The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

then what next?

Mimi nadhani tunahitaji viongozi waliotofauti na sifa ulizotaja ili wawezi kuliondoa Taifa kwenye hili bwawa la matatizo. Its true kwamba tatizo letu kubwa lipo kwenye fikra. most of Tanzanians are opportunists, but we must get out of this pool. Tusikate tamaa, tupige moyo konde.

Tu -import- kutoka nje ya africa..'kubinafsisha uongozi wa juu'..
safu ya uongozi iwe;
prezidee-USA
w-mkuu-UK
w-kilimo-china
w-pesa-Uk
w-miundombinu-china
elimu-German
mambo ya ndani- Slaa
nishati- Prof. mark

hapo wakuu with in 5yrs...TZ itakuwa na mwelekeo... ni afadhali kutawaliwa kuliko huu upuuzi...47yrs free?!!!!!!maoni tu...
 
- Huu ni wakati muafaka kwa wasomi, wana-dini, na viongozi wetu wa siasa kukaa chini na kujaribu kutafakari kwa makini, kwa sababu sio siri kwamba taifa letu limekumbwa na crisis kubwa sana ya character, Mwalimu alitupatia national ID basi lakini nationally kwenye character kwa maoni yangu tume-fail miserably.

- Sisi wananchi ni waongo, I mean taifa zima ni waongo, wezi, waumini wa uchawi, wanafiki, halafu masikini ya Mungu tunategemea viongozi wetu wa siasa wawe tofauti na sisi wananchi, it does not work tumekwama maana sasa nani wa kumfunga kengele paka?

- Hili ni taifa gani ambalo wote tumeharibikiwa?


Mkuu FMES hapa umemaliza, nimeguswa mno na haya maoni yako. Na kinachonitatiza siku zote ni kwamba viongozi wetu na wananchi walio wengi hawajatambua hili na tuko bize na kutafuta solutions kijuu juu wakati no body tries to go to the source na kujaribu kutengeneza utaratibu sustainable wa mustakabali wa nchi yetu.

When I think of this country by 2050 tukiendelea kwa mwendo huu huwa sipati jibu.
 
- Huu ni wakati muafaka kwa wasomi, wana-dini, na viongozi wetu wa siasa kukaa chini na kujaribu kutafakari kwa makini, kwa sababu sio siri kwamba taifa letu limekumbwa na crisis kubwa sana ya character, Mwalimu alitupatia national ID basi lakini nationally kwenye character kwa maoni yangu tume-fail miserably.

- Sisi wananchi ni waongo, I mean taifa zima ni waongo, wezi, waumini wa uchawi, wanafiki, halafu masikini ya Mungu tunategemea viongozi wetu wa siasa wawe tofauti na sisi wananchi, it does not work tumekwama maana sasa nani wa kumfunga kengele paka?

- Hili ni taifa gani ambalo wote tumeharibikiwa?

FME hivi katiba na kanuni za sheria zetu zikiweka wazi kuwa kiongozi akithibitika mwongo wakati akitumikia taifa kifungo chake kadhaaa, akiwa mwizi ndani ya uongozi wake au akifanya uzembe wa wazi miaka kadhaa na kumfilisi kujaza pengo alilosababisha pana fisadi atakayependa uongozi? Huyu Chenge ndio mentor wa mambo yote tuliyonayo kwani ndiye aliye twist kila kitu ndani ya katiba baada ya mwalimu kufariki, alihakikisha kunakuwa na loop holes za kusevu endapo baya litatokea kama sasa tunavyoona kwa BWM,mwisho napenda kukataa kuwa tumeharibika ila ni viongozi wetu, na sio wote lakini wengi wameharibika
 
- Huu ni wakati muafaka kwa wasomi, wana-dini, na viongozi wetu wa siasa kukaa chini na kujaribu kutafakari kwa makini, kwa sababu sio siri kwamba taifa letu limekumbwa na crisis kubwa sana ya character, Mwalimu alitupatia national ID basi lakini nationally kwenye character kwa maoni yangu tume-fail miserably.

- Sisi wananchi ni waongo, I mean taifa zima ni waongo, wezi, waumini wa uchawi, wanafiki, halafu masikini ya Mungu tunategemea viongozi wetu wa siasa wawe tofauti na sisi wananchi, it does not work tumekwama maana sasa nani wa kumfunga kengele paka?

- Hili ni taifa gani ambalo wote tumeharibikiwa?

Mkuu FM ES, Heshima mbele!

Agreed with your arguments, lakini mkubwa sasa tunaanzia wapi kubadilika? nani awe ni chachu ya mabadiliko ya kweli, yenye kutukuza uzalendo na utaifa wetu na umoja na amani ya KWELI hapa TZ? mimi kwa mtazamo wangu, narudi kwa viongozi wetu, hawa ndio hutunga sera, sheria, kanuni na kuzisimamia utekelezaji wake......hawa ni washika dola, sasa ndugu yangu sisi wananchi wakawaida tutaanzia wapi kuleta real changes hapo? kuharibikiwa kwetu kunatokana na the fact that....we are trying hard to struggle for the fittest ndani makucha makali ya hawa viongozi wenye roho za ubinafsi na ufisadi!

Kwangu mimi, nafikiri tuanze na a good tune at the top, then hii iwe replicated down the ladder
 
Last edited:
FMES, mkuu you have had some very harsh words, but I think that we definitely need them. Lazima tuanze kubadilika, lakini kwa kuwa hata kuharibikiwa kwetu was top to bottom, basi hata mabadiliko lazima yaanze juu kwenda chini.

I know that mimi binafsi huwa nachekwa sana na kuitwa mshamba kwa kuwa si mtoto wa mjini na si mjanja, lakini sikubali kuyumbishwa katika principles zangu. Lakini simhukumu mtu ambaye anaamua kuyumba na kushawishiwa kuchukua kitu kidogo. After all kama viongozi wetu wana-behave as if that is normal then that is what it is NORMAL, lakini when viongozi wetu wata-behave that it is unacceptable, that is what it will be. Kwa hiyo issue ya Chenge na wenzake kukubali na kujiuzulu au to step aside ni jukumu lao na hawawezi kutumia general morality ya jamii ya watanzania kama sababu.
 
- Huu ni wakati muafaka kwa wasomi, wana-dini, na viongozi wetu wa siasa kukaa chini na kujaribu kutafakari kwa makini, kwa sababu sio siri kwamba taifa letu limekumbwa na crisis kubwa sana ya character, Mwalimu alitupatia national ID basi lakini nationally kwenye character kwa maoni yangu tume-fail miserably.

- Sisi wananchi ni waongo, I mean taifa zima ni waongo, wezi, waumini wa uchawi, wanafiki, halafu masikini ya Mungu tunategemea viongozi wetu wa siasa wawe tofauti na sisi wananchi, it does not work tumekwama maana sasa nani wa kumfunga kengele paka?

- Hili ni taifa gani ambalo wote tumeharibikiwa?

In a nutshell, viongozi wetu ni reflection yetu sisi wenyewe.....
 
- Huu ni wakati muafaka kwa wasomi, wana-dini, na viongozi wetu wa siasa kukaa chini na kujaribu kutafakari kwa makini, kwa sababu sio siri kwamba taifa letu limekumbwa na crisis kubwa sana ya character, Mwalimu alitupatia national ID basi lakini nationally kwenye character kwa maoni yangu tume-fail miserably.

- Sisi wananchi ni waongo, I mean taifa zima ni waongo, wezi, waumini wa uchawi, wanafiki, halafu masikini ya Mungu tunategemea viongozi wetu wa siasa wawe tofauti na sisi wananchi, it does not work tumekwama maana sasa nani wa kumfunga kengele paka?

- Hili ni taifa gani ambalo wote tumeharibikiwa?

Mkuu tupo pamoja.Ukiangalia kwa makini kuna tatizo hapa. Tukichukua mfano wa kichaa ni kwamba roho anayo,mwili anao pia na ndo mana anaishi.Tatizo ni nafsi(mind)yake imeharibika. Ili tufikie mabadiliko ya kweli lazima nafsi zetu zibadilike.Namna tunavyofikiri na kuamua mambo pia tubadilike. Kama jamii nzima ikibadilika na kuwa safi ni dhahiri hata viongozi watakuwa safi maana watatoka katiak jamii yetu!
 

- Sisi wananchi ni waongo, I mean taifa zima ni waongo, wezi, waumini wa uchawi, wanafiki, halafu masikini ya Mungu tunategemea viongozi wetu wa siasa wawe tofauti na sisi wananchi, it does not work tumekwama maana sasa nani wa kumfunga kengele paka?

- Hili ni taifa gani ambalo wote tumeharibikiwa?


Hell no, huna haki ya kusema wananchi wana sifa hizo. Wewe ni nani umewajudge (sijui vipi) na kuwaongelea wananchi wote. kama wewe ni katika hao waongo, wezi, waumini wa uchawi, wanafiki; ujue na uelewe vizuri kwamba tuko wananchi ambao ni wakweli, waadilifu, hatuamini uchawi na sio wanafiki hata kidogo.

Watu wa tabia zenu ndio mmetupelekea Taifa letu likafika hapa, mnajifanya mna uchungu kwa Taifa kumbe ni unafiki mtupu. Mungu hamfichi mnafiki na za mwizi ni 40. At lat umeconfess.
 
Jamani Tatizo la kwanza ni sisi tunaojiita wasomi.

Je ni watu wangapi miongoni mwetu tumepiga kura atleast the past 2 General election, nakuhakikishia ni less than 20%. Hivyo tunakubali kuchuguliwa mamluki na tunalalamika.

Je sisi leo tunaojiita wakosoaji ni wangapi kati yetu walau alijaribu kuchukua form ya kutaka kuchaguliwa kwenye public office yeyote in the last 2 general election? jibu nadhani either ni less than 0.2%. Msiulize nimetumia vigezo gani.

Hivi ni kweli katika majimbo yetu ya uchaguzi ni fulani tu ndio anafaa kuwa mwakilishi wa wananchi kwa miaka 10 -20 hata kama hawafanyii chochote wananchi?????? Ni Moshi vijijini nimeona wameweza wa kubadilisha mwakilishi kila baada ya 5yrs.

Huu si wakati wakuitana waongo, wapenda uchawi n.k. Si kweli ni kuoneana aibu? kutukuzana sehemu za kazi ndio boss, boss kasema hata kama yupo wrong tunamsaport.

Je katika sehemu yako ya kazi ni mara ngapi uliwahi kumkatalia boss wako kufanya kitu kilichopo kinyume na taaluma ya kazi yako????

Hivi ni kweli kwa taaluma zetu tulizo nazo tunaweza kusema watu say 50 walioharibu basi watanzania wote 35mplus tupo kama wao?????

Nakuhakikishia Polisi, CID, usalama wa taifa, TAKUKURU na mahakama na vyombo vingine vya kuenforce laws wakifanya kazi yao kama taaluma yao inavyowaruhusu, haya madudud yote yatakwisha in less than a year.

Ndio maana wakati mwingine mimi naprefer uongozi wa kijeshi maana when an order is given has to be implemented effectively and no exception
 
Hell no, huna haki ya kusema wananchi wana sifa hizo. Wewe ni nani umewajudge (sijui vipi) na kuwaongelea wananchi wote. kama wewe ni katika hao waongo, wezi, waumini wa uchawi, wanafiki; ujue na uelewe vizuri kwamba tuko wananchi ambao ni wakweli, waadilifu, hatuamini uchawi na sio wanafiki hata kidogo.

Watu wa tabia zenu ndio mmetupelekea Taifa letu likafika hapa, mnajifanya mna uchungu kwa Taifa kumbe ni unafiki mtupu. Mungu hamfichi mnafiki na za mwizi ni 40. At lat umeconfess.

Bro, utake usitake huo ndio ukweli wenyewe.....kama wewe ni exceptional to this thank sir God for that, na nivyoelewa mchangiaji hakusema watanzania wote i.e more than 40mil in all, wameharibika....still kuna waadilifu, labda ni pamoja na wewe!
 
Last edited:
FMES, mkuu you have had some very harsh words, but I think that we definitely need them. Lazima tuanze kubadilika, lakini kwa kuwa hata kuharibikiwa kwetu was top to bottom, basi hata mabadiliko lazima yaanze juu kwenda chini.

I know that mimi binafsi huwa nachekwa sana na kuitwa mshamba kwa kuwa si mtoto wa mjini na si mjanja, lakini sikubali kuyumbishwa katika principles zangu. Lakini simhukumu mtu ambaye anaamua kuyumba na kushawishiwa kuchukua kitu kidogo. After all kama viongozi wetu wana-behave as if that is normal then that is what it is NORMAL, lakini when viongozi wetu wata-behave that it is unacceptable, that is what it will be. Kwa hiyo issue ya Chenge na wenzake kukubali na kujiuzulu au to step aside ni jukumu lao na hawawezi kutumia general morality ya jamii ya watanzania kama sababu.

Totally Agree. Good post.
 
Sikubali mimi sio muongo, mchawi wala mnafiki...tatizo sijawahi kupiga kura (sikuwa nyumbani Tanzania) labda ndio maana hatuna viongozi makini (kwa sababu walikosa kura yangu)...lazima nijipange niwe nyumbani nipige kura 2010.!!

Then again....hivi hao wananchi makini huwa wanagombea hizi nafasi za ubunge n.k!!!!
 
Last edited by a moderator:
Uzito wa Tuhuma na Utamaduni wa kuwajibika

Na. M. M. Mwanakijiji

Tunapoendelea kujadili suala hili naomba niongeze haya kidogo. Katika nchi ya utawala wa sheria au inayojaribu kujenga misingi ya demokrasia tuhuma dhidi ya kiongozi yeyote yule wa umma (anayechaguliwa au kuteuliwa) zipimwe uzito wake na kwa kuangalia uzito huo na hasa uzito wa ushahidi unaotolewa (preponderous of evidence) ufikie mahali kutosha kumwajibisha mtu.

Mojawapo ya ulaghai wa watawala wetu ni kudai "tusubiri mahakama" au tusimhukumu mtu hadi mahakama ifanye uamuzi. Sasa hilo kwa juu linatosha kuvutia macho lakini ninaamini katika uongozi wa kisiasa au wa umma utamaduni wa kuwajibika utaanza kujikita pale tu ambapo tuhuma nzito haziwezi kuendelea kuvumiliwa.

Katika sakata la Chenge tukumbuke kuwa hakujiuzulu kwa sababu ya tuhuma kuwa anafedha kiasi fulani nje ya nchi. Kilichomtibulia Chenge ni maneno ya kuziita fedha hizo kuwa ni "vijisenti vichache". Watanzania wengi walichukizwa na maneno ya "vijisenti" kuliko fedha alizokutwa nazo au jinsi alivyokutwa nazo. Nina uhakika kama Chenge angefunga mdogo wake na kulia "tusubiri mahakama na uchunguzi uishe" wala asingekwenda popote.

Baada ya aliyekuwa Mkuu wa Tabora Bw. Ditopile Mzuzuri kutuhumiwa kufanya mauaji nilikuwa mtu wa kwanza tena kutaka ajiuzulu mara moja au Rais amsimamishe kazi mara moja. Sikuhitaji mahakama kuniambia kuwa mazingira ya tuhuma zinazotolewa ni nzito mno kiasi kwamba hawezekani kuendelea kuwa mtumishi wa serikali wakati huo huo. Tuhuma za mauaji dhidi yake na uzito wa ushahidi (picha, damu, n.k) vilitosha kabisa kumfanya ajiuzulu dakika inayofuata.

Ndio maana nilichukizwa na kitendo cha Rais kusubiri masaa mengi hadi Dito alipojiuzulu wadhifa huo na hivyo kulinda pensheni yake n.k Cha kushangaza zaidi alionesha maneno ya huruma ambayo naamini yalikuwa na lengo la kuntaint mchakato wa sheria kwa kumwagia huruma kwa Ditopile.

Uzito wa tuhuma dhidi ya Chenge na Dr. Idris ni mkubwa mno. Tuhuma hizi hata hivyo zimekuwepo kwa muda. Inawezekana vipi watu hao wakaendelea kudhaminiwa uongozi wa taifa na hata kupewa nafasi ya Ubunge?

Kwamba Chenge imeshasema hajatoa taarifa ya mali yake kwenye Tume ya Maadili kinyume na sheria ya Maadili ilitosha kabisa kutopata nafasi ya kugombea kule Bariadi. Lakini cha kushangaza ni kuwa alipewa nafasi ya kugombea Ubunge, akateuliwa Waziri mara mbili na mojawapo ya Wizara ambazo alipewa kusimamia ni ile ya Miundo Mbinu (ambayo ilikuwa inahusika na rada!)

Chenge alistahili awe amevuliwa madaraka yake yote mara moja hata kama si kwa mujibu wa utamaduni wa uwajibikaji lakini kwa kuangalia Katiba ya CCM na Mwongozo wa Maadili wa 2002. Katika mwongozo wa maadili CCM yenyewe inasema hivi kuhusu kiongozi wake "Jukumu la Kiongozi wa CCM katika kukijenga na kukilinda Chama ni kubwa. Athari katika Chama za Kiongozi kutenda maovu, au kutotimiza wajibu, ni kubwa kiasi kwamba Maadili yake yakitetereka Chama kitavurugika; na nchi itakwenda mrama."

Je kutetereka kwa uongozi wa CCM na kwenda mrama kwa nchi kumesababishwa na ubovu wa baadhi ya viongozi wa ngazi za juu wa CCM na hivyo kuonesha uhusiano wa moja kwa moja wa matendo ya mtu mmoja na hatima ya taifa?

Kwenye suala la Chenge inashangaza zaidi; mtu ambaye anatuhumiwa kupinda sheria, anatuhumiwa kuvunja sheria na ambaye amegubikwa na tuhuma za ufisadi hadi na vyombo vya nje ndiye yeye wakati huo huo anapewa nafasi ya kuongoza Kamati ya Maadili ya CCM ambayo kichama ndiyo inatakiwa kumchunguza hata yeye mwenyewe? Na ndiye huyo huyo aliyepewa nafasi ya kutoa maoni yake kuhusu maadili ya viongozi wengine wakati yeye amezibwa na ukungu mkubwa mweusi wa kashfa!

Dr. Idriss kwa upande wake ni hivyo hivyo. Tuhuma dhidi yake siyo ngeni pia lakini inashangaza kuwa wakati alipopata nafasi ya kujiuzulu na alipotaka kuachia ngazi badala ya kumuacha aondoke angalau aonekane kama shujaa sasa kuna kila dalili ataondoka kwa kashfa.

Haya yote yanatulazimisha kuhoji swali moja kubwa:

Je, yawezekana kuwa ile imani kuwa Usalama wa Taifa wanafanya uchunguzi (vetting) ya viongozi watarajiwa haina msingi wowote katika ukweli? Je yawezekana shughuli hiyo isifanywe na usalama wa taifa bali na tume ya maadili ya viongozi wa umma ambayo inatakiwa iwe huru kutoka mikono ya uteuzi wa Rais na iwajibike moja kwa moja kwa Bunge? Je yawezekana kwa kuwa na mchakato mbovu kabisa wa kupata viongozi wa juu ndivyo vivyo hivyo nchi yetu itaendelea kuwaweka madarakani viongozi, wabadhirifu, walaghai, wenye tamaa na ambao ndani ya mifupa yao chembe za ufisadi zinatengenezwa kila sekunde?

Wakati umefika wa uzito wa tuhuma dhidi ya kiongozi yeyote na hasa ushahidi unaoneshwa mbele vitoshe kabisa kumfanya kiongozi huyo aachie ngazi na hayo ya kisheria au mahakamani yaendelee mbele ya safari.
 
- Huu ni wakati muafaka kwa wasomi, wana-dini, na viongozi wetu wa siasa kukaa chini na kujaribu kutafakari kwa makini, kwa sababu sio siri kwamba taifa letu limekumbwa na crisis kubwa sana ya character, Mwalimu alitupatia national ID basi lakini nationally kwenye character kwa maoni yangu tume-fail miserably.

- Sisi wananchi ni waongo, I mean taifa zima ni waongo, wezi, waumini wa uchawi, wanafiki, halafu masikini ya Mungu tunategemea viongozi wetu wa siasa wawe tofauti na sisi wananchi, it does not work tumekwama maana sasa nani wa kumfunga kengele paka?

- Hili ni taifa gani ambalo wote tumeharibikiwa?

Wakiiba tunaowapenda tunataka sijui viongozi wa dini, wasomi etc lakini wakiiba tusiowapenda kila siku kushika bango waende lupango kwi kwi kwi kwi
 
- ..........- Sisi wananchi ni waongo, I mean taifa zima ni waongo, wezi, waumini wa uchawi, wanafiki, halafu masikini ya Mungu tunategemea viongozi wetu wa siasa wawe tofauti na sisi wananchi, it does not work tumekwama maana sasa nani wa kumfunga kengele paka?

- Hili ni taifa gani ambalo wote tumeharibikiwa?

.......ndio maana siwashangai akina Nyani na mikoba yao...........its frustrating.......now should we just sit and relax..........na hawa wapuuzi wanaendelea kuiharibu nchi kila kukicha....?
 
Nina ushauri ya jinsi vipi nchi yetu itaweza badilika:

Badala yakutegemea viongozi wetu kuwa na tabia ya uadilifu, kuwa wakweli, kuto iba, n.k. je kwanini tusihamasishe hii tabia ianze chini [bottom-up approach]. Tutapo zidi kupata hamasisho kutoka kwa wananchi, tutapozidi subscribers toka kwa wananchi wa kawaida, for sure viongozi will start to notice.

Viongozi know they have nothing to loose, so why change? Wataendelea kufanya vioja vyao for as long as we keep voting them to power.

Tanzania hatuhitaji ku-import viongozi, viongozi wapo ila the right ones wana aibu kujitokeza. African politics is a very dangerous prefesion.
 
Hatutaki kukubali ukweli kuwa mabadiliko lazima yaanzie kwa wananchi wenyewe ndio maana ukisema kuwa tanzania bado tuko safari ndefu ya kuondokana na matatizo tuliyonayo watu wanabisha.

Hivi mnafikiri kubadilisha viongozi wa juu ndio solution ya matatizo yetu wakati wote watakao kaa madarakani wote ni wezi, waongo, wazinzi, and the like. Tunahitaji kubadilika sisi wenyewe kwanza tu practice what we preache.

Hapa hapa JF kwa wale wanaofanya kazi ukiwauliza mshahara mtu kama ana mshahara mkubwa ni 300,000 lakini angalia matumizi kwa mwezi ni nearly 10 times the salary, hiyo 300,000 anatumia kunywa kwa mwezi, sasa hili huge gap linajazwa na nini.

Ni vigumu sana kuleta mabadiliko kama wananchi wenyewe hatujabadilika na kuanza na sisi, ndio maana mtu akipewa 10,000 wakati wa uchaguzi anampigia kura mtu hata kama ni mbovu kiasi gani kwani ni kawaida yetu kupokea rushwa na kulipa fadhila.

Sasa tunapiga kelele na viongozi na ufisadi lakini tukumbuke kuwa kila mbuzi hula kulingana na kamba yake.
 
I would like to rule this country and give me five years to clean up no politics just work.All my ministers will be CEO,s no politics. Basss
 
Kinachoweza kuwabadilisha watu ni kusimamisha sheria...
Sisi sote ni reflection ya viongozi wetu kwa sababu sheria zetu ni butu, lakini kama tunaweza kuchukia Ufisadi kama tunavyochukia vibaka wa Kariakoo basi bila shaka wananchi wote kwa ujumla tutabadilika...
Ni kweli kabisa kuwa hujuma yoyote dhidi ya uchumi wa Taifa huitwa ujanja..ni sifa kubwa kuvuta deal serikalini ukifahamu kwamba nyayo zako ziko covered na sheria butu.

Mimi nina hakika kabisa kusimamisha sheria ndio msingi wa mienendo ya binadamu wote..maneno matupu na viapo kuwa rushwa ni adui wa haki - sintatoa wala sintapokea rushwa ni hadithi tupu kama hakuna sheria na utamaduni unaofikisha ujumbe huu kwa wananchi wote...Na kwa bahati mbaya CCM wamekuwa mbele kuweka ubani kufukiza azimio lao la Zanzibar...

Mnategemea nini kama kiongozi wa chama mtu kama Makamba anayekuja wambia wananchi wake kwa ujeuri na majigambo kuwa chama ni safi isipokuwa kuna baadhi ya watu ndio wachafu wakati mwongozo wa chama chake unasisitiza kuwa:-

"Kiongozi wa CCM katika kukijenga na kukilinda Chama ni kubwa. Athari katika Chama za Kiongozi kutenda maovu, au kutotimiza wajibu, ni kubwa kiasi kwamba Maadili yake yakitetereka Chama kitavurugika; na nchi itakwenda mrama."
 
Kinachoweza kuwabadilisha watu ni kusimamisha sheria...
Sisi sote ni reflection ya viongozi wetu kwa sababu sheria zetu ni butu, lakini kama tunaweza kuchukia Ufisadi kama tunavyochukia vibaka wa Kariakoo basi bila shaka wananchi wote kwa ujumla tutabadilika...
Ni kweli kabisa kuwa hujuma yoyote dhidi ya uchumi wa Taifa huitwa ujanja..ni sifa kubwa kuvuta deal serikalini ukifahamu kwamba nyayo zako ziko covered na sheria butu.

Mimi nina hakika kabisa kusimamisha sheria ndio msingi wa mienendo ya binadamu wote..maneno matupu na viapo kuwa rushwa ni adui wa haki - sintatoa wala sintapokea rushwa ni hadithi tupu kama hakuna sheria na utamaduni unaofikisha ujumbe huu kwa wananchi wote...Na kwa bahati mbaya CCM wamekuwa mbele kuweka ubani kufukiza azimio lao la Zanzibar...

Mnategemea nini kama kiongozi wa chama mtu kama Makamba anayekuja wambia wananchi wake kwa ujeuri na majigambo kuwa chama ni safi isipokuwa kuna baadhi ya watu ndio wachafu wakati mwongozo wa chama chake unasisitiza kuwa:-

"Kiongozi wa CCM katika kukijenga na kukilinda Chama ni kubwa. Athari katika Chama za Kiongozi kutenda maovu, au kutotimiza wajibu, ni kubwa kiasi kwamba Maadili yake yakitetereka Chama kitavurugika; na nchi itakwenda mrama."


Utawala wa sheria vipi wakati dola na mahamana ndio wanaongoza kwa rushwa?
 
Back
Top Bottom