Wanawake tujikumbushie vituko vya leba

Naonaga hainisaidiii huwa hakuna unafuu jamani
 

Nimekusoma mkuu
 
nakumbuka niliingia leba na mme wangu asa uchungu ulipokolea nikawa kama nataka kuwa chizi
yani namwambia mme wangu nasikia kama nataka kuwehuka basi akaanza maombi yani ile anaaza tu nikambinya mkono adi akatoa sauti nusu anikabe
yani niliona kama ananipigia kelele kisa maombi!
jamani uchungu unauma aisee
baadae nikamwambia kwa nguvu kibofu kinapasukaaaa dk 5 mtoto huyu
sijui kwanini eva alimshawishi adamu wale tunda jamani !popote alipo eva adhabu aongezewe yani moto ukolezwe zaidi
 
Uzi nauogopaga huu hapa nilicomment km mkimbizi as if ni rahisi vile!!
 
Hili ndo jibu lililosababisha niufufue uzi huu

Mtu anabisha eti uchungu hauleti bond kati ya mama na mtoto

Hapo kwenye mtoto akipata tatizo unahisi tumbo kuuma

Mwaka jana mwanangu mdogo alipotea kwenye michezo na wenzie akanogewa mpaka jioni narudi home mtoto hayupo tafuta mtaa mzima sikumpata kigiza kikaanza hata nguvu za kumtafuta sikuwa nazo tumbo likaanza kunitetemeka nilishaanza kupiga na ukunga majirani zangu kama wanne wakaanza kumtafuta ...

Alipatikana mida ya saa mbili na nusu na wenzie kumbe walikuwa wameenda beach kuogelea
 
WAIFU alinisimulia alivyomkojolea DOKTA...waifu kamwambia dokta mkojo umenibana,dokta akamwambia hapa huendi chooni Kojoa tukuone...WAIFU AKALIACHIA KOJO KOOOOO
 
Ni kweli lakini inataka mjasiri yaani moyo mgumu kama wa jiwe wanawake wote hatuna hiyo

Kuna mmoja alizalishwa na mtawa wakati wa uchungu ilibidi amuulize mtawa, hivi na nyie huwa mkizaa mnaumwa hivi kama mimi,,,, ukumbuke mtawa hawazai
 
Hili ndo jibu lililosababisha niufufue uzi huu

Mtu anabisha eti uchungu hauleti bond kati ya mama na mtoto
NI KWELI KABISA KABISA KABISA mwanamke aliezaa na uchungu hata malezi ya mwanae ni tofauti na ya mama aliezaa kwa kisu..Nimelishuhudia hilo kwa macho yangu mawili ya nyama.

Mke wangu mtoto wa kwanza alijifungua kwa kisu...ki ukweli mwanangu yule nilikua namhangaikia mimi kiasi kwamba hadi nikawa nahisi huyu mke wangu WALINIBADILISHIA HOSPITALI NINI mbona hamjali mtoto kabisa? Basi nikapuuzia kwakua muda mwingi waifu anakaa na mtoto nkajua anakua anachoka na yeye so haikunipa shda kumuhudumia mwanangu.

Afya ya mwanangu wa kwanza haiku vile nitakavyo,mtoto akikataaa kula mke wangu hamlazimishi kula yani anaishi na mtoto the way mtoto anavyotaka...bhas miaka ikaenda kwa shda ivyo ivyo had mtoto amekua na sasa ana afya nzuri maana anakula mwenyewe nk.

MTOTO WA PILI WAIFU KAJIFUNGUA KWA UCHUNGU

Jamani Jamani Jamani sijawahi kuona upendo na caring ile ya uzazi aliyokua nayo mke wangu kwa mtoto,ki ukweli mtoto wangu wa pili anapendwa na mke wangu hadi mi namwambiaga ukweli BABE HUYU MTOTO UNAMPENDA BWANA basi ananijibu simple "HUJUI MAUMIVU YA UCHUNGU WEWE" natamanigi nimrudishie jibu moja hilooooo Sema namstahi namwachaga.

so kusema ukweli mwanamke zaaa kwa UCHUNGU tu...najua ina uma lakini kama unataka mtoto wako umpende 100+100+100% zaa kwa uchungu...Kuzaa kwa opareshen tusidanganyane MAMA atakua na upendo lakini nasema hiviiiii upendo wa MAMA kwa mtoto wake aliemzaa kwa oparesheni Unapitwa na upendo wa BABA kwa mtoto.

nina uhakika asilimia 100000 mimi nampenda first born wangu kuliko mke wangu anavyompenda...na hii ni sababu first born alikuja kwa kisu...ila nina uhakika 100000 pia mke wangu anampenda sec born wangu kunipita hata mimi hilo nakiri kwakweli.
 
Fika leba kaka ndo utajua nini wanawake tunapitia

Mkeo ni bahati yake tu wapo wasioumwa uchungu ule mkali upo wa kawaida na upo komesha yenyewe na wa muda mrefu na kuna tofauti kati ya uchungu wa mtoto wa kike na wa kiume....wa kike nasikia unazidi wa kiume
nyie nashangaa mnalalamika uchungu mtoto mwenyewe wa kwanza,mi wife kajifungua watoto wa3 kwa mpigo yuko kawaida tu,hongera sana msambaa wangu
 
Pole sana
 
Manesi wa kike wengi roho mbaya tu, nilizalishwa na mwanaume nzao ya pili kwa huduma alonipa nakuhakikishia dunia ingeshajaa hii
Kuna watu wanapenda kesi balaa, hata ukimtazama anaweza kukushtaki. Manesi hutoa maneno ya kebehi ili uwahi kujifungua.
 
kila mtu apambane na Hali yake
mnajua maumivi kupigwa teke la mapumbu?
kutafuta kwa jasho?
 
Aisee pole tena kwa mara nyingine

Story km yangu ya first born,, huyo nesi shombo zake km nilizopewa mimi, nilisaidiwa na mfanya usafi tu, nilikuwa nimezungukwa na wakunga wanne wote wanaogopa kunigusa kwa hofu ya kuwafia mikononi mwao ndipo huyo mfanya usafi kuingia akakuta nahaha nguvu sina uchungu unapoa na mtoto hajatoka, akavaa gloves na kunibinya chini ya kifua kwa nguvu mtoto akatoka,

Alilia kidogo tu ilikuwa asubuhi alikuja kulia tena usiku saa tatu ni wazi nilimtolea padogo tu ....angekufa,,,
 
Samahani ila wengi huumia tu kwa kutojua matumizi sahihi ya midomo yao,ukijua nesi ana frastresheni zake wala hupati taabu.!utajua namna gani useme naye na kauli nzuri hulainisha moyo mgumu.
Ni jukumu lao mbona wakunga wa kiume au wa kike ambae hajazaa huwa na huruma na wanatimiza majukumu yao pasipo tatizo lolote?
 
Hospital za serikali nyingi huduma ni hizo sio huko moro tu mpaka inaonekana kama kuzaa salama ni muujiza kumbe sio
Badae nilikuja kuanza kuhisi labda ni mawakala wa mashetani, ,sio kawaida,, ingawa Morogoro Hosp hayo mambo ni kawaida sana
 
Nimecheka huku nakuona huruma sana aise, nimepara pic wife alivyoteseka kunizalia vidume vyangu viwili! Pole na hongera,
 
Yawezekana maombi ndiyo yalimleta huyo kijana aliyetoa msaada acha watu waabudu kwa imani zao kuzaa ni kujitoa uhai maana yake kifo kinakuwa karibu,,, acheni waombe
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…