The Radar Scandal: Investigation & Progress

The Radar Scandal: Investigation & Progress

Je tunaweza kupiga ngoma na kucheza kuwa wakati wa mafisadi umefika? maana naona list inaongezeka kila siku, bado baba yao che nkapa.
 
Tina mdogo wangu

Katika ushauri!! wengi wamekupotosha hapo juu. Kwamba utafanya nini ama kwamba unataka moyoni kufanyaje na huyo Master mind wa MAFISADI hiyo si rahisi inihusu sana. Ila kuwa macho yawezekana yeye si fisadi wa fedha tu hata mengine. Mhhh miye naogopa miye Asijekopwa mtoto wa mtu akanililia bure.

Ninafikiri utusaidie jambo moja huku nyumbani. Hebu fuatilia shuku aliyoitoa SHY. Halafu ututaarifu matokeo yajke tafadhali.
 
Tina mwanangu mkamue huyo babu mpaka achanganyikiwe. Mie naona hivyo vijisenti bora awekeze kwako kuliko kuvipeleka ktk kile kijisiwa cha Chenge. au mbaya zaidi kama alivyofanya balaa huko malikani ambaoko kachimbia vijisenti huko ughaibuni. lakini usisahau kuchangia Forum yetu kwi kwi kwi vingine tutakuita FISADI kwi kwi kwi kwi kwi kwi!!!!""##$$%&&('())
 
Ukienda kwenye topic ya Chenge hayawi hayawi yamekua, nilisema toka last week kuwa Chenge ndiye aliyetangulia huko London, baadaye Rostam na Karamagi, walifuatia, na kisha Lowassa naye akatinga huko London kwenye the same ishu nijuavyo mimi, isipokuwa kuna chombo kimojakilinionya kuacha kuweka dataz zaidi on the ishu.

duh was jus readin kama gazeti lakini nilipoona hiyo listi ya waliokuja huko uk..kama ni kweli je ni kwa fweza zao ama ndo hivyo tena jasho letulatumika kuwasafirisha na accomodate them kipindi choote wakiwa huko?
 
Hivi wana JF walioko huko London hamwezi kuwa tip mapapparazi ili wapigwe picha hayo jamaa wakiwa huko? kama walivyofanyiaga mke wa Mugabe
 
Somaiya Yule Chakaramu Wa Kenya ?

No jina kamili ni TANIL SOMAIYA, mmiliki wa SHIVACON, INCAR,ULTIMATE SECURITY na makao yake makuu yatakuwa hapo jengo la zamani la WFP lililoko barabara ya Ali HAssan Mwinyi maana ndo kalinunua hili jengo
 
Tina Wangu umekimbilia wapi mdogo wangu mbona unaanzisha mada halafu unakimbia ? Hivi kumbe siku hizi unaishi Uingereza Nilifikiri bado uko Kwa bush

Duh,naona umekua king'ang'anizi kweli.Na kama ulijilazimisha kwa polisi hivyo tena basi ni kaazi kweli kweli.


Tina si umalizane na huyu Shy kwanza? Maanake anatia huruma mno!
 
Jamani nimemuona Chenge jmosi usiku pale G8(Bar) kinondoni, wakati mi naingia (kwenye saa tano usiku) yeye ndo alikuwa anaondoka na kumwana mmoja (sikuweza kujua kama ndo huyo mkewe mpya au vp) kamwaga ofa pale halafu akaanza, UK kaja lini, au hii post imetumwa hapa lini.... nisije nikawa nyuma na wakati

Duh! Kumbe kweli JF tuko kila kona! Kuna mtu alinipigia simu jumamosi akaniambia Chenge yuko Hunters na mkewe wanakula nyama!
 
Duh! Kumbe kweli JF tuko kila kona! Kuna mtu alinipigia simu jumamosi akaniambia Chenge yuko Hunters na mkewe wanakula nyama!

Af jamaa alikuwa na kiburi chake kama kawa tuu.... yani kama hakijatokea kitu
 
Chenge Mbona Yuko Kila Kona? Mie Mwenyewe Nilimdekshia Majuzi Ya Wiki Iliyopita Pale Mitaa Ya Oysterbay Kwenye Hotel Karibu Na Club Ya Maisha, Kwanza Aliingia Na Mjamaa Mmoja Mshombe Shombe Kavaa Mikanzu Myeupe, Halafu Akaingia Nadhani Ndo Mkewe, Walikuwa Katika Discussion Nzito Inavyoonekana, Lakini Mkewe Hakukaa Nao Aliwaacha Yeye Chenge Na Huyo Jamaa, Nikajisemea Ningekuwa Na Ki Laptop Changu Ningeita Squad La Jf Livamie Kiaina.
 
Chenge Mbona Yuko Kila Kona? Mie Mwenyewe Nilimdekshia Majuzi Ya Wiki Iliyopita Pale Mitaa Ya Oysterbay Kwenye Hotel Karibu Na Club Ya Maisha, Kwanza Aliingia Na Mjamaa Mmoja Mshombe Shombe Kavaa Mikanzu Myeupe, Halafu Akaingia Nadhani Ndo Mkewe, Walikuwa Katika Discussion Nzito Inavyoonekana, Lakini Mkewe Hakukaa Nao Aliwaacha Yeye Chenge Na Huyo Jamaa, Nikajisemea Ningekuwa Na Ki Laptop Changu Ningeita Squad La Jf Livamie Kiaina.


Kwi kwi kwi.... haya bwana mi si muda mrefu nimeshushuliwa kwa kuambiwa kuwa chenge bado yuko UK
 
inawezakana alikwisharudi tangu wiki iliyopita, mara kwanza nilikuwa sina uhakika hadi nilipomuona mkewe nikajua haswa ndio mzee mwenyewe wa vijisenti, mkewe alikuwa amevaa polo shirt na suruali na begani kajiweka mtandio, mzee alikuwa ametilia suti ya mao tse........ na kama nilivyowatonya na huyo babu wa kiberushi alikuwa na mikanzu myeupe.
 
Jamani, wakati tunaambiwa Chenge amekuja London kwa ajili "Mambo yake" na SFO, Lowassa ana nini London? ama ndio amekuja kumsajilia mshikaji wake (Chenge)? au ndio katika kupumua? Au .......... please help, niko tayari kumpa raha na kumtembeza japo wanasema "RAHA JIPE MWENYEWE" kama kweli amekuja kupumzika au kupumzishwa

Inawezekana kavutiwa na Vijisenti sasa wanaona bora wajipange 2015, Chenge awe PM. (Maoni yangu tuu)
 
Naona tangu Tina asema anataka kumpa Lowassa raha basi kila mtu ameanza kuwa ndugu; sasa na mimi kwanini nijivunge? Tina miye ni yule binamu yako wa mbali... sasa tuwasiliane tuone jinsi gani tunaweza kuhakikisha habari za EL zinaifikia jamii! Eh Tina, umenisikia? Mkakati wako ni mzuri sana.
 
Nani aliwaambia Ikulu kwamba ni rahisi kumchunguza mshika mkoba wa mafisadi? 😕

Posted Date::5/27/2008
Ikulu: Ni kazi kubwa kumchunguza Chenge

* Simba asema taarifa kamili baada ya siku mbili

* Chenge arejea kimya kimya kutoka Uingereza

Na Muhibu Said
Mwananchi

SERIKALI imesema uchunguzi wa tuhuma za kumiliki dola za Marekani 1 milioni (zaidi ya Sh1.2 bilioni) kwenye akaunti ya aliyekuwa Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge, iliyoko katika Kisiwa cha Jersey, bado unaendelea kwa vile ni kazi kubwa kuufanya.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba, alisema jana kuwa kutokana na hali hiyo, ni vema vyombo vya uchunguzi vikaachwa ili vikamilishe kazi yake.

"Kifupi, uchunguzi unaendelea. Tusubiri kazi iendelee. Ni kazi kubwa, tuviache vyombo" alisema Waziri Simba alipoulizwa na mwandishi wa Mwananchi jana.

Hata hivyo, Waziri Simba alisema atakuwa na taarifa kamili kuhusu suala hilo baada ya siku mbili, kuanzia jana.

Chenge ambaye ni Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), anachunguzwa na Taasisi ya Kuchunguza Makosa Makubwa ya Jinai ya Uingereza, ijulikanayo kwa jina la Serious Fraud Office (SFO).

Hivi karibuni Chenge aliondoka nchini kuelekea Uingereza na tayari amesharejea nchini.

SFO inamchunguza Chenge, ili kubaini kama fedha anazodaiwa kuzimiliki katika kisiwa hicho, zina uhusiano wowote na zile zinazoaminika kutolewa kwa njia ya rushwa wakati Tanzania iliponunua rada ya kijeshi kutoka Uingereza kwa Paundi za Uingereza milioni 28 (Sh70 bilioni), mwaka 2002.

Biashara ya ununuzi wa rada hiyo, ilifanywa kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya BAE Systems ya Uingereza.

Waziri Simba alisema uchunguzi kuhusu biashara ya ununuzi wa rada hiyo, nao unaendelea.

Tuhuma dhidi ya Chenge za kujilimbikizia fedha hizo, ziliibuliwa na Gazeti la The Guardian la Uingereza katika toleo lake la Aprili 12, mwaka huu ambalo lilieleza kuanza kwa uchunguzi dhidi yake, kutokana na akaunti yake kukutwa na kiasi hicho cha fedha.

Wiki chache, baadaye serikali ilisema Chenge anachunguzwa na vyombo mbalimbali vya kitaifa na kimataifa, ili kubaini kama ana kesi ya kujibu mahakamani, kuhusiana na tuhuma zinazomkabili.

Katika taarifa hiyo, Waziri Simba alisema kama serikali itajiridhisha kuwa Chenge ana kesi ya kujibu, atafikishwa mahakamani ambako mambo yote yatajulikana.

Awali, Waziri Simba alipoulizwa na mwandishi wa Mwananchi anachukuliaje taarifa za waziri kumiliki fedha nyingi kiasi hicho, alijibu: "Hata mimi nashangaa kama wewe, kama alizipata kihalali au la."

"Lakini kuna mtu nimemwambia, labda kauza ng'ombe wao wote ndio alipata hizo pesa, au ana biashara nyingine," alisema Waziri Simba.

The Guardian katika habari yake hiyo iliyowekwa katika mtandao wa intaneti, liliripoti kuwa taarifa hizo zinakuja ikiwa ni miaka mitatu sasa tangu Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru), kwa kushirikiana na SFO na taasisi za uchunguzi za Uswisi na Jersey zilipoanza kuchunguza kuhusu kashfa nzima ya ununuzi wa rada.

Gazeti hilo lilimkariri Chenge, akikiri kwamba fedha hizo ni mali yake na akatumia fursa hiyo kukanusha kuwapo kwa uhusiano wowote, kati ya fedha hizo na kashfa ya ununuzi wa rada, uliofanywa wakati yeye akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), katika serikali ya awamu ya tatu.

Septemba 15, mwaka jana, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa na Mwanasheria wa chama hicho, Tundu Lissu, walimtaja Chenge katika orodha ya vigogo 11, wakiwamo viongozi kadhaa wa serikali nchini kuhusika na ufisadi wa mabilioni ya shilingi za walipakodi.

Baadaye, Septemba 19, Waziri Chenge aliliambia gazeti hili kuwa walioibua hoja ya ufisadi dhidi ya viongozi wa serikali kama wakipata au kama wana ushahidi, yeye binafsi anatoa ruksa waupeleke katika vyombo vya dola ili ufanyiwe kazi.

Chenge alisema hapendi malumbano, isipokuwa yote yaliyozungumzwa atahitaji kuyaona kwa maandishi na uonyeshwe ushahidi wa yeye kuhusika moja kwa moja na ufisadi uliotajwa.

Aprili 17, mwaka huu, alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam (JNIA), Chenge aliwaambia waandishi wa habari kuwa tuhuma za Sh 1 bilioni anazodaiwa kumiliki katika akaunti Uingereza, ni za "vijisenti".

Alipoulizwa na waandishi wa habari juu ya kuziita vijisenti Sh1.2 bilioni, alisema: "Kila mtu ana viwango vyake na ana haki ya kusema anavyotaka. Na mtu akikutuhumu, unajua nafsini mwako".

Hata hivyo, siku mbili baadaye, Chenge alikaririwa na vyombo vya habari akiwaomba radhi Watanzania kutokana na kauli yake hiyo, akisema kuwa ilitokana na kuathiriwa na kabila lake la Kisukuma.

Siku chache baadaye, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Salva Rweyemamu, alikaririwa na vyombo vya habari akitangaza kuhusu uamuzi wa Chenge wa kujiuzulu Uwaziri wa Miundombinu, uliopongezwa na Rais Jakaya Kikwete kwamba, ni jambo pekee alilokuwa akilitegemea kutoka kwa Chenge.
 
Mwisho wa mazungumzo baada ya habri kamili ,huyu jamaa ni bora ajiuzulu kila kitu,ukishakuwa na kitita kama hicho sijui unatafuta nini katika kazi za kujihusisha na siasa na uongozi,hii nakumbuka mzungu mmoja alieleza kuwa ukiwa una uwezo basi achana na mambo ya siasa na uongozi serikalini kwani mwisho watakwabia unaiibia serikali ,sasa naona ukweli upo mbele kabisa na hauna utata.Aidha tatizo alizidi kunieleza kuwa ni uhaba elimu wa kuweza kuiendeleza fedha hiyo katika kuiwekea vitega uchumi.
nikiangalkia Chenge kwa fedha aliyoiokota angeweza kuziekeza fedha hizo kwa kufungua hoteli za kisasa kila mkoa na zenye kiwango cha juu.Na yeye mwenyewe akabaki pembeni kama sie akifuatilia kwa mbaali maendeleo ya hoteli zake ndivyo baadhi ya mamilioneya wanavyofanya huwa hawajitokezi na unaweza usiwahisi kabisa kama ni watu wenye fedha mambo yao yanakuwa kwa machati kabisa bila ya kumuumiza mwengine.
 
Kama kazi ya kuendesha nchi inawashinda si mseme tu?

Ikulu hamna kazi ndogo, mfagizi wa Ikulu kazi yake kubwa maana anaweza kuokota memo ya usalama wa taifa.Ndiyo maana hata wafagizi wote manyoka waliokwishanyweshwa maji ya bendera.Ndiyo maana pakawa "Ikulu" na sio "Idogo", hamna dogo pale.Katika neno hili "Ikulu" mzizi wa neno ni "kulu" maana yake katika lugha nyingi za kibantu za Tanzania ni "kubwa" as in big, complex, not simple.

Sasa mnavyosema ni kazi kubwa nyinyi mlitaka kufanya kazi rahisi tu?

Tell me something that I don't know right now, like how Chenge got the millions.

That this is not a simple case does not interest me.
 
Saa nyingine ni bora Sophia Simba akae kimya kama hana la maana la kuongea
 
Mambo ya public relations na kujua nini la kusema hadharani bado ni concept ngeni sana kwa viongozi wetu. Hatujafika huko bado!
 
Back
Top Bottom