Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga

Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga

Kwani Pasco amepatwa na nini, mbona amebadilika ghafla. Anayejua atujuze.

Amebadilika? Labda umemjua jana au juzi. Huyu ni yule yule shabiki wa Lowassa na Zitto. Nakushangaa wewe unayemshangaa
 
Kama vile damu ya Habili ilivyolilia haki ya kuishi kutoka mavumbini dhidi ya muuaji wake Kaini ndivyo damu za yule kijana wa Singida, Igunga na Arumeru zinavyomlilia Mwigulu Nchemba. Ni jambo la mda tu, hakika Mungu YAHU atazilipia kisasi. Ole mkuu uko kwa Yeyote atakayejaribu ku-divert mshale wa kisasi wa Mungu ambao tayari usharushwa juu ya anga la Tanzania.
.
 

Ushahidi mwingine

Kwa mujibu wa Wakili Lissu, yamepatikana pia mawasiliano ya mtu aitwaye Dennis Msacky akimpigia simu Lwakatare, ambapo wamemuuliza Lwakatare iwapo ni kweli aliwasiliana na mtu mwenye jina hilo (ambaye kwenye charge sheet ya pili, polisi wameonesha ndiye aliyekuwa akipangiwa kutekwa/kufanyiwa vitendo vya ugaidi), naye amekubali kuwa ni kweli alimpigia simu siku moja kabla ya tukio la kurekodiwa, akimuuliza kama amerudi Dar es Salaam, naye akamwambia alikuwa njiani kutoka Bukoba.
Pasco utakumbukwa sana kwenye hili. Siku ile nakumbuka watu walisema njaa itakupeleka pabaya na kukupa majina mengi sana. Lakini kadri habari zinavyounfold wale bendera fuata upepo wanaanza kuona kile ulichowaambia.

Kwahiyo Msacky na Lwakatare ni watu ambao wana casual conversitions!!!

Ile video ya Slaa akimtetea Lwakatare itunzeni vizuri...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mpaka Kieleweke,
Kwanza poleni kwa yote!.
Pili mnayo team nzuri sana ya wanasheria, lakini nashauri, mara moja moja, muwe mnasikiliza maoni ya ma layman kama sisi kupitia humu jf.

Nasikitika kuwaambia kitendo cha kufungua kesi kuhoji mamlaka ya DPP, its a wastage of time!. Mamlaka ya DPP haihojiwi na mamlaka yoyote hata rais wa nchi, hawezi kuyahoji, hivyo you are fighting a loosing battle!.

Ni kweli timu yenu ya sheria is a good team, nashauri please seek legal opinion ya best criminal lawyers around, kwa sababu baadhi ya wanasheria wenu ni politiciancs, wajiangalie wasije wakaipoliticise hii kesi kuonekana its a political case, bali muendelee kuipigania iwe abduction na sio terrorisim!.

Mwisho mtake msitake, lazima Chadema kama chama, kitoe statement kuwa whatever mashitaka yanayomkabili Rwakatare, ni yake mwenyewe kama Rwakatare, vingenevyo hali ikiachwa ilivyo, kuna hatari ya jamii kuaminishwa kuwa hayo yaliiyotendeka, yamendwa kwa maelekezo ya chama, hivyo kuja kuwaingiza hata wasiokuwemo!.

Huu ni ushauri wa bure tuu toka kwa layman.

Pasco.

imeshaeleweka kuwa mpango wa ccm ni kubambikia kesi viongozi wa chadema. unataka Lwakatale aachiwe kesi, ili ikifika zamu ya Dr.Slaa kubambikiwa kesi naye mshinikize atoswe kwa sababu Lwakatale alitoswa. mwisho wa siku ionekane chadema hawana umoja....kwa taarifa yenu kama ilivyo kwa viongozi wetu wa ngazi yajuu. na sisi wanachama wa kawaida msimamo ni mmoja "ccm inawakandamiza chadema":...............mkuu naona umejikita rasmi kwenye meli ya Edo.!!
 
Mkuu,nilikuwa ninashangaa anavyokiri kila kitu na kukataa sauti katika statement ya police.Chafya inaweza kuwa ugaidi hivi leo kama unamafua ya ndege na kwa makusudi ukaama kuyaeneza sio jinai?

Mingoi

Umeulizwa kama ni ugaidi au si ugaidi, wewe unasema ni jinai, jamani vipi! Kwani hata kama ingekuwa ni jinai kama unavyotaka tena iwe, jinai zote ni ugaidi?
 
".... saa 5:59 Ludovick aliwasiliana na mtu aitwale Mwigulu Nchemba!!!!!!!
 
The only big difference between cdm n ccm is that, cdm inapendwa na watu wanaoipenda mno nchi yao na chama chao,hujitolea bure kukilinda na kujenga chama chao

Ccm ni chama kinachojipenda chenyewe basi, chochote wafanyacho ni kwa manufaa binafsi na chama chao hata kama mambo hayo hayana manufaa kwa nchi na mwananchi. Juhudi nyingi zinafanywa kuidhoofisha chadema si kwa manufaa ya nchi bali ya chama chao na yao binafsi, na si nchi.

Wanaogopa cdm ikishika dola huenda wakadai mabilioni waliyokwiba.

Mungu ibariki cdm kwa mustakabali mwema wa nchi yetu pendwa:what::thumbup:
 
Machadema bana bure kabisa. Sasa hata kama anahusika ikiwa mumeshampatia maswali si atakuwa na muda kutosha kuyapangua?

Eti chama mbadala! Yangu macho.
 
ngoja nimjibie Ludovick ni tarishi wa Denis Msacky,Zitto Kabwe,Mwiguru Nchemba wote kwa pamoja kuanzia tarehe 27 dec 2012- 2-February 2013 walikuwa kwenye mawasiliano mazito ya kuchonga video, je ndio TISS ya Tanzania inavyofanya kazi kujiacha uchi trace thread ya wanasheria wa chadema utapata habari hii
Thanks.
Hata hivyo swali langu nilielekeza kwa Ben Saanane huku nikiwa na matumaini makubwa kama atasepa
 
Last edited by a moderator:
Mnateteaje waovu? Haingiu akilini wote humu mnatetea magaidi
 
Mwigulu atawaumbua sana. Jamaa hayuko mnavyomfikiria. Aliposema ana cd mlisema mropokaji sasa mbona mnahangaika baada ya magaid kupelekwa lupango. The way I know the person is soo smart na ana taarifa nyingi sana za mauaji ya chadomo
 
This is getting interesting. Jf tuwekeni hiyo video wengine tunaisikia tu. harafu mhe Lissu tunamwomba aende mbele zaidi
kutunyambulia sheria inayoruhusu kunyakua habari za email ama sms za mtu mwingine. Na kama tuhuma kuwa hio video ni ya kughushi, je ana uthibitisho gani kuwa sms na email tajwa si za kughushi?
 
Hahahaaa dpp huyu huyu mulimsifu kwa kumnyima dhamana ponda vp leo munamkejeli
 
Back
Top Bottom