ASANTE Sky. Kuwa last born raha sana isipokuwa pia kuna adha zake kama kutumwa tumwa hovyo. Unakula na wanaume nje kwenye kikome unaambiwa ufuate mboga ukiileta hata hujakaa jamaa wameshachukua nyama zote wamebakiza mchuzi. Unapiga tonge moja la ugali mzee mwingine anataka maji ya kunywa, kundi jingine huko limeishiwa mboga, huyu mwingine naye keshamaliza kula anataka moto wa kuwashia sigara yake inabidi uende ukamletee. Usipokuwa mjanja unaweza ukashinda na njaa. Inabidi ujanjaruke mapema na katika kujanjaruka huku ndo unajifunza maisha na heka heka zake kungali mapema.