Haina maana kwenda polisi wakati tuna vyombo vinavyotakiwa kufuatilia swala hili, hawa watu wanahatarisha usalama wa taifa, je hao watu wa kijitonyama a.k.a USALAMA WA TAIFA wanafanya nini? au kazi yao ni kuchakachua tu?
Hao watu wanaojiita wa Intelligence kwa bahati mbaya most of them are not intelligent. Kama wangekuwa na intelligence kidogo tu wangetambua kwamba nchi inapelekwa mrama na watu wachache sana kwa maslahi binafsi. Wangekuwa intelligent wangemuonya JK kuacha kuzungumzia suala la UDINI wa kusadikika wakati anaelewa fika kwamba watanzania hawana upuuzi huo wa UDINI. Nashangaa kuona kiongozi mkuu wa nchi anachochea UDINI, na sitashangaa kusikia kuwa anaunga mkono upuuzi wa hiyo radio na hata hawa waliojitokeza siku za karibuni na kujifanya kuwaonya maaskofu.