Sina nia mbaya, naomba kujua Elimu ya Babu Tale

Hyo elimu unayoitaka haisaidii watu kibao wanaangaika kitaa.
Na elimu yako bila kujiongeza utabaki kuwa zero
Weweeee huko kujiongeza kwa wasio elimu ni sawa na ni jambo la maana ila usisahau kuwa kujiongeza kwa wasio elimu kumo ndani ya mifumo eliyoandaliwa na wenye elimu.
Hata hivyo elimu hutafutwa ila akili mtu huzaliwa nayo. Hakuna mwenye akili asiyemtafuta elimu(a power tool)
 
Kila nikisikia haya maneno Naona aibu mimi , c bora awe anakaa kimya tu , anazid kututia hasira mbwa huyu , na laana ya kumtoa kafara mke wake itaendelea kumtafuna
Hata mm naona aibu mimi, bora asichangie hata hoja
 
Shukrani kwa wote. Hivi kwanini hii nchi mtu akiwa na influence kidogo tu anakimbilia siasa? Wasanii, Comedian waigizaji wote wanataka Ubunge, hivi wana uelewa wa kutosha kuwapa dhamana ya kutuwakilisha bungeni kweli?

Unaweza kuwa mzuri kwenye muziki lakini haimaanishi hata kwenye ubunge unatosha hapana. Tupambane sana tupate tu katiba mpya maana,tunajidhalilisha sana.

Mbona Musukuma ni STD7 lakini ana point za kuwakilisha jamii? Nikipata CV yake na quote zake mbalimbali labda kwenye mitandao ni sawa pia.
Elimu yake ni Form Four tu ila tayari Maisha kashayakatia Denge! Elimu kubwa bila kuwa na pesa ni Upumbavu tuu
 
Huyu mwamba nakumbuka last time tulifukuzwa kwa kosa la kuiba maandazi ya shule nzima chekechea

Sijui Kama alirudi maana Mimi nlihamishwa mkoa

Kolabo yetu ilitikisa wilaya
 
Nasikia amasoma "bachelor of science in wizard management "

Badae akaunga "masters of bongo fleva crisis "

Diamaond akamuajiri ...!
 
"naomba vyeo vya Rais viondolewe mfano sijui rais wa tff itolewe Rais abaki samia tu, mfano unakuta mtu kiatu chake kina vumbi, ni kulidhalilisha neno Rais, ndio maana mimi nilijiita babu"

Na huyu ndio anategemewa kutunga sheria😀😀😀
Niliposikia ile speech kilichonijia cha kwanza ni huyu elimu yake ni nini ?

Most ignorant speech in history of Parliament. Anasahau kwamba watu wa kwao Ifakara na Tanzania kwa ujumla the vast majority hatuna magari, tunavaa chachacha na ndara kwenye njia za vumbi. Ukisema maneno kama yale unakuwa umewadharau watu wengi sana kwa sabaubu marais na viongozi wa vikundi kibao huko vijijini wanavaa ndara na wana vumbi miguuni.

Hana elimu na pia naturally hana chochote kichwani.
 
Mh.Tale yuko sahihi......

Kigezo cha UBUNGE ni kujua kusoma na kuandika .....

BUNGE SI LA WASOMI WA ELIMU ZA JUU TU.....

#KaziIendelee
 
Kigezo Cha kuwa mbunge ni kujua kusoma na kuandika tu
Hapa ndipo CCM inapotukosea na kutoitendea haki Nchi hivi ni kwanini kigezo cha chini cha kuomb/ kugombea ubunge isiwe angalau Kidato cha sita (form six)?
 
Huyu mwamba nakumbuka last time tulifukuzwa kwa kosa la kuiba maandazi ya shule nzima chekechea

Sijui Kama alirudi maana Mimi nlihamishwa mkoa

Kolabo yetu ilitikisa wilaya
Enzi wewe na yeye mnasoma chekechea zilikuwepo?

Mimi najua enzi zetu ni direct darasa la kwanza
 
ni ujinga mtupu darasa la 7 kwenda kujadili mambo sensitive kama uchumi na kutunga sheria za nchi!! Tumekabizi vichaa rungu
 
Back
Top Bottom