Thomas Sabaya: Mkichagua Wapinzani Serikali haitawaletea Maendeleo

Heparin

Senior Member
Sep 24, 2021
127
420
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Arusha Thomas Ole Sabaya amewaonya wakazi wa Longido kutokuchagua wapinzani kwenye uchaguzi ujao wa serikali za mitaa, kwani serikali haitopeleka huduma muhimu kwenye maeneo yatakayokaliwa na viongozi wasiotokana na CCM.

Sabaya aliyekuwa akizungumza kwenye kikao cha Halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Longido ametoa kauli hiyo muda mfupi, baada ya kufanyika kwa maandamano ya CHADEMA mkoani Arusha.


Amesema yeyote atakayechaguliwa nje ya CCM atawajibika yeye na wananchi wake kujitafutia huduma muhimu na Mkuu wa mkoa hatokanyaga katika maeneo yenye kuongozwa na wapinzani.

Kauli ya Ole Sabaya imekuwa na hisia mseto mitandaoni,watumiaji wengi wa mtandao wa X (zamani twitter), wakisema kuwa rais Samia Suluhu Hassan hajaeleweka vyema na wasaidizi wake serikalini na ndani ya chama chake kutokana na kutoishi kwenye falsafa yake ya maridhiano.

Wengine pia akiwemo mwanasiasa John Heche anasema kauli kama hizo zinasababisha chuki zisizo na msingi kwenye jamii kwa kuaminisha watu kuwa watanzania walio nje ya CCM hawana haki kama walizonazo wanachama wa chama hicho tawala.

Rais Samia alitambulisha falsafa yake ya Maridhiano na upatanishi katika kujenga upya Tanzania tuitakayo, suala ambalo ndani yake linahimiza ushirikiano,ustahimilivu na kufanya kazi kwa pamoja na vyama pinzani katika kujitafutia maendeleo.
 
Huyu mzee mjinga sana..zama hizi unaleta siasa za kifala hivi kwani hao anaowaita wapinzani sio watanzania? Hawafai kuwa viongozi? Hawawezi kutoa mchango wowote kwa Taifa lao? Hawalipi kodi?
Haki ya kuchagua ipo wapi? Basi kusiwe na uchaguzi
 
Huyu mzee mjinga sana..zama hizi unaleta siasa za kifala hivi...kwani hao anaowaita wapinzani sio watanzania?...hawafai kuwa viongozi?...hawawezi kutoa mchango wowote kwa Taifa lao?...hawalipi kodi?....
Haki ya kuchagua ipo wapi?...basi kusiwe na uchaguzi

Chadema udini na ukabila unawaponza japo sio wote wapo hivyo, wabadilike


Lake zone oyeeeeeee
 
20240302_172237.jpg


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Arusha Thomas Ole Sabaya amewaonya wakazi wa Longido kutokuchagua wapinzani kwenye uchaguzi ujao wa serikali za mitaa, kwani serikali haitopeleka huduma muhimu kwenye maeneo yatakayokaliwa na viongozi wasiotokana na CCM.

Sabaya aliyekuwa akizungumza kwenye kikao cha Halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Longido ametoa kauli hiyo muda mfupi, baada ya kufanyika kwa maandamano ya CHADEMA mkoani Arusha.

Amesema yeyote atakayechaguliwa nje ya CCM atawajibika yeye na wananchi wake kujitafutia huduma muhimu na Mkuu wa mkoa hatokanyaga katika maeneo yenye kuongozwa na wapinzani.




Kauli ya Ole Sabaya imekuwa na hisia mseto mitandaoni,watumiaji wengi wa mtandao wa X (zamani twitter), wakisema kuwa rais Samia Suluhu Hassan hajaeleweka vyema na wasaidizi wake serikalini na ndani ya chama chake kutokana na kutoishi kwenye falsafa yake ya maridhiano.

Wengine pia akiwemo mwanasiasa John Heche anasema kauli kama hizo zinasababisha chuki zisizo na msingi kwenye jamii kwa kuaminisha watu kuwa watanzania walio nje ya CCM hawana haki kama walizonazo wanachama wa chama hicho tawala.

Rais Samia alitambulisha falsafa yake ya Maridhiano na upatanishi katika kujenga upya Tanzania tuitakayo, suala ambalo ndani yake linahimiza ushirikiano,ustahimilivu na kufanya kazi kwa pamoja na vyama pinzani katika kujitafutia maendeleo

MY TAKE
Angeongezea tu kwamba, Serikali haitokusanya kodi toka kwa wananchi wanaoishi maeneo yanayoongozwa na wapinzani. Hapo tutaelewana.
 
Ni bora kunyamaza kuliko kulazimisha kuongea. Kauli hizi zikemewe Kwa afya ya demokrasia maana mara nyingine maamuzi yanayofanywa ya kuteua wasiouzika ndio yanapelekea CCM kushindwa. Mfano, 2015 bila sababu za msingi ,jina la Hayati Mahiga lilikatwa katika kinyang'anyiro Cha ubunge Iringa mjini na kupelekea CCM kushindwa na CHADEMA. Mfano huu unatosha kuelezea ni nani anayetakiwa kuwajibika Chama kinapofanya vibaya na sio kutwisha mzigo wananchi ambao kama ukiwachagulia mtu mzuri na anayependwa atachaguliwa.

Badala ya kulaumu Kwa nini wapinzani wamechaguliwa ,CCM ikae chini na inawe mikono, mchakato wa uteuzi wa wagombea uzingatie vigezo vifuatayo.
Kwanza, mtu anayeuzika
Pili, mtu anayeheshimika
Tatu, mtu asiye na makandokando
Nne. Mtu mwenye upeo
Tano, mtumishi wa watu

Kama vigezo hivyo vikitumika nakihakikishia,chama dume ushindi wa kishindo ila kama wakipindua meza na kuja na majina ya wagombea mifukoni basi hapo tutaandika historia ya maumivu
 
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Arusha Thomas Ole Sabaya amewaonya wakazi wa Longido kutokuchagua wapinzani kwenye uchaguzi ujao wa serikali za mitaa, kwani serikali haitopeleka huduma muhimu kwenye maeneo yatakayokaliwa na viongozi wasiotokana na CCM.
Mwehu akapimwe mkojo, maneno kama haya ndiyo hupelekea watu kumegana nchi
Basi hiyo serikali isichukue kodi za wapinzani
 
Sijafurahishwa na kauli hiyo na hasa Kwa kuwa inatoa hukumu ya jumla badala ya hukumu Kwa mtu mmoja mmoja.

Falsafa za viongozi kuanzia wa alamu ya kwanza mpaka sasa ni kuhakikisha maendeleo ya watu yanapatikana bila kujalisha din zao, kabila zao au vyama vyama ila Leo umetumika ubaguzi wa uchama ambao ni hatari Kwa afya ya demokrasia na siasa safi.

Maamuzi ya wazazi yasiwe sababu ya watoto kuumia au kuumizwa. Kwa sababu Kwa Sheria za nchi yetu mtu aliye chini ya miaka 18 anatambuliwa kama mtoto hivyo Sheria ya uchaguzi pia imemkataza mtoto kutopiga kura.

Kwa mantiki hiyo, kauli ya Mwenyekiti sabaya inaweza kuwa ni chanzo Cha watoto kutopewa haki zao za msingi kama elimu Kwa sababu ya maamuzi ya upigaji kura ya wazazi wao. Tumeanza kuwabagua watu Kwa vyama vyao, tutakuja kuwabagua Kwa kabila zao na mwishowe Kwa dini zao. Hilo likemewe Kwa nguvu zote, Rais ameonesha dhamira ya dhati kabisa kuunganisha watu wote
 
CCM kauli za kijinga kama hizi kwao ndio sifa , yaani ujinga ni kigezo kikuu cha uongozi huko ccm
 
Huu ujinga sijui hatakama unavumilika,unasema nikichagua mpinzani huleti maendeleo ilhali KODI ya kufanyia maendeleo inakusanywa kutoka kwa wafuasi wa vyama vya upinzani na wafuasi wa chama tawala,huo si ujinga?
Mzee na baadhi ya wanachama wa CCM,watanabaishe kua MKICHAGUA viongozi wa vyama vya upinzani,muwalipe kodi hao viongozi,wawaletee maendeleo,uone kama kutakua kelele.
Haiwezekani wakusanye pesa kwa kina la KODI,halafu hizo pesa ukafanyie maendeleo kwingine,huo ni uporaji.
Wabadilike.Sisi tusiokua na vyama,ikitokea mpinzani akapita maeneo yetu,tukose huduma muhimu kisa wapinzani wamechaguliwa halafu kodi tulipe,ni haki kweli?
 
Sijafurahishwa na kauli hiyo na hasa Kwa kuwa inatoa hukumu ya jumla badala ya hukumu Kwa mtu mmoja mmoja.

Falsafa za viongozi kuanzia wa alamu ya kwanza mpaka sasa ni kuhakikisha maendeleo ya watu yanapatikana bila kujalisha din zao, kabila zao au vyama vyama ila Leo umetumika ubaguzi wa uchama ambao ni hatari Kwa afya ya demokrasia na siasa safi.

Maamuzi ya wazazi yasiwe sababu ya watoto kuumia au kuumizwa. Kwa sababu Kwa Sheria za nchi yetu mtu aliye chini ya miaka 18 anatambuliwa kama mtoto hivyo Sheria ya uchaguzi pia imemkataza mtoto kutopiga kura.

Kwa mantiki hiyo, kauli ya Mwenyekiti sabaya inaweza kuwa ni chanzo Cha watoto kutopewa haki zao za msingi kama elimu Kwa sababu ya maamuzi ya upigaji kura ya wazazi wao. Tumeanza kuwabagua watu Kwa vyama vyao, tutakuja kuwabagua Kwa kabila zao na mwishowe Kwa dini zao. Hilo likemewe Kwa nguvu zote, Rais ameonesha dhamira ya dhati kabisa kuunganisha watu wote
Ameshaonesha upande wa CCM inaouficha usionekane.

Kama angelikuwa ameikera CCM, angeshaitwa Kamati ya Nidhamu Dodoma
 
Back
Top Bottom