Sio kwa ubaya ila Ali Kamwe ni matunda ya kulelewa na mzazi mmoja,vijana lindeni ndoa zenu

Sio kwa ubaya ila Ali Kamwe ni matunda ya kulelewa na mzazi mmoja,vijana lindeni ndoa zenu

mdukuzi

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2014
Posts
22,312
Reaction score
55,969
Mtoto aliyepata malezi bora ya baba na mama utamjua ukubwani,huwa hawana adabu na hawajui waongee nini na wakati gani.

Kuna familia wazazi wote wapo pamoja ila mmoja yuko bize sana mpaka analelewa na house girl badala ya wazazi.

Kuna waliotengana kwa sababu mbalimbalihivyo mtoto kukosa upendo ba mafundisho ya wazazi wote wawili.

Ali Kamwe sina uhakika ila nina uhakika asilimia 90 kalelewa na mzazi mmoja
,Akiwahi kumtukana Juma Mgunda,mzee wa watu mwaka 1989 kipindi anakiwasha Coastal union ,Ali Kamwe alikuwa hajazaliwa,mzee Mgunda mstaarabu sana alisema namuachia Mungu.
Ali kamwe amekuwa akitoa matamshi mpaka sisi kakazake tunashsngaa huyu dogo vipi
 
Ali Kamwe yuko sahihi kumjibu vle na tutmuunga mkono Kamwe daima.... Kiongozi wa serikali atekeleze majukum yake ya kiserikali na awe na mipaka... Kushutumu timu kama yanga sio jambo dogo alipaswa apelekwe mahakamani ajibu tuhuma hizo huyo mpuuzi.
 
Mkuu vijana wa siku hizi bila kujali wamelelewa nani ukija kichwakichwa wanakupa za taya mapema tu.

Hizo mbanga za mzee, sijui mtu mzima labda kanisani na msikitini mitaani hasa mijini hizo mambo hamna kabisa...

Huyo dogo huenda kaishi na masela sana, ndio huwa hivyo wana heshima ya kubumba tu.
 
"That is just a flamboyant person like any other. A man cannot engage in such nonsense in front of people who are self-aware."
Kwani unafaidika nini ukisema una mademu wengi??
Kuna wale team #nofap kuna wale hawanjunji kwa imani yao, wengine ni maamuzi yao tu au wazee wa nyeto.

Sio jambo la ajabu yeye kusema ivo na si ajabu hafanyi hivyo alivyosema.
 
Mtoto aliyepata malezi bora ya baba na mama utamjua ukubwani,huwa hawana adabu na hawajui waongee nini na wakati gani.

Kuna familia wazazi wote wapo pamoja ila mmoja yuko bize sana mpaka analelewa na house girl badala ya wazazi.

Kuna waliotengana kwa sababu mbalimbalihivyo mtoto kukosa upendo ba mafundisho ya wazazi wote wawili.

Ali Kamwe sina uhakika ila nina uhakika asilimia 90 kalelewa na mzazi mmoja
,Akiwahi kumtukana Juma Mgunda,mzee wa watu mwaka 1989 kipindi anakiwasha Coastal union ,Ali Kamwe alikuwa hajazaliwa,mzee Mgunda mstaarabu sana alisema namuachia Mungu.
Ali kamwe amekuwa akitoa matamshi mpaka sisi kakazake tunashsngaa huyu dogo vipi
Cha kushangaza wewe uliyelelewa na wazazi wako wote wawili akili yako ni kama tu ya yule Mkuu wa Mkoa asiyetambua mipaka ya kazi yake. Yaani akili ya kukulia ugali na maharage kuanzia umri wa miezi miwili.

Ally Kamwe alikuwa sahihi kumjibu mtu asiyejua hadhi ya cheo chake! Na kupitia yale majibu yake, nina imani wakati mwingine hatokuja tena kurudia ule upuuzi wake wa kujigeuza kuwa Christina Mwagala.
 
Ali Kamwe yuko sahihi kumjibu vle na tutmuunga mkono Kamwe daima.... Kiongozi wa serikali atekeleze majukum yake ya kiserikali na awe na mipaka... Kushutumu timu kama yanga sio jambo dogo alipaswa apelekwe mahakamani ajibu tuhuma hizo huyo mpuuzi.
Inashangaza kuona watu wakimtetea Mkuu wa Mkoa aliyeamua kwa makusudi kuacha majukumu yake ya msingi, na kujiingiza kwenye usemaji na pia ushabiki maandazi wa timu ya mpira wa miguu.

Yanga imeenda kucheza kwenye Mikoa mbalimbali ndani ya hii nchi! Lakini hatujawahi kumsikia huyo Ally Kamwe akimtukana/akitupiana maneno ya vijembe na hao wakuu wa Mikoa husika? Kwa nini atupiane maneno na Mkuu wa Mkoa wa Tabora tu? Kwa nini tusiamini huyu Mkuu wa Mkoa ana matatizo ya kuingilia mambo yasiyomhusu/hatambui mipaka ya kazi yake?
 
Back
Top Bottom