Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga

Sakata la Lwakatare: Wanasheria CHADEMA walonga

Hivi sasa wanasheria wa CHADEMA wanafanya mkutano na waandishi wa habari kuhusiana na tukio la Lwakatare na makosa ambayo alishitakiwa nayo.

Anaeleza kuwa kama ameshitakiwa kwa ugaidi lazima makosa hayo yawe ni ya kigaidi, ila makosa ya Kidnapping na abduction ni makosa ya kawaida ya jinai , na kama ili yawe ya kigaidi ni lazima hayo makosa yawe yamefanyika kwa malengo ya kigaidi , na hata hati ya mashitaka haina maelezo ya makosa ya ugaidi .


Nyongeza: kuhusu video amesema tayari kuna ushahidi wa kimawasiliano baina ya Mwigulu Nchemba ya tarehe 28.12.2012 wakiwasiliana na Ludovick saa 5:55 asubuhi , na Lwakatare amesema kuwa yeye alikutana na Ludovick kuanzia saa tano asubuhi tarehe 28.

Aidha , ameongeza kuwa tarehe 27.12.2012 Denis Msacky alimpigia simu Lwakatare wakati akiwa njiani kurejea akitokea Kagera , akiwa Morogoro na kumuuliza kama yupo DSM , akamjibu yuko njiani.

Tatu, tarehe 29.12.2012 Mwigulu Nchemba , akiwa na Zitto na Mtatiro Star Tv , kipindi cha tuongee asubuhi ndipo alisema kuwa ana mkanda wa viongoz i wa chadema wakipanga mauaji ......sasa haya yote yatajulikana mahakamani.

Ziada .

Maelezo aliyotoa Lwakatare polisi kuhusu maneno yaliyoko kwenye video alisema kuwa yeye anakumbuka siku ya tarehe 28, alikuwa nyumbani kwake na Ludovick ndio alienda kwake , ila picha ya video ni ya kwake , sura ni ya kwake ila baadhi ya maneno yaliyoko sio ya kwake na ameandika hivyo , kwa hiyo kuhusu ukweli wa mkanda majibu ya kina yanatakiwa kutoka polisi , Mwigulu na Denis ndio wanajua nini kipo kwenye mkanda . Hivyo picha limeanza kuonekana , na kwa taarifa zaidi ni kuwa polisi wana video yenye dakika 27.06 na maneno yanatofautiana sana na yaliyoko kwenye You tube iliyowekwa kwenye mitandao .

Sasa polisi nao waliulizwa ni kwanini hawajamkamata aliyeweka hiyo you tube kwenye mitandao walitoa majibu yao na mawakili wanaendelea na uchunguzi wao.

Mtahangaika sana ila sheria itachukua mkondo wake. SWALA LA MSINGI NI KWANINI APANGE KUTEKA WATU NA KUWAPA WATU DAWA ZA USINGIZI? HAIJALISHI VIDEO IMEPATIKANAJE. ILA NI KWANINI APANGE HAYO?
 
How? alisema nini? na unahisi umati ulicheka kwasababu gani? umati ulimcheka Lisu au ulichekeshwa kwa jambo lingine? ZeMarcopolo ni miongoni mwa watu wachache sana nisiowaelewa kabisa hapa Jamvini!!!!
how is that?,kwanini humwelewi bana,una matatizo gani?au kwakua haungi mkono mawazo yako eeh?
 
Last edited by a moderator:
Mtahangaika sana ila sheria itachukua mkondo wake. SWALA LA MSINGI NI KWANINI APANGE KUTEKA WATU NA KUWAPA WATU DAWA ZA USINGIZI? HAIJALISHI VIDEO IMEPATIKANAJE. ILA NI KWANINI APANGE HAYO?

Inaelekea nawe ni mshirika utatusaidia kwenye ushahidi basi,hilo sio tija
 
Mtahangaika sana ila sheria itachukua mkondo wake. SWALA LA MSINGI NI KWANINI APANGE KUTEKA WATU NA KUWAPA WATU DAWA ZA USINGIZI? HAIJALISHI VIDEO IMEPATIKANAJE. ILA NI KWANINI APANGE HAYO?

Kwa kuwa imeongezwa maneno kwa maana ya kupunguza maneno ya awali video ni feki lakini linaondoa kabisa dhamira nzima ya kurekodiwa kama alirithia. Kama ni mpango tu wakuitumia hiyo video kwa njia ya kumrekodi mtu bila ridhaa yake ndiyo umebuma mahakama yo yote itayosikiliza itatudhihirishia kilichopo nyuma ya pazia na akina nani
 
Hii nchi ukiwa na roho nyepesi unaweza fanya ndivyo sivyo ukawapa maadui pointi
 
Jipeni moyo!
Ooh, Sorry Dude, kumbe jiwe langu nililolusha gizani limekupata. Ukweli mara nyingi ni Mwiba.

Ukweli ulivyo mwiba, hata kujibu swali dogo uliloulizwa umeshindwa kulijibu. Ninakuuliza tena,

JE, UNAMFAHAMU LUDOVICK, na Kama NDIYO. unamfahamu VIPI?.
 
Yeah, Wapo wengi tu hata hapa JF waliokuwa wameshupaa na mawazo kama ya Dr. Slaa.

Dr Slaa kakosa nini tena jamani Kusema video fake kwani ni uongo DPP kavuliwa nguo mchana kweupe kabadilisha hakimu,kesi kairudisha nyuma hajua afanyalo rejea Vuta -Nikute juzi kesi ilikuwa na 37 jana imekuwa na 6 chezea jopo la wanasheria wa chadema, nakwambia DPP mwaka huu lazima tuijue CV yake
 
Mamlaka ya DPP ni kufuta kesi kama kufanya hivyo kutakuwa ni kwa masilahi ya taifa au kwa nia ya kulenga kupata haki, hivyo hatua za kufuta kesi jana hazikuwa kwa masilahi ya taifa bali ilikuwa ni kuizuia mahakama kutoa haki, kilichofanyika jana ni matumizi mabaya ya mamlaka ya DPP,

HATUA TULIZOCHUKUA.
1. Leo tumefungua kesi mahakama kuu kwa hati ya dharura , kwa kuiomba mahakama iitishe mafaili yote mawili ,ili iyachunguze ione kama haki imetendeka kwa mujibu wa sheria za nchi yetu.

2. Wameiomba kama itakubali ifute ile hati ya DPP ya kufuta mashitaka, na ifute amri ya mahakama ya kufuta kesi iliyofanyika jana ,

3. Ielekeze mahakama ya hakimu mkazi kisutu , iendelee na utaratibu wa kutoa hukumu kama ilivyokuwa imepangwa , na hii ni kwa masilahi yab haki ionekane inatendeka.

Kilichofanyika n a mwendesha mashitaka wa serikali ni kuingilia uhuru wa mahakama katika kutenda haki.
Mkuu Mpaka Kieleweke,
Kwanza poleni kwa yote!.
Pili mnayo team nzuri sana ya wanasheria, lakini nashauri, mara moja moja, muwe mnasikiliza maoni ya ma layman kama sisi kupitia humu jf.

Nasikitika kuwaambia kitendo cha kufungua kesi kuhoji mamlaka ya DPP, its a wastage of time!. Mamlaka ya DPP haihojiwi na mamlaka yoyote hata rais wa nchi, hawezi kuyahoji, hivyo you are fighting a loosing battle!.

Ni kweli timu yenu ya sheria is a good team, nashauri please seek legal opinion ya best criminal lawyers around, kwa sababu baadhi ya wanasheria wenu ni politiciancs, wajiangalie wasije wakaipoliticise hii kesi kuonekana its a political case, bali muendelee kuipigania iwe abduction na sio terrorisim!.

Mwisho mtake msitake, lazima Chadema kama chama, kitoe statement kuwa whatever mashitaka yanayomkabili Rwakatare, ni yake mwenyewe kama Rwakatare, vingenevyo hali ikiachwa ilivyo, kuna hatari ya jamii kuaminishwa kuwa hayo yaliiyotendeka, yamendwa kwa maelekezo ya chama, hivyo kuja kuwaingiza hata wasiokuwemo!.

Huu ni ushauri wa bure tuu toka kwa layman.

Pasco.
 
Ooh, Sorry Dude, kumbe jiwe langu nililolusha gizani limekupata. Ukweli mara nyingi ni Mwiba.

Ukweli ulivyo mwiba, hata kujibu swali dogo uliloulizwa umeshindwa kulijibu. Ninakuuliza tena,

JE, UNAMFAHAMU LUDOVICK, na Kama NDIYO. unamfahamu VIPI?.

ngoja nimjibie Ludovick ni tarishi wa Denis Msacky,Zitto Kabwe,Mwiguru Nchemba wote kwa pamoja kuanzia tarehe 27 dec 2012- 2-February 2013 walikuwa kwenye mawasiliano mazito ya kuchonga video, je ndio TISS ya Tanzania inavyofanya kazi kujiacha uchi trace thread ya wanasheria wa chadema utapata habari hii
 
Dah!kumbe ndo mambo yenyewe,viongozi wa nchi hii kwa sasa wamepoteza uhalali wa kuongoza.
 
TISS, UWT na CCM kama hamtamuonya Mwigulu hii nchi mtaitumbukiza pabaya,.................
 
Mkuu Mpaka Kieleweke,
Kwanza poleni kwa yote!.
Pili mnayo team nzuri sana ya wanasheria, lakini nashauri, mara moja moja, muwe mnasikiliza maoni ya ma layman kama sisi kupitia humu jf.

Nasikitika kuwaambia kitendo cha kufungua kesi kuhoji mamlaka ya DPP, its a wastage of time!. Mamlaka ya DPP haihojiwi na mamlaka yoyote hata rais wa nchi, hawezi kuyahoji, hivyo you are fighting a loosing battle!.

Ni kweli timu yenu ya sheria is a good team, nashauri please seek legal opinion ya best criminal lawyers around, kwa sababu baadhi ya wanasheria wenu ni politiciancs, wajiangalie wasije wakaipoliticise hii kesi kuonekana its a political case, bali muendelee kuipigania iwe abduction na sio terrorisim!.

Mwisho mtake msitake, lazima Chadema kama chama, kitoe statement kuwa whatever mashitaka yanayomkabili Rwakatare, ni yake mwenyewe kama Rwakatare, vingenevyo hali ikiachwa ilivyo, kuna hatari ya jamii kuaminishwa kuwa hayo yaliiyotendeka, yamendwa kwa maelekezo ya chama, hivyo kuja kuwaingiza hata wasiokuwemo!.

Huu ni ushauri wa bure tuu toka kwa layman.

Pasco.

Pasco wa JF you have a best interest na hii kesi we are watching am optmistic wewe ni teja wa walio post video hiyo si bure kwa nini nasema hivyo unakatisha watu tamaa ,na unadhani mahakama kuu inafanya kazi ya suggestions za kwenye JF
 
Mbona wanasheria hawasemi ile video ni fake?

Kama ule mkanda nk genuine basi huo ni ugaidi.
Basi wapangie adhabu haraka! Hakuna sababu ya kumtia mtu hatiani kabla ya mahakama, halafu ukakaa kimya bila ya kutoa adhabu ya kosa lao. Hebu tuambie, faini au miaka mingapi?
 
Back
Top Bottom