Rais Samia: Kila mtu awe na namba moja ya utambulisho

Rais Samia: Kila mtu awe na namba moja ya utambulisho

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
82,487
Reaction score
88,627
Akizindua idara ya kutunza taarifa binafsi, Rais Samia Aametoa muda hadi Disemba kuhakikisha Waziri Mkuu anasimamia mifumo yote ya Serikali kusomana.

View: https://twitter.com/MfanyakaziNews/status/1775480907102638499?t=OHIesMI5IwoYE1RKLnryvg&s=19

Aidha Samia ameagiza Kuwa na Namba Moja ya Utambulisho badala ya kuwa na Utitiri wa makadi.

Watanzania wote, kila mtu awe na namba yake mwenyewe, [Wizara ya Habari] wameipa jina Jamii Namba. Haiwezekani mtu mmoja una identity [utambulisho] tatu, lazima uwe na identity moja, akiitwa Samia Suluhu rekodi ni hizo kila mahali [...]

Muwatake wananchi wa-update [huishe] taarifa zao, watambulikane vile wanavyotaka watambulikane ili turahisishe huduma katika nchi yetu.

--
Hongera sana mh.Rais Kwa kuendelea kutupunguzia mizigo isiyo na msingi.

Unakuta unaenda Benki inajaza NIDA still mtu anataka finger print wakati zilishachukuliwa kisa mifumo haisomani. Upuuzi mtupu.


My Take
Naunga mkono Kwa Nguvu zote,Hilo lifanyiwe kazi haraka sana.
 
Watu wa IT upepo wa kisurisuri uliokuwa unapeleka kware jangwani kwa wana israel umewafikia
Kazi kwenu
 
Nitatoa katiba,Leo katiba baadae ya miaka miatatu,juzi katiba ni kijitabu tu
 
Kweli kuna umuhimu huo,hata mimi vitambulisho vyangu taarifa zipo tofauti.
 
Back
Top Bottom