Wana JF!
"HESHIMA MBELE NA MASLAHI YA WATANZANIA MBELE".
Dhahama hii wanayoipata kinamama wa Tz ni haki yao. Tukumbuke kwamba wakati ule pilikapilika za kuutafuta utawala, kamapeni kubwa ilielekezwa kwa akinamama. Kumbukeni "Nyumba kwa nyumba, chumba kwa chumba, kitanda kwa kitanda na hata shuka kwa shuka". Khanga na vitenge teletele kwa raha zao. Hatimaye wakashangilia hadi wengine tangu kuzaliwa kwetu, hatukuwahi kuyaona magego yao, lakini siku ile niliweza kuyaona hadi vidaka tonge kwa furaha waliyokuwa nayo.
Matokeo yake ndiyo haya. Acha waminyane kwenye hizo wodi nadhani ndiyo watajirudi na kutia akili.
Ni jambo ninaloliamini kwamba kama nusu ya hao kinamama watauunga mkono katika kuleta mabadiliko ya kiuongozi Tanzania, nina hakika kwamba enzi za mateso haya zingekwisha kabisa.
Kuna ndugu yangu aliwahi kuniambia kwamba "Kinamama wangekuwa si wasahaulifu wasingezaa mara mbili". Hivyo kwenye picha hizo wanaonekana wana nyuso za huzuni na simanzi lakini ngoja ifike Oktoba 2010, yote hayo watakuwa wamesha yasahau.
"MUNGU WAPE KINAMAMA WETU PUMZI YA KUTOKUSAHAU ILI ANGALAU NUSU YAO IUNGE MKONO MAPAMBANO YA KUIKOMBOA NCHI YETU KUTOKA MIKONO YA MAFISADI". AMINA!
"HESHIMA MBELE NA MASLAHI YA WATANZANIA MBELE".
Dhahama hii wanayoipata kinamama wa Tz ni haki yao. Tukumbuke kwamba wakati ule pilikapilika za kuutafuta utawala, kamapeni kubwa ilielekezwa kwa akinamama. Kumbukeni "Nyumba kwa nyumba, chumba kwa chumba, kitanda kwa kitanda na hata shuka kwa shuka". Khanga na vitenge teletele kwa raha zao. Hatimaye wakashangilia hadi wengine tangu kuzaliwa kwetu, hatukuwahi kuyaona magego yao, lakini siku ile niliweza kuyaona hadi vidaka tonge kwa furaha waliyokuwa nayo.
Matokeo yake ndiyo haya. Acha waminyane kwenye hizo wodi nadhani ndiyo watajirudi na kutia akili.
Ni jambo ninaloliamini kwamba kama nusu ya hao kinamama watauunga mkono katika kuleta mabadiliko ya kiuongozi Tanzania, nina hakika kwamba enzi za mateso haya zingekwisha kabisa.
Kuna ndugu yangu aliwahi kuniambia kwamba "Kinamama wangekuwa si wasahaulifu wasingezaa mara mbili". Hivyo kwenye picha hizo wanaonekana wana nyuso za huzuni na simanzi lakini ngoja ifike Oktoba 2010, yote hayo watakuwa wamesha yasahau.
"MUNGU WAPE KINAMAMA WETU PUMZI YA KUTOKUSAHAU ILI ANGALAU NUSU YAO IUNGE MKONO MAPAMBANO YA KUIKOMBOA NCHI YETU KUTOKA MIKONO YA MAFISADI". AMINA!