SMS iliyoniamsha.. kuna kusalimika?

Its pity tupo busy tunajadili udaku Im out...

masatu....udaku, masatu...udaku, masatu..udaku, masatu.udaku, masatuudaku. Mm!! the resemblance is intriguing. Could it be one and the same? Just food for thought, happy weekend.
 
masatu....udaku, masatu...udaku, masatu..udaku, masatu.udaku, masatuudaku. Mm!! the resemblance is intriguing. Could it be one and the same? Just food for thought, happy weekend.
Isn't it amazing. Hii kaiona ni udaku lakini kwenye thread nyingine kaleta udaku kuhusu Dr. Slaa without attribution na anamtaka Dr. Slaa athibitishe kama ni true au false. Amazing indeed.
 
The greatest udaku from JF,

1. Jamani Amina Chifupa yuko hatarini kufa huyo, akafa kweli,

2. Jamani Balali atakufa sasa hivi, akafa kweli,

3. Wangwe apigwe risasi, akafa kweli,

Labda kuna maana nyingi za neno udaku, na one of them ni ukweli toka JF.

Mkulu Mwanakijiji, ubarikiwe tu! na JF mbele zaidi!
 
Udaku, as far as JF is concerned,ni kutoa taarifa ya jambo fulani kabla ya wakati wake tena kinyume na matakwa ya wenye jambo.
 
Mkuu
Ni moja ya njia lakini si hiyo tu mkuu wangu.
ndio maana unaweza kujirekodi bila kutumia mtandao wa aina yoyote ile Lakini bado waka trace na kugundua ni sehemu gani ulikua wakati wa kujirekodi.
Sauti ama picha haipotei Angani hubaki ina elea elea miaka nenda miaka rudi.


Law ya conservation ya Energy: energy can not be created or destroyed.

...again no disrespect, nakuomba upunguze tu kuangalia star trek!

...IMEI triangulation ni njia mojawapo na ni njia mojawapo iliyokubwa zaidi. Unless hizo mobile handsets zinatengenezwa vichochoroni na kisha kuconnect kwenye GSM, CDMA au network nyingineyo yoyote kisha kuunganishwa kwenye mitandao undetected bila kuji-identify yenyewe na pale ilipo. Simple protocols, there is simply no getaway router (in digital communications) that will connect you to a network before identifying who you are and where you are. The only difference here is that the degree of identification varies with authentication. Anyway, let me call it quits, like Icadon implied, these stuffs deserve a different thread.
Baadae.
 
Mkuu MMJ,

Kwanza heshima mbele na hii nyeti, hatimaye nimeithibitisha kuwa ni kweli,

1. Kama kawaida hawa wakuu wamekuwa wakikutana kwa siri kupanga mikakati, na moja wapo ilikuwa ni kutafuta njia ya kuwaondoa Sitta, Mwakyembe, na Mama Kilango.

2. Kwa bahati nzuri au mbaya, hawakujua kua kila siku ya Mungu wako chini ya scrutiny kali sana, tena masaa 24, maana sasa hawaaminiki tena na kila kiongozi wajuu, mpaka wa chini wasiokuwemo kwenye kundi lao.

3. Habari ikapatikana kwa wahusika, Kubenea akamwaga wazi wakashituka! Kushituka wakamuita mkulu wa manjago na kutaka mlinzi wa mmmoja wao aondolewe kwa sababu ndiye anayetoa info, mkulu akawajibu kuwa atashughulikia, to their shock ni mlinzi wanayempenda ndiye akatolewa yule wasiyemtaka akabaki, it is so bad kwamba sasa hata wakienda haja kubwa au ndogo zinahesabiwa na kuripotiwa.

4. Walipoona hivyo kwa hasira wakaamua kumpaka rais, kwa info za Lowassa kuwa waziri wa nje, na kwamba wanashirikiana naye ni habari ndefu sana ninayo hapa, wamekuwa wakiisambaza kwa baadhi ya wananchi na ninayo bado ninaipitia na kuangalia upepo kabla sijaiweka hapa wazi, ambapo wamefikia hatua sasa hata ya kumtaka muungwana kuondoka kwenye power!

Now let me say this, hatimaye this ufisadi na the rest of the story now it is just starting to get interesting and very serious, ninatabiri kuwa in the next few months, wananchi wa Tanzania tutajionea makubwa sana katika hawa wakuu kugombea power!

Mkuu MMJ, respect kwa courage ya kuileta hii kitu, ni sawa kwa 100%, na when all is cleared nitaimwaga hapa the original message ya majibu yao kwa hasira ya kujulikana ya kudai kuwa Lowassa atakuwa waziri wa nje!

Ahsante Wakuu!
 
Mkuu
Ni moja ya njia lakini si hiyo tu mkuu wangu.
ndio maana unaweza kujirekodi bila kutumia mtandao wa aina yoyote ile Lakini bado waka trace na kugundua ni sehemu gani ulikua wakati wa kujirekodi.
Sauti ama picha haipotei Angani hubaki ina elea elea miaka nenda miaka rudi.

Law ya conservation ya Energy: energy can not be created or destroyed.

Duh!!! I give up....Ngoja tusivuruge mjadala wa watu.
 
Hofu yangu kubwa wala haiko kwa kina Mwakyembe na Sitta... moyo wangu ni mzito zaidi kwa ajili ya mtu mmoja tu. The cards are stacked heavily against the person. Tutahitaji kuliombea Taifa very soon.
 
State of denial "aah haiwezekani, watanzania hatujafikia kiwango hicho" jiulizeni kufuli la EPA, RADAR, IPTL, Richmond yalipofunguka kwa ulaini, kuna watu waliambiwa "wanachota" lakini sauti zile zile zikasema "aahh haiwezekani, ni uzushi"

Sasa tunahangaika na mapovu kututoka tukimsaka mbaya aliyechokonoa kufuli na kujitwalia EPA!
 
Hapa sisi wadogo inabidi tusubili mpaka vita ya panzi ndo sisi tuje tufrahia yaani watibuane wao kwa kwanza kisha sisi ndo tunaneemeka zaidi.....ngoja wasigane wao weeeeee wachafuane weeeeee mpaka kitaeleweka tu.....
 
Nakumbuka katika vikao vya mwisho mwisho vya bunge lililoisha wiki iliyopita spika Sitta alitangaza ugeni wa madiwani kutoka jimboni mwake Urambo ambapo alisema kuwa hao ndo wategemezi wake wakuu kwa shughuli za kisiasa pale jimboni kwake na walikwenda bungeni kumpasha habari za mchezo mchafu unaoendelea juu yake huko jimboni kwake.

Na akasema kuwa hao wanaofanya hivyo wanawatajirisha tu wananchi wa urambo lakini hilo jimbo ni lake tu mpaka atakapoamua kustaafu kugombea, so nyie mnaosema kuwa hili jambo ni udaku sijui mnafikiria nini any way ngoja tuone maana tumeshazoea kuwa na subira....
 
Sisiemu ni chama cha mafioso, mafisadi na majambazi, vitendo kama hivyo siajabu ndio maana wakawaondoa haraka mashahidi wakuu wa wizi EPA, Balali na Mbatia, au kuna mtu anabisha kuwa vifo vyao havina uhusiano ugaidi wa EPA?!
 
Siyo tu kuchomoa sim card au kuhama sehemu, unaweza ukawa na visimu vingi tu vya bei poa na sim cards kibao, ukimaliza unatupa. Sijui kama tracing ni rahisi kwa mtindo huo.
KWA KWELI YA KUWA NA VIJISIMU VINGI INAWEZEKANA KABISA.Nilikuwa tz kama mwezi umepita na nikabahatika kukatiza kariakoo kwa kweli nilishikwa na butwaa kusikia simu zinauzwa kwa mnada tena kwa sh 10000 na 15000.
 
Hmmmm!!! KUna thread tumezungumzia maswala ya ku-triangulate simu za mkononi kwa kutumia IMEI.
HII inawezekana kabisa lkini sijui kwa masuala kama haya.mana mimi nilipoteza simu yangu nikatoka taarifa vodacom wakaomba imei no wakanijulisha hiyo simu inatumika mahali fulani.nikafuatilia.niliipata LAKINI SASA KUNA RAFIKI angu kapoteza simu ya gharama kwa kweli na ilikuwa ina mambo yake mengi tu ya maana kaenda polisi ,na polisi wakaandika barua kwa voda waitrace ili wajue inatumika kwa mtandao upi tz mpaka leo ni zaidi ya mwezi hawataki kutoa hiyo printout.WANAJIBU tu kwa kumpigia simu inavyoonekana haitumiki.
 
sizani kama wanaweza m-trace.
mfano kila akituma sms anachomoa simu kadi anaitupa ama anaizima simu kabisa maana kazi ya simu hiyo ni mambo hayo tu.Na akitaka kutuma sms mfano yeye anaishi mbezi anaenda moro ndio anaifungua simu dakika moja anatuma sms anachomoa kadi anaitupa na anazima simu anarudi kwake mbezi.

..wanaweza.

..kila simu ina ID yake, hivyo wakitaka hawatatumia namba ya kawaida, bali ID ya simu.

..kumbuka kuwa, wahalifu wote hufanya makosa na wengine hawako-smart kihivyo. so, atafanya kosa dogo litakalomnasa. at times, it needs sometime and maybe a lot of it!

..hamna kinachoshindikana, bali nia ndio hukosekana katika mambo kama haya.
 
HII inawezekana kabisa lkini sijui kwa masuala kama haya.mana mimi nilipoteza simu yangu nikatoka taarifa vodacom wakaomba imei no wakanijulisha hiyo simu inatumika mahali fulani.nikafuatilia.niliipata LAKINI SASA KUNA RAFIKI angu kapoteza simu ya gharama kwa kweli na ilikuwa ina mambo yake mengi tu ya maana kaenda polisi ,na polisi wakaandika barua kwa voda waitrace ili wajue inatumika kwa mtandao upi tz mpaka leo ni zaidi ya mwezi hawataki kutoa hiyo printout.WANAJIBU tu kwa kumpigia simu inavyoonekana haitumiki.

..inawezekana huwa haitumiki mara kwa mara au haitumiki kabisa au kuna mtu hajafanya kazi yake.

..pengine imekosa charger! na hivyo kushindwa kutumika. kama kweli ilikuwa ya bei mbaya!

..au imekuwa locked na haijafunguliwa mpaka leo.
 
Mkuu polisi au uwt, wakiamua kuku-trace kwa kutumia simu yako wanaweza tena ni rahisi sana, wanaenda kwenye kampuni ya simu yako, it takes labda dakika tano tu kujua ulipo,

Kama huamini tafuta ile documentary ya yule muuza unga wa kimataifa wa Colombia, kwa jina la Pablo Escobar that is exactly how they nabbed him ni kwa kum-trace simu yake, infact walimfuatilia mpaka wakafikia mahali akawa anaangaliana nao bila ya yeye kujua akiwa kwenye simu,

Labda the best thing you can do na simu ni kuongea kwa dakika mbili tu na kukimbia mbali sana na pale, na yule uliyempigia naye afanye hivyo hivyo! Lakini ukiongea zaidi ya dakika kumi tu wanakushika tena kirahisi sana!
 
..inawezekana huwa haitumiki mara kwa mara au haitumiki kabisa au kuna mtu hajafanya kazi yake.

..pengine imekosa charger! na hivyo kushindwa kutumika. kama kweli ilikuwa ya bei mbaya!

..au imekuwa locked na haijafunguliwa mpaka leo.
Hapana yeye anadai alichunguza na ilikuwa iko na mteja wa voda ndio mana akaamua kwenda polisi kupewa barua tatizo voda wanadai sijui mwanasheria wao bado hajaifanyia kazi mana mwenye simu aliomba aamiwe pia kwa mara ya mwisho hiyo no ya voda ilitumika lini mana anayo hiyo no. na huyu mtuhumiwa.sasa nisaidieni ni kweli voda wanaweza kutrace hata kama haitumii ntandao wa voda?
 
Hapana yeye anadai alichunguza na ilikuwa iko na mteja wa voda ndio mana akaamua kwenda polisi kupewa barua tatizo voda wanadai sijui mwanasheria wao bado hajaifanyia kazi mana mwenye simu aliomba aamiwe pia kwa mara ya mwisho hiyo no ya voda ilitumika lini mana anayo hiyo no. na huyu mtuhumiwa.sasa nisaidieni ni kweli voda wanaweza kutrace hata kama haitumii ntandao wa voda?

..sidhani kama wanaweza!

..itabidi ajaribu kwenye networks nyingine kama tigo,zain na zantel.

..ukiwa na simu ya bei mbaya ni vema ku-back up data na settings za simu yako mara kwa mara, hizi zitakusaidia utakaponunua nyingine mambo kuwa kama awali. na kama utaona inafaa ipige phone lock simu yako. ilimradi isiwe rahisi kwa mtu atakayeiiba kuitumia bila kuhangaika.
 
Back
Top Bottom