MADELA WA-MADILU umenena, glove zinazosungumzwa hapa si zile kama za kuendeshea pikipiki au za hospitali bali ni glove za kumfanya mhusika asipate madhara na anachokishika na haziwezi kuonekana kwa macho ya kawaida na si rahisi hata kuhisi unapogusana na mtu aliyevaa hizo glove.
Kubenea sasa amejanjaruka, zamani alitumiwa sms za vitisho na mara ya kwanza aliambiwa kuhusu gari na baadaye likaunguzwa kwelo japo hayakuwa madhara makubwa, akakoswa koswa kugongwa na gari (aligongwa kidogo) baada ya kutumiwa sms ya kujulishwa, ikaja sms ya kuvamiwa akavamiwa kweli, akapata ujumbe mwingine kuhusu polisi akavamiwa kweli.... Na mara zote akiwaambia watu, wanasema, "wewe acha woga, mtu anayetaka kufanya kweli hatumi sms".
Lengo hasa ni kutisha ili watu wasiwafuate fuate na usipotishika wanakujaribu ukiendelea na jeuri sasa wanafanya kweli.
Kuna mbinu za kukabiliana na vitisho hivyo, na kwa wengine tuliovizoea kwa zaidi ya miaka saba sasa, tumekua tukipambana navyo na hata hapa nilipo napambana na ndio maana naandika ujumbe huu ikiwa ni saa 10.10 Alfajiri hapa nyumbani Tanzania nilipo kwa sasa