Vitu vya kuzingatia unapopewa Lifti

Vitu vya kuzingatia unapopewa Lifti

Unalikuta limtu umelipa lifti halafu lisimu lake linaita mlio mkali, anachelewa kupokea na akipokea anaaza kuzungumza kwa sauti muda mrefu na mazungumzo yake ambayo kwako ni kichefuchefu hayaishi. Nashauri ukiwa mstaarabu hata ukiwa kwenye maonezi na watu simu yako ikiita nenda pembeni kabisa kamalize dharura yako ya mazungumzu kwa privace na utulivu mkuu baadaye rudi ungana na wenzako. Usiwakatishe wenzio wasikilize siri au maujinga yako inaboa
Kweli mkuu ustarabu muhimu
 
lift ilishawahi kunicost ndugu yangu sina hamu,nilipewa lift ndani ya gari walikuwa mke na mume tena wao walinikuta njiani wakasimama sasa nikawa na mvutano wa nafsi mbili moja inasema watose tu waende zao nyingine inasema jumuika nao tu kuonyesha ujamaa..!1ebwanaee kumbe ile nafsi yenye chembechembe za uungwana ikaniponza kumbe wenzangu kuna mahali wanapita kufika wakaniomba niwasubiri au nijoin nao sasa sikuona kujoin nao kama inamantiki mimi nikawaambia ntabaki kwenye gari,wakani promise hatuchelewi...!!mayowanee nilikaa kwenye gari saa zima yaani mpaka nikajiona kituko nikajuta kwanini nisngeendelea nasafari zangu ningekuwa nishafika home,walivyorudi wakani please ila nikatathimini tu kuwa hiyo pleasing ilikuwa yakunambia ukome kudandiadandia vya watu...!!😕😕😕😕😳😳
tehe tehe tehe unataka kufanana na traffic police mmoja, alisimamisha gari, bila kuuliza muhusika anaelekea wapi, yeye huyo fasta akaingia kwenye gari na ku enjoy safari, dereva kaanza kukanyagia sasa, speed za kutosha, mara mayowe yakaanza kwa traffic police, jamani unanipitiliza mbona? alipokuja kushushiwa sidhani kama aliiomba tena lift bila kumuuliza dereva anapoelekea
 
Mwenye gari hata asipochekesha wewe Cheka tuuuuuu dadeki bure inatutesaaa bora lifti ya baiskeli kwenye tifutifu mpewa lifti anapewa kazi ya kusukuma ukifika jasho mpaka kolomije huko
 
Mateso hayo yote ya nini?Si bora nijipandie zangu daladala tu niwe huru kabisa kuliko hayo mateso
 
Umenikumbusha kuna dogo tulikuwa ofisi moja na tunakaa njia moja, so asubuhi nampitia na jioni naondoka naye.

Sasa siku moja ndo nikaona karatasi yake ya bajeti ya matumizi kwenye nauli kaweka 0, na kawe lift yangu kama mbadala.
tehe tehe tehe umenichekesha kweli, eti kaweka zero, dereva wake upo, lift nzuri eti
 
tehe tehe tehe umenichekesha kweli, eti kaweka zero, dereva wake upo, lift nzuri eti

Sikumwambia ilibidi nianze kimya kimya kumpiga chini, make hata siku moja hakuwahi kutoa hata 5,000/- kuongezea mafuta.
 
Kuna siku wadada wawili walipewa lifti, gari ilipofika maeneo ya tazara kuna kitu kikakorofisha ko wakapaki pembeni na kumpigia simu fundi. Mdada mmoja akashuka eti ana haraka sana akaenda kituo cha daladala kusubiri usafiri. Huku nyuma fundi akamuelekeza mzee nini cha kufanya na gari ikawaka na safari ikaendelea. Sasa wakapita hapo kituoni bila ata haya yule mdada akalisimamisha tena gari jamani!!! Kila mtu kwenye gari alifura na kusonya.
Mi ningejifanya sijamuona vinginevyo labda awe aliomba idhini ya kutangulia kwa dharuta inayoeleweka ndio nasimama kumchukua
 
Sikumwambia ilibidi nianze kimya kimya kumpiga chini, make hata siku moja hakuwahi kutoa hata 5,000/- kuongezea mafuta.
tehe tehe tehe hajui kula na kipofu huyo, sasa hivi ataweka budget ya usafiri
 
Hiyo namba12 duuuh!! Kwani mimi nimechangia kwenye makosa yake?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom