Jinsi Paulo na Muhamad walivyopata utume
Paulo alivyopata utume:
Alipewa utume na Yesu mwenyewe wkt akiwa ktk safari yake ya kwenda Dameski, Yesu alimtokea na kumwagiza yapasayo kufanya Matnd 9:1-8. Na utume wake, Bwana Yesu akauthibitisha kupitia mwanafunzi wake Anania kwa kumwambia anania yafuatayo ktk maono matendo 9:11-15 Basi palikuwapo Dameski mwanafunzi jina lake Anania. Bwana akamwambia katika maono, Anania. Akasema, Mimi hapa, Bwana. Bwana akamwambia, Simama, enenda zako katika njia iitwayo Nyofu, ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu aitwaye Sauli, wa Tarso; maana, angalia, anaomba;naye amemwona mtu, jina lake Anania, akiingia, na kumwekea mikono juu yake, apate kuona tena.Lakini Anania akajibu, Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kwa watu wengi, mabaya mengi aliyowatenda watakatifu wako Yerusalemu;hata hapa ana amri itokayo kwa wakuu wa makuhani awafunge wote wakuitiao Jina lako. Lakini Bwana akamwambia, Nenda tu; kwa maana huyu ni chombo kiteule kwangu, alichukue Jina langu mbele ya Mataifa, na wafalme, na wana wa Israeli. Na pia Anania ndiye aliyembatiza Paulo, matnd 9:18.
Na Paulo naye akiitikia wito wa kitume aliopewa na Bwana Yesu…akisema yafuatayo ktk warumi 1:1 Paulo, mtumwa wa Kristo Yesu, aliyeitwa kuwa mtume, na kutengwa aihubiri Injili ya Mungu;
Je kweli Paulo alitimiza utume huo wa kupeleka injili kwa mataifa na kisimama mbele ya wafalme na wana wa Israel? Jibu ni ndiyo…zifuatazo ni nchi Paulo alizo hubiri Uarabuni, Athene-ugiriki, Dameski-syria, Roma-italy, Yerusalemu-israel, Spain, Efeso, Galatia, korintho,filipi, Thesaloniki. Krete nk, na kote huko alikutana na changamoto zilizompelekea kusimamishwa mbele ya wafalme na maliwali na mbele ya wana wa Israeli. Tazama (Galatia 1:17; matendo 9:19,20,26-29; 17:16-22; 18:19;19:35; 28:16-30; warumi 15:24:28 na kuhusu kusimama mbele ya wafalme na wayahudi tazama matendo kuanzia sura ya 21-28).
Muhamadi alivyopata Utume
Ktk kitabu cha maisha ya nabii muhamad kilichoandikwa Sheikh abdalah Farsy uk 11-13,81 kina maelezo yafuatayo….
Hata siku moja ktk mwezi wa ramadhan tarehe 17 jumatatu, muhamad akiwa ana miaka 40 unusu wa umri wake, Mtume alimwona mtu kasimama mbele yake bila ya kumwona wp katokea, akamwambia soma mtume akamwambia sijui kusoma kwn sijapata kujifundisha kusoma. Yule mtu akaja akamkamata akambana akamwambia soma mtume akamwambia jawabu lake lilelile, ht mara ya tatu akamwambia soma iqra bismi rabbika akamsomea sura ya 96 mpaka kati yake, kasha mtume akamsomea km alivyosomewa. Mara Yule mtu akatoweka mbele yake asimwone kaenda wapi. Na mtume naye akarejea kwake kwa hofu imemshika, na alipofika nyumbani bibi khadija alidhani anahoma akamfunika maguo gubigubi na akakaa mbele yake akimsikiliza anavyoweweseka, hata homa ilivyomwachia alimweleza bibi khadija yaliyomtokea. Na bibi khadija akamtuliza moyo wk akamyakinisha ya kuwa hpn lolote baya litakalomzukia, mara bibi khadija akaenda kwa jamaa yake bwana waraqa bin Naufal akampa hbr yote, iliyompata mumewe naye akamwamrisha amwite mumewe na mtume akaenda akamweleza hbr yote,bwana Waraqa akamwambia huyo ndiye Gibril aliyemshukia nabii Musa na Nabii Issa. Basi jibashirie kuwa ww ni mtume kwa umma huu, name natamani kuwa hai nikuone unavyosimama kuwatengeneza jamaa zako inshallah ntakuwa mkono wk wa kulia. Ilikuwa December 610, hivyo utume wake alibashiriwa na Waraga mbele ya bi khadija.
Na ukisoma kitabu kiitwacho wakeze mtume wakubwa na wanawe kina maelezo yafuatayo
Kwa ufupi: muhamad alivyotoka pangoni kuelekea kwake baada ya kubanwa na Yule mtu hasiye julikana katoka wapi, homa ilimpanda akataka afunikwe maguo mara akawa anatetemeka kwa nderema na kuweweseka na kusema najiofia nafsi yangu kuchezewa na mashetani na kuniharibu akili yangu na kunizuga, bibi khadija pale pale alimdakiza na kumtia moyo kwamba sivyo hivyo …………….na kumwambia mm naona ushakuwa mtume. Na baada ya muhamad kusinzia bi khadija alitoka na kwenda kwa waraqa bin naufal padre wa kinasara na akamjuvya na Yule padre akamwambia utume huo kashapata mumeo bahati yako. Upesi khadija akarejea nyumbani na kumkuta muhamad kashaamka akamwambia twende kwa waraqa ili umsimulie yaliyokufika, wakaondoka mguu kwa mguu mpaka kwa huyo bwana mkubwa, mtume akamwadithia yote. Na bwana waraqa akamwambia nakubashiria muhamad huo ndio utume uliomwendea nabii musa na nabii issa na wengineo na krb hv utapewa amri ya kufundishwa dini ya haki, nikiwa hai ntakuwa mkono wk wa kulia nikusaidie kila namna na ni kupiganie.
Kwa ufupi utume wa muhamad ni wa kubashiriwa na bwana Waraqa pamoja na bi khadija, na waraka akimwahidi muhamad kuwa mkono wake wa kulia. Maana ya mkono wa kulia ni utendaji mkubwa, km vile Yesu alivyofufuka na kupaa kwenda mbinguni ni kuketi ktk mkono wa kuume(kuume) wa Mungu BABA, yaani inamanisha Yesu ni mtendaji mkuu wa wokovu wetu. Kwa hiyo bwana waraka ni mtendaji mkuu wa muhamad na uislam maana isingekuwa yy muhamad asingekuwa mtume.
View attachment 1793930
View attachment 1793931
View attachment 1793932