The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

vilaza wapo dodoma wanahemea per day,yaani inakatisha tamaa tulioibiwa hakuna hata mbunge mmoja ambaye angalau kachomekea neno hadi leo,wabunge wa uingereza wana uchungu utafikiri pesa iliyoibiwa ni yao wetu aah kimyaa wanaogopa kamati za chama na wale wa upinzani wanaogopa kunyimwa vitripu vya kuandamana na muungwana zomboka

Mzee Phillemon Mikael,

Ukifuatilia mienendo ya wanasiasa wengi wa nchi zetu masikini utakata tamaa ya maisha. Ni bahati mbaya tunawapata viongozi wenye vyeo bila ya kuwa na sifa za uongozi na watu wenye sifa za uongozi ambao hawana vyeo vya kuwapa nafasi ya kutumia sifa hizo kwa manufaa ya jamii zetu. Matokeo yake ni kwamba wenye vyeo wataendelea kuvurunda utawala wa jamii zetu, wakati wale wenye sifa bila vyeo wanalazimika kuendeleza uongozi wao kwa njia zisizo rasmi. Napenda kuwapongeza wadau wote wa jambo forum kwa kuendeleza uongozi katika njia hii isiyo rasmi. Ni matumaini yangu kuwa taasisi zetu zote (Bunge, Vyombo vya habari, Mahakama, Wanafunzi, Waalimu, Madaktari, wakulima, Wafanyakazi, Vyama vya siasa, wazululaji, changu doa, na wadanganyika wote) wataondoa ukungu uliogubika macho yao na kufuata nyao za Jambo forum

Kuongoza ni kuonyesha njia. Nakupongeza sana Mwana Kijiji kwa kuonyesha njia. Kitu ulichokifanya, sisi wa kwa Mfugwa Mbwa tunaita "Education for Liberation". Ni matumaini yangu kuwa wanafunzi wote wa nyumbani wataachana na "old fashioned tricks" za kugomea masomo. Migomo ilikuwa na mafanikio zamani wakati tunatawaliwa na viongozi waliokuwa na maono kuwa nchi haiwezi kuendelea bila kuwasomesha watu wake. Migomo haiwanyimi usingizi watawala wetu wa sasa. Nawashauri wanafunzi wawe wanapitia Jambo Forum ili wapate mbinu za kupambana na hawa waheshimiwa.

Nani kasema kuwa mataifa makubwa kama Uingereza na Marekani hayawezi kuzuiwa kutembeza ubabe na kuwakandamiza raia wa nchi masikini? Ukitaka kutumia mtutu wa bunduki utakata tamaa na huwezi kamwe! Lakini kumbuka haya mataifa yamefika hapa yalipo kwa sababu ya kutumia "bongo" na "Karamu". Ndio njia hiyohiyo inayoweza kutumika kuyasambaratisha. Mara nyingi wanaofanya ubabe, unyonyaji, na ukandamizaji ni viongozi wao wakishirikiana na watawala wetu wenye uwezo mdogo wa kuona mambo. Raia wengi wa hizi nchi hawakubaliani na matendo ya viongozi wao. Vivyo hivyo, raia wengi wa nchi zetu hawakubaliani na watawala wetu. Kwa mtindo huu wa Mwana Kijiji wa kuweza kuwasiliana moja kwa moja na raia wa hizi nchi katika wakati muafaka, tunaweza kuwaweka kiga, na kuwapiga kabali la nguvu hawa waheshimiwa wetu, hivyo kujikomboa. Bado naamini kuwa raia wa Uingereza/Marekani wana uwezo mkubwa wa kuzisimamisha serikali zao. Kinachotakiwa ni sisi kutoa somo kwa hao raia na likaeleweka.

Hongera sana Mwana Kijiji pamoja na wadau wote wa Jambo Forum
 
Kyoma, nashukuru sana. nitaiandika tena kidogo ile makala ya "Ukweli kuhusu Rada lazima Ujulikane" na kutuma nakala kwa wabunge wote wa Tanzania, muda wa kukaa kimya umepita, muda wa kuliamsha taifa kuthubutu umefika! Kama hawataki kuongoza, watajikuta wanafuata!!!
 
heri ya mwaka mpya na karibu tena Mzee Kyoma!
 
baada ya maneno mazito ya Kyoma mimi Lunyungu naomba ile barua ipelekwe kwa wabunge zaidi wakiwemo wa Upinzani . Usiache kumpa Chifupa maana anasifiwa sana tuone kama anaweza kuibua hoja . Mzee MKJJ naomba barua iendelee kuingia kwenye EU na mabunge yao . Tusikate tamaa tupo tayari kusimamia na kusambaza .

jambo la mwisho naomba wale wenye connection na vyuo vyetu huku Malampaka wawape taarifa tukutane hapa . Waje waseme nasi kaka zao na baba zao tutafanya kazi kuiokoa Tanzania .

Mzee MKJJ tuwasiliane kulee mahala tuendelee na kazi .
 
heri ya mwaka mpya na karibu tena Mzee Kyoma!

Mzee Ogah, heshima yako kwanza! na Heri yako pia

Binafsi, nawapongeza washika dau wanaoonekana na wasioonekana, ilimradi wote lengo lenu moja la kuirutubisha na kuipa siha njema JF. Kutaja wachache tu, Mzee Mkandara, Mzee Mwanakijiji (Mungu akujalie mibaraka fori), Mzee Mwanasiasa, Mama Lau, Mzee ES, Mzee Jasusi, Mzee Ogah, Mzee Invisible, na Mzee DrWHO. Mzee Ogah, sio siri nilitokomea. Kwa kipindi kile, mijadala mingi ilielemea kulenga kuwajadili watu badala ya kujadili ‘issues”. Pia baadhi ya wadau walijisitiri kwa vibakuli vya matusi katika vibambaza vya komputa zao, hata hawakusita kuwalushia wenzao kiholela. Kuhepuka zohari, niliazima busara za Kunguru mwoga.

Hata hivyo, nilipochungulia tena hivi karibuni, nikakubaliana na wahenga waliotuhasa kuwa Rome haikujengwa kwa siku moja. Kumbe ‘Meli ilipokumbwa na dhoruba, mabaharia uchwara mithili ya Kyoma tukajitosa baharini”. Ndio maana wadau niliowataja majina, na wote ambao sikuwataja napenda mburudike na kibao kilichochalazwa na DDC Mlimani Park Ochestra cha ‘MV mapenzi meli ya wapendanao bendera inapepea safari yaendelea”. Kibwagizo: ‘Baharia wenye upendo wameikabili dhoruba, ushirikiano wa ninyi ndio siraha yenu ya ukweli, na upendo ni sawa na .......”.

‘Papa na Nyangumi wenye uchu wamenikosa”, hivyo ‘nipo na nimejaa tele”
 
Kyoma, ndugu yetu umerudi?....
Safi sana, Augustine Moshi atafurahi sana kwani sasa jikiwe kile cha bsctimes kimetimia.

Mzee Mwanakijiji,
Hongera tena sana maanake umecheza kama vile Zidane.. bonge la ndooo!
Potelea mbali... heshima mbele.
 
Tulikwisha sema tangu mwanzo ukiingia hapa kwa pupa utatolewa mkuku, sasa haya ya mabwana/mabibi wanaovamia tuu bila kuangalia kwa kina nini kinaendelea hapa ndio matatizo yao.

Huwezi ukawa na postings tatu tu halafu unatoa mashambulizi ambayo ni baseless aidha umetumwa kuja kufanya fujo au uelewa wako ni finyu. Maneno tafadhali wacha fujo ingawaje umekunwa pale ambapo hukufikiria utakunwa. Tupo hapa 27/7 365 days a year.

MKJJ kazi tuliyoanza ndio kwanza mbegu zinachipua mavuno bado sana, Samora (R.I.P.) alisema Aluta continua aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa JF idumu.
 
SASA NAONA DR.WHO UMEKOSA LA KUONGEA. HUYO ZITO KABWE NDIYO NANI KATIKA HILI. MIE NAFIKIRI HUJUI UNACHOKISEMA. HUYU MWANAKIJIJI AMEFANIKIWA KUINGIZA UJUMBE NDANI YA PARLIAMENT UNAJADILIWA NA HAKUNA LOLOTE LA ZIADA. MIE NAFIKIRI ACHA SIASA ZAUJINGA., WEWE NI PANDIKIZI TUMESHAKUSHTUKIA...U MNAFIKI AMBAYE SIJUI UKAE WAPI. NAKUONEA HURUMA KWA SABABU NYINYI NDIYO WALE KAMA WAKINANANII WANAOJIFANYA KWAMBA NI WEMA KUMBE HAKUNA LOLOTE WANATUMIWA NA HAO MABWANA NIWAITE.TOA HABARI AMBAZO HAZIHUSU.

SHAME ON YOU FOR A POINTLESS.




labda ungeniuliza kwa nini niliingiza ya zito kabwe

Kwanza ni Mbunge wa CHADEMA ambaye kwa sasa yuko ziarani hapa UK

Pili CHADEMA an CONSERVATIVES wanauhusiano wa karibu japo CHADEMA hawajawa open kulidiscuss hilo

Tatu wabunge waliokuwa wakilibebea bango sana hiii issue kule House of Commons ni wa Conservatives

Nne humu ndani tuko independent kufikiria sasa kuna ubaya gani akaja mtu amabye hukubaliani naye kimawazo?
 
DrWho, maneno yako mazito siyo coincidence.. wenye maandiko wanasema "chuma hunoa chuma"....
 
Kyoma, ndugu yetu umerudi?....
Safi sana, Augustine Moshi atafurahi sana kwani sasa jikiwe kile cha bsctimes kimetimia.

Mzee Mwanakijiji,
Hongera tena sana maanake umecheza kama vile Zidane.. bonge la ndooo!
Potelea mbali... heshima mbele.

Mkandara, umenikumbusha ile ndoo ya Zidane... that was a classic!!
 
Habari Zinazoshabihiana

*Apewa kinga ya Bunge na atoboa siri zote
*Vigogo waandaliwa kuburuzwa mahakamani

WAZIRI wa zamani wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza, Bi. Clare Short, amelithibitihia Bunge la nchi hiyo, kuwa upo ushahidi mzito kuwa rushwa ilitumika katika kuchagiza Serikali ya Tanzania kununua rada iliyogharimu zaidi ya sh. bilioni 40 mwaka 2002.

Bi. Short ambaye alipinga kwa nguvu zote ununuzi wa rada hiyo akisema ni mzigo mkubwa na usio na manufaa kwa nchi changa kama Tanzania, alivuta hisia za wabunge wengi, alipokuwa akichangia mjadala huo, juzi usiku.

Kwa mujibu wa gazeti la The Guardian la Uingereza toleo la jana na taarifa kutoka Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), Bi. Short kabla ya kutoa ushuhuda huo mzito, kwanza aliomba kuhakikishiwa kinga ya Bunge ya kutoshitakiwa kwa maneno ambayo angeyasema.

Akilihutubia Bunge hilo, Bi. Short alisisitiza kuwa suala la kutumika rushwa katika ununuzi huo lilikuwapo na kwamba alipewa siri za ndani kutoka Idara ya Kuchunguza Makosa ya Ulaghai (SFO) ya Uingereza inayochunguza suala hilo, ikithibitisha.

"SFO wamemthibitishia Clare Short kuwa kuna nyaraka nzito zinazoonesha kwamba rushwa ilitumika katika uuzaji wa rada kwa Serikali ya Tanzania," lilisema The Guardian likinukuu alichokisema mwanasiasa huyo bungeni na kusema upo uwezekano wa baadhi ya vigogo kufunguliwa kesi.

Bi. Short alikaririwa zaidi akisema hata baadhi ya viongozi wa Serikali ya Uingereza walijihusisha katika kufanikisha ununuzi huo.

Aliuita ununuzi huo kuwa ni 'uchafu' na kuomba wabunge waunganishe nguvu zao kutaka sheria kali zaidi zitungwe kuibana Serikali katika aina ya mauzo ya vifaa vya kijeshi itakayopaswa kuruhusu siku zijazo.

"Serikali ya Tanzania ingefurahi kama Serikali ya Uingereza (ili kuonesha kwamba nayo haikufurahi juu ya mauzo ya rada hiyo) ingewanyima wauzaji hao (BAE) leseni ya usafirishaji, kwa kigezo kwamba ingeathiri maendeleo ya Taifa hilo changa (Tanzania)," alikaririwa akisema Bi. Short.

Bi. Short alisisitiza kuwa hata mkopo ambao Tanzania iliupata kutoka benki ya Barclays ili kununua rada hiyo, ulikuwa na walakini, kwani Benki ya Dunia ilidanganywa hasa juu ya ukubwa wa mkopo wenyewe.

Bw. Andrew Mitchell ambaye ni Waziri kivuli wa Wizara ya Maendeleo ya Kimataifa, naye alitilia nguvu maoni ya Bi. Short kwa kuiponda rada hiyo, akisema Tanzania imeuziwa mtambo wa kizamani ambao hautaweza kuisaidia kama inavyodhani.

Alipobanwa katika kikao hicho, Waziri wa sasa wa Maendeleo ya Kimataifa ambaye mwaka 2002 alikuwa msaidizi wa Bi. Short, Bw. Hilary Benn, alikataa kuzungumzia chochote juu ya tuhuma, kwamba kuna kamisheni ya sh. bilioni 12 iliyotolewa na kampuni ya BAE Systems, ili kuchagiza ununuzi wa rada hiyo, ila akatetea kuwa Tanzania haijaathirika kiuchumi.

"Kabla ya kuuziwa hiyo rada, Serikali ya Tanzania iliulizwa kama kusingekuwa na madhara makubwa kwenye uchumi wao, ikasema hakuna," alisema Bw. Benn huku akikwepa pia kuzungumzia suala kuwa rada hiyo ni mbovu na teknolojia yake imepitwa na wakati.

Katika hatua nyingine, ilibainika kupitia kikao hicho cha Bunge kwamba tayari kampuni ya BAE imeanza kuchunguzwa pia nchini Afrika Kusini, inakodaiwa kutoa kamisheni zinazofikia zaidi ya sh. bilioni 100 kwa wanasiasa wa ANC, ili kupata mikataba na zabuni mbalimbali kuanzia mwaka 1995.

Tayari Idara ya Uendeshaji wa Mashitaka na Upepelezi ya Afrika Kusini, Scorpions, imeanza kushirikiana na wenzao wa Uingereza kufanya uchunguzi huo.

Mbunge wa chama cha upinzani cha Independent Democratic, Bi Patricia de Lille, amejitolea kwenda London, Uingereza, kutoa ushahidi wa vitendo hivyo vya rushwa kati ya BAE na baadhi ya maofisa wa ANC
 
Blair blasted over Tanzania radar deal

2007-02-01 10:28:57
By Guardian Reporter and Agencies


The UK sold a ``useless`` air traffic control system to Tanzania in 2001 in a ``scandalous`` and ``squalid`` deal, the House of Commons has been told.

Ex-International Development Secretary Clare Short joined the Tories in accusing Tony Blair of pushing through the ?28m sale by BAE Systems.

Ministers said the deal had not damaged Tanzania?s economy or its development.

The Serious Fraud Office (SFO) is currently investigating claims that BAE bribed Tanzanian officials.

Short, who is now an independent MP, has consistently argued Tanzania could have paid much less for the same equipment.

``I believe that all the parties involved in this deal should be deeply ashamed,`` she said in a Commons debate on Tuesday night.

She said the deal was ``useless and hostile to the interests of Tanzania`` and had beenopposed by senior cabinet members including Chancellor Gordon Brown.

She said Barclays Bank had ``colluded`` with the government by loaning Tanzania the money, but lying to the World Bank about the type and size of the loan.

Lynne Featherstone, of the Liberal Democrats, said Britain had to be ``squeaky clean`` if it wanted to ``retain any influence, reputation or credibility in world affairs``.

``Somewhere between the government, BAE and Barclays - and perhaps all three - our reputation worldwide is in tatters,`` she said.

Shadow international development secretary Andrew Mitchell said BAE had used ``ageing technology`` and said the system was ?not adequate and too expensive``.

Mitchell said the deal had ?all the warning signs of impropriety - a vastly inflated price, an unsuitable product and unorthodox financing``.

``Despite the opposition of all the most informed, respected and qualified observers approval for the licences was forced through a divided cabinet by the prime minister.``

He called on his opposite number, Hilary Benn, to explain the government`s ``profoundly unattractive`` conduct.

Benn said the government had considered whether ?the export would seriously undermine the economy or seriously harm the sustainable development of the recipient country``.

``The government at the time judged it would not and, looking back from this vantage point, it would be hard to argue that it did.``

He said he could not comment on bribery allegations because they were under investigation.

Officials from the SFO have already visited Tanzania to look into claims BAE gave bribes to ensure the deal would go through.

BAE says it is co-operating fully with the inquiry, but has strongly denied operating a secret slush fund to sweeten deals.

The SFO recently decided to drop a long-running BAE corruption probe into a huge arms deal with Saudi Arabia.

Reports said the Saudis had threatened to pull out of a new BAE deal unless the probe was brought to an end.

Opposition politicians accused the government of putting cash before principle.

Two Tanzanian businessmen admitted recently that they were secretly paid $12 million by BAE.

The two businessmen made the admission to British detectives who recently flew into the country to investigate graft allegations in the controversial sale of the radar.

President Kikwete recently blamed UK for allowing one of its companies to `steal` taxpayers money from a poor country like Tanzania.

The radar deal between the government and Britain?s BAE started to hit newspaper headlines in 2002 when people started to ask the motive behind the project.

SOURCE: Guardian
 
President Kikwete recently blamed UK for allowing one of its companies to `steal` taxpayers money from a poor country like Tanzania.

Hapa sielewi...kwani walioiba si ni waTanzania? Hawa BAE wamefacilitate huo wizi tu.Kwani leo mimi nikiwa nauza gari shs laki tano,akaja mtu katumwa na tajiri, akanipa laki tano zangu then akasema niandike kuwa ni milioni moja na nusu,mwizi ni mimi au mnunuzi?
Maana hata ule mfano ambao Tafiti alimnukuu JK kuwa..'hio ni sawa sawa na kwenda kwa wakwe kuchukua mke kwa kulipa mahari,then baadae unapata ujumbe kuwa wakwe wanagombea mahari,hayo hayakuhusu'

Mwendo mdundo!
 
Tatizo ni kwamba sizani kwamba hiyo rada yenyewe kama ishamaliziwa malipo!
 
Kama watakuwa hawajamaliza kulipa watakuwa machizi basi,maana walikopeshwa pesa na Barclays.

Hii ya radar haina tofauti na ile ya Prof Mahalu.
Issue ni 'cha juu'.Mahalu tumeona kafikishwa mahakamani,basi na huyo wa radar naye afikishwe mahakamani.
 
Back
Top Bottom