The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Mkuu nakurekebisha
Chenge alipewa hizo $1.5 million na yeye akampa Dr Rashid $600,000 ambazo amedai alimkopesha kufanya biashara ya fenicha
Sasa huu si upuuzi mtupu pesa yote kapata muhindi na heshima wamepoteza wao
Chenge kama asingefanya huu utaahira angefika mbali sana kwani CCM wanamtegemea kwamambo mengi sana

Mambo ya wizi? Ku.******ke
 
Makachero SFO wabaini maovu mapya ya Chenge

2009-02-03 10:26:30
Na Mwandshi Wetu​

Matata mapya yamemkuta Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge, baada ya uchunguzi wa makachero wa Uingereza wa Kitengo cha Makosa Makubwa ya Jinai (SFO) kugundua kwamba mwanasiasa huyo, hakuwahi kutaja katika fomu zake za kutangaza mali kwa Kamishna wa Maadili, kiasi cha Dola za Marekani milioni 1.5 alizokuwa ameweka kwenye akaunti yake kisiwani New Jersey.

Taarifa za uhakika ambazo Nipashe imezipata kutoka vyanzo vya kuaminika, SFO wanaochunguza rushwa katika ununuzi wa rada ya Tanzania iliyonunuliwa kwa bei ya Dola za Marekani milioni 40 na kiasi cha Dola milioni 12 (zaidi ya Sh bilioni 15) kutolewa kama rushwa ili kufanikisha ununuzi huo, wanashauri Chenge ashitakiwe.

Vyanzo vya uhakika vya habari kutoka SFO vinasema kwamba hakuna wakati wowote ambao Chenge, wakati huo akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, alitangaza kumiliki fedha hizo katika akaunti hiyo ughaibuni.

Chenge alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuanzia mwaka 1995 hadi 2005.

Kwa taarifa hizi mpya, SFO wamependekeza kwamba Chenge anaweza kufunguliwa mashitaka ya jinai kwa sababu ya kudanganya chini ya kiapo.

Kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi, kila mwaka kiongozi anayekalia ofisi ya umma anawajibika kujaza fomu maalum ya kueleza mali zake na mkewe pamoja na za watoto walio chini ya miaka 18, pia anawajibika kutangaza madeni yake kwenye fomu hiyo.

Akizungumzia utaratibu wa kujaza fomu ya kutangaza mali, Wakili wa kujitegemea, Mabere Marando, alisema kwamba kama mtu akithibitika amesema uongo chini ya kiapo ni kosa la jinai ambapo adhabu yake ni kufungwa na faini.

``Kwa sasa sina uhakika ni kifungo cha miaka mingapi, lakini hilo ni kosa la jinai, hivyo adhabu yake ni kufungwa,`` alisema Marando

Naye wakili wa kujitegemea wa Mahakama Kuu, Juvenalis Ngowi, alisema kwamba ni kosa la jinai kusema uongo chini ya kiapo.

``Jambo lolote ambalo unafanya chini ya kiapo, lazima useme ukweli. Usipofanya hivyo unakuwa umetenda kosa la jinai ambapo ni kufungwa,`` alisema Ngowi.

Kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995, kiongozi wa umma ambaye chini ya kifungu cha 22 na 23 akijua kwamba anatoa taarifa za uongo atakuwa anatenda kosa baada ya kuthibitika ambalo adhabu yake si chini ya Sh 200,000 na kiasi kisichozidi Sh milioni moja au kufungwa jela kwa kipindi kisichozidi miaka miwili.

Uchunguzi wa SFO unaonyesha kwamba Chenge akiwa kiongozi wa umma hakuwahi kusema anamiliki kiasi hicho cha fedha katika akaunti yake, na hata alipohojiwa juu ya fedha hizo alitoa majibu ya kukinzana.

Awali alisema fedha hizo ni malipo kwa ajili ya huduma ya kisheria aliyokuwa anatoa, lakini mara ya pili alibadili maneno na kusema kwamba zilitokana na akiba ya familia yake pamoja na urithi, pia alieleza kwamba asilimia 25 ya fedha hizo ni mali ya mkewe.

Chenge andaiwa na SFO kuwa mtu muhimu wakati wa mchakato wa ununuzi wa rada ya Tanzania, kwa sababu alitakiwa atoe ushauri wake wa kisheria kwa serikali.

Bila yeye mpango mzima wa ununuzi usingefanikiwa.

Kulingana na vyanzo vya habari, hata kama Chenge ataweza kuthibitisha vyanzo halali vya fedha alizochimbia New Jersey kwenye akaunti ya benki ya Barclays, bado atakuwa na kesi ya kujibu kwa kudanganya chini ya kiapo.

Chenge alijiuzulu nafasi ya Waziri wa Miundombinu Aprili mwaka jana, kutokana na kuwa chini ya uchunguzi wa SFO, akituhumiwa kwamba fedha alizojiwekea New Jersey zilitokana na mgawo wa rushwa ya ununuzi wa rada. Chenge amekanusha kuchukua rushwa.

Ununuzi wa rada hiyo ulisababisha mvutano mkubwa baina ya mawaziri wa serikali ya Waziri Mkuu wa Uingereza, Tony Blair, hali iliyomlazimu aliyekuwa Waziri wa Misaada ya Maendeleo, Claire Short, kuhitilafiana na serikali na mwishowe alijiuzu.

Short alisema ingawa hakuwa na ushahidi mahususi, ununuzi wa rada ya Tanzania kutoka kampuni ya kuuza vifaa vya kijeshi ya Uingereza, BAE System, ulikuwa umegubikwa na rushwa.

Kabla ya rada hiyo kununuliwa, kuliibuka mjadala mkali nchini, wengi wakipinga kwa sababu ilikuwa ina gharimu pesa nyingi wakati Tanzania ingeweza kupata rada mbadala kwingineko kwa gharama chini ya nusu ya hiyo.

Hata hivyo, serikali ya awamu ya Tatu ya Rais Benjamini Mkapa ilisisitiza kununuliwa kwa rada hiyo.

Hii ni mara ya kwanza taarifa za Chenge kudanganya chini ya kiapo zinafichuliwa, zikifuatia habari za kina zilizoandikwa na gazeti dada la The Guardian on Sunday wiki iliyopita jinsi Chenge alivyolipwa mabilioni kwenye akaunti yake namba 59662999 inayomilikiwa na kampuni ya Franton Investment Limited.

SOURCE: Nipashe
 
BAK hiyo habari inavutia sana. lakini ninachojiuliza bila kupatamajibu ni kuwa huyo Chengeatashitakiwa na nani? DPP/ Serikali ya Tanzania? Kama ndiyo, atashitakiwakwa makosa gani? Kama ni haya mashitaka ya kina Yona, Mramba et al ya kutumia vibaya madaraka adhabu yake itatosha kutoa funzo kwa viongozi wengine wa aina yake?

It a matter of time, lets wait.
 
Sasa serikali inasubiri nini hapa? Huyu should be showing up pale Kisutu wajameni?
 
Chenge hayupo Nchini au hamna habari ? Ameshayayuka ,pengine mkaambiwa ameenda kimatibabu na si muda mkaambiwa kakitoa.
 
Chenge hayupo Nchini au hamna habari ?
Ameshayayuka ,pengine mkaambiwa ameenda kimatibabu na si muda mkaambiwa kakitoa.

Tupe habari ndugu yetu Mwiba.........! Wakati kikao cha bunge kinafunguliwa last wiki nilimwona bungeni? Ameondoka lini, kaenda wapi na kwa sababu zipi?
 
Inawezekana kabisa mimi ni mtazamaji wa kipindi cha bunge hajaonekana
 
Mi naendelea kusema hii yote ni cinema tu, na starring wetu Chenge aka Vijisenti hauwawi!
Huyu ataibuka tu msafiiii, mshindwe nyie kupigizana kelele JF!
Yaani kwa kweli ingawa nimeweka hii hapa kimzaha lakini inakera sana! Because it is obvious he will walk away from this....
 
Mkuu nakurekebisha
Chenge alipewa hizo $1.5 million na yeye akampa Dr Rashid $600,000 ambazo amedai alimkopesha kufanya biashara ya fenicha
Sasa huu si upuuzi mtupu pesa yote kapata muhindi na heshima wamepoteza wao
Chenge kama asingefanya huu utaahira angefika mbali sana kwani CCM wanamtegemea kwamambo mengi sana

Pole ndugu yangu humjui Chenge - laiti ungemjua na madudu yake yooooote, usingethubutu kusema hivyo. We acha tu..!!!
 
toleola25.jpg
 

Attachments

Mkuu nakurekebisha
Chenge alipewa hizo $1.5 million na yeye akampa Dr Rashid $600,000 ambazo amedai alimkopesha kufanya biashara ya fenicha
Sasa huu si upuuzi mtupu pesa yote kapata muhindi na heshima wamepoteza wao
Chenge kama asingefanya huu utaahira angefika mbali sana kwani CCM wanamtegemea kwamambo mengi sana

Huyu anatia aibu kwa Wanyantuzu wote, jituzima linazidiwa akili na watoto? Chenge kazaliwa 1946 kamzidi Tanil K C Somaiya (1965) miaka 19, wakati Shailesh P Vithlani (1964) kamzidi miaka 18, ukisema shule ndio kabisaaaaa wale jamaa ni teee! sasa nini haswa kilimsukuma bar******i huyu kubakwa akili na watoto zake?
 
Utamaduni wa kuwajibika Afrika bado ni ndoto kubwa.

Juzi nilisikia kuna mteule mmoja wa Obama amekataa uteuzi kwa sababu eti alichelewa kulipa kodi. Nilitamani sana utamaduni kama huu ungekuwapo huku kwetu Afrika. Lakini shida ni nani atabaki!
 
Nilitamani sana utamaduni kama huu ungekuwapo huku kwetu Afrika. Lakini shida ni nani atabaki!

- Huu ni wakati muafaka kwa wasomi, wana-dini, na viongozi wetu wa siasa kukaa chini na kujaribu kutafakari kwa makini, kwa sababu sio siri kwamba taifa letu limekumbwa na crisis kubwa sana ya character, Mwalimu alitupatia national ID basi lakini nationally kwenye character kwa maoni yangu tume-fail miserably.

- Sisi wananchi ni waongo, I mean taifa zima ni waongo, wezi, waumini wa uchawi, wanafiki, halafu masikini ya Mungu tunategemea viongozi wetu wa siasa wawe tofauti na sisi wananchi, it does not work tumekwama maana sasa nani wa kumfunga kengele paka?

- Hili ni taifa gani ambalo wote tumeharibikiwa?
 
-- Sisi wananchi ni waongo, I mean taifa zima ni waongo, wezi, waumini wa uchawi, wanafiki, halafu masikini ya Mungu tunategemea viongozi wetu wa siasa wawe tofauti na sisi wananchi, it does not work tumekwama maana sasa nani wa kumfunga kengele paka? - Hili ni taifa gani ambalo wote tumeharibikiwa?

Hapo umesema FMES. Tuna tatizo kubwa sana. Wengine tulishasema toka mwanzo kwamba mfumo wetu utawala ni mbovu. Huwezi kuwa na mfumo wa kiwizi-wizi halafu utegemee watu wasiwe wezi. Nchi hii utapeli kwa kwenda mbele, wabunge wanaopiga kelele wengi wao wamehonga ili wazipate nafasi. Rais anachaguliwa baada ya kuhonga vitu kama khanga na kadhalika. Watu wakipata madaraka wanachagua rafiki zao. Hivi ulishawahi kusikia wapi Waziri anazunguka Mikoani kutangaza uzuri wa bajeti ya serikali. Kwani bajeti ya serikali imekuwa magonjwa mabaya yanayohitaji kampeni za viongozi?


Ndiyo maana wenzio toka mwanzo tulishasema hata hao wanaomshikia bango Mkapa kwamba wakamwondolee kinga ni wanafiki tu. Maana kama wangekuwa wako makini kweli basi wangeangalia jinsi watu wanavyogawana vyeo ili kuibia nchi hii.

Sasa suala la rada lilishaanza toka mwaka 1992 wakati wa Mzee Ruksa. Huyo Dr Idrisa wengine humu walimsifia sana tu.
 
Sisi wananchi ni waongo, I mean taifa zima ni waongo, wezi, waumini wa uchawi, wanafiki, halafu masikini ya Mungu tunategemea viongozi wetu wa siasa wawe tofauti na sisi wananchi, it does not work tumekwama maana sasa nani wa kumfunga kengele paka?

then what next?

Mimi nadhani tunahitaji viongozi waliotofauti na sifa ulizotaja ili wawezi kuliondoa Taifa kwenye hili bwawa la matatizo. Its true kwamba tatizo letu kubwa lipo kwenye fikra. most of Tanzanians are opportunists, but we must get out of this pool. Tusikate tamaa, tupige moyo konde.
 
Mkuu Mwenzangu FMES,

Nchii ilianza kuangakuka Pale viongozi walipoamua kuwa matajiri kupitia Vyeo vyao walivyopewa. Dhambi hii ilianzishwa na wachache na wengine wakaamua kuifuata kwa kuogopa kuchekwa wakimaliza uongozi wao serikalini. Serikalini hakuna Maadili hata kidogo, kila mtu anajiona yeye ana uwezo wa kimaamuzi kuliko mtu yeyote.

Nchi ilianza kupotea pale Wafanyakazi wa Umma waliopoanza kuajiriana kutokana na ukabila,Udini na ukanda. Hii ilichangai kuvunja maadili na miiko ya Uongozi sababu kila mtu ana mtu nyuma yake... Hata Masha ana mtu nyuma yake kwa sasa!

Watu wa kulaumiwa katika hili,mmoja wapo na Mamvi nd ndiyo maana Mwalimu alikuwa akimpinga,Huyu ndiye aliyeonesha kuwa unaweza ukawa Tajiri kupitia Uongozi.Kinachoniuma ni hawa wachungaji na maaskofu kumkumbatia huyu mwenye historia chafu na asliyeshindwa kujisafisha mbele ya Mwalimu na waumini wote wa kitanzania.

Nakubaliana na maneno ya Zitto Kabwe kuwa Kunahitajika suluhisho la kitaifa katika mambo yahusuyo Nchi hii na wala siyo chama cha siasa.

Mzee Mwanakijiji umenena!
 
Lakini shida ni nani atabaki!
Kama wote wanaisha basi na waishe.... (ila bado naamini kuna waadilifu japo wachache).
Tatizo letu la misingi ni kwamba wale ambao wameshajneemesha (isivyo halali) hawataki kuondoka kwa hiari yao....wamejijengea mizizi mirefu na imara kwenye ngazi zote za utawala, kwa kutumia yao isiyo neema halali!
Watu wakiamua kuing'oa mizizi yao wanaweza, japo yaweza kuchukua muda mrefu.
 

Nakubaliana na maneno ya Zitto Kabwe kuwa Kunahitajika suluhisho la kitaifa katika mambo yahusuyo Nchi hii na wala siyo chama cha siasa.

Wakuu kwa kadri ya uelewa wangu SULUHU ni makubaliano hasa kwa pande mbili zinazokinzana(tofautiana) sasa mheshimiwa Zito alimaanisha nini ktk hili?

-Je kuna makundi yaliyofalakana kwenye jamii yetu? kama ndio yapi?
-Je bila vyama vya siasa suluhu hii itapatikana kwa njia gani?
-Nani mwakilishi wa makundi yaliyofalakana ktk majadiliano ya kutafuta suluhu?
-Nani mwenye jukumu la kuanzisha mchakato wa kutafuta suluhu?

Kama nimepotea maana ya neno hilo niko tayari kusahihishwa (Tuvumiliane Kiswahili kigumu jamani..!)
 
Back
Top Bottom