Kitu gani cha kawaida kujadiliwa na raia lakin serikali haipendi kuona likijadiliwa?
Mambo gani matatu ambayo serikali ya rwanda ni dhaifu kwayo?
Tabia gani mbaya ambayo wanyarwanda wamezifanya kama tamadun, kama watz walivyo machawa chawa, waongo waongo na wapenda rushwa???
Maswali magumu kama nondo wangu.
-Kuhusu kitu serikali haipendi kuona kikijadiliwa na raia na serikali haipendi, kukaa na kubweteka kwamba kuna mashirika yatatoa misaada, kwamba kisa umesoma lazima upate ajira, kwa ujumla haipendi kuona raia wakipoteza muda kwa mambo yasiyo na manufaa kwao binafsi na kwa taifa kwa ujumla.
-Mambo matatu ambapo serikali ni dhaifu:
a. Wala rushwa wakubwa wakubwa hawashughulikiwi kama wadogo,
b. Kuna kitu kinaitwa targets. Bila kujali huyu ana hali gani, michango ni lazima. Binafsi nakubaliana na serikali kuchangisha fedha hizo, lakini angalau raia wakalishwe, waelezwe kwa nini michango hiyo. Katika vita vinavyoendelea huko mashariki mwa DRC, wanyarwanda, hasa wakazi wa Rubavu(Gisenyi), ndo mashahidi wa ushuru na tozo hizo, japo lilikuwa jambo la siri. Ila, nadhani kwa sasa kila mtu anapeleka ushuru wa watu bila hata kukumbushwa, na wa kuchangia anachangia bila shurti.
c. Udhaifu mwingine naouona, ni kuhusu miundo mbinu. Hasa kama mijini, utakuta ujenzi wa barabara, wahusika hawawazii miaka hata 100 mbere, jambo linalosababisha tena kuhamisha watu mara kwa mara. Kwa kifupi niseme kama ni mipango miji.
d. Udhaifu mwingine nijiongezee wa nne, ni swala la fidia kwa raia ambao mari zao zimeharibiwa wakati wa ujenzi na utekelezaji wa miundo mbinu. Taratibu nyingine zinawaumiza raia, mpaka miaka zaidi ya 10 unakuta kuna mtu hajalipwa fidia yake.
e. Kuhusu tabia ambazo watu wamezifanya kuwa kama tamaduni, uhuru uliopitiliza unasababisha watu kujisahau. Mfano ni kama raia na vyombo vya usalama. Wananchi wapo karibu sana,tena sana na vyombo hivyo, lakini utakuta wengine wameleta dhalau za kijinga. Mambo ya uchawa, Rwanda haina. Kwa sababu bado ni nchi changa, ambayo bado inajijenga katika nyanja zote, hivyo haijafikia ile hatua ya watu kushiba na kuanza kujigamba. Pia, historia yake, hakuna anaetaka ijirudie, hivyo kila mtu yuko makini sana na maisha ya nchi. Si viongozi tu, hata raia wenyewe.