Wachaga ni Noma!

Wachaga ni Noma!

Wakuu mimi si mchaga ila nimemsindikiza jana rafiki yangu huko kwao kilimanjaro.

Sasa nipo huku marangu, ilaa sasa hizi gari ninaziona huku ni balaa yan utafikiri nipo mjini dar es salaam kumbe ni kijijin marangu.

Range Rover Sports hizi za mwaka 2012 nimeshaziona kama nane hadi sa hivi, nimeona pia mikoko ya bmw x6 kwa wingi , yan kwa ufupi kuna gari za kufa mtuuuuuuu.

Big up sana wachaga mpo vizuri kwenye kutafuta dough.

Naomba Kuwasilisha

hata wenye bcycle tupo huku, tuanfukuzana na hizo range rover
 
wewe ndo wale wale, wachaga wameendelea sanaaa and it's a historical fact kwamba wakoloni wengi waliwahi kujieka kilimanjaro walipofika tanganyika wakajenga mashule na makanisa na wakaekeza kilimo huko huko so ni obvious wachaga wangekuja kuendelea tu
Kwa dhana hiyo hiyo tungetegemea kuwepo na maendeleo kama hayo ya Moshi, kule Lushoto, Njombe, Ndanda, Mgeta etc lakini ni kinyume chake!
 
Uliona gari yangu pale kilema karibu kanisani??? Rolls royce phantom.black on black
 
NI kweli Pasco
sasa wewe umefika zamani, kwa sasa barabara ile kuanzia marangu Himo hadi Mwika na ile ya Njia Panda Holili hadi Mwika na kuanzia mwika hadi Rongai sio mchezo......Anne KIlango aliikubali akasema ni ya kwanza Afrika kwa ubora
watu wameangusha majengo sio mchezo ikiwemo gorofa ndani kabisa vijijini humo hata watu wa kukaa hakuna.....ndio wachaga hao.Ukiwa na kazi au biashara lazima uangushe mjengo ili watu wajue una hela
wana ujamaa mwingine wa elimu. Mtoto lazima asome sekondary atasaidiwa na uncle,shangazi na ndugu....
Mkuu Lokissa kiukweli hiyo mijengo kule ni mwisho!
Nikiwa DTV, alipokufa mfanyakazi mwenzetu Amina Mongi (RIP) tukatia timu Marangu!, kufuatia ugeni mkubwa kule baadhi ya Wanamarangu akiwemo Dudley Mawalla, wakatoa acess ya mijengo yao ku host waombolezaji, mimi na baadhi yetu tukapangiwa kufikia nyumbani Dudley hapo Marangu!, mjengo ni balaa!. Ni mgorofa white umepanda kama ikulu!, kila chumba self na TV ya dish kule kijijini!, ememe, maji ni ya bomba hadi hot water!, jumba lote linaishi na mlinzi tuu mwaka mzima ni krismass mpaka krismasi au ukitokea msiba au shughuli ya kumrudisha mmiliki!. Hayo mahoteli ya huko, ikiwemo Capricon, Nakara etc usipime!. Barabara ni lami safi!. Hali ya hewa AC natural!, ukiimagine kule kijijini kwetu mashishokholokubangashee!, Nyumba za udongo zilizoezekwa kwa nyasi!, umeme umepita barabarani tuu tukiangalia waya!, maji ya ya kisima rangi ya udongo!, barabara ni vumbi tupu!, unabaki unajiuliza hivi ni Tanzaniaa hii hii?!.
Pasco
 
Uliona gari yangu pale kilema karibu kanisani??? Rolls royce phantom.black on black

Hahahaha mkuu umetisha sanaaa wewe itakua ni ukoo wa Mbuya, Mawalla, Temu, Moshi au Maliti..???

Halafu nasikia nyie wa'kilema wajeuriiii, mna dharauuuuu lakin wengi mmesoma sanaaaa

Jina lenyewe kilema eti nasikia limetokana na neno kilelelema maana yake walioshindikana
 
Wakuu mimi si mchaga ila nimemsindikiza jana rafiki yangu huko kwao kilimanjaro.

Sasa nipo huku marangu, ilaa sasa hizi gari ninaziona huku ni balaa yan utafikiri nipo mjini dar es salaam kumbe ni kijijin marangu.

Range Rover Sports hizi za mwaka 2012 nimeshaziona kama nane hadi sa hivi, nimeona pia mikoko ya bmw x6 kwa wingi , yan kwa ufupi kuna gari za kufa mtuuuuuuu.

Big up sana wachaga mpo vizuri kwenye kutafuta dough.

Naomba Kuwasilisha

Na tukichagua rais toka huko kila mmoja atamiliki hizo mikoko.
mpe kura lowasaa au dr slaa
 
Nyie wa kuja ndo hamjui! Sisi tunajua! Walioko huku Kilimanjaro tunajua kuwa wengi hukodisha hayo mnayoyaita ma range na nini sijui! Ngoja lipate ajali ndo utajua lake ama vipi!
embu tumia akili kijana nani anaweza kukukodishia hata corolla tu kama u dont worth corrola? embu we kama unauwezo wa corolla nenda kakodishe hiyo range 2012 tuone!
 
embu tumia akili kijana nani anaweza kukukodishia hata corolla tu kama u dont worth corrola? embu we kama unauwezo wa corolla nenda kakodishe hiyo range 2012 tuone!

hahahahaha mkuu embu mwambie huyooooi, anafikiri range rover ni kama boda boda
 
Na tukichagua rais toka huko kila mmoja atamiliki hizo mikoko.
mpe kura lowasaa au dr slaa

mbona mheshimiwa raisi anapaendeleza kwao bwagamoyo kwahyo na wenyewe wakishika me sitaona ajabu wakiwapendelea wachaga wenzao, it's human nature
 
Back
Top Bottom