Wachina waja na maji haya, wanaliteka soko mdogo mdogo

Wachina waja na maji haya, wanaliteka soko mdogo mdogo

ESCORT 1

JF-Expert Member
Joined
Dec 7, 2015
Posts
1,501
Reaction score
3,342
Jana nipo Kariakoo nikaagiza maji nikaletewa maji haya muuzaji akinambia yanaitwa “Mshangazi” ikabidi nicheke.

Nikaambiwa wengine wanayaita “Bonge la Dada”

Mchina kaja na maji mengi kwa bei ileile nafuu, yaani 1.8L

Wazawa wamelala, wakija kushtuka hawana chao
IMG_8960.jpeg
IMG_8961.jpeg
 
Jana nipo Kariakoo nikaagiza maji nikaletewa maji haya muuzaji akinambia yanaitwa “Mshangazi” ikabidi nicheke.

Nikaambiwa wengine wanayaita “Bonge la Dada”

Mchina kaja na maji mengi kwa bei ileile nafuu, yaani 1.8L

Wazawa wamelala, wakija kushtuka hawana chaoView attachment 3532995View attachment 3532997
Karibu mshangazi,enea hata kule kazuramimba kwani ukame kama wote.
 
Watu walidhani mgogoro na mchina utaishia kkoo tu.

Sasa hatimae wafanyabiashara wakubwa wamefikiwa.


Na hii ishu haitoishia hapo tu, ndani ya miaka 6-10 ijayo, tutakua na wachina kwenye siasa.

Vyama vyote vitakua na wagombea wachina

Waheshimiwa wabunge mjiandae vizuri, miaka 6-10 ijayo utakua jimboni unapambana na mchina, wewe unahonga yeye anajenga.

Nyie mkichaguliwa mnahamia dar, chenyewe kikichaguliwa tu,kinalowea huko huko jimboni.

Jinping anacheza draft kwa akili sana.

Trump hakukosea kusema Africa inahitaji kutawaliwa tena.
 
Back
Top Bottom