Ufafanuzi na Mchanganuo Kuhusu Biashara ya Vipodozi na Urembo

Nimemuelewa sana mdau hapo juu ntatumia hii idea
ndugu tuwasiliane mimi nafanya iyo biashara kwa muda sasa.. nachanganya duka la dawa na vipodozi.. njoo tushauriane namna gani unaanza nitakupa list ya vipodozi k.koo maduka mazuri ya bidhaa OG nafahamu. na mengine tutaeleweshana mpka unasimama mwenyewee. nipo hapa 0713752709.. pia kuna makabati ma4 ya vipodozi au pharmacy ya aluminium nauza kama unahitaji uyaone. karibu
 
Naenda kafanye biashara utajifunzaga huko huko kuibiwa nako ni moja ya somo unalotakiwa kufaulu KILALAKHERI BINTI YANGU biashara ni kama ndoa Luna watu inawakubali na kuja watu wanasukumana ila wote wanandoa
 
Maswali mengi hapa ulitakiwa uwe na majibu kabla hujafanya maamuzi ya kodi na vingine

Btw wanakuja wajuzi
Acha roho ya wajumbe mkuu,
Jifunze kuwa positive kwa wengine,
Amethubutu let give her a support zaidi ya kubeza!!
 
Mkuu hayo ya wateja, na competition anayajua mwnyewe adi amefikia kuwa na wazo la kufanya iyo biashara na asifanye nyingine manake anajua fika namna ambayo atapata wateja, pongezi zake kwa kuwa na moyo wa uthubutu mana ata ukiwa na izo skills za entrepreneurship kibongo bongo bila mtaji utakufa ma materials yako kichwani...

Sis tumezoea ukipata mtaji kidgo ufanye ujasiriamali ili Ku manage na Ku maintain pesa yako ili badae ufanye kitu.. Mambo ya business plan sijui Ku calculate ma income ma nn sijui ni less applicable hapa. Otherwise umpe ushauri na sio kum criticize
 
Tusipende sana kukosoa au kuongea ili uonekane umetoa point.. Mdau kauliza ajibiwe na sio kukosolewa. Toa ushauri baada ya ushauri toa changamoto na mrekebishe alipokosea. Ujasiria mali haupo darasani ni more practical than theory. Ndio maana hao wanaofundsha hawana hata genge la nyanya...
we jamaa umeongea point kubwa sana, na zaid ya sana mtu akifikiria zaid.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tusipende sana kukosoa au kuongea ili uonekane umetoa point.. Mdau kauliza ajibiwe na sio kukosolewa. Toa ushauri baada ya ushauri toa changamoto na mrekebishe alipokosea. Ujasiria mali haupo darasani ni more practical than theory. Ndio maana hao wanaofundsha hawana hata genge la nyanya...
Eti wanaofundisha hawana hata genge la nyanya
 
Kwa kusema kweli biashara ya vipodozi inalipa vizuri tu ukiielewa vizuri na kucheza vizuri na soko lako na biashara yenyewe kwa ujumla.

1. Nikiasi gani cha mtaji kinahitajika(minimum amount of capital) = Inategemea na msuli wako. Ila minimum uwe na kama Tsh Millioni Saba Hivi (7,000,000/=) Hivi kwa maeneo ya mjini; i.e.
- Kukodi fremu = Tsh 100,000/= kwa mwezi, miezi 6 >> 600,000/=; dalali utajuana naye mwenyewe
- Kusajili TFDA = 150,000/=
- Leseni halmashauri = 80,000/=
- Kodi TRA kama Tsh 150,000/= hivi kwa mwaka, quarter 1 utalipia Tsh 37,500/=
- Kuweka mashelfu ya aluminium na vioo = 1,000,000/=
- Kabati la chini la aluminium na vioo = 400,000/=
- Vipodozi angalau vya kuanzia = 4,000,000/=
- Pesa ya kukaa standby kwa ajili ya kuongezea vipodozi watakavyokosa wateja = 1,000,000/=
- Pia uwe na akiba ya kuendelea kuishi na kuhudumia familia yako bila kudokoa pesa kutoka kwenye duka lako kwa angalau miezi 3 hivi


2.Ni vipodozi vya aina gani vyenye uhitaji mkubwa sana sokoni(consumer needs) = Soko la vipodozi mara zote ni dynamic; leo wateja wako wanatumia Rinju, baada ya miezi 6 watakuwa wanatumia kitu kingine. Pia inategemea sana na eneo utakaloweka duka lako, kuna maeneo wananunua bei na kuna maeneo wananunua brand. Ukitaka kufanikiwa hapa ngoja wakati ukiwa tayari kufungua duka basi fanya survey maduka ya wenzako wamestock nini kisha nenda kwa duka la jumla la eneo lako mwambie unataka ufungue duka la rejareja na ununue vipodozi kwake, muombe akuambie vipodozi vinavyotembea kwa wakati huo na vipodozi gani vya kuwa navyo anyway. Kwa hiyo ukiwa tayari kuingia sokoni ndo utafiti hili

3.Ni vipodozi gani vina faida kubwa sana = Vipodozi vyote vina faida kubwa sana. Faida inatokana na kasi ya kutoka kwa kipodozi husika na tofauti kati ya bei ya kununulia na kuuzia (profit margin). Kwa ushauri wangu ni bora uangalie mahitaji ya wateja wako kuliko faida. Unaweza kuweka vipodozi vyenye faida kubwa halafu vikawa havina movement kwenye location yako - utaangukia pua. Au unaweza kuweka vipodozi vya bei ya chini ambavyo wateja wako hawaviamini na wala hawavitumii.


4.Hasara ambazo unaweza pata = Hili nimekuwa nikiwafundisha sana watu wanaokuja kujifunza kwetu biashara ya vipodozi A-Z. Zipo nyingi, ila karibia zote zinaepukika. Muuzaji kukuibia, adhabu za TFDA, adhabu za TRA, adhabu za halmashauri, vipodozi kuharibika, gharama za uendeshaji kuwa kubwa kuliko faida ghafi (gross profit) na kadhalika.
List ya vipodozi vilivyoruhusiwa kuuzwa na vilivyokatazwa kuuzwa zote zinapatikana kwenye tovuti ya TFDA: www. tfda. go. tz (Toa hizo space)

5.Sehemu ya kuweka duka(Matter of location) = Location kama kawaida, wewe tu na ubavu wako; ila ukipata mtaa wenye wakazi wengi au sehemu yenye movement nzuri ya watu - hususan akina dada basi umewin. Iwe ni njia ya kwenda university, mtaa wenye biashara ambazo wateja wake wengi ni wanawake, mtaani wanakokaa hao akina mama, mjini, sokoni nk. Zingatia sheria za TFDA, kuna baadhi ya maeneo hutakiwi kuweka duka la vipodozi (mfano karibu na kituo cha mafuta) hata kama kibiashara ni strategic location (Please kabla ya kulipia fremu kaonane na TFDA, eneo lako lisije kukataliwa wakati umeshalipia)!

6.Sehemu nzuri ambayo naweza fungasha mzigo kwa bei rahisi sana( iwe nje au hata ndani ya nchi hapa mkoa wowote ule) = Kariakoo is the best (ila usipokuwa makini inawezakuwa the worst)! Siku za kwanza nenda na mwenyeji tu hadi utakapomaster, vinginevyo utanunua kwa walionunua na hivyo kupata vipodozi kwa bei mbaya na kuuza kwa bei mbaya - kumbuka akina mama ni very sensitive kwenye suala la bei kwa hiyo ukiuza bei juu hata kwa tofauti ya Tsh 500/= tu basi watapita duka lako na kwenda kununua kwa jirani yako au hata mbali sana; unaweza kuhisi umerogwa, ila 500/= mwenzako anapata vocha!
Ila kitu kimoja - changieni maduka ya jumla ya mikoani kwenu. Kwa hiyo kama haupo Dar es salaam basi usinunue kutoka Kariakoo, tafuta maduka ya jumla hukohuko mkoani kwenu.

I am done & Out!

Ukihitaji kujua zaidi ya hayo basi karibu nitakupa darasa zaidi maana kuna mambo kama 21 hivi ambayo nitakufundisha kwa wiki 1 (Kila siku nitakufundisha mambo matatu makubwa) kuhusu kuanzisha, kusimamia na kuendeleza duka lako la vipodozi (Ila utanipodha soda mbili maana ni consultancy eti :):):))

Viva JF!

AFYA ZAIDI (AZ) CONSULTANTS
0719326693 | 0743422883 | afyazaidi@gmail.com
Asante kwa maelezo yaliyoshiba vizuri mkuu
 
Naomba kushauriwa juu ya biashara ya vipodozi. Wazo langu ni kuuza mafuta ya kuondoa chunusi na makunyanzi usoni.

Naomba kufaamishwa ni mafuta gani mazuri yatayo pendwa na wateja. Nimewaza ili biashara yangu iwe ya tofauti nahitaji kupata mafuta ambayo ni mazuri na haya patikani Tanzania kwa wingi ili nisipate ushindani mkubwa kwenye soko.

Ninayo platform kubwa ya kutangaza biashara ,YouTube Facebook, Instagram nina watu walio ni follow na subscribers jumla 500k.

Naombeni ushauri na changamoto za biashara.
 
Vipodozi vipo vya aina nyingi tu, unachotakiwa kufanya ni kutafanya utafiti ili kugundua ni vipodozi vipi ambavyo vinaruhusiwa kuingia nchi na vinatoa matokeo chanya kwa mtumiaji(mteja)

Kuna vipodozi aina 933 ambavyo vimetambuliwa na kusajiliwa na mamlaka ya dawa vifaa tiba na vitendanishi (TMDA) zamani (TFDA) vya ndani na vya nje ya nchi, ambavyo havina viambato sumu aina ya hydroquinone na nyinginezo.

Vipodozi zimegawanyika katika makundi mbalimbali kama ifuatavyo;-
Krimu,losheni,nywele,jeli,pafyumu,dawa za meno,roll on, sabuni,shampoo, poda,vipodozi vya kunyolea (after shave),cleansers, na mafuta ya maji(oil).

Kila kundi katika vipondizi hapo juu lina majina yake, nitakupa mfano mdogo hapa chini;
Krimu; 4u cream, Almondo kesar, heel cream na clear tone
Losheni;Avon herbal care,elegance lotion na miss lotion.
Vipodozi vya nywele;coco vanila soft na L' oreal dark
Jeli; afro jelly,bossy jelly na far shower gels

Kifupi tu nimesemi vipo vipodozi vya aina nyingine tofauti tofauti kutoka kwa makampuni mbalimbali.

Lakini pia vipo vipodozi kutoka nje ambayo ni pendwa ila haviruhisiwi kuingia nchi kutokana na kuwa na viambato sumu, ambavyo watumuaji wengi hasa wanawake wanavipenda, vipodozi hivi vinatoka sana Congo, hivi ukijihusisha navyo vitakupa ugumu kuvipigia promo katika ukrasa wako.
 
Vipodozi vipo vya aina nyingi tu, unachotakiwa kufanya ni kutafanya utafiti ili kugundua ni vipodozi vipi ambavyo vinaruhusiwa kuingia nchi na vinatoa matokeo chanya kwa mtumiaji(mteja)

Kuna vipodozi aina 933 ambavyo vimetambuliwa na kusajiliwa na mamlaka ya dawa vifaa tiba na vitendanishi (TMDA) zamani (TFDA) vya ndani na vya nje ya nchi, ambavyo havina viambato sumu aina ya hydroquinone na nyinginezo.

Vipodozi zimegawanyika katika makundi mbalimbali kama ifuatavyo;-
Krimu,losheni,nywele,jeli,pafyumu,dawa za meno,roll on, sabuni,shampoo, poda,vipodozi vya kunyolea (after shave),cleansers, na mafuta ya maji(oil).

Kila kundi katika vipondizi hapo juu lina majina yake, nitakupa mfano mdogo hapa chini;
Krimu; 4u cream, Almondo kesar, heel cream na clear tone
Losheni;Avon herbal care,elegance lotion na miss lotion.
Vipodozi vya nywele;coco vanila soft na L' oreal dark
Jeli; afro jelly,bossy jelly na far shower gels

Kifupi tu nimesemi vipo vipodozi vya aina nyingine tofauti tofauti kutoka kwa makampuni mbalimbali.

Lakini pia vipo vipodozi kutoka nje ambayo ni pendwa ila haviruhisiwi kuingia nchi kutokana na kuwa na viambato sumu, ambavyo watumuaji wengi hasa wanawake wanavipenda, vipodozi hivi vinatoka sana Congo, hivi ukijihusisha navyo vitakupa ugumu kuvipigia promo katika ukrasa wako.
Ahsante sana mkuu
 
Back
Top Bottom