Mkuu Lokissa kiukweli hiyo mijengo kule ni mwisho!
Nikiwa DTV, alipokufa mfanyakazi mwenzetu Amina Mongi (RIP) tukatia timu Marangu!, kufuatia ugeni mkubwa kule baadhi ya Wanamarangu akiwemo Dudley Mawalla, wakatoa acess ya mijengo yao ku host waombolezaji, mimi na baadhi yetu tukapangiwa kufikia nyumbani Dudley hapo Marangu!, mjengo ni balaa!. Ni mgorofa white umepanda kama ikulu!, kila chumba self na TV ya dish kule kijijini!, ememe, maji ni ya bomba hadi hot water!, jumba lote linaishi na mlinzi tuu mwaka mzima ni krismass mpaka krismasi au ukitokea msiba au shughuli ya kumrudisha mmiliki!. Hayo mahoteli ya huko, ikiwemo Capricon, Nakara etc usipime!. Barabara ni lami safi!. Hali ya hewa AC natural!, ukiimagine kule kijijini kwetu mashishokholokubangashee!, Nyumba za udongo zilizoezekwa kwa nyasi!, umeme umepita barabarani tuu tukiangalia waya!, maji ya ya kisima rangi ya udongo!, barabara ni vumbi tupu!, unabaki unajiuliza hivi ni Tanzaniaa hii hii?!.
Pasco