Sofia Simba na Sakata la Mafisadi na Wapiganaji!

Sofia Simba na Sakata la Mafisadi na Wapiganaji!

Makaayamawe,
Mkuu wangu kamati ya Mwinyi haikukaa kujadili Malecela hata kwa jambo moja..nadhani unakumbuka yaliyotokea hadi JK kuteua hii kamati.. Leo, waziri mzima unaitwa kujieleza unaweka habari ambayo haikuwepo kabisa! nini makusudio yake haswa!
 
Lakini kama waziri wa utawala bora anadiriki kuhalalisha rushwa? Kwamba kwa kuwa kina malecela walifadhiliwa na fisadi basi wakae kimya wakiona wengine wanajihusisha na ufisadi. huu ndio utawala bora kweli?

Muheshimiwa hapo juu nakuunga mkono kwa hoja yako. Halafu huyu waziri Simba huwa ananichanganya sana kwa hoja zake za ajabu ajabu. Lakini inaonyesha siku zao zinakaribia mwisho.
 
Haya sasa. Wacha wapiga kelele nao wafisadiwe.njaa zao wanajiona wasafi
 
- This is very interesting,
- Kuhusu harusi na ufadhili wake, Auntie Sophia hakusema ukweli kwa sababu harusi iliandaliwa na kamati maalum kama inavyokuwa kwenye harusi zote bongo, Mwenyekiti wa kamati alikuwa Chiligati, akishirkiana na DC wa Dodoma Mjini, ikiwa ni pamoja na wanakamati kama Kimbau na Kitwana Kondo, na kina General Gau, sasa hawa hasa Chiligati wangetakiwa kuonyesha mahesabu waliyoyatumia ili kuweka ukweli unapotakiwa, kwa sababu ninazo copies zote za matumizi ya ile harusi na pesa zilizochangwa na majina wala sio tatizo.

- Maneno ya Auntie Sophia, siyaamini hata kidogo na ni uzushi mtupu kwa sababu ni mimi ndiye niliyetoa hela zangu za mfukoni kwanza kununua suti zote mbili za bwana harusi, na pia nilitoa hela zangu za mfukoni za kulipia honeymoon yao, ama sivyo hata honeymoon isingekuwepo, na kama kawaida yangu huwa ninatunza risiti ya kila kitu ninachofanya duniani, kwa hiyo ninasema kwamba Auntie Sophia, ana kazi kubwa sana kuthibitisha madai yake akiwa waziri wa Usalama wa taifa, kwa sababu ninazo risiti nyingi sana za hela zangu nilizotumia on the harusi, sasa kama kweli harusi ilifadhiliwa na fisadi, mimi na ndugu zangu hatukuwa na sababu ya kutoa hela nyingi sana tulizotumia kwenye ile harusi.

- Ya kugombea urais, hivi Mzee si alikuwa na hela za Iran, zilizobaki toka mwaka 1995. Halafu Auntie Sophia hapa tena anakuwa sio mkweli wala anayejali sheria, kwa sababu kampeni za urais wagombea wote walipokea hela toka kwa watu na sekta mbali mbali na haikuwa uvunjaji wa sheria za jamhuri, na ukweli niujuao ni kwamba kampeni ya mzee ilifadhiliwa na Shabibu, na kampeni ilikuwa na hela ndogo sana ndio maana haikufanikiwa, unless Shabibu ni fisadi then kweli mzee alichukua hela chafu, na kama ilivyokuwa kampeni ya Rais wa sasa ambako Auntie Sophia alikuwa mshiriki sasa angelinganisha hela zilizotumiwa na kambi zote na walikozitoa hela zao ndio ingependeza, lakini si kweli kabisa kwamba Patel ndiye aliyefadhili ile kampeni,
Ahsanteni.

William.

ASANTE WILLIAM

- Auntie Sophia, anajidhalilisha sana ...
- Halafu hii maneno ya harusi ndio uongo wake utakapoishia na kuanzia, kwa sababu yes alikuwepo na tumeshirikiana naye akiwa mbunge wa viti maalum, na pia tumeshirikiana na viongozi wengine wengi sana, na hata siku mzee analalamika kwamba hana hela za honeymoon yeye alikuwepo na viongozi wengine kama Mzee Mwinyi, Marehemu Sammy Mdee, Mama Zabeni, Mzee Msuya, Mama Nyoni, na Mama Makinda wote tulikuwa pamoja kule Area C, nyumbani kwa then Mheshimiwa Kilango alipokuwa akiishi zamani, na kila aliyekuwepo pale alipigwa na mshangao kwamba Mzee Malecela hana hela za honeymoon!, kabla sijajitokeza kubeba msalaba.

- Kwenye haya ya harusi na hela za kampeni Auntie Sophia amejishusha hadhi sana na ninajaribu sana kumuomba Mheshimiwa Kilango, asimchafue Auntie Sophia siku ya zamu yake maana itakuwa kiama hiyo siku, I mean utamuanzia wapi na kuishia wapi huyu masikini ya Mungu! kila mahali ni aibu tupu, inatia kinyaa sana!


William.

Umesikika William

Pole mkuu kwa yote, mi nilidhani ni jina tu unatumia na hakuna uhusiano wowote na JS Malecela maana wengine tulimzoea sana Ipyana (RIP).


LIMBANI WEWE!!

MSITUCHANGANYE HAPA.
 
LIMBANI WEWE!!

MSITUCHANGANYE HAPA.

Veracity,

Inaonekana Limbani amemquote William ila akasahau au kushindwa kuweka maandishi ya William kwenye quotes. Paragraph ya mwisho ndiyo inaonekana kama ni ya Limbani.
 
Wote wachafu...ingawa wanatofautiana kwa wingi wa uchafu walio nao, kundi la mama Simba na wenzake wao wanatetea uchafu kwa nguvu zote, kundi la kina mama Kilango wanauma na kupulizia na ni ndumilakuwili....lakini kwa ujumla wote wachafu....WIZI MTUPU.

😀..........wacha mie nipalilie kiunga changu cha minazi....😀
 
we are witnessing the heights of stupidity within our leadership. Siamini kama WAZIRI, Mwanamke kubehave kama mtoto msichana wa shule ya msingi. Ni kwamba anamwonea wivu mwenzie? au ni kwamba wana beef yoyote personal? ya kugombania Bwana? or what?

Vizuri ni kuwa amekiri Jeetu ni fisadi, kwa kusema "alifadhiliwa" na fisadi kwa hiyo anunga mkono ufisadi na hapingi ufisadi. At least anatuonesha kuwa kwa upande mmoja ametoa insight nzuri kwamba hata yeye anatambua kuwa kuna ufisadi na anauunga mkono.

Lakini yakuanza kumlipua mwenzake kwa mambo binafsi ambayo hayana uhusiano kabisa na issue nzima, shame on her. Good thing ni kuwa things are becoming public and slowly we are getting there.

Kweli tuna waziri "mwanamke".
 
Veracity,

Inaonekana Limbani amemquote William ila akasahau au kushindwa kuweka maandishi ya William kwenye quotes. Paragraph ya mwisho ndiyo inaonekana kama ni ya Limbani.


Bora kama ndio ivo maana nilishangaa inakuwaje watu wawili wawe na maandishi verbatim almost!
Asante na samahani kwa wahusika.
 
Bora kama ndio ivo maana nilishangaa inakuwaje watu wawili wawe na maandishi verbatim almost!
Asante na samahani kwa wahusika.

Hata mimi nilidhani hivyo mwanzoni ila baada ya kuona alichojibu William baada ya hilo bandiko la Limbani ndio nikagundua kinachoendelea.
 
we are witnessing the heights of stupidity within our leadership. Siamini kama WAZIRI, Mwanamke kubehave kama mtoto msichana wa shule ya msingi. Ni kwamba anamwonea wivu mwenzie? au ni kwamba wana beef yoyote personal? ya kugombania Bwana? or what?

Vizuri ni kuwa amekiri Jeetu ni fisadi, kwa kusema "alifadhiliwa" na fisadi kwa hiyo anunga mkono ufisadi na hapingi ufisadi. At least anatuonesha kuwa kwa upande mmoja ametoa insight nzuri kwamba hata yeye anatambua kuwa kuna ufisadi na anauunga mkono.

Lakini yakuanza kumlipua mwenzake kwa mambo binafsi ambayo hayana uhusiano kabisa na issue nzima, shame on her. Good thing ni kuwa things are becoming public and slowly we are getting there.

Kweli tuna waziri "mwanamke".

Huu udhaifu wa mtu mmoja usichukuliwe kuwa ni udhaifu wa kundi, kabila, jinsia..
Mbona kuna malumbano ya Dr Mwakyembe na Dr Hosea au nao wana beef ya kugombea bibi?..lets not trivialise issues..lets stick to the principles.Hapa tunaangalia utendaji wa kiongozi.
 
we are witnessing the heights of stupidity within our leadership. Siamini kama WAZIRI, Mwanamke kubehave kama mtoto msichana wa shule ya msingi. Ni kwamba anamwonea wivu mwenzie? au ni kwamba wana beef yoyote personal? ya kugombania Bwana? or what?

Vizuri ni kuwa amekiri Jeetu ni fisadi, kwa kusema "alifadhiliwa" na fisadi kwa hiyo anunga mkono ufisadi na hapingi ufisadi. At least anatuonesha kuwa kwa upande mmoja ametoa insight nzuri kwamba hata yeye anatambua kuwa kuna ufisadi na anauunga mkono.

Lakini yakuanza kumlipua mwenzake kwa mambo binafsi ambayo hayana uhusiano kabisa na issue nzima, shame on her. Good thing ni kuwa things are becoming public and slowly we are getting there.

Kweli tuna waziri "mwanamke".

This has nothing to do with gender.

Huyu waziri ni mchemfu na hafai kabisa kuwa waziri wa usalama wa taifa ila kwa sababu anafit profile ya mawaziri wa Kikwete, basi akapewa hiyo ofisi muhimu ya nchi.

Angalia context yake na -

1. Mkullo
2. Nchimbi
3. Ngeleja
4. etc

na katibu mkuu wa ccm Makamba.

Kikwete anajijua ni mchovu kwa hiyo anajiweka karibu zaidi (msisitizo kwenye zaidi) na wachovu wenzake ili wasimfunike.
 
- Ninamfahamu sana huyu waziri tena kwa karibu sana, na kwa yoyote anayemfahamu vizuri anajua kwamba haya ni maneno yake binafsi kwa sababu ndio kawaida yake kuzungumza maneno low na out of sense.

- Angekua ametumwa basi wangempa hoja nzito kidogo kuliko hizi ngonjera, ambazo hawezi kuzithibitisha. Kinachosikitisha ni kwamba huyu ni Waziri wa wizara muhimu kama aliyonayo na pia ni Mwenyekiti wa Umaoja wa Wanawake wa Tanzania,

- Sasa akija mgeni toka nje ya nchi yetu, kwanza anahitaji kuelewa kwamba huyu waziri wa ofisi ya rais je huyo rais anafanana vipi? Na hao wanawake wa Tanzania kama huyu ndiye Mwenyekiti wao wanafanaje? Na wananchi wa Tanzania kwa ujumla kama tuna viongozi wa juu kama huyu na sisi tunafananaje?

- It is very sad!

William.

Bwana 'Intellijentsia' kwa haya uliyoyasema ninaamini kuna makubwa yatatokea. data zako zina kawaida ya kuwa factual.
 
- Labda wewe na Hosea mngetuonyesha ushahidi, badala ya kuwapigia simu wabunge na kwenda kujikomba kwa Spika,

- Ninamheshimu sana DK, kazi yake kubwa kwenye taifa, ya kuanzisha kampuni ya umeme nilisema wazi kwamba kweli kulikuwa na conflict of interest, sasa kama tuna sheria on that basi alitakiwa achukuliwe hatua za kisheria, otherwise tunawahukumu wananchi wengine kwa ushahidi na sio ngonjera na viroja! ndio sababu tulienda shule!

- Wananchi wenye mawazo kama wewe ndio sababu kina Sophia watakuwa marais wetu in the future!

Ahsante.


William.

Yakhe, ukifanya tahmini angalia pande zote mbili za sarafu. Mbona hoja ya Dk. kubwia posho mara mbili mbili hutaki kuizungumzia?
 
Yakhe, ukifanya tahmini angalia pande zote mbili za sarafu. Mbona hoja ya Dk. kubwia posho mara mbili mbili hutaki kuizungumzia?

Sio lazima aiseme yeye, hata wewe unaweza kuusema huo udaku wa posho mbili kama ulivyofanya tayari ^^^^ hapo juu.
 
Wakti makeke ya bunge la awamu ya Nne yalipoanza niliwahi kuchallenge huko siku za awali kuwa tujaribu kujiridhisha na motives za hao 'wawasha moto' kwa sababu ya 'harakati zao' ambazo ziliongezeka exponetially & astronomically ktk kipindi kifupi, lakini watu wakanijia juu eti 'paka ni paka al ilimradi tu anakamata panya', sasa twaona wazi kuwa wote tu ni mapanya hakuna paka hata mmoja ..wote tu wanatoboa gunia letu..lol
 
Jifunzeni kabla ya kutoa shutuma mjishughulishe kidogo! Mngekuwa mmepitia posts zote, msingekuandika hivyo! Kuna wadau wengine wameshasema kila kitu alichosema SS incl. mkuu PASCO pitieni....thread nzima u will know nini mama kasema!

Unajua tena u-great thinker ni kazi ngumu!
 
Uliyoyasema kwenye kamati ya mzee Mwinyi ni ya aibu kwa aliyekuteua na wale uliojaribu kuwatetea. Sitaki niyarudie lakini kwa heshima yote uliyobakia nayo your time is up ma'am. Thank you for your unforgetable diservice to our country. Tukiamka tusikie umejiuzulu na kuwa mfano wa utawala bora. Usisubiri uundiwe kamati.

Kweli mambo aliyoyaongea huyu mama ni UTUMBO mtupu, na huyu ndiye waziri mambo ya utawala bora.......mmmh kweli Tanzania ni kchwa cha Mwenda wazimu.

Sasa kama alijua kuwa Malecela na mkewe walifadhiliwa kwenye ndoa yao au Malecela alilamba m200, yeye kama Waziri wa wizara husika kwa nini hakufuatilia hadi asubiri tume hiyo ya Mwinyi ndo atoe upupu huo??

Huyu kweli ni waziri Tanzania,.....mmmh ONLY in TANZANIA
 
Back
Top Bottom