SMS iliyoniamsha.. kuna kusalimika?

SMS iliyoniamsha.. kuna kusalimika?

Akieleza zaidi kuhusu taarifa alizozipata zinazolenga kumwangusha kisiasa, alisema baadhi ya wanasiasa, bila kuwataja majina, lakini akisema wanatokea ndani ya chama chake, wamepeleka mabilioni ya fedha jimboni kwa ajili ya kuwahonga wapiga kura wake, ili wamkatae kuwa mbunge wao katika uchaguzi mkuu ujao.

Alisema taarifa za uhakika alizonazo zinaeleza kuwa yeye pamoja na wabunge 23 wa CCM ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kupambana na ufisadi serikalini, mipango imeandaliwa ili kuhakikisha hawarudi bungeni, jambo aliloeleza kuwa baada ya muda litabainika kwa kila Mtanzania.


Hah hah hah Mzee Six mnafiki since when Fisadi akawa mpinga ufisadi? anaaka ku derail hoja ili watu wasichunguze ufisadi wake tu.

Talk abt kulialia na kutaka sympathy ya wananchi....
 
Kwa hali ilivyo Tanzania vita dhidi ya ufisadi inakumbana na vikwazo kwa kuwa walioko kwenye mtandao wa ufisadi ni watu wazito na wenye fedha nyindi sana.

Naamini kuwa kwa kuwa wakimya na kuogopa hatutaisaidia nchi hii ila kwa kupambana hata kwa kuutoa uhai wetu ni kielelezo tosha cha uzalendo wetu.Vyombo vyetu vya usalama vinatakiwa kuwalinda raia wema na siyo kununuliwa kwa fedha za mafisadi .Kama wanashindwa kutambua wajibu wao basi hatutasalimika Tanzania.Nguvu yetu watanzania haipo kwa vyombo vya kutoa haki na kutetea maslahi yetu ,ipo ndani yetu tu.Ni dhamira yetu na moyo wa mapambano usiotishwa kwa hadaa za mafisadi waliokubuhu.

Maka kieleweke
 
Kwa hali ilivyo Tanzania vita dhidi ya ufisadi inakumbana na vikwazo kwa kuwa walioko kwenye mtandao wa ufisadi ni watu wazito na wenye fedha nyindi sana.

Naamini kuwa kwa kuwa wakimya na kuogopa hatutaisaidia nchi hii ila kwa kupambana hata kwa kuutoa uhai wetu ni kielelezo tosha cha uzalendo wetu.Vyombo vyetu vya usalama vinatakiwa kuwalinda raia wema na siyo kununuliwa kwa fedha za mafisadi .Kama wanashindwa kutambua wajibu wao basi hatutasalimika Tanzania.Nguvu yetu watanzania haipo kwa vyombo vya kutoa haki na kutetea maslahi yetu ,ipo ndani yetu tu.Ni dhamira yetu na moyo wa mapambano usiotishwa kwa hadaa za mafisadi waliokubuhu.

Maka kieleweke

Watu wanacheza, nchi haijatulia. Fedha, madaraka na mapenzi (urafiki) vitatufikisha pabaya. Tutauana
 
In the proverbial "makali na mpini"... kwa kadiri mambo yanavyokwenda inaonekana wao wameshika mpini...

Yes!! And this is what makes ushindi wa watu na umma wa Watanzania ...utakaotokea kuonekana ni miijuzi ya ajabu...but it is there ...soon coming to happen. Kwa kuwa msingi wa kugawanyika utwawezeshwa na wao wenyewe.
 
Ukitaka kujificha hapa duniani usitumie any electronic gadget, vinginevyo wajanja watakunasa tu.

Kuna technologies za kutosha hapa duniani kunasa hata wale wanaojifanya wajanja sana.

Watu wengi wananaswa shauri ya wanawake na simu.

Nadhani inawezekana kutumia electronic gadget na asikunase mtu.

Usipokuwa unaelewe vizuri na vya kutosha technologia unayotumia inafanyaje kazi, watakudaka tu. Na usilaumu electronics, kwa sababu hilo litakuwa ni tatizo lako binafsi ...
 
Nadhani inawezekana kutumia electronic gadget na asikunase mtu.

Usipokuwa unaelewe vizuri na vya kutosha technologia unayotumia inafanyaje kazi, watakudaka tu. Na usilaumu electronics, kwa sababu hilo litakuwa ni tatizo lako binafsi ...

Mkuu,

Labda tuambie ni vipi unaweza kukwepa mkono wa serikali kwa kutumia hizo electronic gadgets kama ni mhalifu?

Wengine tunapata mlo kwa kuhangaika na vitu kama hivyo na nakuhakikishia hakuna iliyosalama kwa wachunguzi wanaojua kazi zao.
 
Kweli hili jambo sio la kupuuzia,ni jambo la kiusalama zaidi hivyo walengwa wataarifiwe wawe makini katika maisha yao ya kila siku.
H.Mwakyembe na Sitta.
Hawa jamaa wanazidi kua mbogo,wananchi we need to act now upon them.
Why should they use us as colateral for their wealth?
 
Mkuu,

Labda tuambie ni vipi unaweza kukwepa mkono wa serikali kwa kutumia hizo electronic gadgets kama ni mhalifu?

Wengine tunapata mlo kwa kuhangaika na vitu kama hivyo na nakuhakikishia hakuna iliyosalama kwa wachunguzi wanaojua kazi zao.

Hili halihusu kukwepa mkono wa serikali ili uvunje sheria.

Nakubaliana na wewe kwamba huwezi ukahakikisha kwa asilimia 100 kwamba kuna usalama unapotumia vifaa vya electronic ambavyo vipi kwanye aina moja au nyingine ya mtandao.

Lakini ukielewa hiyo technologia unayotumia vizuri, na ukielewa uwezo (wa kitechnologia na fedha) wa unayetaka kujilinda naye, pengine unaweza ukachukua hatua mahususi kuifanya iwe ngumu kupita kiasi kwa yeye kufanikiwa.

Na kama umeuliza ili kupata magic-bullet, sahau hilo. Kila technologia inabidi uifikirie kivyake. Labda ungesema ni techonologia gani unayotaka kutumia na unataka kujilinda, halafu kama ninaielewa naweza kukushauri. Kama siielewi nitakuwa nakosea kama nikihitimisha kwamba mtu hawezi kamwe kujihakikishia usalama wake akiwa anatumia technologia hiyo.

Labda nitoe mfano. Nimeona kwenye thread thingine watu wanalalama kuhusu wafanyakazi wa makampuni ya simu kuchungulia na hata ku-print SMS za watu. Sasa tuchukulie tatizo lako ni kwamba unataka tu content za SMS zako kati yako na mtumiaji mwingine ziwe siri yenu.

Kwa hilo kuna haka ka program kanaitwa SMS Salama. (Try googling "SMS Salama" ). Yenyewe ina-encrypt SMS before sending such that yeyote atakaye intercept anakuta madudu tu.

Lakini unaweza ukauliza, je, mtu mwenye utaalamu zaidi ya hao wafanyakazi wa kampuni za simu atashindwa kuona content zako?

Jibu lake ni kwamba unaweza ukaifanya iwe ngumu kupita kiasi (kwa kadiri unavyotaka). Kivipi? Inakuja kwenye kuelewa kwenye kuelewa technologia unayotumia. SMS Salama inatumia Advanced Encryption Standard (AES), ambayo ni military grade encryption algorithm (may be not our military). Na kama unavyojua, ku-break AES ni function of computing power uliyonayo na length of key iliyotumika. The longer the key the harder it is it break. SMS Salama nadhani uses 256 bit key. Ambayo nadhani is beyond all of your personal enemies.

Lakini kama ukiniambia kwamba your foos can easily break AES using 256 bit key, then tell me and we can always make a version that uses longer keys, and hence make your foos' lives a little more miserable.

Kwa hiyo kama tatizo lako ni kulinda SMS zako zisichunguliwe-chunguliwe tu, sasa unajua inawezekana.

Huo ni mfano mmoja tu.

Disclaimer: Sipoendekezi kuvunja sheria.
 
hiyo sms ni danganya toto tuu katika mambo ya kutishana. Ila pia kuna Mamafia bongo kwenye medani za siasa huwa wanawakolimba watu kimya kimya. No posibility of leakage. Msiwe na wasiwasi na danganya toto.
 
Hili halihusu kukwepa mkono wa serikali ili uvunje sheria.

Nakubaliana na wewe kwamba huwezi ukahakikisha kwa asilimia 100 kwamba kuna usalama unapotumia vifaa vya electronic ambavyo vipi kwanye aina moja au nyingine ya mtandao.

Lakini ukielewa hiyo technologia unayotumia vizuri, na ukielewa uwezo (wa kitechnologia na fedha) wa unayetaka kujilinda naye, pengine unaweza ukachukua hatua mahususi kuifanya iwe ngumu kupita kiasi kwa yeye kufanikiwa.

Na kama umeuliza ili kupata magic-bullet, sahau hilo. Kila technologia inabidi uifikirie kivyake. Labda ungesema ni techonologia gani unayotaka kutumia na unataka kujilinda, halafu kama ninaielewa naweza kukushauri. Kama siielewi nitakuwa nakosea kama nikihitimisha kwamba mtu hawezi kamwe kujihakikishia usalama wake akiwa anatumia technologia hiyo.

Labda nitoe mfano. Nimeona kwenye thread thingine watu wanalalama kuhusu wafanyakazi wa makampuni ya simu kuchungulia na hata ku-print SMS za watu. Sasa tuchukulie tatizo lako ni kwamba unataka tu content za SMS zako kati yako na mtumiaji mwingine ziwe siri yenu.

Kwa hilo kuna haka ka program kanaitwa SMS Salama. (Try googling "SMS Salama" ). Yenyewe ina-encrypt SMS before sending such that yeyote atakaye intercept anakuta madudu tu.

Lakini unaweza ukauliza, je, mtu mwenye utaalamu zaidi ya hao wafanyakazi wa kampuni za simu atashindwa kuona content zako?

Jibu lake ni kwamba unaweza ukaifanya iwe ngumu kupita kiasi (kwa kadiri unavyotaka). Kivipi? Inakuja kwenye kuelewa kwenye kuelewa technologia unayotumia. SMS Salama inatumia Advanced Encryption Standard (AES), ambayo ni military grade encryption algorithm (may be not our military). Na kama unavyojua, ku-break AES ni function of computing power uliyonayo na length of key iliyotumika. The longer the key the harder it is it break. SMS Salama nadhani uses 256 bit key. Ambayo nadhani is beyond all of your personal enemies.

Lakini kama ukiniambia kwamba your foos can easily break AES using 256 bit key, then tell me and we can always make a version that uses longer keys, and hence make your foos' lives a little more miserable.

Kwa hiyo kama tatizo lako ni kulinda SMS zako zisichunguliwe-chunguliwe tu, sasa unajua inawezekana.

Huo ni mfano mmoja tu.

Disclaimer: Sipoendekezi kuvunja sheria.

Manitoba,

Ndio maana nikakuuliza mfano. Jibu ni kwamba inategemea unamficha nani.

Kama ni suala ambalo wengine tulikuwa tunaongelea, yaani la kupambana na system (serikali) basi electronic gadgets karibu zote zinaweza kukuponza.

Inategemea na serikali wako prepared kwenda mbali kiasi gani.

Watu wengi wananaswa kwasababu ya kuamini kama ulivyoandika hapo juu kwamba
unaweza kufanya ujanja. Mfano yule jamaa aliyetaka kulipua mabomu UK, akakimbilia Ufaransa, akawasha handset yake baada ya kutoa simcard akiamini yuko salama, haikuchukua saa akawa mikononi mwa polisi.

Kama ni mafia wa kimataifa basi jitahidi usiguse electronic gadgets maana watakunasa tu.

Kama unapambana na hao polisi wetu basi unaweza ukasalimika kwenye baadhi ya mambo.

kwa taarifa yako hakuna Encryption iliyo salama, hata ibuniwe na nani.
 
Manitoba,

Ndio maana nikakuuliza mfano. Jibu ni kwamba inategemea unamficha nani.

Kama ni suala ambalo wengine tulikuwa tunaongelea, yaani la kupambana na system (serikali) basi electronic gadgets karibu zote zinaweza kukuponza.

Inategemea na serikali wako prepared kwenda mbali kiasi gani.

Watu wengi wananaswa kwasababu ya kuamini kama ulivyoandika hapo juu kwamba
unaweza kufanya ujanja. Mfano yule jamaa aliyetaka kulipua mabomu UK, akakimbilia Ufaransa, akawasha handset yake baada ya kutoa simcard akiamini yuko salama, haikuchukua saa akawa mikononi mwa polisi.

Kama ni mafia wa kimataifa basi jitahidi usiguse electronic gadgets maana watakunasa tu.

Kama unapambana na hao polisi wetu basi unaweza ukasalimika kwenye baadhi ya mambo.

kwa taarifa yako hakuna Encryption iliyo salama, hata ibuniwe na nani.

Nakuelewa mzee, lakini mimi bado naamini kwamba kama unaelewa vizuri hiyo technologia unayotumia ndio unaweza kuchukua hatua muafaka.

Nadhani mamafia wa kimataifa ndio wanatumia electronic gadgets kuliko hata sisi wengine. They spend time and money kuelewe technolojia ipo wapi na inaenda wapi. Wenzangu na mie tunapenda vitu rahisi rahisi tu bila kushirikisha akili. Wakikudaka unasema technolojia imekuponza. Umejiponza mwenyewe.

Inaonekana unaogopa sana serikali mzee. Kuna maeneo ambayo hata kama wanataka kwenda mbali vipi, utakuwa na jinsi yako ndogo ya kuwapoteza. Cha msingi ni kwamba unatakiwa uielewe technolojia unayotumia na wanayotumia. Kama huielewi watakudaka tu na usilaumu techonologia, ni tatizo lako binafsi.

Kama huyo jamaa uliyetolea mfano angekuwa anajua vizuri GSM inavyofanya kazi, na wanaomtafuta watakuwa wanatumia technologia gani, asingethubutu kutumia simu hiyo hiyo. Hata wewe nadhani uyanatambua hili, hata kama hujui ni kwa nini. Simu yako ina unique id inayoitwa IMEI (http://en.wikipedia.org/wiki/International_Mobile_Equipment_Identity )
na hiyo ndiyo wanayoitumia ku-track simu yenyewe (na sio sim-card). Wanokwambia utupe simcad halafu mchezo utakuwa umeisha wanasahu kwamba atakaye kuwa anatrack simu yenyewe wanakudaka hata kama umebadili sim-card.

Hiyo unayoiita system au serikali haitumii technologia zinazotoka mbinguni. Na waliopo huko ni watu wenye bongo kama wewe.

Iwe ni system au ni mtu mwingine, nadhani ni overstatement kusema kwamba kama unataka kuficha mambo yako basi usitumie techonolojia. Hiyo ni kweli kama wewe huielewi kiundani hiyo technolojia unayotaka kutumia. Unaenda kununua tu kwenye shelf kwa sababu umeona tangazo kwenye TV linaloelezea inafanya mambo gani. In fact, kama huielewe technolojia unayotaka kuitumia , i bora usiitumie maana itakuponza kweli.

Kwa mfano ushajiuliza inakuwaje watu wengine wana-hack computer za taasisi za maana tu duniani na they disapear without a trace? Ndio wapo wanokamatwa na haimaanishi kwamba walikuwa ni mbumbumbu. Lakini wapo wasio kamatwa na sababu ni kwamba wanaelewa wanachokifanya na wanachokitumia kufanya wanachokifanya.

Baba, elewa technologia unayotumia, usiilaumu pale unaponaswa.

Mimi napenda kufanya vitu kwa vitendo. Wewe sema unataka kufanya nini kuizunguka "system", as long as siyo kuvunja sheria (kwa sababu naamini sheria zinahitaji kuheshimiwa) pengine tunaweza kupata suluhisho. Na sio kufikiri tu kwamba "system" ndio mwanzo na mwisho wa techonolojia.
 
Jamani tumesema Tanzania hakuna uwezo huo wa Kiteknolojia na matokeo yake usalama wa Taifa na mambo mengi uko mashakani. Hatusemi kuwa hakuna teknolojia inayoweze kutumika kutrace calls kutoka kwenye cell au hata kutrace sms.

Fikiria kuwa makampuni ya simu za mkononi Tanzania hayatakiwi kuretain messages (sms) kwenye systems zao sasa utaweza vipi kuthibitisha x amekutumia ujumba ambao wewe uliiufuta au unadai ulikuwemo kwenye simu yako?
 
Jamani tumesema Tanzania hakuna uwezo huo wa Kiteknolojia na matokeo yake usalama wa Taifa na mambo mengi uko mashakani. Hatusemi kuwa hakuna teknolojia inayoweze kutumika kutrace calls kutoka kwenye cell au hata kutrace sms.

Uko sawa kabisa. Hata huko ambapo technolojia ipo juu, unaweza kuwa-fool, ingawa inahitaji kushirikisha akili zaidi. Na hapa kwetu nadhani ndio itakuwa bwerere kabisa ...

Na uko sawa kwamba mtu anayefikiria katika mstari wa usalama wa Taifa moyo unaweza kupata mapigo mengi zaidi ya inavyotakikana ...

Fikiria kuwa makampuni ya simu za mkononi Tanzania hayatakiwi kuretain messages (sms) kwenye systems zao sasa utaweza vipi kuthibitisha x amekutumia ujumba ambao wewe uliiufuta au unadai ulikuwemo kwenye simu yako?

Ukweli ni kwamba yapo makampuni yanayo-retain sms, na huwa wanazitoa wanapotakiwa kufanya hivyo. Na ndio maana kuna ripoti kwamba kuna ndoa zimeingia mushkeri baada ya mwenza mmoja kupata mtu ndani ya hizo kampuni na kuprintiwa sms za mwenza wake ... Nadhani wasingeweza kuzi-print kama zingekuwa haziwi re-tained ...
 
siyo kweli kabisa kwa sababu kila call au sms inakuwa record katika data kama huamini ingiza code za aina ya simu yako utaona watchdog on maana yake simu yako ipo kwenye record za kumbukumbu
 
2h4avrk.gif
Good old days
 
Sijaelewa una maana gani mkuu!! Au kwa vile ile thread ya mMKJJ kushikiliwa na uhamiaji imepotea humu sasa unataka kuibua mjadara mahali pengine??
ni kweli hujanielewa..... nina tabia ya kurejea posts za zamani hasa nikiwa free na kuzisoma upya, hiyo picha ya GT ni tosha kabisa kunipa nafasi ya ku-comment, au siruhusiwi kupitia threads za zamani?
 
ni kweli hujanielewa..... nina tabia ya kurejea posts za zamani hasa nikiwa free na kuzisoma upya, hiyo picha ya GT ni tosha kabisa kunipa nafasi ya ku-comment, au siruhusiwi kupitia threads za zamani?

Hapana mzee nilikuwa nauliza tu....................maana kuna thread hapa imepotewa kiajabu leo hii. Niliiona nikataka kuchangia then ikagoma mara ikapotea. Sasa nilifikiri unaichokonoa kijanja.
 
Back
Top Bottom