Uliza chochote kuhusu Rwanda

Uliza chochote kuhusu Rwanda

Acha ubwege wewe unaishia kujutana na maafisa ugavi tu hakuna unachojuwa kuhusu TPDF
Kuna jeshi gani Tanzania wakati tulikuwa na Kanali mnywarwanda kakimbia na kwa sasa mkuu wa majeshi ana ndugu wa karibu Rwanda na Congo. Tuna Jeshi gani ndugu yangu ? Unaongea pumba mpaka unasema Sativa katembea na mke wa mtu unavyozidi kuongea ndio unavyozidi kuonekana mjinga anaetetea ujinga.
 
Kwani kuwa mwana betting na kutekwa kinahusisna vp, mambo ya utekaji kwani yameanzia kwa sativa au wote waliotekwa wana vinasaba vya kutembea na wake za watekaji??? Issue yake kutekwa ilihusishwa na yeye kuwa frontline kuhusu suala la wafanyabiashara wa k/koo kugoma kufungua maduka
Hiyo ndiyo excuse yenu ya kibwege. Yeye ana biashara gani sokoni Kariakoo mpaka awe FRONT?
 
Unaandika upumbavu tu kwa vile na wewe ni Mnyarwanda. Kitu pekee anachojivunia Paul Kagame ni sympathy ya dunia dhidi ya genocide ya 1994.

Dunia inamhurumia, period. Mwakibolwa mwaka 2013 wakati wa KIKWETTE aliwasha moto na Kagame anaujua
Kwa nini Magu alilindwa na wanajeshi wa Rwanda ? Kwa nini M23 ameteka mji mwingine na dunia nzima hakuna wanachofanya ? Baada ya Rais Filipe Nyusi kuja kuomba msaada . Kwa nini JWTZ ilishindwa kwenda msumbiji na kuangamiza magaidi waliowaua watanzania huko ? Amka usingizini hatuna jeshi na Rwanda ikiamua inachukua nchi nzima.
 
Kuna jeshi gani Tanzania wakati tulikuwa na Kanali mnywarwanda kakimbia na kwa sasa mkuu wa majeshi ana ndugu wa karibu Rwanda na Congo. Tuna Jeshi gani ndugu yangu ? Unaongea pumba mpaka unasema Sativa katembea na mke wa mtu unavyozidi kuongea ndio unavyozidi kuonekana mjinga anaetetea ujinga.
Kubishana na nnyarwanda mtutsi ni kupoteza muda
 
Kubishana na nnyarwanda mtutsi ni kupoteza muda
Hamna ndugu yangu leta facts hapa kwamba tuna jeshi. Jeshi letu imegfanya nini la maana ndani ya miaka kumi iliyopita. Kama sio kusafisha miji wapinzani wakiandamana ?
 
Una chochote unachojiuliza kuhusu Rwanda?

Una chochote unachotaka kujua kiundani zaidi?

Una chochote ulichokisikia na bado umebaki njia panda!!

Iwe jambo la maana, iwe utani, iwe siasa, chochote, uliza utajibiwa hapa hapa.



Rwanda ndo nchi pekee barani Afrika, ukiingia huulizwi utakaa siku ngapi na unaenda kufanya nini. Kama unataka, funga mizigo yako hamia, kama una biashara yako, fanya, kama una ujuzi wako, omba ajira, ukipewa hakuna wa kuja kuuliza mbona huyu si mnyarwanda, kasoro serikalini tu. Ila na penyewe ikiwa una ujuzi ambao wanyarwanda hawana, kupata ajira ni simple.
Kwakuwa Rwanda ni ndogo sana ni kwanini isifanywe mkoa wa Tanzania.
 
Kubishana na nnyarwanda mtutsi ni kupoteza muda
Kwa wale mnaotetea ujinga kuwa Tanzania ina jeshi someni hapa. ,👇👇👇


Screenshot_20250320-001145.jpg


https://www.reuters.com/world/africa/m23-rebels-enter-outskirts-east-congo-town-walikale-2025-03-19/

Na hakuna wa kumfanya kitu Kagame
 

Attachments

  • 1742545061049.png
    1742545061049.png
    833.7 KB · Views: 17
Unazidi kuonyesha ujinga wako kafuatilie post za Sativa twitter kabla hajatekwa amka usingizini unatetea vitu ambavo havipo
Haya post ya mwisho ya Sativa kabla hajatekwwa hii hapa. Nipe uhusiano wake na Soko la Kariakoo

Screenshot_20250321_111931_Photos.jpg
 
Hivi wale wa Tutsi kama sio wanyarwanda waliojazana kwa wingi kuanzia ukingo wa ziwa chamchuzi, maeneo ya halmashauri ya wilaya ya kyerwa ukiwa unaelekea Kaisho, pamoja na wale walio sehemu za kihanga barabara ya kuelekea mto kagera, walio poli la nyaishozi mpaka kule mbele panaitwa kyanyamisa kuelekea pori la benako mpaka burigi mna taarifa nao sahihi kwa maana ya idadi yao na wapo nchini hapa kwa mission gani, maana sio idadi kubwa kiasi kile kuna mda unafika maeneo Yale mpaka unaingiwa na hofu kana kwamba usha visit Rwanda, hivi jinsi walivyo wengi huku kwetu ni sawa na wa bongo walio vuka huko upande wa Rwanda???

1. Haiwezekani kuwa na idadi kamili. Kwa sababu ambao walijiandikisha nchini, hao wanajulikana. Lakini pia, kumbuka;
maeneo ya mpakani lazima yawe na muingiliano, upende usipende. Hivyo, wapo walioowana na watanzania, wapo ambao ni watanzania, mnaowaita wanyarwanda.
Pia, nahisi wewe unachoongelea kuwa ni wanyarwanda, ni sura tu. Mbona hata tukisema wale mnaopenda kudai kwamba wanyarwanda wana wanawake wazuri; Tanzania si wapo warembo kuwazidi wanyarwanda?

Je, kwa misambwanda mnaongoza nadhani Afrika nzima, mwenye inyeeeee, akionekana Rwanda tumuite mtanzania?


2. Ndo maana unasikia issue za ujirani. Tanzania ingewaona wa kuhatarisha usalama wake, wasingekuwepo.
Pia, wingi wao una faida kubwa kwa Tanzania. Kwa sababu, wanapofanya shughuli zao, wanufaika wa kwanza ni watanzania.
Wasingekuwepo, hata shughuri za kimaendeleo zisingekuwepo.
Pia usisahau. Kwa wale wazinzi, akifika huko si anakwama kabisa! Je, wasingekuwepo? Visit Kyerwa na kwingineko isingekuwepo.

3. Penye ukweli mi nakuwaga mkweli, unipende kwa hilo au unichukie kwa hilo: wapo watanzania wanaopenda waishi kule, na wanafanya shughuli zao.
Lakini sasa, si kila mtu hukimbilia anapoona pana unafuu? Tanzania ina unafuu kwa wanyarwanda kuliko Rwanda ilivyo kwa Watanzania kupata unafuu wakiwa kule.
 
Haya post ya mwisho ya Sativa kabla hajatekwwa hii hapa. Nipe uhusiano wake na Soko la Kariakoo

View attachment 3278474
1742545772070.png

1742545812574.png

1742545863709.png

1742545963295.png

☝️ ☝️ ☝️ ☝️ Nimeshaleta ushahidi kuwa alikuwa anakosoa serikali ndio maana akatekwa leta ushahidi wako kuwa alikuwa anatembea na mke wa mtu. Hizi ni post za sativa kabla haajatekwa .
 
Majeshi ya Tanzania yanahusikaje sasa na hiyo taarifa ya M23 kuufikia mji wa Walikale? Wewe akili zako ziko matakoni tu
Jeshi la Tanzania linahusika kwa sababu Jeshi hilo pamoja na Jeshi la Afrika Kusini lilishindwa kupambana na M23. Hii ikapelekea Kanali wa Jeshi laTanzania kukipimbia mapigano kupitia mpaka wa Rwanda. Na cha kuongezea M23 wanaosaidiwa na Rwanda wameteka mji mwingine. Na afrika nzima nzima hakuna nchi inayotoa tamko . Namalizia kwa kukuuliza kati ya Tanzania na Rwanda nani ana jeshi ? We endelea kutukana na kutetea Ujinga.
 
Ase katika nyuzi za maan hii ni ya kwanza wacha niulize maswali kidogo ya utaftaji
1: Masoko ya mazao rwanda yapoje na usalama wa malinkwa ujumla
2: Inawezekan mfanya biashara mdogo kuekeza rwanda? Na kama ndio. Nidokezee utitiri wa makodi ni kama tz au laa
3: Je inawezekan mtanzania kumiliki eneo rwanda
4: Vip biashara ya magari ina nafasi gani katika sok la kawaida
 
Una chochote unachojiuliza kuhusu Rwanda?

Una chochote unachotaka kujua kiundani zaidi?

Una chochote ulichokisikia na bado umebaki njia panda!!

Iwe jambo la maana, iwe utani, iwe siasa, chochote, uliza utajibiwa hapa hapa.



Rwanda ndo nchi pekee barani Afrika, ukiingia huulizwi utakaa siku ngapi na unaenda kufanya nini. Kama unataka, funga mizigo yako hamia, kama una biashara yako, fanya, kama una ujuzi wako, omba ajira, ukipewa hakuna wa kuja kuuliza mbona huyu si mnyarwanda, kasoro serikalini tu. Ila na penyewe ikiwa una ujuzi ambao wanyarwanda hawana, kupata ajira ni simple.
Kuki Rwanda na Tanzaniya bahora bagirana amakimbirane kenshi? Ubusanzwe byatangiye kera, hanyuma ku ngoma ya Kikwete barasubirana, ku bwa Magufuli bikomeza kuba byiza, none kuri Perezida Samia byongeye gutangira. Utekereza ko ni iki kibitera??
 
1, vp na Rwanda kuna festival za matamasha ya kimuziki kama fiesta, ukiondoa the ben ni wasanii gani wengine wanafanya vizuri ktk industry ya music, pia lile kundi la ambassadors of Christ lilifia wapi, na pia kuna lilifuatia nalo pia halikufua dafu ama ndio wanatoa ma song yanaishia nchini mwenu humo humo,

2, Pamoja na hilo Rwanda kuna wana harakati na wakosoaji wa serikali kama akina martin, Maria serungi, Hilda na watu kama hao pamoja na hilo, vp kuhusu wasanii wanaomba harakati kama Roma, nay wa mitego na wengine kama hao nanyi mpo nao pia???
3, Bunge lenu Lina jumla ya wabunge wangapi, wote ni wa chama kimoja tawala ama kuna wa upinzani pia??
4, ligi yenu ina jumla ya team ngapi zinazoshiriki ligi, pia mna derby baina ya team mbili kubwa ama ndio mnayo moja pekee???
5, niliwahi kusikia kuwa kuna baadhi ya wizara miaka ya nyuma kidogo PL aliweka wazungu waziongoze, vp bado wanaziongoza wizara hizo ama alishawatoa??
6, unapokutana na binti wa kinyarwanda/mwenye asili ya ki Tutsi Mara nyingi response Yao huwa kama ya dharau tofauti na wanavyosemeshwa na wanaume wa mfananio wao je, kuna mapandikizi gani ya malezi kutoka kwao kwenda kwa matabaka mengine kuyadharau linapokuja suala zima la kuonyesha kuvutiwa nao, ama ndio ile dhima mlionayo kuwa wa Tutsi mliumbwa na wengine tulichongwa(hii nina evidence nayo kuna binti alinijibu hivi pale kayanga mjini 😁😁)

7, tayari mpo ktk jumuiya ya EA lakini ajabu ni kuwa Mara nyingi nikiwa mipakani huko karibu na Rwanda masaa yanabadilika, kitu ambacho huwa kinanishangaza majira ya jua ni yaleyale yaani jua likiwa linachoma bongo ni sawa na nyie tuu pia hata likiwa linazama japo kuna tofauti kidogo sana… why hamjaamua kuyarudisha masaa ya Rwanda kuendana na yale ya sie wenzenu wa EA??
Dahhh maswali marefu kama shida za wakimbizi jamani: Ila ntakujibu tu

1. Zipo. Lakini haziwezi kuwa na shamla shamla kama za kwenu, kwa sababu huko hawana hela za kuchezea kama Bongo. Ka nchi kao kadogo, na vyanzo vya mapato kwa watu wa kawaida, si vingi kama kwenu, hivyo wanakula kwa mahesabu, huku nyie mnajua yote uliyo nayo ukiitumia, kesho unapata nyingine 😉 😉 😉
Kuhusu wasanii, wapo, na wanafanya vizuri kwa lugha yao, na wanaowaelewa. Kikubwa tu mdundo. Unadhani wangapi wanaelewa anachoimba Daimondi? mdundo upo, fresh. Ambassador of Christ ipo. Ila, haiwezi kuwa na nguvu kivile, kwa sababu waanzilishi wa miaka ile, sasa hivi wengine wana majukumu ya kifamilia, makazi ya mbali mbali, uwezo tofauti tofauti, hivyo si rahisi kutamba kama miaka ile.
Hilo lingine unalolisema, lipo ni la wanachuo(Chuo kikuu cha Kigali, ULK). Na wao ndo kama hivo, walipoanza wote walikua chuo, na sasa wamemaliza, na wametengana kimaisha kutokana na majukumu. Ila wao, kuna wakati wanakutana na kutumbuiza. Wakristo wanapata raha duniani(sio ile ya Kingwendu lakini).

2. Rwanda ni nchi changa ujue! Ukiachana na jina, ujue mwaka 1994, ilianzia zero,haikuwa na kitu. Ukisikia watu wanadai kwamba wakimbizi walirudishwa kwao kwa nguvu, nahisi haikuwa na watu zaidi ya milioni 4 kipindi hicho. Wasomi wengi waliuliwa, wengine walikimbia, kila sekta ilikuwa ni kuanza upya. Mpaka wa leo, ni nchi inayopiga hatua, lakini haiwezi kufika mlipo nyie kwa kila jambo.
Hao watu sasa, ukiweka kwenye mzani, utaona hakuna jipya wanaloliongelea, mbali na kutaka kujaza matumbo yao tu. Japo pia hata hao ni watu waliopo nje ya nchi, wala siyo watu wanaojua uhalisia wa maisha ya Rwanda kwa sasa. Na ndio maana, hata vinavyojiita vyama vya upinzani, vina misingi ya chama tawala, na wanachokifanya ni kuelekeza serikali wapi wanaona mapungufu. Sasa, kwa kuwa havina uwezo wa kufanya chochote, ikiwa kuna jambo kweli haliko sawa na lina tija, bunge linajadiliana kama la Rwanda, si kama la vyama tofauti. Bajeti ya jambo furani inapitishwa,inatafutwa, na jambo linatekelezwa.
Kuhusu wasanii, kumbuka wengi ni watoto wa juzi hata yaliyotokea hawayajui, hivyo, wanajitafutia tu cha kuwaendeleza kimaisha, basi.
Watu kama kina Maria Sarungi wapo. Japo pia kama ilivyo kwake, hata wa Rwanda wapo nje. Yupo mmoja yupo Ulaya huko, yeye ana serikali yake kabisa, ila ni yale tu ya kwamba mi ni mtoto wa furani, na mimi natakiwa nipate mgao kwa nchi yangu.
Mara, zamani tulikuwa na vitu hivi na hivi, laima tuendelee kwa mfumo huo. Sasa basi, mtu akiona ni tofauti, lazima atakuwa kama hao.


3. Bunge la serikali ya Rwanda, lina Jumla ya wabunge 80. Hapana, siyo wa chama kimoja, hata wa vyama vingine wapo.

4. Hapa ndo nimepotea, mambo ya mpira kwa kweli mi ni zero brain. Nachojua kuna timu mbili(APR na Rayon Sport), zikicheza, ujinga ujinga unaofanyika ni kama wa Simba na Yanga.
Kama kuna mtu humu anaeelewa(Najua wapo sema tu hawataki wajulikane), anisaidie akupe majibu ya hili kwa mapana.

5. Hawajawahi.
Kinachokuwagepo, ni kwamba kama inaoneka nchi haina watu wenye uwezo(hasa washauli), wanaajiri watu kutoka nje.
Japo pia, baada ya kuliona hilo, serikali mpaka leo inasomesha watu katika kila idara kuondoa kesi kama hizo za ukosefu wa watendaji wazawa, maana kutumia wageni, gharama zinakuwa kubwa.
Lakini pia, wapo ambao ni raia wa Rwanda, na wenyewe bila kujali rangi ya ngozi, wanaajiliwa kama raia. Nahisi miaka ya nyuma Rwanda ilikuwa na mwanajeshi mzungu.

6. Hili lipo aina mbili: Wanyarwanda, si wazinzi kama watanzania. Ile umekutana nae kwenye gari, mkishuka mnaenda Guest, sahau. Labda Bar, na penyewe ukute ni yule anaetaka hela. Hivyo, majibu utapewa kulingana na approach yako. Nachojua mimi, ni kwamba wengi wa wanawake hao, hufanya uzinzi tu kama sehemu ya maisha, wengine, idadi ndogo, ni yale makulumbembe yaliyoshindikana(yanayojua kuna mwanaume alieumbwa kuyahudumia), hayo na yenyewe yapo.
Kuhusu kwenda kwa matabaka mengine, mifano ni mingi ya familia za kitusi,zinazooana na familia za kihutu zilizohusika na mauaji ya familia za watutsi hao. Kwa hiyo, kuhusu kuangukia kwa tabaka lako, ni asilimia ndogo sana, na yenyewe hutoka kwa wazazi wao kuliko inavyoweza kuwa kwa watoto wao wenyewe. Kuhusu huyo wa Kayanga, pole kwa kuyatimba.
Mwanamke wa kinyarwanda,japo wengine mnawaita wanyarwanda kisa maumbile na sura zao, pengine ni wenu. Kama anajielewa, kumpata utasumbuka sana. Hata kwa kumdinya tu. Wengine bado wana heshima ya familia(malezi), wengine wanaridhika na maisha yao, sio yale madude yanayolilia Iphone huku kwao hata choo hawana. Hawaigizi, wanaishi maisha yao halisi.

Labda umpate anaejiuza, hapo sawa. Japo pia, unaweza mpata anaejiuza na akawa mstaarabu.

7. Hili swali, naomba urudi shule ukasome. kwa kaujuzi kidogo niliko nako, kupishana masaa kwa nchi, kunatokana na mistari wakoloni waliyochora, ambayo wengi hujua kwama GMT. Mfano hai, nchi ya Russia, najua inapishana masaa 11. Hivyo, kuna sehemu Russia huko, wakati jua linachomoza,wengine wanajiandaa kulala.

Congo, jirani, ina masaa matatu . Kama Goma ni saa tatu, Basi Kinshasa utakuta ni saa moja. Hivyo basi, wazo lako, haliwezekani kutokana na majira tunayotumia ni hayo ya wakoloni, na EAC ni jumuia sio nchi. So, ukiiweka pamoja, bado itakuwa na majira tofauti.
 
Kuki Rwanda na Tanzaniya bahora bagirana amakimbirane kenshi? Ubusanzwe byatangiye kera, hanyuma ku ngoma ya Kikwete barasubirana, ku bwa Magufuli bikomeza kuba byiza, none kuri Perezida Samia byongeye gutangira. Utekereza ko ni iki kibitera??
Ukitaka nikujibu kwa Kinyarwanda, ntaipeleka jukwaa la Rwanda nikujibu huko huko.
Ila kwa hapa, lugha ya jukwaa hili ni kiswahili.


Umeuliza kwa nini Rwanda na Tanzania wanakwazana mara kwa mara. Ukasema yameanza zamani. Kwa Kikwete walikuwa sawa, na kwa Magufuli, na kwa Samia. Umeuliza nini chanzo?

Ntajibu mimi kama mimi, sitojibu kama mtu wa siasa:

1. Nchi za kiAfrika, ndo maana unaona wazungu wanacheza na akili zetu, umoja hakuna, urafiki wa maana hakuna, ni biashara tuuuuu. Wata wanakaa kwa ajili ya mikataba, ambayo inahusisha nchi, mwisho wa siku wanageukana. Mi napinga hili jambo. Wangekuwepo kwa masrahi ya wananchi, matatizo haya unayoyaona yasingekuwepo.

wanyarwanda na watanzania, raia wa kawaida, wakikutana watasalimiana, watasaidizana, wanaozeshana. Lakini yakija ya siasa, watahangaika raia.

Japo, nachokipenda kwa Rwanda, mpaka leo hii, nchi zote Tanzania, Uganda, Burundi na DRC, wakiwa na hali zao za kuvutana, raia wa hizi nchi wakiwa Rwanda wana usalama wa 150%. Kwa hiyo, tatizo la Rwanda na Tanzania, pia na chi nyingine, ni viongozi wenyewe wala siyo nchi
 
Ase katika nyuzi za maan hii ni ya kwanza wacha niulize maswali kidogo ya utaftaji
1: Masoko ya mazao rwanda yapoje na usalama wa malinkwa ujumla
2: Inawezekan mfanya biashara mdogo kuekeza rwanda? Na kama ndio. Nidokezee utitiri wa makodi ni kama tz au laa
3: Je inawezekan mtanzania kumiliki eneo rwanda
4: Vip biashara ya magari ina nafasi gani katika sok la kawaida
1. Rwanda ni sehemu salama kwa kila mtu, endapo hujishughulishi na mambo ya ugaidi na wizi. Rwanda, ukiibiwa kitu labda uamue kupotezea, ukilipoti kwa muda, hata miaka iwe 10, kitapatikana tu. Kikubwa uwe na vielelezo vya kujitosheleza kuwa ni mali yako halali.
Kuhusu soko la mazao, chakula kinahitajika. Kama una uwezo, soko ni la uhakika.


2. Rwanda hatuna cha muwekezaji mkubwa wala mdogo, kama wewe ni mkazi wa nchi mojawapo za jumuia ya Afrika Mashariki. Una mtaji wako, una kitambulisho chako(kwa ajiri ya TIN Number), utafanya biashara. Rwanda hakuna cha huyu haruhusiwi kufanya hiki wala kile, kwa wakazi wa EAC.
Kodi inategemea na mtaji, mauzo na aina ya biashara. Ila kodi hazikwepeki. Rwanda kwa sasa mfumo wa kielektroniki ndo umeshamili, mambo ya shortcut, ni ya kulenga kwa manati. Ila, ukitaka uishi vizuri,bila bughda, fuata taratibu. maana adhabu za kukwepa kodi, utajuta.

3. Kuhusu hili, kwa kweli sijui kivile, labda nitafute taarifa za uhakika. Ila, kyutokana na bei ya ardhi na mlivyozoea nyie, sijui kama kuna mtanzania ana mpango wa kununua ardhi Rwanda. Ila, kiwanja kama makazi tu, haina tatizo. Changamoto itakuja kwenye hati miliki. Mfumo unakubali tu ID za Rwanda, kwa watu wa nje, sijajua itakuwaje. Ila, kama ukioa au kuolewa, mwenawako anaandikishwa, na mkioana kishelia, lazima na wewe utatambulika kama mmiliki kwa asilimia 50.
Ukionyesha nia ya kukaa hawana makuu mzee.

4. Biashara hizo kubwa kubwa, labda uweze kudeal na taasisi kubwa. Maana si kama kwenu mtu anawanunulia magari demu zake 5, unanunua hili, ukilichoka unapaki unachukua lingine.
Kwanza magari ya kuanzia miaka 20 na kuendelea, ushuru wake ni mkubwa sana.

Pili, Rwanda inajaribu kupunguza umiliki wa magari, kwa sababu ya miundo mbinu. Hivyo, magari yanayohitajika, si mengi kivile. Magari mapya, gharama ni kubwa, wenye uwezo ni wachache. Mtumba, ndo hivo vikwazo ni vingi.
 
Back
Top Bottom