Siasa za Umeme: Kwa vile Umeme wa Stigler's utatosha na ziada kuuza nje. Je, TANESCO kusaini PPA mpya 6 toka kwa 6 IPPs, sio ufisadi mpya wa kisasa?

kwamba niwambie nitazikwa wapi😂😂😂😂..
Pamoja katika ujenzi wa taifa.goja nitafte fact 100% then nakuja hapa tena.

Kumbe hata hukuwa na facts? Si ulisema sijasikia ufafanuzi kutoka kwa mamlaka husika, kwa mantiki ya kuwa ww ulisikia? Haya boss, kasake facts uje uzimwage hapa jukwaani. Tena hizo facts uzifungulie uzi wake kabisa.
 
Kumbe hata hukuwa na facts? Si ulisema sijasikia ufafanuzi kutoka kwa mamlaka husika, kwa mantiki ya kuwa ww ulisikia? Haya boss, kasake facts uje uzimwage hapa jukwaani. Tena hizo facts uzifungulie uzi wake kabisa.
msssiuuu eti sikuwa na fact!! Sasa nimejuwaje yote hayo?? Unaanza kukwama wapi mkuu?? Au kusema nitafte ukweli zaidi unaona kama umeshinda hii battle??
Sipendi kubishana bila evidance,sipendi uongo napenda ukweli na nitasema ukweli daima. Tatzo unakurupuka kuja kutoa mapovu bila kufanya utafti kama wenzako.Tatfa ushahidi then uje hapa,usilete story za kwenye kahawa mkuu.Sijapenda...
Sifungulii uzi wala nini,nitakutafta nikupe ushahidi woooote,nadhani baada ya ukweli huo nitakuwa nimekuokoa na kazi ya kuabudu hapo ufipa.
#Lengo ni kujenga sio kubomoa!!
 
Wanabodi,

Kwa vile hii ni mada technical, yaani ni mada ya kitaalam, naomba kuanza bandiko hili kwa elimu kidogo kwa members wenzangu ambao sio wataalam wa mambo ya power na energy.

Watu wanadhani siasa ni kusimama tuu majukwaani na kupiga domo, issues yoyote yenye impact kubwa kwa taifa ni siasa, hivyo hivyo zozote zinazohusu utilities, maji, umeme, gesi, mafuta, na public transport ni siasa, na kwa nchi zinazotegemea mkate kama chakula kikuu, issue yoyote. ya mkate ni siasa! kuna nchi inayotegemea mkate kama chakula chake kikuu, bei ya mkate ilipanda kwa thumuni tuu!, wananchi waliingia barabarani na serikali ilipinduliwa!. Hivyo issues za Umeme sio habari mchanganyiko ni siasa!

Kwa vile tumeelezwa umeme wa Stigler ukikamilika utatosha na ziada kuuzwa nje!, Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani Desemba 14, 2020 akiwa katika ziara ya kukagua ujenzi wa Mradi mkubwa wa kufua umeme wa Megawati 2115 kwa njia ya maji wa Julius Nyerere, amesema inatarajiwa kwa mwaka 2023 mahitaji ya umeme Nchini yakaongezeka kwa zaidi ya mara mbili mpaka kufikia megawati 2,770.

"Leo hii mahitaji kwa siku ni megawati 1,177.20. Kukamilika kwa mradi huu wa Julius Nyerere kutaongeza megawati 3,973 ambazo zitatumika katika shuguli za maendeleo ya kiuchumi na kijamii hivyo tunahitaji umeme wa kutosha, utakaobaki tutawauzia majirani zetu" amesema Dkt. Kalemani.

Leo asubuhi, nimesoma mahali kuwa Tanesco imesaini mikataba mipya 6 ya PPA (Power Purchase Agreements) koka kwa wazalishaji binafsi IPPs (Independent Power Producers ) wapya 6, ili kununua megawati 19.16 na kuziingiza kwenye gridi ya taifa, ndani ya miezi 18 ijayo, Jee huu sio aina mpya ya ufisadi mpya wa kisasa kama ulivyokuwa ufisadi wa Richmond, Dowans na IPTL?!.

Hebu kwanza jisomee story yenyewe

TANZANIA: TANESCO to buy 19.16 MW of green electricity from six IPPs


By Inès Magoum - Published on December 14 2020 / Modified on December 14 2020

TANZANIE : la Tanesco va acheter 19,16 MW d’électricité verte à six IPP©abriendomundo/Shutterstock

Six Independent Power Producers (IPPs) have just concluded power purchase agreements with the Tanzania Electric Supply Company (TANESCO). These private companies are developing renewable energy projects in Tanzania with a total capacity of 19.16 MW.​


The state-owned Tanzania Electric Supply Company (TANESCO) is signing power purchase agreements (PPAs) with six independent power producers (IPPs) that are developing several renewable energy projects in Tanzania. TANESCO agrees to purchase 19.16 MW of electricity, under the supervision of the Energy and Water Regulatory Authority (EWURA) of Tanzania.

Among the selected IPPs is Nishati Lutheran Investment, which is implementing a 36-kW hydropower project at the Ijangala Falls in Makete. Similarly, Madope Hydro is implementing the 1.7 MW Madope Hydroelectric Project on the Madope River. Luponde Hydro is also signing a PPA with Tanesco for its Luponde hydroelectric project (9 kW) on the Luhololo River in Njombe. Lung’ali Natural Resources, which is implementing the Maguta hydroelectric project (1.2 MW) on the Lukosi River Falls in Kilolo, will sell its production to the utility.

Commercial operation in 18 months​

The other IPP selected is NextGen Solawazi which is working on a 5 MW hydropower project in the Kigoma Special Economic Zone. SSI Energy Tanzania, which is currently building a 10 MWp solar power plant in Kahama, will also sell its production to Tanesco. According to the public company, the six private companies will have to start marketing their production within 18 months.

In the meantime, TANESCO is developing other electricity projects in Tanzania. In this way, TANESCO is supporting the Tanzanian government’s policy of achieving a 75% electrification rate by 2035. Among its projects is the construction of the Rumakali and Ruhudji hydroelectric power plants which will have capacities of 222 MW and 358 MW respectively. In July 2020, TANESCO selected Multiconsult Norge AS, a Norwegian engineering consulting firm, to provide consulting services for the two projects.

My Take:
Japo mimi ni mwandishi wa habari, na sasa nimeisha staafu rasmi, lakini kwa vile kazi ya uandishi iko kwenye damu, hivyo ikitokea habari inahitaji ufuatiliaji, mimi nitaiweka tuu humu jf, wahariri watakao iona it's newsworthy, watatuma waandishi wao kuifuatilia, au waandishi watakaona ni habari, wataifuatilia, mimi nitakuwa nimetimiza wajibu wangu kwa jamii, ila ikitokea kweli ukawa ni ufisadi mwingine, utakuja kujulikana mwaka 2025 kabla ya uchaguzi ujao, nitakachokifanya ni kuwakumbusha tuu kuwa tulinusa, tukasikia harufu, tukauliza, na hayo ndio matokeo, ila pia, sio kila unaposikia harufu ya ufisadi ni ufisadi, harufu nyingine ni harufu tuu na hakuna ufisadi wowote, vitu vingine ni ukosefu tuu wa transparency, kama zile Bilioni 1.5 kwenye ripoti fulani ya CAG, watu wakadhani ni ufisadi, ikaja kukutikana hakuna ufisadi wowote.

Maswali ni haya.
  1. Kwanza maendeleo yoyote ya ujenzi wa mioundo mbinu wa umeme wa maji, ni maendeleo, endelevu, hivyo wakati Watanzania tukiusubiri huu umeme wa Stigler kuingizwa kwenye gridi ya Taifa, hakuna ubaya kwa Tanesco kuendelea kununua umeme toka kwa wazalishaji binafsi waliopo, kwa vile kuna wazalishaji wengi na mikataba imesimamishwa, kwa nini Tanesco wasiendelee nao na badala yake wanasani mikataba na wazalishaji wapya?. What is so special na hawa wapya, wakati wa zamani wapo, mikataba imesitishwa na wengine wametushitaki kwa kuvunja mikataba yao?
  2. Kama umeme wa Stigler, unatosha, hizi PPA's 6 mpya zinazosainiwa sasa ni za nini?.
  3. Kule nyuma tulivunja mkataba wa Dowans kwa tuhuma za ufisadi wa kulipishwa capacity charge kubwa na Tanesco kununua umeme wa bei juu toka kwa hawa IPPs na kuuza kwa bei ya chini!, Jee this time kwenye hii mikataba mipya jee Tanesco wananunua kwa bei gani per unit na kuuza kwa bei gani, tusije kuwa tunatwanga maji kwenye kinu?
  4. Baada ya kuvunjwa kwa mkataba wa Dowans, tulishitakiwa, tukashindwa kesi, tukadaiwa fidia iliyotwa Tozo ya Dowans, waheshimiwa wetu kule Bunge, wakajiapisha kwa maneno kama "over my dead body!" hatulipi! did you know what happened?....we paid every single cent kimya kimya na umeme ukapandishwa bei, Watanzania wote kwa ujumla wetu, tukafidia. Kitu cha ajabu sana katika hili, kampuni ile ile ya Dowans tuliovunja nayo mkataba, ikajibadili jina kujiita Simbion, mitambo ile ile, capacity charge ile ile, na mkataba ule ule, ikaingia tena mkataba na Tanesco, na tukakawa tunawalipa hadi JPM alipoingia, akaukataa ujinga huu, ndipo mkataba wa Simbion ukasitishwa na mpaka sasa kesi iko mahakamani, sijui tumefikia wapi! Kawa haya ndio mambo ya Tanesco na hizi PPA's zake, vipi hizi PPA's sita mpya are they clean?, transparent?.
  5. Kuna wakati kule nyuma, Tanesco ilikuwa inaelemewa na madeni ya umeme wa hawa PPA's na situation ya Tanesco kwa sasa ikoje hadi kuendelea kununua umeme kwa hawa wazalishaji binafsi, ili Tanesco ipate faida ni lazima inunue kwa bei ya jini na kuuza kwa bei ya juu, sasa kama Tanesco haina uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha, kwa nini hao wazalishaji binafsi wasiruhusiwe kuuza umeme wao direct kwa watumia kwa bei ya chini, wananchi ndio wafaidike?.
  6. Japo tunaelezwa Stigler ikikamilika Tanzania tutakuwa na umeme wa kutosha na ziada kuuza nje. Hawa jamaa wanasema "In the meantime, TANESCO is developing other electricity projects in Tanzania. In this way, TANESCO is supporting the Tanzanian government’s policy of achieving a 75% electrification rate by 2035", wakimaanisha huo mwaka 2035, Tanzania ndio tutafikisha 75% ya mahitaji yetu ya umeme!, sasa nani anasema kweli?, jee ni kweli tutajitosheleza na ziada kuuza nje, au tutajitosheleza kwa mahitaji ya sasa kwasabu bado hajaweza ku electrify nchi nzima, hivyo hiyo ziada tutakayouza nje, tutauza huku baadhi ya vijiji vyetu havina umeme kwasababu hatuna miondombinu ya kutosha ku i electrify nchi nzima?. Which is which?.

Paskali
Update
Habari yenyewe

TANESCO yasaini mkataba wa kununua umeme kwa wazalishaji wadogo​

KUSAINI MKATABA KATI YA TANESCO NA WAWEKEZAJI WADOGO



Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeingia mkataba wa kununua umeme kutoka kwa wazalishaji wadogo wa kampuni sita binafsi, utakaoingia moja kwa moja kwenye kwenye gridi ya Taifa na kutumika katika maeneo mbalimbali Nchini.

Akizungumza katika hafla fupi ya kusaini mikataba kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Meneja Mwandamizi Uwekezaji, Mhandisi Costa Rubagumya alisema wawekezaji hao wamekidhi vigezo kwa mujibu wa kanuni zilizoidhinishwa na EWURA.

"Kwa mujibu wa kanuni zinazosimamia uendelezaji wa miradi midogo ya kuzalisha umeme, inaitaka TANESCO kuingia mikataba na wazalishaji umeme wadogo kwenye maeneo ambayo gridi ya Taifa bado haijafika", alisema Mhandisi Rubagumya.

Aliainisha vigezo vingine ni maeneo ambayo yanatatizo la umeme mdogo ili kuimarisha ubora wa umeme na kigezo kingine ni maeneo ya usambazaji umeme ambapo njia za umeme za TANESCO ni ndefu hivyo kusababisha upotevu wa umeme.

Mhandisi Costa alizitaja kampuni hizo kuwa ni, Kahama Solar Power Project MW 10.0, Kigoma Solar Power MW 5.0, Nishati Lutheran (DKK) Investment Ltd MW 0.36.

Makampuni mengine ni, Madope Hydropower MW 1.7, Luponde Hydropower MW 0.9 na Maguta Hydropower MW 1.2.

Wakizungumza Kwa niaba ya Wazalishaji wadogo wa umeme, Padre Luciano Mpoma na Nicholas Richardson wameishukuru Serikali kupitia TANESCO kwa kukubali kufanya nao biashara ya umeme.

Waliongeza kuwa safari ilikuwa ni ndefu lakini hatimaye wamekuwa na furaha kwani lengo la Serikali ni kuhakikisha nishati ya umeme inamgusa kila mwananchi.

Makampuni hayo yanatakiwa kuanza kuiuzia TANESCO umeme ndani ya miezi 18 kuanzia leo Disemba 08, 2020.

Update 2.
Mchango very constructive
Ingekuwa vizuri ungeweka conclusion baada ya kuweka bei ya huo umeme. Vile vile inaonekana mradi huu wa wazalishaji wadogo haukuanza leo, information za ziada zinahitajika ili kuwa na ushahidi usiokuwa na mashaka. Je walianza huo mpango lini? Kama unafahamu ingekuwa jambo la maana kulifahamu.

BTW mradi wa JNHPP utakuwa unategemea maji ndio sababu kama sikosei kutakuwa na mabwawa ya ziada endapo kutatokea ukame nk. Kama tutakuwa na umeme mwingi sio vibaya tukawauzia majirani ambao watakuwa wanahitaji. Solar energy in a long run ndio utakuwa nafuu zaidi lakini mwanzo ni ghali. Ni vizuri Tanzania kukumbatia kila aina ya nyezo ya kuwezesha kuwa na wigo kubwa wa upatikanaji wa umeme.
 
msssiuuu eti sikuwa na fact!! Sasa nimejuwaje yote hayo?? Unaanza kukwama wapi mkuu?? Au kusema nitafte ukweli zaidi unaona kama umeshinda hii battle??
Sipendi kubishana bila evidance,sipendi uongo napenda ukweli na nitasema ukweli daima. Tatzo unakurupuka kuja kutoa mapovu bila kufanya utafti kama wenzako.Tatfa ushahidi then uje hapa,usilete story za kwenye kahawa mkuu.Sijapenda...
Sifungulii uzi wala nini,nitakutafta nikupe ushahidi woooote,nadhani baada ya ukweli huo nitakuwa nimekuokoa na kazi ya kuabudu hapo ufipa.
#Lengo ni kujenga sio kubomoa!!

Nimecheka kwa nguvu haya maelezo yako. Nilijua lazima utapanick. Haya nasubiri hizo facts, ili niache kusujudia Ufipa.
 
Ingekuwa vizuri ungeweka conclusion baada ya kuweka bei ya huo umeme. Vile vile inaonekana mradi huu wa wazalishaji wadogo haukuanza leo, information za ziada zinahitajika ili kuwa na ushahidi usiokuwa na mashaka. Je walianza huo mpango lini? Kama unafahamu ingekuwa jambo la maana kulifahamu.

BTW mradi wa JNHPP utakuwa unategemea maji ndio sababu kama sikosei kutakuwa na mabwawa ya ziada endapo kutatokea ukame nk. Kama tutakuwa na umeme mwingi sio vibaya tukawauzia majirani ambao watakuwa wanahitaji. Solar energy in a long run ndio utakuwa nafuu zaidi lakini mwanzo ni ghali. Ni vizuri Tanzania kukumbatia kila aina ya nyezo ya kuwezesha kuwa na wigo kubwa wa upatikanaji wa umeme.

Iwapo bwawa la JNHPP kutatokea ukame, sasa ikitokea ukame hayo mabwawa mengine huo ukame hautafika?
 
Matumizi ya umeme wa gas ile tuliyokuwa tunaimbishwa uchumi wa gas kama wendawazimu yameishia wapi?
Hivi kichwa chako kina kamasi? Mara ngapi umeambiwa JK alishaikula hiyo gas na umeme wake utakuwa wa bei juu sana. Hii iwe mara ya mwisho kukueleza jambo hili
 
Hivi kichwa chako kina kamasi? Mara ngapi umeambiwa JK alishaikula hiyo gas na umeme wake utakuwa wa bei juu sana. Hii iwe mara ya mwisho kukueleza jambo hili
Amechukuliwa hatua gani, kulikuwa na Mahakama ya mafisadi mbona hatukuona yoyote huko? Je kama JK Kala ya gas na ameachwa, tuna uhakika gani mradi huu wa SG hatuliwi?
 
Amechukuliwa hatua gani, kulikuwa na Mahakama ya mafisadi mbona hatukuona yoyote huko? Je kama JK Kala ya gas na ameachwa, tuna uhakika gani mradi huu wa SG hatuliwi?
JK sheria inamlinda bwashee. JPM kuona hilo akautia pembeni ili waliotoa hela wamdai waliomhonga. Hata hili huoni kuwa JPM alifanya la maana?
 
JK sheria inamlinda bwashee. JPM kuona hilo akautia pembeni ili waliotoa hela wamdai waliomhonga. Hata hili huoni kuwa JPM alifanya la maana?

Uko sahihi sana, kwahiyo sheria inalinda mwizi? Na jiwe akitupiga itakuwa sawa tu maana sheria inamlinda? JK katupiga, kisha mkewe akapewa ubunge, na sasa mtoto na mke wako bungeni! Katika mazingira hayo unaamini vipi kwa sasa hatupigwi? Na uko hapa unatetea hayo!?
 
Uko sahihi sana, kwahiyo sheria inalinda mwizi? Na jiwe akitupiga itakuwa sawa tu maana sheria inamlinda? JK katupiga, kisha mkewe akapewa ubunge, na sasa mtoto na mke wako bungeni! Katika mazingira hayo unaamini vipi kwa sasa hatupigwi? Na uko hapa unatetea hayo!?
JPM hana ubavu wa kutuchapa kama JK. Huelewi aliyeanza kutuchapa katika madini alikuwa JK akiwa waziri wa Nishati na Madini. Prof Mwandosya akiwa Katibu Mkuu wake. Mikataba mibovu ya umeme JK, we acha tu! Ila kwa mbali JPM kamkomesha. Tuyaache tumchunge JPM asije akakengeuka. Ila nina imani JPM hawezi kuwa fisadi kiasi cha JK
 
Uko sahihi sana, kwahiyo sheria inalinda mwizi? Na jiwe akitupiga itakuwa sawa tu maana sheria inamlinda? JK katupiga, kisha mkewe akapewa ubunge, na sasa mtoto na mke wako bungeni! Katika mazingira hayo unaamini vipi kwa sasa hatupigwi? Na uko hapa unatetea hayo!?
Wewe ambae unauhakika na imani kuwa tunapigwa tunaomba uthibitisho na ushahidi.
 

TANESCO yasaini mkataba wa kununua umeme kwa wazalishaji wadogo​

KUSAINI MKATABA KATI YA TANESCO NA WAWEKEZAJI WADOGO



Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeingia mkataba wa kununua umeme kutoka kwa wazalishaji wadogo wa kampuni sita binafsi, utakaoingia moja kwa moja kwenye kwenye gridi ya Taifa na kutumika katika maeneo mbalimbali Nchini.

Akizungumza katika hafla fupi ya kusaini mikataba kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Meneja Mwandamizi Uwekezaji, Mhandisi Costa Rubagumya alisema wawekezaji hao wamekidhi vigezo kwa mujibu wa kanuni zilizoidhinishwa na EWURA.

"Kwa mujibu wa kanuni zinazosimamia uendelezaji wa miradi midogo ya kuzalisha umeme, inaitaka TANESCO kuingia mikataba na wazalishaji umeme wadogo kwenye maeneo ambayo gridi ya Taifa bado haijafika", alisema Mhandisi Rubagumya.

Aliainisha vigezo vingine ni maeneo ambayo yanatatizo la umeme mdogo ili kuimarisha ubora wa umeme na kigezo kingine ni maeneo ya usambazaji umeme ambapo njia za umeme za TANESCO ni ndefu hivyo kusababisha upotevu wa umeme.

Mhandisi Costa alizitaja kampuni hizo kuwa ni, Kahama Solar Power Project MW 10.0, Kigoma Solar Power MW 5.0, Nishati Lutheran (DKK) Investment Ltd MW 0.36.

Makampuni mengine ni, Madope Hydropower MW 1.7, Luponde Hydropower MW 0.9 na Maguta Hydropower MW 1.2.

Wakizungumza Kwa niaba ya Wazalishaji wadogo wa umeme, Padre Luciano Mpoma na Nicholas Richardson wameishukuru Serikali kupitia TANESCO kwa kukubali kufanya nao biashara ya umeme.

Waliongeza kuwa safari ilikuwa ni ndefu lakini hatimaye wamekuwa na furaha kwani lengo la Serikali ni kuhakikisha nishati ya umeme inamgusa kila mwananchi.

Makampuni hayo yanatakiwa kuanza kuiuzia TANESCO umeme ndani ya miezi 18 kuanzia leo Disemba 08, 2020.
So long hakuna janja janja ya kulipana capacity charges au mashariti mabovu kama ilivyokuwa kwa Dowans, Iptl na Richmond, hili ni jambo jema.
 
Uko sahihi sana, kwahiyo sheria inalinda mwizi? Na jiwe akitupiga itakuwa sawa tu maana sheria inamlinda? JK katupiga, kisha mkewe akapewa ubunge, na sasa mtoto na mke wako bungeni! Katika mazingira hayo unaamini vipi kwa sasa hatupigwi? Na uko hapa unatetea hayo!?
Kila nikisoma post zako humu JF huwa naona kama huwa umejeza matope kichwani. Habari za familian JK zinaingia vipi hapa?
 
Pasco hizo hesabu za megawati zinaweza kuwa kama zile za kilimo cha tikiti, unaweka milioni 5 unavuna milioni 15.

Hesabu za karatasi huwa ni tamu sana ila kwa graundi inaweza kuwa tofauti. Cha msingi tulia kunywa mtori, nyama zipo chini !
 
Wanabodi,

Kwa vile hii ni mada technical, yaani ni mada ya kitaalam, naomba kuanza bandiko hili kwa elimu kidogo kwa members wenzangu ambao sio wataalam wa mambo ya power na energy.

Watu wanadhani siasa ni kusimama tuu majukwaani na kupiga domo, issues yoyote yenye impact kubwa kwa taifa ni siasa, hivyo hivyo zozote zinazohusu utilities, maji, umeme, gesi, mafuta, na public transport ni siasa, na kwa nchi zinazotegemea mkate kama chakula kikuu, issue yoyote. ya mkate ni siasa! kuna nchi inayotegemea mkate kama chakula chake kikuu, bei ya mkate ilipanda kwa thumuni tuu!, wananchi waliingia barabarani na serikali ilipinduliwa!. Hivyo issues za Umeme sio habari mchanganyiko ni siasa!

Kwa vile tumeelezwa umeme wa Stigler ukikamilika utatosha na ziada kuuzwa nje!, Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani Desemba 14, 2020 akiwa katika ziara ya kukagua ujenzi wa Mradi mkubwa wa kufua umeme wa Megawati 2115 kwa njia ya maji wa Julius Nyerere, amesema inatarajiwa kwa mwaka 2023 mahitaji ya umeme Nchini yakaongezeka kwa zaidi ya mara mbili mpaka kufikia megawati 2,770.

"Leo hii mahitaji kwa siku ni megawati 1,177.20. Kukamilika kwa mradi huu wa Julius Nyerere kutaongeza megawati 3,973 ambazo zitatumika katika shuguli za maendeleo ya kiuchumi na kijamii hivyo tunahitaji umeme wa kutosha, utakaobaki tutawauzia majirani zetu" amesema Dkt. Kalemani.

Leo asubuhi, nimesoma mahali kuwa Tanesco imesaini mikataba mipya 6 ya PPA (Power Purchase Agreements) koka kwa wazalishaji binafsi IPPs (Independent Power Producers ) wapya 6, ili kununua megawati 19.16 na kuziingiza kwenye gridi ya taifa, ndani ya miezi 18 ijayo, Jee huu sio aina mpya ya ufisadi mpya wa kisasa kama ulivyokuwa ufisadi wa Richmond, Dowans na IPTL?!.

Hebu kwanza jisomee story yenyewe

TANZANIA: TANESCO to buy 19.16 MW of green electricity from six IPPs


By Inès Magoum - Published on December 14 2020 / Modified on December 14 2020

TANZANIE : la Tanesco va acheter 19,16 MW d’électricité verte à six IPP©abriendomundo/Shutterstock

Six Independent Power Producers (IPPs) have just concluded power purchase agreements with the Tanzania Electric Supply Company (TANESCO). These private companies are developing renewable energy projects in Tanzania with a total capacity of 19.16 MW.​


The state-owned Tanzania Electric Supply Company (TANESCO) is signing power purchase agreements (PPAs) with six independent power producers (IPPs) that are developing several renewable energy projects in Tanzania. TANESCO agrees to purchase 19.16 MW of electricity, under the supervision of the Energy and Water Regulatory Authority (EWURA) of Tanzania.

Among the selected IPPs is Nishati Lutheran Investment, which is implementing a 36-kW hydropower project at the Ijangala Falls in Makete. Similarly, Madope Hydro is implementing the 1.7 MW Madope Hydroelectric Project on the Madope River. Luponde Hydro is also signing a PPA with Tanesco for its Luponde hydroelectric project (9 kW) on the Luhololo River in Njombe. Lung’ali Natural Resources, which is implementing the Maguta hydroelectric project (1.2 MW) on the Lukosi River Falls in Kilolo, will sell its production to the utility.

Commercial operation in 18 months​

The other IPP selected is NextGen Solawazi which is working on a 5 MW hydropower project in the Kigoma Special Economic Zone. SSI Energy Tanzania, which is currently building a 10 MWp solar power plant in Kahama, will also sell its production to Tanesco. According to the public company, the six private companies will have to start marketing their production within 18 months.

In the meantime, TANESCO is developing other electricity projects in Tanzania. In this way, TANESCO is supporting the Tanzanian government’s policy of achieving a 75% electrification rate by 2035. Among its projects is the construction of the Rumakali and Ruhudji hydroelectric power plants which will have capacities of 222 MW and 358 MW respectively. In July 2020, TANESCO selected Multiconsult Norge AS, a Norwegian engineering consulting firm, to provide consulting services for the two projects.

My Take:
Japo mimi ni mwandishi wa habari, na sasa nimeisha staafu rasmi, lakini kwa vile kazi ya uandishi iko kwenye damu, hivyo ikitokea habari inahitaji ufuatiliaji, mimi nitaiweka tuu humu jf, wahariri watakao iona it's newsworthy, watatuma waandishi wao kuifuatilia, au waandishi watakaona ni habari, wataifuatilia, mimi nitakuwa nimetimiza wajibu wangu kwa jamii, ila ikitokea kweli ukawa ni ufisadi mwingine, utakuja kujulikana mwaka 2025 kabla ya uchaguzi ujao, nitakachokifanya ni kuwakumbusha tuu kuwa tulinusa, tukasikia harufu, tukauliza, na hayo ndio matokeo, ila pia, sio kila unaposikia harufu ya ufisadi ni ufisadi, harufu nyingine ni harufu tuu na hakuna ufisadi wowote, vitu vingine ni ukosefu tuu wa transparency, kama zile Bilioni 1.5 kwenye ripoti fulani ya CAG, watu wakadhani ni ufisadi, ikaja kukutikana hakuna ufisadi wowote.

Maswali ni haya.
  1. Kwanza maendeleo yoyote ya ujenzi wa mioundo mbinu wa umeme wa maji, ni maendeleo, endelevu, hivyo wakati Watanzania tukiusubiri huu umeme wa Stigler kuingizwa kwenye gridi ya Taifa, hakuna ubaya kwa Tanesco kuendelea kununua umeme toka kwa wazalishaji binafsi waliopo, kwa vile kuna wazalishaji wengi na mikataba imesimamishwa, kwa nini Tanesco wasiendelee nao na badala yake wanasani mikataba na wazalishaji wapya?. What is so special na hawa wapya, wakati wa zamani wapo, mikataba imesitishwa na wengine wametushitaki kwa kuvunja mikataba yao?
  2. Kama umeme wa Stigler, unatosha, hizi PPA's 6 mpya zinazosainiwa sasa ni za nini?.
  3. Kule nyuma tulivunja mkataba wa Dowans kwa tuhuma za ufisadi wa kulipishwa capacity charge kubwa na Tanesco kununua umeme wa bei juu toka kwa hawa IPPs na kuuza kwa bei ya chini!, Jee this time kwenye hii mikataba mipya jee Tanesco wananunua kwa bei gani per unit na kuuza kwa bei gani, tusije kuwa tunatwanga maji kwenye kinu?
  4. Baada ya kuvunjwa kwa mkataba wa Dowans, tulishitakiwa, tukashindwa kesi, tukadaiwa fidia iliyotwa Tozo ya Dowans, waheshimiwa wetu kule Bunge, wakajiapisha kwa maneno kama "over my dead body!" hatulipi! did you know what happened?....we paid every single cent kimya kimya na umeme ukapandishwa bei, Watanzania wote kwa ujumla wetu, tukafidia. Kitu cha ajabu sana katika hili, kampuni ile ile ya Dowans tuliovunja nayo mkataba, ikajibadili jina kujiita Simbion, mitambo ile ile, capacity charge ile ile, na mkataba ule ule, ikaingia tena mkataba na Tanesco, na tukakawa tunawalipa hadi JPM alipoingia, akaukataa ujinga huu, ndipo mkataba wa Simbion ukasitishwa na mpaka sasa kesi iko mahakamani, sijui tumefikia wapi! Kawa haya ndio mambo ya Tanesco na hizi PPA's zake, vipi hizi PPA's sita mpya are they clean?, transparent?.
  5. Kuna wakati kule nyuma, Tanesco ilikuwa inaelemewa na madeni ya umeme wa hawa PPA's na situation ya Tanesco kwa sasa ikoje hadi kuendelea kununua umeme kwa hawa wazalishaji binafsi, ili Tanesco ipate faida ni lazima inunue kwa bei ya jini na kuuza kwa bei ya juu, sasa kama Tanesco haina uwezo wa kuzalisha umeme wa kutosha, kwa nini hao wazalishaji binafsi wasiruhusiwe kuuza umeme wao direct kwa watumia kwa bei ya chini, wananchi ndio wafaidike?.
  6. Japo tunaelezwa Stigler ikikamilika Tanzania tutakuwa na umeme wa kutosha na ziada kuuza nje. Hawa jamaa wanasema "In the meantime, TANESCO is developing other electricity projects in Tanzania. In this way, TANESCO is supporting the Tanzanian government’s policy of achieving a 75% electrification rate by 2035", wakimaanisha huo mwaka 2035, Tanzania ndio tutafikisha 75% ya mahitaji yetu ya umeme!, sasa nani anasema kweli?, jee ni kweli tutajitosheleza na ziada kuuza nje, au tutajitosheleza kwa mahitaji ya sasa kwasabu bado hajaweza ku electrify nchi nzima, hivyo hiyo ziada tutakayouza nje, tutauza huku baadhi ya vijiji vyetu havina umeme kwasababu hatuna miondombinu ya kutosha ku i electrify nchi nzima?. Which is which?.

Paskali
Update
Habari yenyewe

TANESCO yasaini mkataba wa kununua umeme kwa wazalishaji wadogo​

KUSAINI MKATABA KATI YA TANESCO NA WAWEKEZAJI WADOGO



Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeingia mkataba wa kununua umeme kutoka kwa wazalishaji wadogo wa kampuni sita binafsi, utakaoingia moja kwa moja kwenye kwenye gridi ya Taifa na kutumika katika maeneo mbalimbali Nchini.

Akizungumza katika hafla fupi ya kusaini mikataba kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Meneja Mwandamizi Uwekezaji, Mhandisi Costa Rubagumya alisema wawekezaji hao wamekidhi vigezo kwa mujibu wa kanuni zilizoidhinishwa na EWURA.

"Kwa mujibu wa kanuni zinazosimamia uendelezaji wa miradi midogo ya kuzalisha umeme, inaitaka TANESCO kuingia mikataba na wazalishaji umeme wadogo kwenye maeneo ambayo gridi ya Taifa bado haijafika", alisema Mhandisi Rubagumya.

Aliainisha vigezo vingine ni maeneo ambayo yanatatizo la umeme mdogo ili kuimarisha ubora wa umeme na kigezo kingine ni maeneo ya usambazaji umeme ambapo njia za umeme za TANESCO ni ndefu hivyo kusababisha upotevu wa umeme.

Mhandisi Costa alizitaja kampuni hizo kuwa ni, Kahama Solar Power Project MW 10.0, Kigoma Solar Power MW 5.0, Nishati Lutheran (DKK) Investment Ltd MW 0.36.

Makampuni mengine ni, Madope Hydropower MW 1.7, Luponde Hydropower MW 0.9 na Maguta Hydropower MW 1.2.

Wakizungumza Kwa niaba ya Wazalishaji wadogo wa umeme, Padre Luciano Mpoma na Nicholas Richardson wameishukuru Serikali kupitia TANESCO kwa kukubali kufanya nao biashara ya umeme.

Waliongeza kuwa safari ilikuwa ni ndefu lakini hatimaye wamekuwa na furaha kwani lengo la Serikali ni kuhakikisha nishati ya umeme inamgusa kila mwananchi.

Makampuni hayo yanatakiwa kuanza kuiuzia TANESCO umeme ndani ya miezi 18 kuanzia leo Disemba 08, 2020.

Update 2.
Mchango very constructive
Nanusa harufu ya ufisadi, naanza kupata mashaka, renewable energy ndio iwe sababu ya kutetea deal kama hizi? Hakuna 10%? Mbona hata usa Hydroelectric ndio mkombozi wao! China na Brazili wanaongoza kwa kuzalisha HEP kwa nini kuhangaika na kununua umeme wakati tunasubiri Mw 2115? Hizi Mw 19 za nini?
 
Kwa post hii uko sawa kabisa. Sasa nijibu hiki nitakachokuuliza kwenye hii post. Tunawekeza $6.5b kwenye bwawa la SG kufua umeme wa 2,115mw. Lakini kabla ya awamu hii tulikuwa na umeme wa gas ambao tayari bomba liko hapa Dar. Kwenye ujenzi wa hilo bomba hadi Dar tulikopa $1.2b na tunazalisha zaidi ya 300mw mpaka sasa. Je ni kwanini tunawekeza $,6.5 kwenye mradi mpya wa maji ambao tuliambiwa tatizo ni mabadiliko ya tabia nchi, tuache kuwekeza kwenye umeme wa gas ambao tayari tumekopa $1.2b, na miundombinu imekamilika? Je hizo $6.5n tusingepata umeme mwingi zaidi ya hizo 2,115mw? Nahitaji majibu hapo kwani siasa haina nafasi hapo.
Mkuu nisamehe kwa kuchelewa kukujibu majukumu mengi. Tukirudi kwenye swali lako ni kwamba kipindi cha nyuma ishu nyingi zilikuwa zinaanzishwa ili watu wapige pesa, mfano mzuri benki ya Standard Chartered HongKong imetumiwa Sana kutukopesha ili watu wapige pesa bila kujali huko mbele itakuwaje, na waliweka mikataba tata sana ambayo kuivunja ni ngumu. Sababu ya pili umeme wa gesi una limit. Gesi inaisha ardhini na ina mwisho wake kabisa. Kadiri unavyoitumia ndo inavyopungua ardhini. Ni Kama mtungi wa Kg45 jikoni kwako inavyopungua kadri unavyoitumia,sema huko ardhini ni Kama mtungi mkubwa sana, so ukiwekeza $bil.6.5 huna uhakika Kama zitarudi gesi haijaisha ardhini. Gesi ni natural reserve ambayo composition yake inachukua muda mrefu sana. Lakini Stigler Gorge inategemea maji kwa 95% au zaidi na ukifatilia umeme wa maji bado ni wa uhakika Sana tofauti na gesi. JPM ni mwanasayansi mzuri sana na anayajua haya yote na wameshayajadili, tatizo wengi humu wamekaa mkao wa kupinga lolote atakalofanya. Sijui Kama nimeeleweka vizuri mkuu.
 
JPM hana ubavu wa kutuchapa kama JK. Huelewi aliyeanza kutuchapa katika madini alikuwa JK akiwa waziri wa Nishati na Madini. Prof Mwandosya akiwa Katibu Mkuu wake. Mikataba mibovu ya umeme JK, we acha tu! Ila kwa mbali JPM kamkomesha. Tuyaache tumchunge JPM asije akakengeuka. Ila nina imani JPM hawezi kuwa fisadi kiasi cha JK

Mtu anayenajisi uchaguzi anatoa wapi uadilifu?
 
Mkuu nisamehe kwa kuchelewa kukujibu majukumu mengi. Tukirudi kwenye swali lako ni kwamba kipindi cha nyuma ishu nyingi zilikuwa zinaanzishwa ili watu wapige pesa, mfano mzuri benki ya Standard Chartered HongKong imetumiwa Sana kutukopesha ili watu wapige pesa bila kujali huko mbele itakuwaje, na waliweka mikataba tata sana ambayo kuivunja ni ngumu. Sababu ya pili umeme wa gesi una limit. Gesi inaisha ardhini na ina mwisho wake kabisa. Kadiri unavyoitumia ndo inavyopungua ardhini. Ni Kama mtungi wa Kg45 jikoni kwako inavyopungua kadri unavyoitumia,sema huko ardhini ni Kama mtungi mkubwa sana, so ukiwekeza $bil.6.5 huna uhakika Kama zitarudi gesi haijaisha ardhini. Gesi ni natural reserve ambayo composition yake inachukua muda mrefu sana. Lakini Stigler Gorge inategemea maji kwa 95% au zaidi na ukifatilia umeme wa maji bado ni wa uhakika Sana tofauti na gesi. JPM ni mwanasayansi mzuri sana na anayajua haya yote na wameshayajadili, tatizo wengi humu wamekaa mkao wa kupinga lolote atakalofanya. Sijui Kama nimeeleweka vizuri mkuu.
Hii sio fact, hayo ni maoni yako.
Sote tunajua duniani kote umeme wa maji sio jambo la kudumu, kadri muda unavyokwenda na mabadiliko ya tabia nchi basi na nguvu ya kuzalisha umeme kwa kutumia maji inapungua.

Upande wa pili, kuzalisha umeme kwa kutumia maji kuna kwenda sambamba na uharibifu ya ikologia ya viumbe hai.

Jambo moja kuu kuhusu umeme wa maji ni cheaper but limited. Gharama iko kwenye kuwekeza zaidi kuliko uendeshaji wake lakini hawezi kuzalisha zaidi ya kiwango cha juu kilichotegemewa.
 
Mkuu nisamehe kwa kuchelewa kukujibu majukumu mengi. Tukirudi kwenye swali lako ni kwamba kipindi cha nyuma ishu nyingi zilikuwa zinaanzishwa ili watu wapige pesa, mfano mzuri benki ya Standard Chartered HongKong imetumiwa Sana kutukopesha ili watu wapige pesa bila kujali huko mbele itakuwaje, na waliweka mikataba tata sana ambayo kuivunja ni ngumu. Sababu ya pili umeme wa gesi una limit. Gesi inaisha ardhini na ina mwisho wake kabisa. Kadiri unavyoitumia ndo inavyopungua ardhini. Ni Kama mtungi wa Kg45 jikoni kwako inavyopungua kadri unavyoitumia,sema huko ardhini ni Kama mtungi mkubwa sana, so ukiwekeza $bil.6.5 huna uhakika Kama zitarudi gesi haijaisha ardhini. Gesi ni natural reserve ambayo composition yake inachukua muda mrefu sana. Lakini Stigler Gorge inategemea maji kwa 95% au zaidi na ukifatilia umeme wa maji bado ni wa uhakika Sana tofauti na gesi. JPM ni mwanasayansi mzuri sana na anayajua haya yote na wameshayajadili, tatizo wengi humu wamekaa mkao wa kupinga lolote atakalofanya. Sijui Kama nimeeleweka vizuri mkuu.

Sina tatizo na maelezo yako mazuri, ila wakati tunaambiwa umeme wa gas ndio sahihi maana hiyo gas tutaitumia zaidi ya miaka 50, huyu anayetekeleza umeme wa maji alikuwa waziri kwenye serikali hiyo hiyo, mbona hakupinga? Wakati ule Utetezi wa umeme wa maji dhidi ya gas, tuliambiwa matatizo ni mabadiliko ya tabia nchi. Je baada ya utawala kubadili hayo mabadiliko ya tabia nchi yameboreka? Kama mtu aliweza kukalia kimya upotoshaji ule, unaweza kumuamini vipi sasa kwenye hili?

JPM ni mwanasayansi mzuri sana, je uanasayansi wake ulianza baada ya mkataba wa umeme wa gas? Mbona hakuyajadili hayo huko nyuma kwenye vikao vya gas? Sisi hatupingi lolote, bali hatukubali lolote bila maelezo ya kina, tumeshaumwa na nyoka. Hatuna imani na Magu wala chochote cha kwake, angekuwa mtu muadilifu angejitenga na huo wizi wa kwenye gas. Toka amaeingia madaraka hakuna uchaguzi wowote umefanyika kwa uadilifu, kama mtu anaweza kuchezea uchaguzi wa nchi, uadilifu anautoa wapi?
 
Back
Top Bottom