio maana tumekuwa watumwa wa akili
 
Mkuu BUBU katika hoja za leo niligusia kuwa imefika mahali pa Watanzania kuonekana WAJINGA na WAJINGA NDIO WALIWAO. hebu mtu alete JUSTIFICATION kutoka bilioni 95 mpaka bilioni 222. Kuna WIZI wa mchana hapa nadhani ni bora tudai hili ZOEZI ZIMA LA VITAMBULISHO lismamishwe mara moja. nina hakika mahali fulani BLA BLAA ya faida ya hivyo vitambulisho itakuwa imezungumzwa au kuelezewa nafikiri kuna haja ya kusita na kufikiria tena.

Mkuu Jujuman, 'viongozi' wetu wamekuwa wakipita huku na kule kuwatangazia Watanzania kwamba wasinunue bidhaa za nje kwa sababu bidhaa zetu za ndani zina ubora karibu sawa au sawa na bidhaa za nje.

Shilingi bilioni 127 ni nyingi sana. Zinaweza kuelekezwa katika ununuzi wa vitanda katika mahospitali yetu ili kuhakikisha hakuna Mtanzania mgonjwa au mjamzito atakayelala chini hospitali au kushare kitanda kimoja na wenzake ambao hufikia hadi saba!!! Sijui kitanda kimoja kinaweza kutumika na wagonjwa/wajawazito saba kwa wakati mmoja. Baadhi ya pesa hizo zinaweza kuelekezwa kununua madawati na kujenga madarasa yenye hadhi ili kuhakikisha hakuna mwanafunzi wa darasa la saba anayepasi lakini kukosa nafasi ya kuendelea kwa sababu ya 'upungufu wa madarasa', zinaweza kuelekezwa katika kuwasomesha walimu ili kuhakikisha shule za msingi na sekondari hazina upungufu wa walimu. Hili pia litasaidia kucreate employment kubwa kwa walimu katika mshule yetu ya msingi na sekondari.

Watanzania tunasubiri kuisikia 'siri kali' itasema nini kuhusiana na hii habari kwamba hizo ID zinaweza kutengenezwa nchini kwa bei ndogo ukilinganisha na bei tunayoijua sasa ta shilingi bilioni 222. Sitta kwa mara nyingine anaweza kutamka kwamba wacha tu mchakato uendelee maana umeshafikia hatua ya mbali hata kama kuna ushahidi wa taratibu za mchakato huo kukiukwa na baadhi ya viongozi au hata kama kuna ushahidi kwamba kama ID hizo zikitengenezwa nchini basi Taifa litaokoa shilingi bilioni 127 ambazo ni sawa na $127 millioni (approximately).
 
Last edited:
Vitambulisho: Mpigachapa wa Serikali angechapa kwa Sh95bn badala ya Sh222bn: Government Printer apewe hii zabuni kwa Sh95bn alizo-quote katika tender yake. Hata kama itakuwa ni lazima baadaye aongezewe fedha zaidi, Tanzania tutakuwa tumeweka misingi ya kuendelea kuchapisha vitambulisho hapa nchini bila kutumia tena fedha za kigeni. Serikali isaidie hata kuleta mitambo stahili ikiwa ni lazima.

Inavyoeleweka ni kwamba tukishaanza kutoa vitambulisho vya uraia, kama taifa, zoezi hilo litaendelea kila wakati Watanzania raia wanavyozaliwa na kukua kuhitaji vitambulisho. Kwa sasa siyo tu tutaokoa matumizi ya fedha za kigeni katika malipo kwa wachapishaji, bali ajira itaongezeka na watu wetu watapata uzoefu. Hayo ndiyo maendeleo ya kiuchumi thabiti.

Wale wanaotaka vitambulisho vya "high quality" au "state of the art" , lazima tuwe na confidence kwamba watu wetu wanaweza pia, bora tu wapate mtaalam atakayekuja na huo mtambo kuonyesha. Hata hivyo mimi binafsi naamini vitambulisho vya Uraia siyo hati (documents) zinazoweza kughushiwa kwa wingi na kuleta madhara kwa umma. Najua katika kutoa vitambulisho kutakuwa na Afisa wa Serikali atakayesaini kila kitambulisho, pamoja na kutia muhuri wake.

Kwa hiyo ningeshauri kwa dhati kabisa kwamba Rais Jakaya Kikwete atupilie mbali zabuni zote za kigeni zilizopokelewa, na zabuni ya uchapishaji wa vitambulisho vya uraia apewe Mpigachapa wa Serikali. Uamuzi kama huo utaondoa utata wa ufisadi na kuharakisha utoaji wa hati hizi muhimu kwa utambulisho wa uraia wetu.

Kilasara (JF Member)
 
Sober
Am sure we need National IDs. Its also true that cheap sometimes is expensive! but when we will start using our proffesionals in our country? Wanatakiwa wafanye kazi ya ku-prove we always judge them wrong! Hatutaendelea kuabudu na kuamini kuwa vyote vilivyobora ni lazima vitoke ama vitengenezwe na watu wa nje.
Mfano
Wakati wa mkutano wa Sullivan pale arusha, tulikuwa na wataalamu wetu pale na walitengeneza Ids za chap chap na ni bora tu. Tunachotakiwa hapa ni Chibogoyo atueleze namna anavyotaka kutengeneza hizo IDs ili ziendane na technogy ya sasa. Its time we start using our people now!

Big up, on top of that, making something expensive doesn't signify quality. It can be just price discrimination or other way round. The MP's argued that the same can possibly be made domestically after visiting the right man so surely they were convinced by the available technology for the task at hand.
 
Hivi serikali ya JK ilishawahi kufanya tathmini ya kujua gharama za ununuzi wa hii mashine? Naamini mashine kama hiyo inaweza kutumia utaalamu huo huo kutengeneza hata LESENI ZA UDEREVA.
Labda ingekuwa vizuri kuinunua mashine kuliko kutoa tenda. Sababu itafika muda tutahitaji Driving licence ambazo zitakuwa za kisasa. Yatakuwa mambo yaleyale ya IPTL, tukishaibiwa ndo tunaanza kujadili kuinunua IPTL au mitambo.
Vitu vingine havihitaji kwenda darasani kupata busara ya maamuzi.
 
Vitambulisho: Mpigachapa wa Serikali angechapa kwa Sh95bn badala ya Sh222bn: Government Printer apewe hii zabuni kwa Sh95bn alizo-quote katika tender yake. Hata kama itakuwa ni lazima baadaye aongezewe fedha zaidi, Tanzania tutakuwa tumeweka misingi ya kuendelea kuchapisha vitambulisho hapa nchini bila kutumia tena fedha za kigeni. Serikali isaidie hata kuleta mitambo stahili ikiwa ni lazima.

Inavyoeleweka ni kwamba tukishaanza kutoa vitambulisho vya uraia, kama taifa, zoezi hilo litaendelea kila wakati Watanzania raia wanavyozaliwa na kukua kuhitaji vitambulisho. Kwa sasa siyo tu tutaokoa matumizi ya fedha za kigeni katika malipo kwa wachapishaji, bali ajira itaongezeka na watu wetu watapata uzoefu. Hayo ndiyo maendeleo ya kiuchumi thabiti.

Wale wanaotaka vitambulisho vya "high quality" au "state of the art" , lazima tuwe na confidence kwamba watu wetu wanaweza pia, bora tu wapate mtaalam atakayekuja na huo mtambo kuonyesha. Hata hivyo mimi binafsi naamini vitambulisho vya Uraia siyo hati (documents) zinazoweza kughushiwa kwa wingi na kuleta madhara kwa umma. Najua katika kutoa vitambulisho kutakuwa na Afisa wa Serikali atakayesaini kila kitambulisho, pamoja na kutia muhuri wake.

Kwa hiyo ningeshauri kwa dhati kabisa kwamba Rais Jakaya Kikwete atupilie mbali zabuni zote za kigeni zilizopokelewa, na zabuni ya uchapishaji wa vitambulisho vya uraia apewe Mpigachapa wa Serikali. Uamuzi kama huo utaondoa utata wa ufisadi na kuharakisha utoaji wa hati hizi muhimu kwa utambulisho wa uraia wetu.

Kilasara (JF Member)

Mkuu uko sawa kabisa
Jee Nani atalipia uchaguzi wa mwaka 2010 ?
 
What about Mpiga Chapa wa Serikali?😕😕😕


Sunday Feb 15, 2009

Six firms race for IDs project

DAILY NEWS Reporter, 15th February 2009 @ 10:18


The government has short-listed six companies from which only one could get a tender to produce the country's first national identity cards using the smart-card technology. The list does not include Sagem Securite company which recently sparked debate over claims that Home Affairs Minister Lawrence Masha was interfering with the tendering process in favour of the company.

Debate was sparked by Karatu MP (Chadema) Dr Wilbrod Slaa who filed a private motion demanding that Mr Masha be taken to task for contravening public procurement regulations. However, the motion was resolved at Parliamentary committee level. A statement released yesterday by the Ministry of Home Affairs said that the six companies were short-listed from 54 companies.

The six companies were identified as Unisys (South Africa), Giesecke & Devrient FZE (Dubai), Iris Corporation Berhad (Malaysia), Madra Security Printers (India), Marubeni Corporation in collaboration with Zetes and NEC (Japan) and Tata Consultancy Services in collaboration with Ontrack Innovations Ltd (India). The statement further explained that the second screening will begin soon, and that it is expected to be finalized soon.


The exercise was done by the ministry's tender board and involved the screening of some 54 eligible firms. The first round saw 33 bidders thrown out and that 13 of them were dropped in the second -- leaving only eight. According to inside information, Sagem Securite company was thrown out in the second round when 13 companies were eliminated – and Mr Masha has refuted claims of attempting to favour the company but admitted to have written to the Prime Minister claiming that he was being sidelined in the whole process.

Members of the tender board include the Permanent Secretary of the Ministry of Home Affairs, Commissioner for Prisons, Inspector General of Police and Head of the Fire Brigade and representative of Prevention and Combating of Corruption Bureau.Two years ago, the government announced the immediate implementation of a multi-billion-shilling National Identification Card Project scheduled for completion this year.

Joseph Mungai, then Home Affairs Minister, said in Dodoma in February 2007 that the Smartcard system would be employed in place of the Barcode one used during the registration of voters for the 2005 General Election.The former minister said the project would cost 192bn/- and an independent National ID Management Agency would be formed and operate under the auspices of the ministry.

Funds had already been secured from various sources, with the World Bank having set aside USD 20m for the project, he added. Speaking with the 'Daily News' over the phone yesterday, the Minister for Finance and Economic Affairs, Mr Mustafa Mkulo, said his ministry was involved in the project as it was wholly administered by the Ministry of Home Affairs.

Comparative advantages of the Smartcard system are storage of abundant information such as DNA analyses, criminal or medical reports, fingerprints and people's birthplaces. Other valid data could be added to the card when necessary, including relevant information for national census purposes and on the number of eligible voters, the birth rate and development plans.
 
Sober
Am sure we need National IDs. Its also true that cheap sometimes is expensive! but when we will start using our proffesionals in our country? Wanatakiwa wafanye kazi ya ku-prove we always judge them wrong! Hatutaendelea kuabudu na kuamini kuwa vyote vilivyobora ni lazima vitoke ama vitengenezwe na watu wa nje.
Mfano
Wakati wa mkutano wa Sullivan pale arusha, tulikuwa na wataalamu wetu pale na walitengeneza Ids za chap chap na ni bora tu. Tunachotakiwa hapa ni Chibogoyo atueleze namna anavyotaka kutengeneza hizo IDs ili ziendane na technogy ya sasa. Its time we start using our people now!
Ni kweli its about time, Tanzania ijengwe na Watanzania wenyewe. Hii ndio pill iliotumiwa na 'The Emerging Economies' kuzitoa katika lindi la umasikini mpaka kuwa mataifa ya neema yenye proper industrialization.
Ni kweli mpigachapa anaweza kuwa hana smart card technology lakini tayari hapa hapa bongo kuna taasisi zinazotumia smart card vikiwemo vitambulisho vya UDSM. Kwa vile mimi sio mtu wa IT, sijui lolote kuhusu latest technology, lakini bado kwa hizo hizo bilioni 222 tungeweza kujenga uwezo hata kwa kutumia data base ya RITA na Vitambulisho vya kupigia kura. Mkemia Mkuu anayo DNA kwa Biometric Data, Mambo ya Ndani wanazo latest machines za finger prints, bado hiyo ID inataka nini zaidi. Tukiziwezesha taasisi zetu na faida ya hiyo bilioni 222 ikabaki hapa nchini.
Viwanda ndio hatuna, tunabakia kuwa masoko ya wenzetu, tukitupiwa every junk products, sasa hata service provision lazima tuwape wageni!?.
'Ama kweli Mwenenacho anaongezewa, na Asiyenacho, ananyang'anywa hata kidogo alichonacho', kwa Tanzania
Hatunyang'anywi bali 'tunakigawa' hicho kidogo tulichonacho!.
 
.........Pengine kabla ya ku-jump kuwa Mchapaji mkuu wa serikali anaweza kufanya kazi au lah.....tujiulize hizi Billioni 222 zinatoka wapi........je ni solely Government money from its own source of income au ni Mkopo toka vyombo vya fedha vya kimataifa........
 
Ni kweli unayosema lakini Je tenda hiyo akipewa mpigachapa wa serikali kazi itakuwa na ubora? ikiwa vitabu vya sheria tu ( Law reports za kuanzia 1983 kama sikosei) zilichapwa south na matokeo yake vinauzwa kwa dola,ndio iwe vitambulisho? Lakini jambo kubwa hapa ni ufisadi,kila kazi inajengewa asilimia kumi,ndio maana tumekuwa watumwa wa akili

Mwanaluguma kaka DONDA ndio hio la 10% limekuwa DONDA NDUGU sasa dawa nini?? KITAMBULISHO hiki kinatakiwa kiwe na hadhi kiasi gani? pia kiwe na data za muhusika kiasi gani? Ukumbuke tunaposafiri nje tayari tuna Paspoti ambayo pia inaweza kutumika kama ID. Waingereza wanatumia Paspoti(localy) Na hivi sasa wana mzozo mkali kuhusu hizo smart cards juu ya GHARAMA na DATA kiasi gani ziingie. Jamaa wanatuburuza na inaelekea tunaburuzika!!!!
 
.........Pengine kabla ya ku-jump kuwa Mchapaji mkuu wa serikali anaweza kufanya kazi au lah.....tujiulize hizi Billioni 222 zinatoka wapi........je ni solely Government money from its own source of income au ni Mkopo toka vyombo vya fedha vya kimataifa........

Ogah Mkuu, SWALI zuri kiasi gani, sasa nani atatujibu, MASHA? au Ofisi ya RAIS??
 
Mwanaluguma kaka DONDA ndio hio la 10% limekuwa DONDA NDUGU sasa dawa nini?? KITAMBULISHO hiki kinatakiwa kiwe na hadhi kiasi gani? pia kiwe na data za muhusika kiasi gani? Ukumbuke tunaposafiri nje tayari tuna Paspoti ambayo pia inaweza kutumika kama ID. Waingereza wanatumia Paspoti(localy) Na hivi sasa wana mzozo mkali kuhusu hizo smart cards juu ya GHARAMA na DATA kiasi gani ziingie. Jamaa wanatuburuza na inaelekea tunaburuzika!!!!

Ahsante sana Jujuman, ulichosema ni kweli kabisa. Na kuna mjadala mkali UK kuhusiana na gharama za hizo ID cards mbazo wengi wanaona ni kubwa mno. Sisi tunaburuzwa tu hivi ni kweli tunahitaji kuwa na vitambulisho hivyo? Kama tunahitaji kuwa navyo je tumefanya tathmini ya kutosha kuona tunaweza kuvitengeneza kwa gharama ipi ambayo ni ya chini mno ukilinganisha na gharama nyingine?
 
Jamaa wanatuburuza na inaelekea tunaburuzika!!!!
Nikweli jamaa wanatuburuza na tunaburuzika kikweli kweli. Issue ya National I.D imepata msukumo mpya baada ya 9/11.
Mmarekani katoa only two choices, 'either you are with us or against us'. Sisi tuko nae, tukasainishwa mkataba wa anga huria unaotoa nafasi kwa midege yao (non commercial hata za kivita)kuja kutua nchini anytime without prior notice, clearance is a must!. Eti na sisi na vindege vyetu tukatue kwao! Kama kwenda Mwanza tuu ni issue itakuwa US!. Wafaidika ni wao.

Wakatutungia Anti Terrorism Act, tukaipitisha kwa faida yao. Wakatuletea mashine za finger prints Immigration yetu, tumepokea. Tukiingia US, ni picha tena na finger prints pale airport. (Na kuna mtu aliniambia ana hamu ya unga wa Bongo na dagaa, nikajifanya mwema kumbebea!. Mbona nilijuta! Maana ni kudhalilishwa!. Kisa eti possible terrorist!)

Kupitia WB, ndio wametoa hiyo pesa ya National I.D na kulazimisha Biometric Data lazima iwemo ili kila mwenye nasaba na Osama types wamjue.
Amini usiamini, kampuni yoyote itakayoshinda ni lazima WB waiaprove na wataweka conditional precedence, 'Data Bank' ni servers za wamarekani.Miradi yote funded by WB, lazima watumie computers za Dell!. Huku ni kupeana ulaji.
Nawaambieni hiyo micro chip lazima itoke kwao na tayari italetwa ikiwa tayari formated kwa convenience yao. Tenda kama hiyo umwachie Mpiga Chapa wetu aje na tekinolojia ya bei poa ya Mchina?!. watu wale wapi?.

Umasikini wetu umefanya watushike pabaya. Tax System walitambulisha Ayscuda++ ili kila biashara iunganishwe na Electrical Tally Machine, Kodi iende moja kwa moja TRA kwa kumoniter every transaction mpaka leo hatujaweza hilo tuu, eti sasa tunakuja na smatcard ID za nini?. Kama kweli issue ni smart card, Mfuko wa Pensheni wa PSPF walianza kitambo kuzitumia na mpaka kesho wastaafu wanasota!.
Matumizi ya Teknolojia ya kisasa ni jambo zuri, swali ni jee tuna miundo mbinu ya kuitumia?.
Tuna kwa ugonjwa ka kutaka makubwa tukiwa hatuna uwezo.
Wakati wa ujenzi wa TVT iliamuliwa kuleta mitambo ya kisasa ya Digital kwa mahela kibao, kumbe Public Broadcast Tech yetu ni Analogy, imeishia kuandaa digital na kurusha analogy (labda sasa) kwenye satelite ndio digital ila ma local transmitter yote ni analogy!.
Kila benki ina ATM, hivyo kila mwenye account ana ATM card, hakuna hata super market moja ye kuswipe! Ukiondoa Tembo Card na Benki yaposta ambazo wameweka vijimashine vyao!.
Kama tumeshindwa kubridge visimple 'digital devide' vidogo-vidogo tuu vya matumizi ya kila siku, ndio itakuwa hii smart card tech!?. Hii ni Radar nyingine ya kijeshi kwa matumizi ya kiraia na Gulfstream nyingine kwa masikini sisi kila ikipaa ni mabilioni kwa kwenda mbele.
Acha tuletewe na hivyo vitambulisho vya
ki-SASA ili Watanzania tuendelee kuwa
Wa-SASA na CCM iendelee kutawala
SASA na HATA MILELE.......AMEN.
 
Sometimes its good to be serious, waheshimiwa wetu included!
...... Give me a break! I'm sorry to say but waheshimiwa hao na mpigapicha wa serikali have no clue to what they are insinuating, period!


Vidunda

Hapo umedundadunda haswaaaa ... wengine hawaelelewi issue ya ID Cards including wabunge wengi tu, wanadhani ni ku-laminate picha za watu. Kipi rahisi kuchapa Passport au ku-issue ID Cards? Si wangewapa tender ya kuchapa passports!
Actually ... inanikumbusha ya enzi ya Mwalimu walipoleta farasi toka Australia eti badala ya magari (kama miaka 30 iliyopita) mbola walikufa njaa maanake hawakuelewa kuwa farasi hawali mabua!

Well put!

ZalendoHalisi
 
Kimetolewa na Mpigachapa wa Kula Breki!!!
indumemwe.jpg
Bei karibu na bure!
 
Tatizo la mawaziri wa kikwete wamewekwa kishikaji hivyo wakichemsha hakuna wa kuwachukulia hatua.wote ni watoto wa mjini.fikiria mkulo alivyotemwa nssf kwa kashfa leo ndo waziri wa fedha,mataka na kashfa ya ppf sasa ndo mkurugenzi mkuu atc na wengine.hebu watanzania tumuulize kikwete hawa watu anawatoa wapi?
 
Leo Masha amejaribu kujitetea wakati anahojiwa na TBC1. Hata hivyo amenishangaza pale aliposema kuwa ile barua kwa PM ilikuwa kwa ajili ya kumweleza maendeleo ya uchambuzi wa tenda (Just a note to give him a sort of progress report)???? Je kwa wale walioiona hiyo barua inafanana na progress report? Pia amekanusha kukutana na Segem huko Uswiss na akasema tarehe zilizotajwa hakuwa Geneva bali aliondoka Dar 5 Oktoba 2008. Nani anasema ukweli hapa?? Yapo mengi aliyojaribu kusema lakini jingine la kushangaza ni kuwa Segem imetolewa kwa sababu ilitoa malalamiko kuhusu tenda bila kufuata utaratibu.

Kwa hiyo LM anasema hana kashfa yoyote na hawezi kujiuzulu. Hata hivyo amesema kama kuna ushahidi wa kuonesha kuwa alivunja sheria yuko tayari kuanchia mchuma.
 
Back
Top Bottom