Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Ameen kwa nasaha zako ,ahsante sana!
Tuombeane
Kamata hii shem lake.

Kwa vile wewe ni mzazi wao, watoto wanaweza wakakupenda na kukuheshimu sana lakini wakawa wamekuzoea. Hata ukiwapa ushauri na nasaha za maana sana wanaona tu ni kawaida na hawatilii maanani kivile. Mama ndo kawaida zake!

Pamoja na kwamba ni jukumu lako kama mama yao kuwaombea kila siku na kuhakikisha wanakua katika misingi sahihi ya kiMungu lakini pia siyo vibaya ukiwa na watu wa nje wachache unaowaamini mkawa mnasaidiana nao katika kuwapa mawaidha na miongozo hasa kipindi hiki kigumu na cha hatari wanachoingia utineja. Anaweza kuwa dada yako au rafiki yako mliyeshibana sana. Wanakwenda huko na kusikia sauti nyingine hata kama ni mawaidha yale yale, lakini kwa mtazamo tofauti. Inasaidia sana lakini hakikisha ni watu unaowaamini sana ndo wanakuwa na access na akina Minza wetu.

Kuna kipindi binti yangu alinigomea kabisa kabisa. Yaani nikimshauri, kwa vile ni mimi baba yake, anaona kama namboa tu. Naona ni stage fulani hivi huwa wanafikia yaani hawataki kabisa kusikia sauti ya mzazi. Utasikia oooh boy here comes the lecture!...na macho wanakuzungushia. Basi nikamtuma kwa rafiki yangu wa kike nikamwambia bwana eeh hebu nisaidie hapa. Wiki moja aliporudi amekubaliana na kila kitu alichoshauriwa kule wakati ni kitu kile kile nilichokuwa namshauri mimi. Hata mimi nilishashauri watoto wengi wa ndugu na marafiki; na wakanisikiliza mimi na kufuata ushauri wangu kuliko wa wazazi wao - kumbe mimi na wazazi wao letu moja!
 
Sasa hivi mkuu hautaki Tena za matoleo mapya? Ni ngumu kweli miaka 15 umekaa nalo tafuta Tena faza chuma hizi
Sasa hivi siliwezi na wameshaacha kuyatengeneza nadhani. Wamepata chalenji kubwa kwa RR mpaka wamebwaga manyanga; na walichelewa kidogo kuyafanya yawe ya kisasa zaidi. End of an era!
 
Back
Top Bottom