JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,267
- 5,367
Baadhi ya watu watabia ya kuongea na simu na wapendwa wao kwa muda mrefu. Licha ya kupata maumivu ya masikio, kichwa na matatizo ya macho, wataalamu pia wamebainisha madhara makubwa yanayoweza kutokea kupitia simu yako ya mkononi.
Shinikizo la damu
Ripoti iliyotolewa na watafiti kutoka Nchini Italia inasema baada ya kuchunguza wagonjwa 94 wenye shinikizo la juu la damu, waligundua kuongea kupitia simu ya mkononi kunaweza kuongeza shinikizo la damu.
Kwenye jaribio la kutafuta uhusiano kati ya simu ya mkononi na shinikizo la damu, watafiti waliwafanyia majaribio wagonjwa wenye shinikizo la damu na matokeo ya jaribio hilo yalionesha wagonjwa hao wanapoongea kupitia simu za mkononi, shinikizo la damu lao huwa juu kuliko wakati ambao hawaongei kupitia simu za mkononi.
Hivyo, watafiti wameshauri watu wenye shinikizo la damu la juu wanapopimwa shinikizo hilo, wasitumie simu za mkononi, ili kuhakikisha usahihi wa matokeo ya upimaji.
Bawasiri
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Daktari Bingwa, Sarah Jarvis kutoka Uingereza, umeonesha watu wengi wanaoingia na simu chooni na kuanza kuzitumia wamepatwa na Bawasiri
Bawasiri ni kuvimba kwa mishipa ya damu iliyopo ndani ya au katika eneo linalozunguka njia ya haja kubwa. Ni hali ambayo inaweza kusababisha nyama kujitokeza nje. Hivyo Bawasiri inaweza kuwa bawasiri ya ndani au bawasiri ya nje.
Daktari huyo amesema kuwa kitaalamu, chooni unatakiwa ujisaidie ndani ya dakika 5 na watu wengi wanaoingia na simu vyooni hutumia zaidi ya dakika 5 kujisaidia.
Sarah amesema kitendo cha kukaa muda mrefu ukiwa unajisaidia haja kubwa husaidia bakteria kuzaliana na kuingia mwilini kwa urahisi.
Kwenye tafiti hiyo, Sarah amesema kati ya watu 500 wanaotumia vyoo vya kukaa, alikuta 10 wamepatwa na Bawasiri na walikiri kutumia simu wanapokuwa maliwatoni.
Shinikizo la damu
Ripoti iliyotolewa na watafiti kutoka Nchini Italia inasema baada ya kuchunguza wagonjwa 94 wenye shinikizo la juu la damu, waligundua kuongea kupitia simu ya mkononi kunaweza kuongeza shinikizo la damu.
Kwenye jaribio la kutafuta uhusiano kati ya simu ya mkononi na shinikizo la damu, watafiti waliwafanyia majaribio wagonjwa wenye shinikizo la damu na matokeo ya jaribio hilo yalionesha wagonjwa hao wanapoongea kupitia simu za mkononi, shinikizo la damu lao huwa juu kuliko wakati ambao hawaongei kupitia simu za mkononi.
Hivyo, watafiti wameshauri watu wenye shinikizo la damu la juu wanapopimwa shinikizo hilo, wasitumie simu za mkononi, ili kuhakikisha usahihi wa matokeo ya upimaji.
Bawasiri
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Daktari Bingwa, Sarah Jarvis kutoka Uingereza, umeonesha watu wengi wanaoingia na simu chooni na kuanza kuzitumia wamepatwa na Bawasiri
Bawasiri ni kuvimba kwa mishipa ya damu iliyopo ndani ya au katika eneo linalozunguka njia ya haja kubwa. Ni hali ambayo inaweza kusababisha nyama kujitokeza nje. Hivyo Bawasiri inaweza kuwa bawasiri ya ndani au bawasiri ya nje.
Daktari huyo amesema kuwa kitaalamu, chooni unatakiwa ujisaidie ndani ya dakika 5 na watu wengi wanaoingia na simu vyooni hutumia zaidi ya dakika 5 kujisaidia.
Sarah amesema kitendo cha kukaa muda mrefu ukiwa unajisaidia haja kubwa husaidia bakteria kuzaliana na kuingia mwilini kwa urahisi.
Kwenye tafiti hiyo, Sarah amesema kati ya watu 500 wanaotumia vyoo vya kukaa, alikuta 10 wamepatwa na Bawasiri na walikiri kutumia simu wanapokuwa maliwatoni.