Japo tunatambua kuwa pesa ndio inathamani kuliko kitu chochote hapa duniani, lakini pia pesa hii hii kuna maeneo mengine haipaswi itawale...
Linapokuja suala la mahusiano,sio vizuri kuipa pesa nafasi kubwa..Kuipa kipaumbele pesa ndicho chanzo cha wewe kukosa mapenzi ya kweli.Tambua wazi kuwa mahusiano yoyote yale yanayotawaliwa na pesa,mara nyingi mwisho wake ni mbaya..
Napenda niwape mfano huu ambao ni wa kweli:
"Nilikuwa na rafiki yangu ambaye alikuwa akifanya kazi katika kampuni fulani. Sio siri pesa alikuwa nayo. Alipata binti mmoja ambaye hata mazingira yenyewe ya kumpata yalikuwa ya pesa. Kwani maeneo tu ambayo walikutana ni sehemu za starehe.
Walifanikiwa kuishi pamoja na ndani ya miaka mitatu ya raha mwaka mmoja tu ndio uliovunja mapenzi yao.
Siku jamaa alipoachishwa kazi na pesa kupoteza mwelekeo, binti yule aliamua kumkimbia na kumwambia kuwa amezoea raha hivyo hawezi kuishi na mwanaume ambaye hana pesa."
Katika mfano huu mimi naamini kuwa kama jamaa angemtafuta binti yule katika mazingira ya kimasikini, sidhani kama baada ya kukosa pesa angekimbiwa.
Jaribu kufanya uchunguzi wewe mwenyewe kwa wasichana wale wote wanaonekana wapenda starehe,hawana mapenzi ya dhati.
Pedeshe akikuhonga pesa ujue atamuhonga hata mwingine hivyo hivyo. Matokeo yake ni kuambukizwa magonjwa ya zinaa.
Kama kweli unahitaji mapenzi ya kweli, usiweke pesa kama kigezo. Mapenzi sio pesa, mapenzi ni moyo wa mtu.