Titicomb
JF-Expert Member
- Jan 27, 2012
- 11,329
- 17,832
Kuna taarifa mpya ya kutekwa mgombea wa CHADEMA kwa ngazi ya UDIWANI na UBUNGE kila baada ya dakika chache ndani ya siku 5 za mwisho kuelekea siku ya leo tarehe 25/08/2020 ya kupitishwa majina ya wagombea na NEC.
Nyingi ya hizi taarifa hazina uthibitisho kiasi kwamba zinaleta hofu kuna watu wamepanga kuichafua nchi kwa makusudi na kutaka kupata uhalali wa kuja kufanya vurugu na kuomba jumuiya za kimataifa kuingilia mambo ya ndani ya Tanzania.
Sasa ifike wakati Tanzania iwe mbele kuliko maslahi binafsi. Kuna uwezekano mkubwa huu ni ushauri hatari uliopendekezwa na watu wa ndani au wa nje ya nchi ambao wana maslahi binafsi. Ninacho kiona ni hatari ya vita kama nchi zingine zilizo ingia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe au kuvamiwa na majeshi ya kigeni kwa mlango wa kukomesha vurugu, kulinda amani na kusimamia demokrasia.
Vita hivi havitachagua familia za wana CCM au wana CHADEMA, ACT, NCCR-Mageuzi, ADC, CHAUMA au CUF pekee.
Mnaofanya mambo haya na kushawishi vijana wasiojielewa kutumika katika mipango hovu, haya mambo yatatudhuru wote na biashara zetu wote.
Msitumike na nchi jirani au watu wa mabara mengine kama hamjitambui.
Napata shida kuishauri serikali hasa Idara ya Usalama wa Taifa, JWTZ, na jeshi la polisi kuanza kuchukua hatua ngumu zaidi kwa waeneza taarifa hizi. Lakini sina budi niwashauri ikiwalazimu fanyeni hivyo, kama media zikishindwa kuwadai uthibitisho zaidi basi ziwekeeni speed governor maana hakuna namna, hapo baadaye watanzania wema watawashukuru kwa kuwaokoa na mkono wa mtoa roho. Wanasema 'the end justifies the means'.
Jukwaa letu pendwa JF nawashauri mjisafishe mikono yenu na damu zinazokaribia kumwagika sababu ya habari hizi za propaganda, jifuteni mikono yenu machozi ya watoto yatima watakao telekezwa na familia zao wakati wa vurugu, picha maarufu ya mtoto wa Sudan aliyekaribia kuliwa na tai baada ya kukosa uangalizi wakati wa vita inatembea kwenye akili yangu na kunitia simanzi sana nikiwaza jambo kama lile linaweza kuwatokea maelfu ya watoto wa kitanzania.
Ile picha ni mbaya kiasi kwamba mpigaji alikufa kwa msongo wa mawazo na kujutia kuchukua picha kama ile ingawa ilimpa utajiri, fikiria wewe unaye leta taarifa za uzushi zikija kusababisha mambo kama yale unafikiri utaishi kwa amani ndani ya nafsi yako hata kama unayemtaka ataingia Ikulu na kukupa ulaji wa keki ya taifa?
Mambo yalianza kama hivi hivi propaganda kwenye media kule kwa wenzetu nchi za jirani maziwa makuu. Yale mafuvu yanatisha zaidi kama ukiona ulikuwa sehemu ya jambo ovu kama lile kutokea.
Yale magofu ya Libya na biashara ya utumwa inasikitisha zaidi kama wewe ni sehemu ya waliochangia kutokea jambo lile.
Mchana mwema.
Nyingi ya hizi taarifa hazina uthibitisho kiasi kwamba zinaleta hofu kuna watu wamepanga kuichafua nchi kwa makusudi na kutaka kupata uhalali wa kuja kufanya vurugu na kuomba jumuiya za kimataifa kuingilia mambo ya ndani ya Tanzania.
Sasa ifike wakati Tanzania iwe mbele kuliko maslahi binafsi. Kuna uwezekano mkubwa huu ni ushauri hatari uliopendekezwa na watu wa ndani au wa nje ya nchi ambao wana maslahi binafsi. Ninacho kiona ni hatari ya vita kama nchi zingine zilizo ingia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe au kuvamiwa na majeshi ya kigeni kwa mlango wa kukomesha vurugu, kulinda amani na kusimamia demokrasia.
Vita hivi havitachagua familia za wana CCM au wana CHADEMA, ACT, NCCR-Mageuzi, ADC, CHAUMA au CUF pekee.
Mnaofanya mambo haya na kushawishi vijana wasiojielewa kutumika katika mipango hovu, haya mambo yatatudhuru wote na biashara zetu wote.
Msitumike na nchi jirani au watu wa mabara mengine kama hamjitambui.
Napata shida kuishauri serikali hasa Idara ya Usalama wa Taifa, JWTZ, na jeshi la polisi kuanza kuchukua hatua ngumu zaidi kwa waeneza taarifa hizi. Lakini sina budi niwashauri ikiwalazimu fanyeni hivyo, kama media zikishindwa kuwadai uthibitisho zaidi basi ziwekeeni speed governor maana hakuna namna, hapo baadaye watanzania wema watawashukuru kwa kuwaokoa na mkono wa mtoa roho. Wanasema 'the end justifies the means'.
Jukwaa letu pendwa JF nawashauri mjisafishe mikono yenu na damu zinazokaribia kumwagika sababu ya habari hizi za propaganda, jifuteni mikono yenu machozi ya watoto yatima watakao telekezwa na familia zao wakati wa vurugu, picha maarufu ya mtoto wa Sudan aliyekaribia kuliwa na tai baada ya kukosa uangalizi wakati wa vita inatembea kwenye akili yangu na kunitia simanzi sana nikiwaza jambo kama lile linaweza kuwatokea maelfu ya watoto wa kitanzania.
Ile picha ni mbaya kiasi kwamba mpigaji alikufa kwa msongo wa mawazo na kujutia kuchukua picha kama ile ingawa ilimpa utajiri, fikiria wewe unaye leta taarifa za uzushi zikija kusababisha mambo kama yale unafikiri utaishi kwa amani ndani ya nafsi yako hata kama unayemtaka ataingia Ikulu na kukupa ulaji wa keki ya taifa?
Mambo yalianza kama hivi hivi propaganda kwenye media kule kwa wenzetu nchi za jirani maziwa makuu. Yale mafuvu yanatisha zaidi kama ukiona ulikuwa sehemu ya jambo ovu kama lile kutokea.
Yale magofu ya Libya na biashara ya utumwa inasikitisha zaidi kama wewe ni sehemu ya waliochangia kutokea jambo lile.
Mchana mwema.