emmanepoultryfarm
Member
- Aug 8, 2015
- 21
- 8
Naam pana amani hapa, namalizia ujenzi wa banda la kuku, nataka niweke kuku 2500 wa kienyeji, nimeendelea kujifunza hapa, nimefurahi sana. mambo ya soko naaminii yapo tu, ni wewe mwenyewe kujifanyia marketing kama vile unavyotongoza!!!
Naanzisha na bustani mbali mbali za mboga na matunda,, nitakuja kuwapa feedback MUNGU akipenda.
Hongera,nakushauri uanze kidogo,kama unajifunza,anza na angalau vifaranga 50 hadi 100,hapo unajifunza vingi sana,hasa kwa sababu umri wa vifaranga ndo umri wenye changamoto nyingi sana katika ufugaji,cha ziada,wachunguze kuku wako Mara kwa mara,ishara ya kwanza ya kukua mgonjwa ni kuzubaa,ukiona kuku amezubaa usipuuze,anza Mara moja kuchunguza tatizo,kila la kheri.