Walokole ni kundi maalum

Walokole ni kundi maalum

Eeh mkuu hata mimi naona hivyo, walokole wengi wamekuwa kama brand ya dini sio dini yenyewe. Wanaonekana kama wamechukua ukristo wa kikoloni na kuupa rangi yao, hata utasikia wanasema "Biblia imesema" lakini wakati wa kufanya maamuzi wanaongozwa na viongozi wao tu, sio Roho Mtakatifu. Na hii dark psychology nayo imeingia sana, kuna baadhi yao wanatumia "ushuhuda" kama njia ya kuwashawishi watu wapate kile wanachokihitaji, sio kwa ajili ya Mungu bali kwa ajili ya kanisa lao. Unajua kuna mahubiri yanajengwa kwa namna ya kukufanya uhisi hatia, kisha ukatoa sadaka zaidi. Hiyo ni mbinu za kisasa za kushawishi watu, sio za kidini. Lakini pia tukubali kuna walokole wazuri, walio kweli. Tatizo ni wale waliopata "umeme" wa ushindi na wanaamini wao ndio wa pekee. Hizo screenshot zinaonyesha watu wanaonekana kujitenga, kama wako katika ulimwengu wao wenyewe. Ni kama wamepoteza ubinadamu wao na kuwa roboti za kanisa.
 
Back
Top Bottom