Inatibika kwa opareshein ya upasuaji nenda kamuone Daktari atakusaidia.
(Hemorrhoids)
Bawasiri ni mojawapo ya tatizo ambalo mara nyingi linapotokea humfanya mtu kuwa na aibu kuelezea au kwenda hospitali ili kupata tiba sahihi. Bawasiri au hemorrhoids husababishwa na kuvimba kwa mishipa ya damu aina ya vena katika eneo la mfereji wa haja kubwa.
Kuna aina mbili za Bawasiri:
i. Nje
Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa, na huweza kuambatana na maumivu, pamoja na kuwashwa kwa ngozi katika eneo hilo. Mara nyingine mishipa hiyo ya damu (vena) hupasuka na damu huganda na kusababisha aina kitaalamu inaitwa Thrombosed hemorrhoid.
ii. Ndani
Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa. Na huwa haimbatani na maumivu na wengi huwa hawatambui kuwa wanatatizo hili.
Aina hii imegawanyika katika mainisho yafuatayo:
Daraja I- Bawasiri kutotoka katika mahali pake pa kawaida
Daraja II- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na kurudi yenyewe baada ya tukio hilo.
Daraja III- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na mtu kuweza kuirudisha mwenyewe baada ya tukio hilo.
Daraja IV- Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa na vigumu mtu kuirudisha baada ya tukio hilo.
Je bawasiri husababishwa na nini?
Bawasiri husababishwa na;
Tatizo sugu la kuharisha
Kupata kinyesi kigumu
Ujauzito
Uzito kupita kiasi (obesity)
Ngono ya njia ya haja kubwa (anal sex)
Kwa ujumla mambo yanayo ongeza shiniko katika tumbo.
Umri mkubwa
Dalili za bawasiri;
Damu kuchanganyika na kinyesi wakati wa kujisaidia (hematochezia)
Maumivu au usumbufu
Kinyesi kuvuja
Kijiuvimbe katika eneo la tundu la haja kubwa
Ngozi kuwasha katika eneo la tundu la haja kubwa
Bawasiri kutoka wakati wa haja kubwa
Matatizo yanayoweza kutokana na Bawasiri:
Upungufu wa damu mwilini (Anemia)
Strangulated hemorrhoids
Vipimo na uchunguzi:
i. Digital rectal examination
ii. Proctoscope
iii. Sigmoidoscope
Matibabu :
Matibabu hutegemea na hali na aina ya Bawasiri
i. Rubber band ligation- Hapa mishipa hufungwa na rubber band ili kuzuia damu kwenda kwenye eneo liloathirika, na hutumika kwenye aina ya ndani ya bawasiri.
ii. Sclerotherapy- Hapa kemikali huwekwa kwa njia ya sindano
iii. Coagulation (infrared, laser and bipolar)
iv. Upasuaji;
-Hemorrhoidectomy
-Stapled hemorrhoidopexy
Jinsi ya kuzuia Bawasiri:
High fibre diet, kula mboga za majani, matunda, na nafaka kwa wingi.
Kunywa maji mengi kwa siku (glasi sita had nane kwa siku)
Punguza kukaa kwa muda mrefu sana hasa ukiwa chooni, kwa sababu unaweza kuongeza shinikizo katika mfereji wa haja kubwa.
Chanzo :Bawasiri (Hemorrhoids) TanzMED(old) - Afya Kwa Wote
Sema tu hapa, hayo matatizo yanawkuta wengi. wote waku PM?Kama utaweza ni PM.
jaman mi nasumbuliwa na taatizo la kutoka vinyama kny mk.. Wakati wa kujisaidia.. Alaafu baada ya hapo vinarudi ndan.. Huu ugonjwa kitaalam unaitwa internal hemmoroids.. Toka nimeanzaa kuugua ni mwez wa 6 sasa.. dawa za hosipitali {anusol} nimetumia lakini ugonjwa unapungua tu kidogo na kurudi tena.. Ni dawa gani nitumie jaman???? Maana nimeckiia huu ugonjwa ukikaa nao sana bdae unapata kansa.. Msaada please!!!!!? Natanguliza shukrani
Pole saana! Acha matabibu wakuje wakusaidie!
Pole sana mkuu...ngoja wataalamu waje watakushauri vyema.
Nimeshindwa kuelewa tatizo lako kama ni ''NDONDA AU MAKILA''. Watakapokuja wanaojua lugha hii na kuniambia tatizo lako kama ni mojawapo ya hayo mawili then nitakupatia ushauri wa tiba.
Mhhhhhhhhhhhhhh! We ni wa jinsia gani? Pole sana ndugu.
hilo tatizo kiswahili linajulikana kama mgolo...nenda temeke kuna dispensary panaitw kwa Dr MPENDA...kuna jamaa yangu aliwahi kuponywa pale..thanx