The Radar Scandal: Investigation & Progress

na muhogo,...mwa na pilipili mwa inakolea ko singo!!!! nakikubali msosi wa kwa mama pale ferry magogoni au holiday inn annexe jirani na kwa prof shaba..we si matani mzee!!! unajua mara nyingine hawa warungu wanadharau misosi yetu so wakifungua outlets wanatujazia ma sandwich na ma hotdog ,,wapi na wapi...ukiwa pale annexe utagundua hata mabosi wamatumbi wenzetu wanakuja...wale wanaogopa protocal wanawatuma madereva na hotpot..ugali ,matembele na dagaa la kigoma topped with maharage ya mbeya,....tsh 600 tu[cents 0.45 usd/belly bursting lunch]..usisahau na ndizi mbivu au parachichi la moro...
 
kikwete alikataa maswali hapa uk kwa kuogopa kuhulizwa hili swala,lakini namkumbusha alipo hulizwa akiwa waziri wa mambo ya nje na bbc world services na alivyotetea hilo swala. swali langu kwake je mpaka sasa anaendelea kuitetea hiyo deal kama alivyofanya mwanzo?
 
Kama kweli tungalikuwa na watu Serious ana tukawa na private prosecutor leo hii mahakamani JK asingalipona . Leo hakuna uchunguzi wa mana utafanyika ambao yeye kasema hawezi kuingilia kwa kuwa JK anahusika moja kwa moja na ununuzi wa Rada. Kumbuka maamuzi yalitoka baraza la Mawaziri ambalo yeye alikuwemo. JK ni mnafiki sana na mfano wake ni ununuzi wa nyumba za serikali . Je hakununua ? Mbona alikaa kimya hadi mwisho ?
 
Duh mazee ununuzi wa nyumba za serikali hebu tuwekee wazi unajua tena wengina tuko mbali na upeo wa macho itakua bomba kama utatoa ya ununuzi wa nyumba za serikali kwa kirefu..
 
nakuambia si mchezo ila mazishi yale sasa ndio nini kupiga picha kwenye maji..
pale mie sijamfagilia hata kwa nini..ila mzee unyanyasaji kweli..kula hela..ya walipa kodi..inauma wangu..kuna siku pale tutaanza kuchinjana kama iraqi wee acha tu
 
Shemzigwa,

hapa ndipo napokoma na viongozi wetu.. hiyo picha pamoja na ile alopiga na Michuzi wakivuka kwa mashua nilidhani ni kampeni moja kubwa kuwa atajenga daraja akichaguliwa, lakini ndio hivyo tenaaa..anaonyesha kuwa yeye pia anaweza kuvuka kama wenyeji.
 
hehehe mzee hapo alikua kazi hana akaona akunje maji avuke surual au huwenda alimiss kuvuka maji si unajua tena...ukizoea kitu inakua tabu kukiacha hahaha ni mzozo ndani ya bongo
 
Lets keep to the point RUSHWA YA RADAR !RUSHWA YA RADAR !RUSHWA YA RADAR !RUSHWA YA RADAR !RUSHWA YA RADAR !RUSHWA YA RADAR !.Wanajambo what is the way forward?
 
 
Jamani, tusifanya mambo kwa haraka, kila kitu its about timing. Sasa, kwanza kabisa kabla hatujafanya lolote, lazime tudefine lengo letu ni nini. Vingine vinakuja baada ya hapo. Mama Lu, lengo la waraka huo ni nini?
 
Jamani, tusifanya mambo kwa haraka, kila kitu its about timing. Sasa, kwanza kabisa kabla hatujafanya lolote, lazime tudefine lengo letu ni nini. Vingine vinakuja baada ya hapo. Mama Lu, lengo la waraka huo ni nini?


Mimi nafikiri mama Lulu ana hoja. Iandikwe barua (au ile uliyokwishaandika) ya kulitaka bunge lianzishe uchunguzi juu ya manunuzi ya radar hasa katika mambo mawili:

i) kama bei iliyonunuliwa ilikuwa ni halali
ii) ni akina nani Tanzania walipewa hizo $30m

Hiyo barua izunguke watu tuweke majina yetu halisi iende kwa speaker na kila mbunge wa bunge letu pamoja na ubalozi wetu uingereza.

Vipi hapo?
 
Naona naanza kueleweka.......pia iende balozi zote nyeti...USA, Uingereza, Scandinavian Countries etc
 
.....PRESSURE PRESSURE WALIOKULA MLUNGULA WAWEZE KUWA PUT TO TASK..AU SIVYO HAWA WAFADHILI WASIMAMISHE HIYO MISAADA INAYOWANUAFAISHA WACHACHE.KAMA TUNAWEZA KU ENTERTAIN ONE PERSON KUPATA 12 BILLIONI WAKATI HOSPITALI HAZINA VITANDA ....
 
Sasa iwe ni barua ya Kiingereza (walengwa ni wafadhili na nchi za nje) au ya Kiswahili (walengwa ni Watanzania wenzetu)?
 
It can be the same letter......in both languages.Ikishindikana kabisa...tuandike ya kiswahili si wana translators?
 
WAFADHILI SI NDIO WALIOSHINIKIZA TUNUNUE HIYO RADA?


Kuna uchunguzi unaofanywa na SFO huko London kwa nini hao jamaa wasipewe nafasi wafikie mahali waseme either wameshindwa au wame-uncover anything...ndio then tulalamike.

Kwa sasa kupeleka barua kwa Wafadhili mimi naona ni sawa na kumpa kesi ya nyani ngedele.
 
Jamani. Pamoja na kwamba naunga mkono suala hili, tusisahau hizi issue tatu nazo ni IPTL, SONGAS na RICHMONDULI. Malipo ya IPTL na SONGAS kwa miezi minne tu (capacity charges) yanafikia "cha juu" alichopata mhindi huyo kama si kuzidi, tukiassume kwamba rada tunaitaka. RICHMONDULI ni zaidi sana ya hizi fedha za rada. Nadhani mikataba hiyo ya umeme (I+S) bado inadai si chini ya miaka 15 ijayo ili iishe. Sasa ukisikia mikataba ya uozo ambayo inabidi irekebishwe, ndio kama hii. hapo bado madini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…