Tunaosimama na Sabaya hatuipingi Serikali, tunapambana dhidi ya dhuluma na uonevu kwa waliojitolea kupambania Taifa

Nigrastratatract nerve

JF-Expert Member
Sep 4, 2019
1,395
3,901
SABAYA FOR CHANGE (S4C)

Another day, better than Yesterday. Katika simu na jumbe nyingi nilizopokea swali lililojirudia mara nyingi ni "Iwapo Sabaya anashtakiwa na Serikali, je nyinyi mliosimama kwa upande wa sabaya mmeamua kupambana na Serikali?"

UFAFANUZI WA KWANZA:
Well, Hatupambani na Serikali, Taasisi, wala Mtu Binafsi. Tunapambana dhidi dhuluma na kile Tunachoamini ni uonevu na kurudishwa Nyuma kwa wale wachache waliojitolea kupambania Taifa hili.

Jambo la kwanza watu waelewe kuwa Sabaya ameshtakiwa kwa tuhuma za Uhujumu Uchumi, kuunda Magenge ya Uhalifu na unyang'anyi wa kutumia Silaha (armed robbery). Makosa haya kisheria ni JAMUHURI dhidi ya MTUHUMIWA na sio Mtu binafsi dhidi ýa Mtuhumiwa, watu binafsi hapa wata- appear Mahakamani kama Mashahidi tu wa upande wa Jamuhuri na hii sio kwa Sabaya pekee bali ni kwa Mtuhumiwa ambaye tuhuma dhidi yake zinadondokea kwenye makosa hayo kwa hivyo hapa serikali imetimiza wajibu wake na sasa ni wajibu wa kila anayeamini Sabaya hana hatia kusimama nae na yule ambaye anaamini ana hatia asimame upande wa Jamuhuri, Machaguo yote Mawili yanaruhusiwa kisheria. Sisi tumechagua "Sabaya" .

MIPANGO:
Katika Dunia hii, Afrika hii na Tanzania hii, mara nyingi wanasiasa Mashupavu kama akina Sabaya hupitia katika masahibu mengi sana na hata kufungwa jela hata kunusurika kuuawa lakini hiyo haiwezi kuzima ndoto zao za kupigania vile vitu vya Msingi wanavyoviamini. Mapambano ya Kisiasa ni kufa na kupona wakati mwingine hata kupoteza Maisha. Wale walileta tuhuma hizi dhidi ya Sabaya sio wajinga, wanajua asili ya makosa hayo na adhabu zake, wanajua wakishinda watakuwa Wamemkomoa na kurudisha nyuma na kukatisha Tamaa watu wote Majasiri aina ya Sabaya.

Ipo dhahiri Tuhuma dhidi ya Sabaya, kuitwa jambazi n.k zilianza kusambazawa na Chadema na Mbunge wa jimbo hilo Mh Mbowe (Mwenyekiti wa Chadema) Tangu Rais Magufuli akiwa Madarakani lakini zimekuja kutekelezwa Mahakamani mara baada Rais Magufuli kufariki. Tumeshuhudia wote namna mambo yalivyokwenda haraka kuanzia Tuhuma mpaka super sonic speed ya DPP Kweka katika swala hili, tena akisafiri mwenyewe kwenda Arusha.

Hakuna asiyejua kuwa Vita ya Sabaya sio Sabaya na Wananchi wa Hai bali ilikuwa ni vita ya Sabaya dhidi ya Wahujumu uchumi wa Hai..Majambazi wa Hai..Magenge ya Uhalifu hai..Wakwepa kodi wa Hai.

MAKOSA MAKUBWA KUMI YA OLE SABAYA
Kosa la kwanza la Sabaya Pale Hai ni kurejesha Ardhi ya Waislam waliyoporwa na Matajiri wa Hai na kuirudisha kwa Bakwata

Kosa la pili la Sabaya ni kurejesha Mashamba ya Ushirika iliyoporwa na matajiri wa Hai na kuwapa wananchi wanyonge walime na kujipatia mlo wao badala ya kukodishwa na Matajiri.

Kosa la tatu la Sabaya ni kufukua mapango ya majambazi wa Magari Arusha, Moshi, Mererani na Dar es salaam yaliyokuwa yanajificha wilayani Hai,

Kosa la nne la Sabaya ni kuwarejeshea Waalimu wanyonge waliyodhulumiwa Pesa zao na Qnet.

Kosa la tano la Sabaya ni kuwapigania wananchi wanyonge waliyoporwa Ardhi yao pale Hai na matajiri wa Kimachame,

Kosa la sita la Sabaya ni kurejesha Jimbo la Hai, Halmashauri ya Wilaya na Halmashauri ya Vijiji mikononi mwa CCM, na Mbowe kukataliwa na wananchi ktk sanduku la Kura.

Kosa la Saba la Sabaya ni kuongeza makusanyo ya Kodi ya TRA na Kodi ya Halmashauri ya Wilaya na kuwadhibiti wakwepa Kodi huko Hai,

Kosa la nane la Sabaya ni kuitoa Hai toka nambari 64 ktk ukusanyaji wa Mapato mpaka nambari 6 Kitaifa mwaka 2019.

Kosa la tisa la Sabaya ni kufuatilia wanufaika hewa na feki wa fedha za Tasaf pale hai na kukuta Mpaka Marehemu wanafaidika wakiwa kaburini akauliza maofisa wa Tasaf, je huwa wanakutana wapi na Marehemu kuwapatia fedha?

Kosa la kumi la Sabaya ni kuwafanya Wananchi wa Hai waishi bila hofu ya Ujambazi na Magenge ya vibaka na wahalifu.

Sasa Kama huu ndiyo Ujambazi wa Lengai Ole Sabaya basi pengine tukawahitaji majambazi wengi zaidi wa aina hii hapa Tanzania ili tuweze kusonga Mbele.

Watalaam wa Utambuzi wanasema ukimwamisha OCD au Mkuu wa Kituo mahali halafu wanaoshangilia sana ni wahalifu halafu wananchi wanyonge wanasikitika "Jitafakari mara Mbili".

Lengai Ole Sabaya kwetu sisi wengine ni shujaa aliyejitoa maisha na Uhai wake kupigania CCM na Taifa hata kabla hajawa Mkuu wa Wilaya, narudia Lengai ole Sabaya ni kati ya vijana wachache ndani ya CCM ambao wako tayari kupoteza Uhai wao kwa kupigania maslahi ya Chama Cha Mapinduzi.

UKIMYA WA CCM
Kuna akili moja inadhani kwamba kesi ikiwa ya Jamuhuri basi ukiwa Mwana-CCM hutakiwi kujitokeza kusimamia upande usio wa Jamuhuri. Leo tunashuhudia Wana-CCM wengi especially wasaka vyeo na teuzi, na wengine Walinda vyeo wapo kimya wakidhani kuuchuna ni kuifurahisha Jamuhuri!

Sina hakika kama Shaka atakaa ofisini kusoma Magazeti kwa amani wakati Comrade Sabaya yupo Selo kwa Tuhuma zenye Mashaka Makubwa. Siamini kama atasahau kuwa anayopitia Sabaya na yeye alipitia wakati akiwa Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro pale aliposimamishwa kwa Uchunguzi kwa Tuhuma za Uongo aliyopandikiziwa na wabaya wake wa Kisiasa, baada ya uchunguzi akaonekana hana hatia Leo hii ndiyo Katibu Mwenezi wetu Taifa.

Viongozi wetu chama lazima watambue kuwa hakuna siku wapinzani wa CCM watamfurahia kiongozi shupavu wa CCM, viongozi wetu wa chama watambue kuwalinda vijana wanaopigania chama kwa gharama yoyote ili kuwatia Moyo vijana wengine wanaopigania chama kama kuna changamoto za Kimaadili chama chetu kina idara maalum ya Usalama na Maadili kwa Viongozi na wanachama wake warekebishane huko. Kusimamishwa kazi kwa Lengai Ole Sabaya inawezekana ikawa ni njia Bora zaidi ya Kumuimarisha kisiasa.

#Note: Leo wakati huu ambao Sabaya anatuhumiwa tunasikia Mbowe na Chadema yake wanashangilia na kuipongeza sana Serikali, ila kesho Sabaya atakaposhinda Kesi hii kwa kishindo utasikia "Serikali imembeba mtu wakee sio hakiii" na hii ni kwa sababu Watu wana Mikeka mifukoni. Chawa promax Mpo? S4C.
 
Kwahiyo Sabaya ameshitakiwa na serikali ya CHADEMA? kama ni serikali ya CCM kwahiyo CCM hakuna haki wanapenda dhuluma? wewe unatakiwa ukamatwe haraka na huyo jangili mwenzako tena mfungwe ikiwezekana mnyongwe wote, mnajificha kwenye koti la wanyonge kumbe ni majangili tupu.
 
Pale hotelini alienda kumtunza Nandy??
Je, dukani Arusha alikuwa anafanya nin??
Alikuwa anaimarisha CCM na yule diwani??

Ashughulikiwe hakuna namna.
Nyie ndiyo mnafanya CCM ionekane ya vibaka.

Everyday is Saturday............................ :cool:
 
Hawa wanamtetea ndo magenge yalikuwa yanafanya uharamia, mirija imekatwa lazima kutapatapa!

Huyu mtu ni muovu, katendea watu uovu anastahili hukumu kwa matendo yake maovu!

Angetenda mema angesemewa mema! Siku nyie na familia zenu yatakapowakuta mabaya ndo mtajua uchungu! Acha na yeye aone alipokuwa anawapeleka wenzake kama ni kuzuri sana
 
Hawa wanamtetea ndo magenge yalikuwa yanafanya uharamia, mirija imekatwa lazima kutapatapa!

Huyu mtu ni muovu, katendea watu uovu anastahili hukumu kwa matendo yake maovu!

Angetenda mema angesemewa mema! Siku nyie na familia zenu yatakapowakuta mabaya ndo mtajua uchungu! Acha na yeye aone alipokuwa anawapeleka wenzake kama ni kuzuri sana
Majangili yote hayo
 
Back
Top Bottom