Waliobadilisha Maisha yangu....

Waliobadilisha Maisha yangu....

Thanks sana Mamndenyi pia nawashukuru wote kwa kuwa pamoja katika maisha haya...tunajifunza mengi na namna ya kuishi!
Thanks kwa wana JF wote
Special thanks kwa Amyner sweetlady Preta Mr Rocky Kipipi Remmy BAGAH @smilling Saint Mzee wa Rula Madame B charminglady Elizabeth Dominic

Sepacial Appreciation kwa Filipo AshaDii Roulette Mamndenyi Arushaone marejesho Ruttashobolwa Baba V St. Paka Mweusi Ruhazwe JR bila kumsahau kaka yangu Judgement popote ulipo.

Best zangu Asprin Bishanga Kaizer na wake zenu cacico gfsonwin snowhite TANMO mtu chake FP na Dena Amsi

Mwisho wanachit chat wote nawakubali sana!

Erickb my son asante kwa kuniona. kwani TANMO mbona umemweka kwenye line na wake za baba zako au bado ugomvi wenu wa kufumaniana unaendelea.
 
Last edited by a moderator:
Thanx Mamdenyi i real appriciate your concern!

Mamndenyi, natoa asante nyingi kwa jf members kwa ujumla wao,
kipekee sana kwa :-

(1) jukwaa la Business & Economic Forum kitengo cha Ujasiriamali ambapo imenisaidia kuanzisha mradi wa ufugaji wa kuku wa kisasa, pia nimeweza kuanzisha mradi wangu wa kutengeneza sabuni.

(2) jukwaa la Matangazo madogo limenipa rafiki walionisaidia kupata shamba la kupanda miti huko mafinga (Love you more my sons), na kupata marafiki walionishauri namna ya kuendeleza shamba langu huko kibaha (more respect lecturer wa OUT), pia kwa kusoma postings za marafiki wengine nikapata ushawishi wa kuanzisha biashara ambayo inasonga vizuri. na mengi mengine nimepata kutoka kwenye hili jukwaa,

(3) Kupitia jf niliweza kumfahamu TBJoshua na kwa kupitia masomo yake nimepona mambo mengi sana.

(4) Ninapata shangamoto nyingi kupitia jukwaa la wakubwa japo sitoi comment.

(5) Naomba niweke haya majina mara zote nayakumbuka hata nikiwa nje ya jf

theboss, RR, Mtambuzi, AshaDii, Kongosho, Arushaone, Bishanga, Boflo, mia, @Ruhazwe (my son), Asprin, Erickb52, Katavi, zomba, charminglady, nugu mamaya, Mwanakijiji, Ruttashobolwa, BadiliTabia, gfsonwin, @Mkiruwa, Mkuu rombo, Baba V, Dena Amsi (Mjukuu), @Saint Ivuga, @Superman (Asante kwa 'like'), Cantalisia, Pdidy na wengine wengi nawapenda sana.

Nimeandika hivi ili wengi wajue kuwa jf siyo mahali pa kupoteza muda bali ni zaidi ya darasa la mafanikio.




 
Last edited by a moderator:
Nikikumbuka hiyo mutu, nakumbuka mutu inautwa Kajumba, Zee la Mecco na Rombian.

Dah... tumetoka mbali muzeya!!

Hahahaaa... Chezeiya Rombian weye? Na zee la meco? Kajumba amekuwa ''mjasiriamali'' huko kibiti!
 
Wakuu.

Kwa namna ya kipekee kabisa nimeguswa na hii thread! Ila kikubwa nimeguswa na jinsi namna baadhi yenu mmeguswa na michango yangu. Sikuwahi kulifikiri hili japo huwa naona "LIKE" zinaongezeka tu! Hahaha. Niwe mkweli, Sikuwahi kufikiri kuwa ndugu yangu na kaka yangu chama anaweza kuja kusema kuwa anaguswa na mchango wangu,(amenishtua kwa hili!) hii ni kutokana na jinsi tunavyo tofautiana ki itikadi na mitizamo kwa mara kadhaa. Asante chama kila jema na lenye kheri lisikuponyoke, nimekupata kikubwa "Upinzani si uadui".

Heshima za dhati kwa waliogusa fikra na mtazamo wangu ki-maono zimfikie Mzee Mwanakijiji na Father of All, michango yenu imenikomaza/inaendelea kunikomaza ki-mtazamo, nakuheshimu sana kaka yangu na mwalimu wangu nje ya darasa Mwita Maranya, umekuwa unatumia hata muda wako kuniandika PM, nilifurahi sana kwa mara ya kwanza kupata PM yako, nilikuheshimu kwa ushauri wako tangu siku ile! Mungu akubariki sana kaka yangu. Hekima zako zitazaa busara ya hali ya juu.

Dada zangu AshaDii, mwaJ, nivea, na TaiJike, huwa nafarijika sana kusoma michango yangu, utamu wa michango yenu nachelea kusema kuwa ndio utamu wa fikra na maono yenu pevu mliyo barikiwa na mwenyezi Mungu (hata utamu ule mwingine bila shaka). AshaDii nimekupenda sana tangu siku ile!(Sio kupenda ile nyingine)! NAKUPENDA.

Kaka Pasco nafurahi sana kusoma neema aliyo kujalia mwenyezi Mungu kutoka ubongoni na kutitirika kwenye viganja vya mikono yako! Niliumia nilipo kukosea heshima siku moja kwa kukuambia "Unafikiri kwa kutumia tumbo" lakini nilijifunza kitu kupitia majibu yako yaliyo sheheni hekima na busara. Nilikuheshimu sana tangu siku ile, nilihisi najibiwa hekima zile na Mwl Lwaitama. Mdogo wako najifunza mengi kutoka kwako.

Yericko Nyerere na Mikael P Aweda, heshima kwenu wakuu, huwa mnanikosha kwa taarifa zenu za kiintelijinsia na kuripoti matukio kwa ufanisi wa hali ya juu. Mbarikiwe sana kwa kuiwaza jf kuilisha habari na matukio mbalimbali.

Invisible heshima yako kaka mkubwa, Mungu aibariki kazi ya mikono yako.

Mkandara Ritz na zomba kila jema na lenye kheri lisiwaponyoke na Mwenyezi Mungu azidi kuwabariki kwenye yote mema na yenye kheri mnayoyafanya. Tofauti zetu kimitazamo na ki-maono ziimarishe udugu wetu na upendo miongoni mwetu.

Mungu awazidishie hekima na busara wanajamii forums wote ambao sikuwataja au hawakutajwa kugusa maisha ya wengine. Jifunzeni kitu kupitia waliotajwa, kwenye jukwaa kama hili lenye watu 1920 na zaidi kuonekana umegusa maisha ya mtu sio jambo la kitoto na rahisi kama kuuacha upepo upite au kupiga mbizi kwa kukosa nauli ya Pantoni kutoka kigamboni kwa kina Yericko Nyerere kwenda gongo la mboto kwa kina chama.

Mwenyezi Mungu amijaze hekima na busara, awapunguzie/kuwaondolea magumu katika maisha, awafungulie milango ya heri na awa epushe na shari. Mkiwa mnaitikia Ameen! Mumkumbushe na Ben Saanane kama atakuwa haitikii. Tuko pamoja sana kaka.

Kijana mwenzenu Mohamedi Mtoi
 
Last edited by a moderator:
ashadii nampenda sana jamani, mtambuzi,nyaniNgabu,smile, R.I.P Regia mtema, kyoma, mwita25,kiranga n.k
 
For two years, I followed very closely what was taking place in this blog, Jamii Forums, as a guest. On May 31st 2008, I decided to register as a member and I am glad I did. The country was going to the dogs and nobody but its true and humble citizens like us could save it.

Mchango wangu wa kwanza ulimhusu Mbunge wa Kyela Dr. Mwakyembe.
Mag3 said:
25 Juni 2008 - Inawezekena kuna waliokuwa na nia njema kabisa wakaingia CCM wakiwa na mawazo ya kuleta mabadiliko from within. Hawa mara nyingi walikuwa wanaota ndoto na immediately walipoamka wakakuta wameachwa kwenye mataa. Nakuwa very skeptical na mwana CCM yeyote anayeweza kuchukua msimamo tofauti na vigogo wenzie wa CCM na akaendelea kubaki ndani yake. Wazungu husema "you cant eat your cake and have it" kwa maana nyingine ni kwamba ama uko nasi au uko nje (either you are with us or you are out).

Mwenye nia njema na thabiti kwa mustakabhali wa nchi hawezi kubaki CCM kwa wakati huu - ni either atajitoa ama watamtosa. Je Mwakyembe yuko tayari kutoswa na kama jibu ni ndio kwa nini yeye na wanakamati wenzake hawakutoa full report kama kweli yako mengine zaidi. Naamini kuwa Dr. anajua fika kuwa wanachi wa Kyela wako nyuma yake kwa hili kufuatana na mapokezi aliyopata hapo awali. Nchi inahitaji kukombolewa na ukombozi huu hautaletwa na wanaCCM ndani ya CCM ...
Mchango wangu wa pili ulihusu tamko la Mbunge wa Same kutoka CCM, Ana Kilango.
Mag3 said:
28 Juni 2008 - Anybody who at this point in time is still a member of CCM by deed and creed can not be expected to help bring change without moving out. Anybody who up to now still believes that the leadership we now have in Tanzania can take us out this murk is in a dream and needs to wake up fast. Ana Kilango is such person and how I pity her and those that believe in her tantrums.[

Trust me CCM to its adherents is more like a religion. It is now a conglomerate of individuals that has tentacles in every sphere of influence in the political and social landscapes of Tanzania. What drives dictators (like Mugabe) the world over is what is driving CCM in and out of Tanzania. Think of the mushrooming CCM branches in places like UK and far-off countries like India. To its worshipers, CCM is first then Tanzania second full stop.

When it comes to controversial issues that affect the millions of our fellow countrymen, CCM applies what I call preemptive political strikes. People like Ana Kilango will come and wriggle their way into the minds some of us and like blind fools we will feel the elephants tail and be convinced that jumbo is just a flexile rod!! Like Shakespeare said "it's all sound and fury signifying nothing".

CCM is beyond repair and again quoting Shakespeare "even all the perfumes of Arabia cannot clean CCM's bloody hands". Anybody connected to CCM is a potential FISADI unless he/she gets out. Ana Kilango is one such person and how I wish we could be discussing something else (tears!!).
Je wana JF, nilikosea? Msimamo wangu ni huo huo hadi leo na umekuwa hivyo toka mfumo wa vyama vingi ulipoanza na CCM (kikundi cha watu wachache) ikajitwalia kwa wizi mali zote zilizokuwa za Watanzania wote (milioni thelathini)

Nilipojiunga JF niliamini humu kuna kundi la watu huru wasiofungamana na upande wowote na ambao kilichowafanya wajiunge na Jamii Forums ni ule uchungu wa kuona taifa lao linateketea. Hawa niliamini wako tayari kuungana na wazalendo wengine wenye mawazo kama hayo ndani na nje ya Jamii Forums kutafuta njia za kuinusuru Taifa kwa amani. Niliamua kuwa ni muda muafaka kwa kundi hili kuwa tayari kusimama na kuhesabiwa katika hizi harakati za ukombozi, naam kulikomboa taifa letu, Tanzania.

Nachukua fursa hii kuwapongeza wana JF wote ambao wameunga mkono juhudi hizi na kusimama kidete kutetea taifa letu tunalolipenda bila kujali itikadi zao. Kwamba nchi inateketea, ni ukweli ambao haitawezekana kuuzika hata kama tutajaribu kuufukia chini ya itikadi, dini, rangi, jinsia, wadhifa, mali na vishawishi vinavyopofusha macho, masikio na zaidi ya yote akili. Kama kawaida wapo watetezi wa status quo wanaoamini Tanzania haiwezekani bila CCM lakini baada ya miaka hii yote kuendelea kujidanganya hivyo ni upofu.

Asante JF kwa kutupanulia wigo wa mapambano, vita vilivyopo mbele yetu kama taifa ni kubwa na ngumu na si kama nilivyofikiria nilipojiunga JF...sikujua humu nitawakuta watu kama Ritz, chama, zomba na wengineo ila nawapongeza wote ambao kweli wanakerwa na tunakoelekea na wanaona umuhimu wa dereva kupumzishwa. CCM inaingia kwenye rekodi ya Guiness book kama chama kilichokaa madarakani kwa miaka mingi huku bado ikijizatiti kung'ang'ania kwa njia zozote zile iwe ufisadi, ukandamizaji na hata mauaji ikibidi.
A luta continua!
 
kuna kifaa ama mashine ilitengenezwa pale FOE ilikuwa na jina kama hili.

Ndiye mvumbuzi wa ile kitu?

For two years, I followed very closely what was taking place in this blog, Jamii Forums, as a guest. On May 31st 2008, I decided to register as a member and I am glad I did. The country was going to the dogs and nobody but its true and humble citizens like us could save it.

Mchango wangu wa kwanza ulimhusu Mbunge wa Kyela Dr. Mwakyembe.

Mchango wangu wa pili ulihusu tamko la Mbunge wa Same kutoka CCM, Ana Kilango.

Je wana JF, nilikosea? Msimamo wangu ni huo huo hadi leo na umekuwa hivyo toka mfumo wa vyama vingi ulipoanza na CCM (kikundi cha watu wachache) ikajitwalia kwa wizi mali zote zilizokuwa za Watanzania wote (milioni thelathini)

Nilipojiunga JF niliamini humu kuna kundi la watu huru wasiofungamana na upande wowote na ambao kilichowafanya wajiunge na Jamii Forums ni ule uchungu wa kuona taifa lao linateketea. Hawa niliamini wako tayari kuungana na wazalendo wengine wenye mawazo kama hayo ndani na nje ya Jamii Forums kutafuta njia za kuinusuru Taifa kwa amani. Niliamua kuwa ni muda muafaka kwa kundi hili kuwa tayari kusimama na kuhesabiwa katika hizi harakati za ukombozi, naam kulikomboa taifa letu, Tanzania.

Nachukua fursa hii kuwapongeza wana JF wote ambao wameunga mkono juhudi hizi na kusimama kidete kutetea taifa letu tunalolipenda bila kujali itikadi zao. Kwamba nchi inateketea, ni ukweli ambao haitawezekana kuuzika hata kama tutajaribu kuufukia chini ya itikadi, dini, rangi, jinsia, wadhifa, mali na vishawishi vinavyopofusha macho, masikio na zaidi ya yote akili. Kama kawaida wapo watetezi wa status quo wanaoamini Tanzania haiwezekani bila CCM lakini baada ya miaka hii yote kuendelea kujidanganya hivyo ni upofu.

Asante JF kwa kutupanulia wigo wa mapambano, vita vilivyopo mbele yetu kama taifa ni kubwa na ngumu na si kama nilivyofikiria nilipojiunga JF...sikujua humu nitawakuta watu kama Ritz, chama, zomba na wengineo ila nawapongeza wote ambao kweli wanakerwa na tunakoelekea na wanaona umuhimu wa dereva kupumzishwa. CCM inaingia kwenye rekodi ya Guiness book kama chama kilichokaa madarakani kwa miaka mingi huku bado ikijizatiti kung'ang'ania kwa njia zozote zile iwe ufisadi, ukandamizaji na hata mauaji ikibidi.
A luta continua!
 
Mimi ni YESU Kwa falsafa zake zilizotumiwa hata na wana jf kuchangia hoja kwa mtazamo wa soma neno mwombe Yesu
 
Mwanangu Mohamed Mtoi nami nimeguswa na jinsi ulivyofaidika nami. Wengi huwa wanafaidika lakini hawasemi. Nashukuru sana kwa kuliona hilo na kulisemea. Nadhani tupo hapa jamvini kujifunza, kufundisha na kusaidiana pale tunapoweza. Kwangu JF ni darasa na mahali pa kukutana kimawazo. Mungu azidi kutupa uzima na busara tuendeleze mijadala yetu.
Wabillahi tawfiq
 
Back
Top Bottom