The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Hivi karibuni Chenge aliondoka nchini kuelekea Uingereza na tayari amesharejea nchini.

Sawa sawa, ina maana dataz zetu zilikuwa ni za kweli, maana ni vyema tuka-maintain credibility kwanza ya Forum, halafu kwetu sisi watoa dataz kwa sababu tulizitolea hapa hizi dataz na tukashambuliwa kama kawaida, sasa ukweli ni huu hapa juu, ahsante Mkuu Bubu kwa hii article!

Wakuu samahani kidogo kwa kutoka nje ya mada, ili tu kukumbushana kidogo.

JF mbele zaidi!
 
They intend to do nothing kuusiana na EPA, ndo maana hata mkapa amekuja juu na ksema anasingiziwa kwa kuwa tayari balali ameshakufa, mzee wa vijisenti hawataweza kumshitaki hata kama ushaidi wa kutosha upo.

Wakimwaga mboga yeye anamwaga ugari.
 
They have to do something about EPA. Ama sivyo zile millioni zilizoahidiwa na Bush zitakamatwa na Congress ya Marekani. Tayari wanazo data za EPA.
 
Hivi mnakumbuka alichosema Ballali alipoitisha waandishi wa habari siku ile... linganisheni na anachosema Mkapa leo... zafanana!
 
Ikulu: Ni kazi kubwa kumchunguza Chenge

Hakuna pesa inayoimgia Bank yoyote bila kuwa documented sasa hiyo kazi kubwa iko wapi? Hata ukiweka paundi moja lazima inakuwa na risiti na kuonyesha umeiweka kwa njia gani check au cash.

Serikali ya CCM inayumbayumba badala ya kufanya kweli na kuwashughulikia hawa MAFISADI.
 
Mkuu Wabunge wengi wanasema kuwa kwenye bajeti ijayo itakuwa ni EPA kwanza, halafu mengine!

Mkuu, hawa wabunge wa CCM mimi siwaamini hata kidogo. Kikao kilichopita tuliambiwa Bungeni kutawaka moto kuhusiana na ripoti ya Richmond na kama unavyojua hakukuwaka moto wowote! wameweka mbele matumbo yao na maslahi ya chama cha mafisadi. Hivyo tusubiri labda safari hii watafanya kweli, lakini ukiangalia trends za bunge la CCM sidhani kama kutakuwa na jipya.
 
Hivi mnakumbuka alichosema Ballali alipoitisha waandishi wa habari siku ile... linganisheni na anachosema Mkapa leo... zafanana!

Masikini Makapa maji baada ya kufika shingoni ameamua kutoa sauti sasa. Nafikiri ameisha jua mvua inayotaka kumunyeshea. Hivi huyu waziri simba anataka kutwambia hatuna serikali?
 
Hivi mnakumbuka alichosema Ballali alipoitisha waandishi wa habari siku ile... linganisheni na anachosema Mkapa leo... zafanana!

...aisee nakumbuka kwa mbaali kidogo kuwa.......Balali naye alisema, watu wenye chuki/wivu kwa kuwa hakuwapendelea kuwapa...........something!!

....dugu moja hawa kwani ulikuwa hujui Mwanakijiji?!!
 
Hakuna pesa inayoimgia Bank yoyote bila kuwa documented sasa hiyo kazi kubwa iko wapi? Hata ukiweka paundi moja lazima inakuwa na risiti na kuonyesha umeiweka kwa njia gani check au cash.

Serikali ya CCM inayumbayumba badala ya kufanya kweli na kuwashughulikia hawa MAFISADI.

Mkuu,

Pitiapitia ujue kwa uzuri kuhusu kisiwa cha Jersey na uwe na ufahamu kwamba ni kwanini watu wanaweka fwedha zao huko.

Hasa kuhusu uchumi wa Jersey.
 
Naona tangu Tina asema anataka kumpa Lowassa raha basi kila mtu ameanza kuwa ndugu; sasa na mimi kwanini nijivunge? Tina miye ni yule binamu yako wa mbali... sasa tuwasiliane tuone jinsi gani tunaweza kuhakikisha habari za EL zinaifikia jamii! Eh Tina, umenisikia? Mkakati wako ni mzuri sana.


Kwa hiyo Mkjj,Shy pia ndugu yako wa karibu? Duh,maanake Tina mdogo'ake Shy
 
Naona tangu Tina asema anataka kumpa Lowassa raha basi kila mtu ameanza kuwa ndugu; sasa na mimi kwanini nijivunge? Tina miye ni yule binamu yako wa mbali... sasa tuwasiliane tuone jinsi gani tunaweza kuhakikisha habari za EL zinaifikia jamii! Eh Tina, umenisikia? Mkakati wako ni mzuri sana.


kwi kwi kwi kwi... sasa kwa mtindo wako EL ndo kabsaa atamkimbia Tina, bora useme mtapanga mikakati ya kusafishia jina af akiingia line ndo muanze kazi
 
Sawa sawa, ina maana dataz zetu zilikuwa ni za kweli, maana ni vyema tuka-maintain credibility kwanza ya Forum, halafu kwetu sisi watoa dataz kwa sababu tulizitolea hapa hizi dataz na tukashambuliwa kama kawaida, sasa ukweli ni huu hapa juu, ahsante Mkuu Bubu kwa hii article!

Wakuu samahani kidogo kwa kutoka nje ya mada, ili tu kukumbushana kidogo.

JF mbele zaidi!


Mkuu heshima mbele

Nilisema hapa lkn kuwa Jamaa nimemuona G8, ikawa tabu kidogo
 
"Lakini kuna mtu nimemwambia, labda kauza ng'ombe wao wote ndio alipata hizo pesa, au ana biashara nyingine," alisema Waziri Simba.

Hii yote ni maandalizi ya majibu rahisi rahisi kama kawaida, juu ya uchunguzi, majibu yamekaa kutetea tetea tuu...

Hii nchi sijui nisemeje?
 
Huyu mama sijui huwa anaongea nini, atajitafutia matatizo bure kwa kauli zisizo na mbele wa nyumba. Nina wasi wasi na kiwango chake cha elimu. Simba angalia ohooooooo
 
Mkuu Wabunge wengi wanasema kuwa kwenye bajeti ijayo itakuwa ni EPA kwanza, halafu mengine!

Habunge wakiendeleza cheche zao kama kwenye Richmond, hata mafisadi wakiendelea kutoa kafara haitasaidia. Hatimaye hata wananchi wa Monduli, Bariadi na Masasi watawazomea badala ya kuwashangilia. Serikali italazimika tu kutumia 'Ukulu' wake
 
Mlipueni na fisadi Mkapa na mafisadi wengine wote wanaohusika na wizi wa shilingi bilioni 288 toka BOT, badala ya kumlipua fisadi mmoja mmoja

Posted Date::5/30/2008
Wabunge wa CCM kumjadili aliyekuwa waziri Chenge
*Ni kuhusu tuhuma za kumiliki mabilioni,wajipanga kumlipua bungeni

Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi

TUHUMA zinazomkabili Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge kuhusiana na mabilioni ya shilingi aliyoyaficha kwenyea akaunti yake moja katika Kisiwa cha Jersey, zinatarajiwa kutikisa Kamati ya Uongozi ya Chama hicho bungeni.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo gazeti hii limezitapata, Kamati ya Uongozi ya CCM bungeni inayoundwa na wajumbe wote wa Kamati Kuu (CC), akiwemo Waziri Mkuu intakutana mara baada ya Mkutano wa Bunge la bajeti kuanza mjini Dodoma Juni 11, mwaka huu kujadili masuala kadhaa likiwemo la tuhuma za Chenge kuficha fedha nje ya nchi.

Taarifa hizo zinadai kuwa baadhi ya wajumbe hao pamoja na kusubiri matokeo ya uchunguzi Taasisi ya Kuchunguza, Kukamata na Kufungua Mashitaka ya Makosa Makubwa ya Jinai (Serious Fraud Office) ya Uingereza, watataka kujua Chenge aliztoa wapi Sh1.2 bilioni.

Inadaiwa kuwa wabunge pia wamekerwa na kauli alizota Chenge kabla ya kujiuzulu kwani alionekana kufanya hivyo baada ya shinikizo kubwa ikiwemo la vyombo vya habari.

Taarifa hizo ziliongeza kwamba, baadhi ya wabunge hao wanahoji kwamba, inawezekana vipi mtu ambaye alikuwa mtumishi wa umma ajilimbikizie kiasi hicho kikubwa cha fedha katika akaunti moja, tena ya kificho.

Chanzo hicho habari kilifahamisha kwamba, baadhi ya wabunge watasubiri hotuba ya Waziri Mkuu, kuona kama atagusia suala hilo ama la.

''Wabunge wanataka kujua vipi mtu aliyekumbwa na tuhuma nzito za ufisadi ajiuzulu kwa shinikizo,'' kilisema chanzo hicho na kuongeza:,

''Hadi aandikwe sana na magazeti ndiyo afikirie kujiuzulu. Mimi ni mmoja wa wabunge watakaotumia jukwaa hilo kumlipua,'' alisema Mbunge mmoja kwa sharti la kutotaja jina.

Mbunge huyo ambaye siku za karibuni amejijengea umaarufu mkubwa kwa kukemea ufisadi kwa nguvu akiwa bungeni, alisema haiwezekani suala la Chenge likaasha kimya kimya.

Kwa nyakati tofauti, baadhi ya wabunge ambao wanaonekana kuwa wakali bungeni katika mambo ya ufisadi, walipoulizwa katika ofisi ndogo za Bunge, jijini Dar es Salaam jana, walithibitisha kuwa jukwaa lao ni bungeni.

"Mimi siwezi kuzungumzia suala hili juu juu, nina 'forum' (jukwaa) ambayo ni Bunge, hivyo tusubiri, lakini nitamlipua," alisema Mbunge mmoja ambaye hakutaka kutaja jina lake litajwe gazeni.

Hilo likitarajiwa kutikisa kamati hiyo na hata baadhi ya wabunge kupanga kumlipua Chenge bungeni, Gavana wa Benki Kuu (BoT) Profesa Benno Ndulu, aliliambia gazeti hili, jana kwamba benki hiyo inasimamia sheria kuhusu uwekaji fedha nje si mtu.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa CCM, ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo, Kapteni John Chiligati, alimtaka mwandishi awasiliane na Katibu wa Kamati hiyo, Ali Ameir Mohamed ambaye ni Mbunge wa Donge (CCM).

"Mimi ni mjumbe tu sijajua ajenda za kamati katika mkutano huu kamati hiyo, ni vema ukamuuliza Katibu wake ambaye ni Ali Ameir," alisema Chiligati.

Alipoulizwa kwamba, kuwa anachukuliaje suala hilo na uwezekano wa kulifikisha katika kamati hiyo, alijibu tena, " nafikiri Katibu ndiye anayejua hilo."

Naye Ameir, alipoulizwa alisema hadi sasa hakuna ajenda kikao hicho iliyoandaliwa kwani kwa utaratibu wa sasa, kikao pia kinategemea mapendekezo kutoka kwa wajumbe.

"Hadi sasa sijaanda ajenda hata moja, ajenda zetu sasa hivi pia zinatokana na mapendekezo ya wajumbe wa kamati na tunatarajia kukutana baada ya kuanza mkutano wa Bunge mjini Dodoma," alisema na kuongeza

"Ajenda ya mjumbe ikifika hapa huangaliwa na ikikubalika hujadiliwa ndani ya kamati".

Alifahamisha kwamba, baada ya kamati ya uongozi kupitisha, ajenda hupelekwa kwa wabunge wote wa CCM.

Wakati Ameir na Chiligati wakisema hivyo, duru kutoka ndani ya kamati hiyo, zilisema sakata la Chenge ambaye pia ni mjumbe wa CC limegusa baadhi ya wajumbe wa kamati na wabunge wengine wa CCM ambao wanataka lijadiliwe kwa kina.

Hayo yakiwa ndani ya CCM, Gavana wa Benki Kuu (BoT) Profesa Ndulu alifafanua kwamba Bbenki inasimamia sheria na si kumjadili Chenge.

Alisema hadi sasa suala la Chenge linachunguzwa na kuongeza kwamba, BoT haiwezi kumjadili mtu badala ya kusimamia sheria.

"Sisi tunasimamia sheria, hatuangalii mtu mtu akibainika hatumjadili yeye bali sheria, sasa hili suala jana (juzi) tumelizungumza kisheria lakini watu wanataka kujadili mtu, kuna uchunguzi unafanyika,"alisema Ndulu.

Chenge ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kwa miaka kumi na kujiuzulu akiwa Waziri wa Miundombinu, anachunguzwa na SFO kuona kama Sh1.2 bilioni anazomiliki kisiwani Jersey, zina uhusiano na ununuzi tata wa rada.

SFO inamchunguza Chenge kuona kama mabilioni hayo ambayo mwenyewe huita 'vijisenti', yana uhusiano na biashara ya kifisadi ya rada kati ya Kampuni ya BAE System na serikali ya Tanzania katika kipindi cha mwaka 2002.

Hata hivyo, mwenyewe alisema ni vema watu wakasubiri uchunguzi wa SFO ambao sasa uko katika hatua za mwisho.
 
Back
Top Bottom