newmzalendo

JF-Expert Member
Mar 23, 2009
1,378
550


Nimeanza ufugaji wa kuku wa kienyeji, bado sija survey soko la kuku wa kienyeji likoje.
Kama kuna mtu mwenye uzoefu na hili anishauri, pros and cons etc.

By the way, nimeanza na Jogoo mmoja, ila natarajia kuongeza kuku within a week, projections ni kuwa na kuku 1,000, hapo ndio nianze kuuza, matarajio yangu ni kuuza via interent - hapa nalenga watu wa DAR, ambao wako bize, I can do delivery maofisini within city center, na baadae kuweka vituo vya kufanya pickup wakati watu wanarudi home jioni, e.g Mwenge Junction, Morocco Petrol Station, etc. Malipo via M-Pesa, SMS banking pia na mahoteli.

Sitarajii faida ya haraka, naomba ushauri kwa wale walifanya biashara hii, au wanajua mtu wa karibu aliyeifanya.


MICHANGO YA BAADHI YA WADAU

 
Mkuu newmzalendo, ukienda kwenye thread za zamani kwenye hili jukwaa la business unaweza kupata ushauri/maoni/uzoefu ambao ulitolewa na wapendwa wanaJF.

Sorry, sina ujuzi wa kuweka link hapa moja kwa moja. Labda wengine wasaidie. Nakumbuka Pearl (kama sikosei) alikuwa ana mradi wa kuuza kuku wa kienyeji, kama alivyoeleza kwenye thread moja hapa jamvini.

Nakutakia kila la heri katika mradi wako huo.
 
Last edited by a moderator:
Hutakosa wateja tena ukitegemea ni kuku wa kienyeji,,,mie nnafanya biashara iyo ila sio Dar.

Nilianza kutafuta wafanyabiashara asa masokoni ili nipate angalizo na soko la jumla au rejareja,pia mahotelini unaweza pitia nk nk. Unajua biashara hii kweli ujue tu kujieleza na ukidhi haja ya wateja kwa uzuri,me ilinsaidia hasa ya masokoni na mnaingia mkataba kabisa.

Pia ukiwa na plani ya biashara (sijui niitaje business plan/profile??) ambayo umeiandika unaweza onyesha wateja asa big customers nk haaa si haba.

Keep it up ndugu
 
Mzalendo unachekesha eh! Hivi ulishawahi kufuga tena ? Maana watu hawaanzagi hivyo! Siku zote watu wanaanza na Majike! maana utaazima mbegu hata kwa jirani lakini wewe umeanza na jogoo!

Anyway Mwanzo mgumu sasa wewe fuga soko no kubwa sana tu. Kwa kuanzia unapeleka tu madukani watanunua. maana hayo mayai ya kienyeji yanatafutwa sana!
 

Comment yako imenifanya ni -smile
 

Hii kali kweli, mimi nilishajua jamaa ana majike tayari kumbe ana majogoo!
 

Nakushauri ufuge wa kisasa - Layers. wa kienyeji it takes time na faida si kubwa vile unavyodhani - nitafute nikupe ushauri wa bure - meanwhile angalia kazi hii hapa

Hawa wako 900, wanatoa Tray 24 kila siku kila Tray 5000- Chakula chao ni kilo 125 approx Tshs 55,000/-

Mtaji wa kuanzia unahitaji kuwa na not less than 6m before you start production. Kama unataka mchakato mzima sema nitakutumia database yangu.

 

Mkuu ushauri mzuri natumaini atauzingatia, ila nimecheka sanaaaaa
 

Duh! nimeipenda sana hii mzee. hata mimi nimevutiwa nayo please kama inawezekano send it even to me. Maana " We normally learn good from the ways of people than from people themselves". Please do it maana nipo katika mchakato huo huo, japo siko Dar.
 
Duh! nimeipenda sana hii mzee. hata mimi nimevutiwa nayo please kama inawezekano send it even to me. Maana " We normally learn good from the ways of people than from people themselves". Please do it maana nipo katika mchakato huo huo, japo siko Dar.

Cheki hiyo imeisha leo - nimefunga mahesabu yangu ya mwezi huu.
 

Attachments

  • Layers Mesh Production - May 2010.xls
    15.5 KB · Views: 4,796

Mkuu hebu tuma hiyo database. So impressed by your set up.
 
Cheki hiyo imeisha leo - nimefunga mahesabu yangu ya mwezi huu.
Asante kwa kutufungua macho, na ninashukuru kwa mchango wako.

Kuna tatizo la mahesabu kidogo. Jumla ya gharama ni 1,590,277 na siyo 1,490,277 na kufanya faida kuwa 1,702,523. Kwa kuwa unatumia Msexcel

nakushauri utumie formulas badala ya kutype figures zote:

Column ya mapato( e3)andika =b3*d3 press enter, jibu litakuja pale. Then click kwenye E3 then kwenye right hand lower corner itakuja alama ya msalaba (+), press your left side mouse usiachie na vuta kwenda chini. Fomula itakuwacopied hadi chini yaani E4 itakuwa =b4*d4 nk. Kuweka jumla mwishoni click kwenye cell unayotaka jibu liwe e34 halafu nenda juu kwenye tool bar click

∑ basi jibu la jumla ya namba hizo itakuja,kwanza itajionyesha kwa kuhighlight, au andika =sum(e3:e33) press enter. Fanya hivyo hivyo kwa upande wa gharama, utapata jibu sahihi. Na profit ni =e34-f34. Hii inapunguza makosa madogo madogo ya kimahesabu

Pili tungefurahi zaidi kama ungetueleza una kuku wangapi? na sikuelewa eggies!

Thanks again
 

Attachments

  • Elnino layers p&l for May 2010.xls
    16.5 KB · Views: 2,343

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…