EZZ CHEZZ
JF-Expert Member
- Apr 10, 2011
- 1,230
- 1,352
Kutotoa 3 kati ya 12, na vifaranga kufa ni uamuzi tu wa mfugaji. Mimi nilipoamua kuzifuta hizo changamoto zilifutika. Kuku wangu nawawekeaga mayai 15 na ni wachache sana ambao hubakiza mayai 3. Sehemu kubwa huangua yote au kubakiza moja.Mkuu hii sishauri mtu aifuate maana ataumia sana kama anategenea kuku haohao, binafsi nilitenga laki 4 nikanunua kuku wa miezi 2 kwa shs 3500 kijijini walikuwa kama 23 hivi, nikajipanga chakula kizuri plus,chanjo zote maana banda lilikuwepo.
kuku walikufa wengine kwamagonjwa ambayo umewapa chanjo wakabaki 15 hivi ndo walivuka salama wakawa wakubwa wote tetea nikanunua jogoo 1 kwa 15.
hapo kuna vifaranga kufa kutokana na sababu fulani kuna kuku kutolalia vizuri unakuta mayai 12 anatotoa 3.....sema naahukuru kipato ninacho so nawahudumia ila sijapata profit yoyote zaidi ya nyama tu.
Kutotoa wanatotoa ila kunachangamoto sana kuvivusha vifaranga kwenda kwenye stage ya 2.
Kulea vifaranga ni kuhusu chakula, vitamin, na chanjo. Mimi huwapa broiler starter kwa mwezi mzima wa kwanza, vitamin na amplolium. Vitamin ninayotumia ni lazima iwe na O.T.C ndani yake. Vifo hutokea kwa vifaranga waliozaliwa dhaifu au walemavu pekee.