SoC01 Watoto wasio na uzoefu wa kushika Pesa huwa na matumizi mabaya ya fedha ukubwani hasa kwa BOOM

Stories of Change - 2021 Competition

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
Elimu ya kutunza pesa wengi wetu imetushinda. Hakuna umasikini mbaya kama kujutia maisha yaliyopita, kama ungetumia pesa vizuri ungefika mbali. Hii elimu ni muhimu kuwafundisha watoto. Wakipata pesa wasihamaki.

Ni kama vike unavyokunywa chai kila siku, hata ukiwa mkubwa chai unakua umeizoea, mtoto akizoea matumizi mazuri ya pesa tangu akilwa mdogo ukubwani haitampa shida.

Wenye uwezo huanza kumpa mtoto shilingi 10,000 kwa wiki kwa matumizi ya shule ya msingi. Lakini ikifika weekend akueleze matumizi yake ya Juma zima. Hapa ukaribu na mtoto unahitajika. Mtoto asikuogope akueleze kabisa alikula mihogo ya kuchoma, chips dume nk. Muulize pia sababu ya kula vitu hivi wakati nyumbani kuna chakula.

Ukiona mrejesho wa 10,000 ni mzuri unaaweza kumpa laki moja, hapa akiwa A level, pia mhimize umuhimu wa kujiwekea akiba. Pia kama una uwezo waweke watoto wawe nadhifu. Watoto waliokuwa na mavazi duni huwa wanapata shida kupata control ya kununua mavazi.

Kuna watu wana milioni 40 bank lakini ana mashati matano na viatu pair mbili, pair nyungine ni trainers 👟. Hivi vinamtosha kabisa. Na wengine watakuambia tangu wakiwa sekondari mzee Christmas aliwapa laki moja ya shopping kila mtu na alijifunza kununua nguo za kumtosha kwa mahitaji yake.

Kuna watoto wana drop out chuo kwakua wanashika boom na hii inakua mara yake ya kwanza kumiliki pesa ndefu. Anafikiri haitaisha, matokeao yake anashindwa kumudu gharama za kujikimu.

Kila mtu anayo style yake ya maisha lakini, lakini kuna vi bibi au wamama wenye class na wana hand bags tatu nzuri. Sasa inamkuta binti ana handbags 20, hizi zote ni za nini na kila msimu una fashion yake. Ukizoea matumizi mazuri ya pesa unajifunza ku balance maisha yako vizuri.
 
Elimu ya kutunza pesa wengi wetu imetushinda. Hakuna umasikini mbaya kama kujutia maisha yaliyopita, kama ungetumia pesa vizuri ungefika mbali. Hii elimu ni muhimu kuwafundisha watoto. Wakipata pesa wasihamaki.

Ni kama vike unavyokunya chai kila siku, hata ukiwa mkubwa chai unakua umeizoea, mtoto akizoea matumizi mazuri ya pesa tangu akilwa mdogo ukubwani haitampa shida.

Wenye uwezo huanza kumpa mtoto shilingi 10,000 kwa wiki kwa matumizi ya shule ya msingi. Lakini ikifika weekend akueleze matumizi yake ya Juma zima. Hapa ukaribu na mtoto unahitajika. Mtoto asikuogope akueleze kabisa alikula mihogo ya kuchoma, chips dume nk. Muulize pia sababu ya kula vitu hivi wakati nyumbani kuna chakula.

Ukiona mrejesho wa 10,000 ni mzuri unaaweza kumpa laki moja, hapa akiwa A level, pia mhimize umuhimu wa kujiwekea akiba. Pia kama una uwezo waweke watoto wawe nadhifu. Watoto waliokuwa na mavazi duni huwa wanapata shida kupata control ya kununua mavazi.

Kuna watu wana milioni 40 bank lakini ana mashati matano na viatu pair mbili, pair nyungine ni trainers . Hivi vinamtosha kabisa. Na wengine watakuambia tangu wakiwa sekondari mzee Christmas aliwapa laki moja ya shopping kila mtu na alijifunza kununua nguo za kumtosha kwa mahitaji yake.

Kuna watoto wana drop out chuo kwakua wanashika boom na hii inakua mara yake ya kwanza kumiliki pesa ndefu. Anafikiri haitaisha, matokeao yake anashindwa kumudu gharama za kujikimu.

Kila mtu anayo style yake ya maisha lakini, lakini kuna vi bibi au wamama wenye class na wana hand bags tatu nzuri. Sasa inamkuta binti ana handbags 20, hizi zote ni za nini na kila msimu una fashion yake. Ukizoea matumizi mazuri ya pesa unajifunza ku balance maisha yako vizuri.
Hakika elimu ya kutunza na kutumia Pesa ni muhimu sana. Hongera kwa bandiko zuri!

Sent from my SM-J730F using JamiiForums mobile app
 
Kuna mkuu mmoja humu ameeleza kwamba anatumiwa 20000 kwa mwezi na haitoshi.Asome hapa na kujifunza ili ajierekebishe.
 
[mention]Sky Eclat [/mention] umeliweka vizuri sana hapo mtoto azoee unadhifu mapema lakini kuna tabia moja hivi mtu ametoka nyumbani, hajapanga kununua kitu fulani lakini huko barabarani ataona hiki anunue, aone kile anunue nadhani hua ni matatizo kuanzia ututoni
 
Unaweza kua na nguo nyingi na usiwe nadhifu, mwingine pea za viatu 30 , wakati kwa mwanaume pea tatu yaani mbili raba au simple, kimoja cha ofisini na sendo ya kuzugia tosha kabisa.
 
[mention]Sky Eclat [/mention] umeliweka vizuri sana hapo mtoto azoee unadhifu mapema lakini kuna tabia moja hivi mtu ametoka nyumbani, hajapanga kununua kitu fulani lakini huko barabarani ataona hiki anunue, aone kile anunue nadhani hua ni matatizo kuanzia ututoni
Nilkua ninasoma Financial Times, kuna kijana alianza kazi akiwa na miaka 24 anasema kwakua alikua na elimu nzuri ya kutunza pesa mshahara wake wa £25,000 kwa mwaka Aliwapa wazazi wake £300 kuchangia chakula anachokula nyumbani, alifanya shopping £500 summer na £500 winter nyingine alitumia kwa usafiri kwenda kazini.

Aliweka pesa ya kutosha akiwa na miaka 30 alimilikii nyumba mbili na zote ameweka wapangaji na zinajilipia mortgage zenyewe.
 
Kumpa mtoto pesa nyingi inaweza kuwa kama kumtia majaribuni, anaweza hata kufeli masomo yake shuleni, lakini pia, kwamba nikimpa kumi kwa wiki halafu nione ameitumia vibaya itabidi niache kumpa, na kuacha kumpa ndio tatizo lako litajirudia mtoto akiwa mkubwa, hapa sijui bora kitu gani.

Matumizi ya pesa is very complicated, wapo wanaosema itumie pesa ikuzoee, wengine wanakwambia muhimu kuweka akiba, na kusema kweli kuwa na pesa mfukoni isiyo na kazi halafu upite barabarani uone kitu kizuri usinunue ni kipaji, financial management sio mchezo, bora kutembea na kiasi kidogo mfukoni kuliko kikiwa kingi mahitaji yake huja automatically.

Hili tatizo naona lipo sana kwetu waswahili, wazungu hawana shida, utakuta mwanafunzi wa kizungu ana dream ya kupanda kilimanjaro ataweka akiba mpaka lengo lake litimie, naona hii ndio sababu wako mbele kimaendeleo compare na sisi, majority ni wazee wa kuponda raha kufa kwaja.
 
Kumpa mtoto pesa nyingi inaweza kuwa kama kumtia majaribuni, anaweza hata kufeli masomo yake shuleni, lakini pia, kwamba nikimpa kumi kwa wiki halafu nione ameitumia vibaya itabidi niache kumpa, na kuacha kumpa ndio tatizo lako litajirudia mtoto akiwa mkubwa, hapa sijui bora kitu gani.

Matumizi ya pesa is very complicated, wapo wanaosema itumie pesa ikuzoee, wengine wanakwambia muhimu kuweka akiba, na kusema kweli kuwa na pesa mfukoni isiyo na kazi halafu upite barabarani uone kitu kizuri usinunue ni kipaji, financial management sio mchezo, bora kutembea na kiasi kidogo mfukoni kuliko kikiwa kingi mahitaji yake huja automatically.

Hili tatizo naona lipo sana kwetu waswahili, wazungu hawana shida, utakuta mwanafunzi wa kizungu ana dream ya kupanda kilimanjaro ataweka akiba mpaka lengo lake litimie, naona hii ndio sababu wako mbele kimaendeleo compare na sisi, majority ni wazee wa kuponda raha kufa kwaja.
Ni hivi, unapompa 10,000 Jumamosi unamuuliza marumizi yake yalikua je, ikiwezekana akuletee balance sheet. Hii ni nayo ni elimu ya introduction to book keeping.

Katika hii balance sheet unamshauri kuwa akiweka 100 kila wiki anaweza kuwa na akiba ya kumsaidia iwapo wewe umesafiri au unaumwa. ikiwezekana unamwambia katika kila mia anayoweka na wewe utamuongezea 100.

Ukimuona ni mwamafunzi anae elewa somo, anavyokua na wewe unamuongezea vijukumu. Mfano kumpa pesa ya shopping yake ya Christmas au Idd.
 
Ni hivi, unapompa 10,000 Jumamosi unamuuliza marumizi yake yalikua je, ikiwezekana akuletee balance sheet. Hii ni nayo ni elimu ya introduction to book keeping.

Katika hii balance sheet unamshauri kuwa akiweka 100 kila wiki anaweza kuwa na akiba ya kumsaidia iwapo wewe umesafiri au unaumwa. ikiwezekana unamwambia katika kila mia anayoweka na wewe utamuongezea 100.

Ukimuona ni mwamafunzi anae elewa somo, anavyokua na wewe unamuongezea vijukumu. Mfano kumpa pesa ya shopping yake ya Christmas au Idd.


Mtoto akuletee Balance sheet??🤣---ili ajifunze accounting mapema ??
 
Umenena vema sana madam,kiukweli wengi wetu tumejifunza matumizi mabaya ya pesa tangu tukiwa utotoni.

Unakuta mtoto akipewa elfu moja na mgeni anatoka kwenda dukani,akirudi amenunua jojo za 500,biskuti na pulizo,pesa imekwisha.

Na mzazi kwakua nayeye hana wazo kua hiyo ni tabia inajijenga inabidi irekebishwe mapema,yeye anakausha tu,mwishowe mtu hata akiwa mkubwa,akipata laki tu,fasta kaingia kariakoo anarudi hana kitu,na pale anapobakiwa na elfu 10,ndo akili inmrudia.

Tujifunze na tuwafunze watoto wetu.
 
Ni kweli watu wenye pesa nyingi hawatumii sana pesa ni lazima watu waishi kwenye bajeti kulingana na vipato vyao kama kipato chako ni kidogo weka bajeti ya msosi malazi na akiba unakuta mtu bajeti ni ndogo anakopesha tena mtu ambaye hajui lini atamlipa ,anatoa misaada na sadaka tusiwe brain drained kama umepata pato kubwa toa sadaka kama umepata dogo acha dhambi na tamaa ridhika na tumi a vizuri pesa jua vitu vilivyo ndani ya uwezo wako ambavyo havipo achana navyo

Unaponunua kitu jiulize kitanipa faida au hasara ukinunua baiskeli itakusaidia kusafiri je tv na kin' gamuzi utatafuta pesa ili uziporomoshee kwenye kifurushi ili uangalie matangazo ya wafanyabiashara au movie zikupotezee mdau na umeme upotee bure

Kabla hujatumia pesa jiulize kipo kwenye bajeti yangu na kama kipo je kweli nakihitaji kitu hiki?
 
Kiukweli kabisa kabisa elimu ya fedha ni muhimu ikaingizwa hata kwenye mitaala yetu ya elimu wanafunzi wawe na msingi imara au hata basics za "financial literacy", tabia na maisha tuliyokuwa nayo kwa bahati mbaya sana hayana msingi wowote wa hili, walio na elimu hii muhimu basi wameipata kwa bahati na wachache sana walipata toka kwa wazazi, ndugu wa karibu ama waliobahatika kuwa na exposure ya mitandao kabla ya kuanza rasmi maisha.
Waajiriwa wengi wanaopata mishahara kila mwisho wa mwezi ni wahanga wa mikopo toka taasisi za kifedha na taasis bubu za mikopo (loan sharks) kwa asilimia za kutisha, takwimu zinabainisha kwamba watumishi wengi wanaisi na moja ya tatu ya mshahara wao, hii inatokana na ukosefu wa elimu hii muhimu, watu wanaishia kukpa bila kuwa na mipango thabiti ya namna ya kuutumia na nini cha kufanya na fedha hizo na wengi huishia kwenye majuto makuu na maisha kuwa magumu zaidi na zaidi bila wao kutegemea. yote hii inatokana na kukosekana kwa elimu ya fedha na namna y kuhandle matumizi, mapato na akiba.
 
Back
Top Bottom