Mpendwa msomaji wetu, yawezekana umekuwa ukiwaza sana nini ufanye ili uweze kufanikiwa na kuondokana na adha za umaskini. Kulalamika tu vyuma vimekaza haitakusaidia kitu kama hutaki kujiongeza ili uongeze kipato chako.

Yako mambo mengi ya kufanya ili kujikwamua kiuchumi. Usitegemee mshahara wako tu. Mimi nataka kukufungua macho kwa jambo moja tu tena kwa uchache. Jambo hili anaweza kulifanya mwenye mtaji mkubwa au mdogo.

Somo ni dogo tu lakini naamini wapo watakaopata mafanikio makubwa sana.
Unaweza kuanza kwa mtaji wa Mil.1 mpaka laki tano au hata chini ya hapo.

Mfano. Unaweza kutumia Tsh 250,000 kununua kuku 25 kwa bei ya Tsh 10,000 kwa kuku mmoja (kadirio la juu) Majogoo watakuwa 5 kwa uwiano wa 1:4.

Hii ina maana kuwa wakishaanza kutaga utakuwa na vifaranga 20 x 10 = 200 Watunze vizuri. Wale vifaranga tunakadiria kuwa majike watakuwa 150 ambao ndani ya miezi 3 au zaidi nao wataanza kutaga.

Utakuwa na kuku 200 + 25( ulioanza nao) =225 ndani ya miezi 6. Miezi 6 inayofuata 225 - (majogoo 55) = 170 Hii ina maana kuwa 170 x 10= 1,700.

Ndugu msomaji, hayo niliyotoa ni makadirio ya chini sana hivyo mpaka mwisho wa mwaka utakuwa na kuku zaidi ya 2000.

Mwaka utakaofuata utakuwa na kuku wangapi baada ya kuuza kuku baadhi ili upate fedha ya kuwalisha ????

Ukiuza kuku 1000, utabaki na kuku 1000, kati yao tuseme majike ni 750. Ndani ya Miaka 2 maanake ni 750(majike) x 10 = kuku 7500 (uza wengine upate pesa ya kutumia kuwalisha) .

Tuseme sasa utabakiwa na kuku jike 3000 x 10( jike moja ni mayai 10) = kuku 30,000.

Hao kuku 30,000 ukiwauza wote utapata; 30,000x 13000( bei ya kawaida kbsa)= 390,000,000. Je, bado utakuwa masikini? Bado vyuma vitakuwa vimekaza?

Nina uhakika, mpaka mwisho wa mwaka huo wa pili utakuwa umefanikiwa sana kuukimbia UMASIKINI.

Kwenye hayo mamilioni, hata ukitoa milioni 100 kwamba tuseme ndo zimetuka kuendeshea mradi wako, bado utakuwa ni milionea tu. Kumbuka huu ni mwongozo tu, fanya utafiti na ufuatilie zaidi.

NB: Ukiyapata hayo mamilioni ya pesa, kumbuka kutoa Zaka, sadaka na kusaidia masikini wasiojiweza ili ubarikiwe zaidi
kwenye nyumba za kupanga inawezekana!? huo muda wa hiyo project unahitaji expence kiasi gani mpaka kuvuna!!? #umeeleweka ila haya mengine ni mawazo yangu tu
 
Mifugo kingine labda lakini kuku ni mtihani
Kuna jamaa aliniuzia dawa na kuku zangu zikawa zinakufa tu kumbe ni dawa fake
Sitaki hata kusikia ufugaji huko nimekoma

Na serikali imetulia tu
Serikali haijatulia mkuu kazi yao wao kusumbua tu wafugaji nimerudi home kutoka site nakuta barua ya wito kutoka ofisi ya mtendaji wa kata eti kosa nafuga kuku bila kibali na mbolea inanuka. Kila siku Rais anasema tufanye kazi tukijiongeza kidogo kwenye uzalishaji hao wanaibuka tunataka kibali, mbolea inanuka.
 
Huyu anaota ndoto. Kuku hawana banda, chakula cha kuanzia, hawauguwi, wanataga na kutotoa mayai yote, na vifaranga hawafi hata mmoja. Huyu ni mwandishi wa tamthilia na hajawahi kufuga kuku. Atawapoteza wengi.

Kama anataka kusaidia watu awe mkweli. Atoe mchanganuo kuanzia gharama za kibanda. Yeye ameanza na kuku 25, anazungumzia kuongezeka lakini mchanganuo huo haoneshi gharama.
Kwani hawa wanaofuga walianzaje??? sehemu nyingine unatakiwa ujiongeze sio kila kitu kutafuniwa.TABATA kuna wachina wameanzisha kilimo cha mbogamboga majirani wanaona wivu ooh kwa nini wachina wanalima mchicha wakati bonde lipo miaka yote na hakuna aliyewahi kufikiria kulima mchicha wala nini,TUJARIBU NA WAKATI HUOHUO TUJIONGEZE!!!
 
Kila mwanadamu huwa ana mawazo tena mazuri sana kichwani au kwenye makaratasi ya nini afanye ili awe tajiri amu atu asiye wa njaa njaaa - sasa challenge huja namna ya kuyahamisha hayo mawazo into reality hapo ndipo kwenye mtego mkuu....

na ndiyo maana tangu kale kuna watu maskini na matajiri...
Wale wanaothubutu na ku take risk (not calculated risk) mara nyingi huwa ndio wanafanikiwa.
 
Mpendwa msomaji wetu, yawezekana umekuwa ukiwaza sana nini ufanye ili uweze kufanikiwa na kuondokana na adha za umaskini. Kulalamika tu vyuma vimekaza haitakusaidia kitu kama hutaki kujiongeza ili uongeze kipato chako.

Yako mambo mengi ya kufanya ili kujikwamua kiuchumi. Usitegemee mshahara wako tu. Mimi nataka kukufungua macho kwa jambo moja tu tena kwa uchache. Jambo hili anaweza kulifanya mwenye mtaji mkubwa au mdogo.

Somo ni dogo tu lakini naamini wapo watakaopata mafanikio makubwa sana.
Unaweza kuanza kwa mtaji wa Mil.1 mpaka laki tano au hata chini ya hapo.

Mfano. Unaweza kutumia Tsh 250,000 kununua kuku 25 kwa bei ya Tsh 10,000 kwa kuku mmoja (kadirio la juu) Majogoo watakuwa 5 kwa uwiano wa 1:4.

Hii ina maana kuwa wakishaanza kutaga utakuwa na vifaranga 20 x 10 = 200 Watunze vizuri. Wale vifaranga tunakadiria kuwa majike watakuwa 150 ambao ndani ya miezi 3 au zaidi nao wataanza kutaga.

Utakuwa na kuku 200 + 25( ulioanza nao) =225 ndani ya miezi 6. Miezi 6 inayofuata 225 - (majogoo 55) = 170 Hii ina maana kuwa 170 x 10= 1,700.

Ndugu msomaji, hayo niliyotoa ni makadirio ya chini sana hivyo mpaka mwisho wa mwaka utakuwa na kuku zaidi ya 2000.

Mwaka utakaofuata utakuwa na kuku wangapi baada ya kuuza kuku baadhi ili upate fedha ya kuwalisha ????

Ukiuza kuku 1000, utabaki na kuku 1000, kati yao tuseme majike ni 750. Ndani ya Miaka 2 maanake ni 750(majike) x 10 = kuku 7500 (uza wengine upate pesa ya kutumia kuwalisha) .

Tuseme sasa utabakiwa na kuku jike 3000 x 10( jike moja ni mayai 10) = kuku 30,000.

Hao kuku 30,000 ukiwauza wote utapata; 30,000x 13000( bei ya kawaida kbsa)= 390,000,000. Je, bado utakuwa masikini? Bado vyuma vitakuwa vimekaza?

Nina uhakika, mpaka mwisho wa mwaka huo wa pili utakuwa umefanikiwa sana kuukimbia UMASIKINI.

Kwenye hayo mamilioni, hata ukitoa milioni 100 kwamba tuseme ndo zimetuka kuendeshea mradi wako, bado utakuwa ni milionea tu. Kumbuka huu ni mwongozo tu, fanya utafiti na ufuatilie zaidi.

NB: Ukiyapata hayo mamilioni ya pesa, kumbuka kutoa Zaka, sadaka na kusaidia masikini wasiojiweza ili ubarikiwe zaidi
Dah...Kama babu angeusoma huu Uzi alivyokuwa kijana...akaufanyia kazi....Kisha baba yangu akaendelea kumsaidia ....Mimi leo ningelipa gharama zote za kujenga stigla joji...kama msaada wangu tu kwa serikali
 
Mleta mada inaweza kuwa lengo lake ni zuri tu kuelemishana na kuleta changamoto zaki maisha... Kaelezea kile anachofaham kama kuna anaejua garama za mabanda nae aongezee kuuweka uzi huu sawa... Tusiwe watu wakukata tamaa kama unataka kufanya biashara yoyote haikosi changamoto tujifunze kukabiliana na changamoto tutazokutana nazo!!! Wapo watakao fanikiwa kwa wazo hili hili la uyu jamaa na wapo watakao feli, ukifeli angalia wapi ulikosea... Ila nimependa iyo inaleta changamoto kwa vijana mwingine hana milioni ila ata ukiwa na lakini unaweza fanya biashara ukafanikiwa na mwenye milioni akafeli... Fursa iyo kwa wapenda kufuga
 
Kuku wa kienyeji wanachukua muda mrefu kukua,na pia ugonjwa ukipita...utashangaa asubuhi wote wamenyoosha miguu.
Kama unataka uingie katika biashara ya kuku,ni bora utafute soko kwanza.Kwa mfano kama kuna soko la kuku 200 kila wiki;ni bora uingie nao mkataba,na wewe ukanunue kwa wafugaji mbalimbali au nawe uingie mikataba midogo midogo na wafugaji.
 
Serikali haijatulia mkuu kazi yao wao kusumbua tu wafugaji nimerudi home kutoka site nakuta barua ya wito kutoka ofisi ya mtendaji wa kata eti kosa nafuga kuku bila kibali na mbolea inanuka. Kila siku Rais anasema tufanye kazi tukijiongeza kidogo kwenye uzalishaji hao wanaibuka tunataka kibali, mbolea inanuka.

Pole mkuu kuna watendaji waliposikia mtajiongeza mbele kwa mbele imekuwa kero sana

Africa ni majanga kwa kweli yaani nifuge mimi halafu walete za kuleta I bet ungewapa kuku wangeondoka huku wanachekelea
 
Pole mkuu kuna watendaji waliposikia mtajiongeza mbele kwa mbele imekuwa kero sana

Africa ni majanga kwa kweli yaani nifuge mimi halafu walete za kuleta I bet ungewapa kuku wangeondoka huku wanachekelea
Asante mkuu, sikuwepo nilikua kwenye mihangaiko nimerudi ndo nimekuta barua ya wito na namba ya simu.
Nimempigia uyo afisa ananiambia niende kesho asubuhi na laki tatu za faini, nimemuuliza kosa ni nini eti sheria za manispaa zinataka niwe na kibali cha ufugaji nimemuuliza kuwa Rais alisema nikiwa na mtaji wa chini ya milioni nne na nimenunua kitambulisho nisisumbuliwe inakuaje tena? akasema we fika ofisini tuyajenge ni kama anatengeneza mazingira ya rushwa.
Tanzania ya viwanda kesho asubuhi badala niamke mapema kwenda kujenga nchi naenda kuitikia wito wa kufuga kuku bila kibali.
 
Mbona hata 1000 (buku) unatajirika? Ingia sokoni majira ya jioni au alfajiri bei ya bidhaa iko chini.

DAY1
Nunua Tikiti zima la 1000 ( buku), nenda sehemu yenye uhitaji katakata pata vipande 5. Jero isevu.

500× 5= 2500

DAY2
Nunua matikiti 2 kwa 2000 na mia tano itumie tu.

Katakata tena safari hii utakuwa na vipande 10.

500× 10 = Sh. 5000

DAY3
Nenda nunua tikiti 5.

Hapa kila tikiti 1 vipande 5 ×5 = 25
500×25 =7,500

DAY 4
Tikiti 8 kwa nikimaanisha 7500 + 500 uliyosevu DAY1 = 8000.

This time tikiti 8 utapata vipande 40
40 × 500 = 20,000

DAY 5
Tikiti 20
Utapata vipande 100

100×500= 50,000

DAY6
Tikiti 50
Utapata vipande 5 × tikiti 50= 250
Vipande 250 × 500 = 75,000

DAY 7
Nenda kachukue tikiti 75 na fungua kijiwe kingine weka kijana afanye internship.

Hapo utakuwa na vipande 375 ukiuza kwa bei yetu 500 unapata Sh. 187500/=

Wiki inayofuata kuwa constant tu kwamba

Kila siku unachukua tikiti 100 za bukubuku kwa Sh. 100,000. Ile 87,500 isevu.

Tikiti 100 kwa wastani wetu wa kila tikiti moja vipande 5 na unauza kwa 500.

Kila siku utakuwa unauza vipande 500 unapata Sh. 250,000/=.

250,000 × siku 30 (mwezi1) = 7,500,000

7,500,000 × mara miezi 12= 90,000,000

Kipato chako kwa mwaka kitakuwa Sh. 90,000,0000.

Huna mtaji wa 1000 (Buku!) Unasubiri nini kuanza.
 
Bonge la idea
Mbona hata 1000 (buku) unatajirika? Ingia sokoni majira ya jioni au alfajiri bei ya bidhaa iko chini.

DAY1
Nunua Tikiti zima la 1000 ( buku), nenda sehemu yenye uhitaji katakata pata vipande 5. Jero isevu.

500× 5= 2500

DAY2
Nunua matikiti 2 kwa 2000 na mia tano itumie tu.

Katakata tena safari hii utakuwa na vipande 10.

500× 10 = Sh. 5000

DAY3
Nenda nunua tikiti 5.

Hapa kila tikiti 1 vipande 5 ×5 = 25
500×25 =7,500

DAY 4
Tikiti 8 kwa nikimaanisha 7500 + 500 uliyosevu DAY1 = 8000.

This time tikiti 8 utapata vipande 40
40 × 500 = 20,000

DAY 5
Tikiti 20
Utapata vipande 100

100×500= 50,000

DAY6
Tikiti 50
Utapata vipande 5 × tikiti 50= 250
Vipande 250 × 500 = 75,000

DAY 7
Nenda kachukue tikiti 75 na fungua kijiwe kingine weka kijana afanye internship.

Hapo utakuwa na vipande 375 ukiuza kwa bei yetu 500 unapata Sh. 187500/=

Wiki inayofuata kuwa constant tu kwamba

Kila siku unachukua tikiti 100 za bukubuku kwa Sh. 100,000. Ile 87,500 isevu.

Tikiti 100 kwa wastani wetu wa kila tikiti moja vipande 5 na unauza kwa 500.

Kila siku utakuwa unauza vipande 500 unapata Sh. 250,000/=.

250,000 × siku 30 (mwezi1) = 7,500,000

7,500,000 × mara miezi 12= 90,000,000

Kipato chako kwa mwaka kitakuwa Sh. 90,000,0000.

Huna mtaji wa 1000 (Buku!) Unasubiri nini kuanza.
 
Hii kitu inawezekana kabisa japo kuna vitu havijaainishwa hapo ila ni suala la mpendwa msomaji kupata picha.
Binafsi nilianza Mei 2019 nikiwa na majike 8 & jogoo 1. Niliweka target kila mwezi nipate vifaranga 30+ . Mwezi julai nilipata vifaranga 27 mpaka sasa wamebaki 22. Mwezi huu nataraji kupata vifaranga 40+ pia nimeongeza majike 7 na jogoo 1 ili mradi uweze kujiendesha kwa kuuza mayai. Kufikia Desemba mwaka huu natageti kuwa na kuku 180+ ambao watatokana na vifaranga. UKWELI NI KWAMBA NIKIRUHUSU MAJIKE WOTE 15 KUHATAMIA KILA BAADA YA MIEZI MIWILI VIFARANGA 150+ WATAPATIKANA (MAYAI 12 KILA KUKU) provided una chanzo kingine kuhudumia kabla ya mradi kuanza kujiendesha.

CHANGAMOTO NINAZOZISHUHUDIA;
1. Gharama za chakula bora
2. Gharama za kuboresha miundombinu (Banda).
NB: Kuku nawafungia kwenye fence muda wote. Sijapata changamoto kubwa katika magonjwa.

Ninachojifunza;
1. Faida itapatikana haraka kama mtaji ni mkubwa 1M+ Mimi nimetumia takribani laki 5 kuanzisha ufugaji huu.
2. Uvumilivu unahitajika kuja kupata faida halisi
3. Usimamizi wa karibu ni wa lazima.

NITALETA MREJESHO DESEMBA MWAKA HUU.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom