The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Taratibu Naona Mwanga Wa Ukombozi Kwani Wananchi Wakianza Kuhoji Viongozi Wao Basi Hapo Jua Nchi Inaanza Kupata Mwanga Wa Kuelekea Mbele.

Chitalilo Ajue Kuwa Watanzania Sio Wendawazimu Haiwezekani Akatamka Maneno Machafu Kama Yale Eti Chenge Kavunja Mlango Wa Nani ...alitumwa Na Wananchi Gani Wakati Alivuta Kitu Kidogo Kutoka Kwa Mafisadi Ili Awatetee?
 
Kwanza hao wananchi anaosema wamempongeza wako wapi? Ni wangapi? Si anaweza kuamka tu na kusema 'wananchi' wamempongeza. Upumbavu mtupu huo.
 
Hivi huyu mpuuzi sell-out si ndio yule ambaye alikuwa na kashfa ya kugushi vyeti vya shule? By looking at his profile i do not understand how this guy was elected to represent anyone. Hana shule na hata ile aliyojaribu kusoma alishindwa kumaliza. Na sasa amenunuliwa na mafisadi anajaribu kuwatetea. Watu wa aina hii ndio wanafaa wananing'inizwa by their "balls" and allow people to stone or beat him like crazy that he is.

Here is his sh-t of a profile:

http://www.parliament.go.tz/bunge/Mp_Cv3.asp?PTerm=2005-2010&fpkey=75&vusername=GUEST")
 
Yaani li-nchi letu na huyu kaka yetu mkubwa ni komedi tupu, yaani tumeenda msalani halafu tunatoka bila kutawaza (kunawa) halafu tunakauka ati hakuna mtu atajua kuwa hatukunawa. Sasa inakuwa issue maana harufu inaanza kutoka na nzi wanapitapita sana, mwisho anatokea mtu kukwambia unanuka, hizi ni akili kweli? Sasa JK atatueleza lipi juu ya huyu mtuhumiwa ambaye siku nyingi amemng'ang'ani kwamba he is clean na kumrudisha serikalini several times kama mtu unavyorudia kupiga muhuri wa wizi kwa uangalifu ati kuhakikisha kuwa hautagundulika ni wa wizi? Mola tuangalizie nchi yetu maana kwa sasa walioibeba washazidiwa na uzito wake na wanatamani kuiweka chini wakimbie kama ingewezekana. Sisi hapa JF tukaze mwendo maana nishaona JF iko effective ki-sawasawa na hata big potatoes wanaiogopa mno. Tukaze mwendo tutafika siku si nyingi kwenye ukombozi wa taifa hili tulilonyang'anya wakoloni na kuwapatia manyapara wachache weusi na weupe wa huko kutokea Asia.
 
Yaani li-nchi letu na huyu kaka yetu mkubwa ni komedi tupu, yaani tumeenda msalani halafu tunatoka bila kutawaza (kunawa) halafu tunakauka ati hakuna mtu atajua kuwa hatukunawa. Sasa inakuwa issue maana harufu inaanza kutoka na nzi wanapitapita sana, mwisho anatokea mtu kukwambia unanuka, hizi ni akili kweli? Sasa JK atatueleza lipi juu ya huyu mtuhumiwa ambaye siku nyingi amemng'ang'ani kwamba he is clean na kumrudisha serikalini several times kama mtu unavyorudia kupiga muhuri wa wizi kwa uangalifu ati kuhakikisha kuwa hautagundulika ni wa wizi? Mola tuangalizie nchi yetu maana kwa sasa walioibeba washazidiwa na uzito wake na wanatamani kuiweka chini wakimbie kama ingewezekana. Sisi hapa JF tukaze mwendo maana nishaona JF iko effective ki-sawasawa na hata big potatoes wanaiogopa mno. Tukaze mwendo tutafika siku si nyingi kwenye ukombozi wa taifa hili tulilonyang'anya wakoloni na kuwapatia manyapara wachache weusi na weupe wa huko kutokea Asia.


Tumeaka kutoka kwenye usingizi mzito, Mapinduzi yameshaanza. They can run but they cant hide! This is a new world. Ni zamu yamu kulazwa sasa...
 
Haya ni matokeo ya kutosikilizwa Bunge kwani mbali ya makelele ya wabunge serikali ilitumia mabavu. Angalau sasa tangu kuingia JK wabunge wanasikilizwa na serikali imeanza kujifunza kuwa kuwa watu wanafatilia uozo unaofanyika serikalini.
 
Haya ni matokeo ya kutosikilizwa Bunge kwani mbali ya makelele ya wabunge serikali ilitumia mabavu. Angalau sasa tangu kuingia JK wabunge wanasikilizwa na serikali imeanza kujifunza kuwa kuwa watu wanafatilia uozo unaofanyika serikalini.
Na hasa hawa huyu Mkapa pamoja na mazuri machache aliyoyafanya alijifanya yeye ndiyo Tanzania na Tanzania ndiyo yeye kwa kuminya demokrasia na kuwatisha watu wasihoji lolote katika serikali yake. Wakati huo huo akijifanya kuna kitu kinaitwa utawala bora kumbe ulikuwa bora utawala.
 
Swiss continue with probe of radar supplier company

THISDAY REPORTER & AGENCIES
Dar es Salaam

SWISS authorities have widened a corruption probe linked to suspicious deals by the British arms manufacturing company BAE Systems Plc, which supplied the highly controversial 70bn/- military radar system to Tanzania.

Federal prosecutors are now conducting three criminal investigations into possible money laundering by BAE Systems, spokeswoman Jeannette Balmer said in the Switzerland city of Bern yesterday.

Previously, prosecutors had confirmed only one probe and Balmer declined to comment on what prompted Swiss authorities to open two additional investigations.

The investigations centre on allegations that BAE used Swiss bank accounts to pay millions of pounds (dollars) in bribes to officials from Saudi Arabia in return for contracts.

An investigation by Britain’s Serious Fraud Office (SFO) was halted in late 2006 after the Saudi Arabian government threatened to withhold cooperation on critical issues of anti-terrorism.

Britain’s House of Lords is now considering whether the SFO was right to end its own probe after the High Court ruled in April this year that the move had been an ’’abject surrender’’ to ’’blatant threats.’’

According to Balmer, Swiss prosecutors were alerted to possible wrongdoing on BAE’s part by the Swiss money-laundering authority.

She declined to say whether money linked to the probe has been frozen in Swiss accounts.

A British request for Swiss legal assistance in the case was put on hold in 2006 after the Serious Fraud Office called off its inquiry. The request has not been formally withdrawn.

Separate requests from the SFO for legal assistance into possible BAE bribes to Tanzania, Romania, Chile and the Czech Republic are still active, Balmer said.

Some of the requests have been decided upon but can still be appealed, she added, but declined to elaborate.

The United States has also expressed an interest in gaining insight into the Swiss bank accounts that BAE allegedly used to run a 60-million pound ($120m) ’slush fund’, offering sweeteners to Saudi officials in return for lucrative contracts as part of the Al-Yamamah � or ’dove’ � arms deal in the 1980s.

BAE has always said it acted lawfully.

The US request last year has not yet been acted upon because it was not specific enough, said Rudolf Wyss, deputy director of the Swiss justice ministry. Washington has not been in touch about the matter since, he said.

BAE Systems has long been under investigation over alleged corruption in the dubious sale of the air traffic control and radar system to former president Benjamin Mkapa’s government in 2002.

The radar deal was opposed by civil society in Tanzania and various international actors including the former UK Secretary of State for International Development, Clare Short.

It is understood that an intermediary, Shailesh Vithlani, was the agent behind the radar deal who arranged for $12m (approx. 15bn/-) to be secretly paid by BAE Systems into a Swiss bank account in return for the purchase by the Tanzanian government of the overpriced military radar.

Vithlani, born and bred in Tanzania of Asian ethnicity, but now said to be a British citizen, remains at large despite an international arrest warrant being issued against him by a Dar es Salaam court on charges of perjury and lying to an investigating officer on the radar deal.

Otherwise, although local investigations by the Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB) on the radar deal are understood to have already reached an advanced stage, there have been no prosecutions to date.
 
Kumbe Dr Idris Rashid naye ana vijisenti vya mgao wa radar nje (uk)?! soma MwanHalisi la leo
 
Last edited:
mtando wa ufisadi hapa nchini ni mkubwa kuliko vile tunavyodhani.
 
Sio msafi kama watu walivyomfikiria wakati anaingia TANESCO na yeye ni mmoja wao pia.
 
Swahiba wa Kikwete ahusishwa na rada
Anamiliki akaunti Uingeleza
Hosea adaiwa kuvujisha siri

Na Saed Kunbenea

Mteule na swahiba wa Rais Jakaya Kikwete amehusishw an kashfa ya ununuzi wa rada inayochunguzwa na makachero wa Uingereza.

Ni Dk. Idrisa Rashidi, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme nchini (Tanesco ) ambaye wakati wa machakato wa ununuzi wa rada alikuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT).

Kwa mujibu wa taarifa za Shirika la Uchunguzi wa Makosa ya Jinai - Serious Fraud Office (SFO) la Uingereza, Dk. Rashidi in mmoja wa watuhumiwa wa ufisadi katika ununuzi wa rada iliyogharimu kiasi cha sh. 40 bilioni.

SFO inachunguza ununuzi wa rada uliofanywa na serikali ya Tanzania kutoka kampuni ya BAE System-PLC ya nchini Uingereza.

Shirika hilo linadai kuwa bei ya rada ilikuwa kubwa kuliko thamani yake na kwamba BAE itakuwa ililipa mawakala kiasi kikubwa cha fedha "kukainisha" baadhi ya viongozi wa serikali ili wakubali bei hiyo.

Dk. Rashidi aliteuliwa na Rais Kikwete Novemba 2006 kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco Mwaka mmoja baadaye, Dk. Rashid aliandika barua ya kujiuzulu lakini rais alimkatalia kujiuzulu.

Uamuzi wa Dk. Rashidi kujiuzulu ulitokana na kile alichoita kuamrishwa na Edward Lowasa, aliyekuwa waziri mkuu, kurudisha umeme aliokuwa ameamua ukatwe, katika kiwand cha Tanga Cement, jambo ambalo Dk. Rashidi alilichukulia kuwa uingiliaji wa kazi na udhalilishaji.

Hata hivyo , siku mbili baada ya Dk. Rashidi kuandika barua ya kujiuzulu, taarifa kutoka serikalini zilisema, Rais Kikwete aliingilia kati na kukataa barua ya Dk. Rashidi ya kujiuzulu.

Badala yake, rais alisema yeyote anayetumia umeme bila kulipa ni mwizi wa umeme, hata kama mutumiaji ni ikulu au jeshi. Alisema anayetumia nishati hiyo sharti alipe na kama hakulipa, aswagwe mahakamani.

Taarifa za kuaminika zinasema Dk. Rashidi anamiliki kampuni yenye akaunti nchini Uingereza na kwamba kampuni yake ilimegewa. Paundi 600,000 za Uingereza (sawa na Sh. 1.32 billion) kutoka akaunti ya kampuni ya Andrew Chenge ambaye tayari anachunguzwa na SFO.

Taarifa za kampuni ya Siemens Plessey System (SPS) zinasema, Dk. Rashidi anatajwa kuwa maratibu mkuu wa "taarifa zote kutoka serikali na BoT." SPS ndio walihusika kufanya majadiliano ya awali ya ununuzi wa rada hiyo kwa niaba ya Serikali, chini ya ofisa wake aliyetajwa kuwa ni jonathan Joseph Horne.

MwanaHALISI imeona dokezo la Horne lililoeleza majukumu ya Dk. Rashidi ambalo lilisomeka kwa Kiingereza, Dk. Rashidi will from now on act as cooridnating point for collecting all documents (etc) from all parties in the Government of Tanzania and Bank of Tanzania.

Mwaka 1992 hadi 1998, Dk. Rashidi alikuwa Gavana wa BoT. Ni wakati alipewa jukumu la kuwa " kiungo muhimu kwa wadau wote ndani ya serikali na BoT," kama maelezo ya Kiingereza hapo juu yanavyoeleza.

Akaunti ya Chenge inayochunguzwa iko katika tawi la benki ya Barclays, katika kisiwa cha Jersey wakati ile ya Dk. Rashidi, imo Royal Bank of Scotland International katika kisiwa hicho hicho.

Kampuni ya Chenge imefahamika kuwa hi Fronton Investment Ltd na ile ya Dk. Rashidi imetajwa kuwa ni Langley Investment Ltd.

Uhamishaji wa fedha umerekodiwa kufanyika 20 September, 1999.

SFO inadai kuwa BAE System PLC, kampuni ya Uingereza inayotengeneza vifaa vya kijeshi, ilitoa asilimia 30 ya bei ya mauzo kwa wakala wake kwa shabaha ya, miongoni mwake, kuhonga maofisa wa serikali nchini.

Hadi kukamilika kwa mradi huo, Tanzania ilikuwa inatumia mafanyabiashara raia wa Tanzania mwenye asili ya ya Kiasia, Shailesh Pragji Vithlani badal ya SPS waloianzisha mchakato.

Ingawa mchakato wa ununuzi wa rada ulianza mwaka 1992, kufuatana na rekodi za SFO, mkataba ulikamilika mwaka 1999. Wakati huo Chenge alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

MwanaHALISI limefahamishwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Dk. Edward Hoseah alisaliti serikali kwa kuvujisha taarifa kwa Chenge na Dk. Rashidi.

Imefahamika kwamba taarifa za SFO kutaka kuwahoji Chenge na Rashidi kwa pamoja zilivujishwa na Hoseah na kuwezesha watuhumiwa kukutana. Hiyo ilikuwa baada ya mawasiliano kati ya SFO na mwanasheria Mkuu wa serikali Johson Mwanyika ya 31 March Mwaka huu.

Ni mkakati huo wa chenge na Dk. Rashidi unaodaiwa kuzaa maelezo kwa makachero wa SFO kuwa fedha ambazo Dk. Rashidi alipokea kutoka kwa Chenge zilikuwa "mkopo wa kuendeleza biashara yake ya samani (fenicha)."

Mawasiliano kati ya SFO na Mwanyika kuhusu kuwahoji Dk. Rashidi na Chenge, yalionyesha pia kuwa yatahusisha mahojiano na Shailesha Pragji Vithlani, Tanil Kurmar Chandulal Somaiya, BAE System ya London, Michael Peter Rouse, Sir Richard Harry Evans, Michael John Turner na Julia Aldredge.

Chenge alihojiwa na SFO mapema mwaka huu baada ya akaunti yake iliyoko Jersey kukutwa na fedha nyingi. kufuatia upekuzi ofisini na nyumbani kwake na kuchukua nyaraka kadhaa, Chenge alilazimika kujiuzulu nafasi ya Waziri wa Miundombinu ili kupisha uchunguzi.

Taarifa nyingine zimesema hadi 13 Septemba 2006, akaunti ya Chenge ya kampuni ya Fronton Investment Ltd, inayomilikiwa na Chenge na mkewe, ilikuwa paundi za uingereza 804,000/= (sawa na Sh. 1.7 bilion).

Kwa mazingira ya sasa, ama Dk. Rashidi ambaye alikuwa gavana wa BoT. afuate nyayo za Chenge na kujiuzulu au asubiri uamuzi wa rais ambao hauwezi kuwa tofauti na ule aliochukua dhidi ya Daudi Ballali.
 
Duh, nmeshtuka kweli, hata huyu? Yaani kumbe nchi hii haina mtu msafi na ndo maana hata vita dhidi ya ufisadi inakuwa ngumu
 
Mambo haya ni mazito! Nchi hii ilipaswa kuwa tajiri sana kama ingekuwa siyo kwa CCM kukumbatia mafisadi.
 
Duh, nmeshtuka kweli, hata huyu? Yaani kumbe nchi hii haina mtu msafi na ndo maana hata vita dhidi ya ufisadi inakuwa ngumu

Yupo mmoja tu! Johnson Mwanyika........ aliwapa challenge waandishi wa habari na wameshindwa kumpata na dosari.
 
Mengine hayooooo........................
kwi kwi.......................
 
Back
Top Bottom