Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,400
Mkuu Kitila,
Pole na uzushi huu ambao Brazamen anajua dhamira (motive) yake ilikuwa ni nini.
Mimi nilijiunga na JF kwa nia njema kabisa ya kushiriki na watanzania wenzangu popote pale walipo iwe ughaibuni au mahali pengine kubadilishana mawazo na kupeana taarifa mbalimbali na mambo mengine.
Pia wanachama wenzangu mkifuatilia sbabu za mimi kujiunga na mtandao huu niliwahi kuziweka huko nyuma katika posting zangu.
Siku hizi ukipita na kukutana na watu utakumbana na maneno eti ukifanya mambo ya kijinga au upuuzi basi utaanikwa JF, hii naona ni moja ya sifa ya uimara wa JF ambao ni- "we dare to talk openly".
Pia sasa kuna baadhi ya wanachama ambao wametumwa kuja hapa JF kuleta zogo mimi nawaambaia sasa muache na muwe makini.
Kwa mtazamo wangu ni kwamba JF imeanza kuwa sumu kwa baadhi ya watu ambao ni MAFISADI na sasa wanaogopa namna ambavyo wataanikwa hapa JF.
Cha msingi ni wale wana JF wote kuhakikisha kwamba tunasimama imara kwa hoja zenye nguvu na zenye vigezo na mantiki zisizo tetereka na kuwa tayari kuwaanika wale wote iwe MAFISADI AU WATOTO WAO na washirika wao kama ambavyo CCM na matawi yake London imejaa watu ambao viza zao zimeisha muda na wengine wamejilipua.
Mkuu Kitila endelea kushiriki JF bila woga na usibabaishwe na makelele ya walio na sera za kifisadi.
Idumu JF!
Pole na uzushi huu ambao Brazamen anajua dhamira (motive) yake ilikuwa ni nini.
Mimi nilijiunga na JF kwa nia njema kabisa ya kushiriki na watanzania wenzangu popote pale walipo iwe ughaibuni au mahali pengine kubadilishana mawazo na kupeana taarifa mbalimbali na mambo mengine.
Pia wanachama wenzangu mkifuatilia sbabu za mimi kujiunga na mtandao huu niliwahi kuziweka huko nyuma katika posting zangu.
Siku hizi ukipita na kukutana na watu utakumbana na maneno eti ukifanya mambo ya kijinga au upuuzi basi utaanikwa JF, hii naona ni moja ya sifa ya uimara wa JF ambao ni- "we dare to talk openly".
Pia sasa kuna baadhi ya wanachama ambao wametumwa kuja hapa JF kuleta zogo mimi nawaambaia sasa muache na muwe makini.
Kwa mtazamo wangu ni kwamba JF imeanza kuwa sumu kwa baadhi ya watu ambao ni MAFISADI na sasa wanaogopa namna ambavyo wataanikwa hapa JF.
Cha msingi ni wale wana JF wote kuhakikisha kwamba tunasimama imara kwa hoja zenye nguvu na zenye vigezo na mantiki zisizo tetereka na kuwa tayari kuwaanika wale wote iwe MAFISADI AU WATOTO WAO na washirika wao kama ambavyo CCM na matawi yake London imejaa watu ambao viza zao zimeisha muda na wengine wamejilipua.
Mkuu Kitila endelea kushiriki JF bila woga na usibabaishwe na makelele ya walio na sera za kifisadi.
Idumu JF!