Habari hizi za wachaga kila mwaka zinajirudia kwa swaga zile zile, mara kuna foleni za magari, mara watu wengi. Hoja ya kujiuliza hivi hakuna mchaga mwenye camera au cmu yenye camera atuwekee hapa picha na afafanue ni wapi zipo hizo foleni.
Kama kweli kuna foleni kwa nini hakuna chombo cha habari hata kimoja kinachoripoti hayo matukio ie ITV, badala yake vyombo vinaripoti msongamano wa abiria kwa kutumia usafiri wa mabasi tu. Ambapo hata wenyeji wa mikoa mingine wanaface hiyo changamoto. Ingependeza kinachozungumzwa kiwekwe na picha au camera hazifanyi kazi huko nipo huku kwa muda ingawa si mwenyeji wa huku na sioni kinachosemwa hapa.