1. Rwanda ni sehemu salama kwa kila mtu, endapo hujishughulishi na mambo ya ugaidi na wizi. Rwanda, ukiibiwa kitu labda uamue kupotezea, ukilipoti kwa muda, hata miaka iwe 10, kitapatikana tu. Kikubwa uwe na vielelezo vya kujitosheleza kuwa ni mali yako halali.
Kuhusu soko la mazao, chakula kinahitajika. Kama una uwezo, soko ni la uhakika.
2. Rwanda hatuna cha muwekezaji mkubwa wala mdogo, kama wewe ni mkazi wa nchi mojawapo za jumuia ya Afrika Mashariki. Una mtaji wako, una kitambulisho chako(kwa ajiri ya TIN Number), utafanya biashara. Rwanda hakuna cha huyu haruhusiwi kufanya hiki wala kile, kwa wakazi wa EAC.
Kodi inategemea na mtaji, mauzo na aina ya biashara. Ila kodi hazikwepeki. Rwanda kwa sasa mfumo wa kielektroniki ndo umeshamili, mambo ya shortcut, ni ya kulenga kwa manati. Ila, ukitaka uishi vizuri,bila bughda, fuata taratibu. maana adhabu za kukwepa kodi, utajuta.
3. Kuhusu hili, kwa kweli sijui kivile, labda nitafute taarifa za uhakika. Ila, kyutokana na bei ya ardhi na mlivyozoea nyie, sijui kama kuna mtanzania ana mpango wa kununua ardhi Rwanda. Ila, kiwanja kama makazi tu, haina tatizo. Changamoto itakuja kwenye hati miliki. Mfumo unakubali tu ID za Rwanda, kwa watu wa nje, sijajua itakuwaje. Ila, kama ukioa au kuolewa, mwenawako anaandikishwa, na mkioana kishelia, lazima na wewe utatambulika kama mmiliki kwa asilimia 50.
Ukionyesha nia ya kukaa hawana makuu mzee.
4. Biashara hizo kubwa kubwa, labda uweze kudeal na taasisi kubwa. Maana si kama kwenu mtu anawanunulia magari demu zake 5, unanunua hili, ukilichoka unapaki unachukua lingine.
Kwanza magari ya kuanzia miaka 20 na kuendelea, ushuru wake ni mkubwa sana.
Pili, Rwanda inajaribu kupunguza umiliki wa magari, kwa sababu ya miundo mbinu. Hivyo, magari yanayohitajika, si mengi kivile. Magari mapya, gharama ni kubwa, wenye uwezo ni wachache. Mtumba, ndo hivo vikwazo ni vingi.