Mimi kukata ticket week kabla ya safari ndiyo tabia yangu labda nipate safari ya dharura na kama safari ni ya dharura huwa situmii basi. Nina allergy na seat za nyuma na nikikosa za mbele huwa natamani hata kulia maana najua safari yangu itaboa tu.
Pale mbele huwa napenda sana company ya wale makonda kwa mfano kwenye mabasi kama Sauli unakuta kuna makonda wengi wengine hadi wanakaa chini pembeni kabisa ya dereva. Basi huwa naenjoy kweli wanavyochangamsha genge na story zao.
Hivi Dar Lux na Rungwe yapo jamani? Enzi zile Rungwe bado inatamba, ukoo mzima wanyaki tunapanda Rungwe, ole wako ukapande bus lingine. Kuna siku karibu na Kitonga ile; sijui bus lilitaka liwake moto. Maana ilianza harufu kali ndani kama ya chemicals; ukaja moshi mzito ndani; daah kumbe nipo mwepesi vile kwenye kuruka dirishani hehehe; maisha matamu jamani mweeh.